Ifakara: Dr. Slaa Hakusalimiana na JK! Kwanini?

Ifakara: Dr. Slaa Hakusalimiana na JK! Kwanini?

Mbona Dr. Slaa haonyeshi ukomavu wa kisiasa. Nanusa harusi mbaya ndani ya CHADEMA! Huenda viongozi wengine CDM walikubaliana kumtambua JK lakini Dr. Slaa hakukubali na hataki kukubaliana na wengi ndio maana hataki kukutana na JK ili kuonyesha kwamba hamtambui. Dr. Slaa wenzio wamemtambua na wameishaenda Ikulu (mwingine mara mbili) basi nawe kubaliana na wenzio umtambue tu JK.

Hii itaonyesha uungwana badala ya kumkwepa mtu mzima mwenzio, hii inaonyesha kukosa ukomavu kisiasa na hali ya kuwa na vinyongo visivyoisha! Watu wanasema katika siasa hakuna uadui wa kudumu.
 
naona kama kuna chumvi kwenye hili swala,kumkwepa jk ili iwe nini mbona juz wamepeana mkono tabata kwa kina regia?waandsh wetu wa habari kwel ni makanjanja!vya maana vya kuandka vmeisha?
 
Nibora amesimiamia ukweli, kuliko kubadili ukweli kuwa uongo au uongo kuwa ukweli..LOGIC..huyu jamaa sio kigeugeu, anasimamia anacho kiamini.
 
Yaani waandishi wa habari banaa hii yote ni kwa ajili wauze gazeti tu yaani kilichoandikwa hapa na nilichoona Ifakara ni vitu viwili tofauti Dk Slaa alipangwa kukaa jukwaa jingine na Kikwete jukwaa jingine sasa watu walikuwa wanataka kwamba Slaa anyanyuke ndio akamsalimie JK yaani mimi sijaona mantiki yoyote kwenye hili suala zaidi ya watu kulifanya kubwa ili wauze magazeti yaani ukiwa haupo kwenye eneo la tukio waandishi wa habari wanaandika vitu vya ajabu na uwongo tu ili wauze magazeti.

Yaani mtu umepangwa kukaa jukwaa la kushoto kama ilivyokuwa kwa Dr Slaa halafu Kikwete ndio kakaa jukwaa kuu ambapo alikuwa pamoja na Mbowe, Zitto, Makinda, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Job Ndugai na wengineo sasa mtu unataka kuniambia Dr Slaa atoke jukwaa la kushoto ili tu akamsalimie JK jukwaa kuu naona ndio mawazo ya watu yalivyo ikumbukwe pia kiprotokali pia ilikuwa imepangwa hivyo tulipokutana na Slaa, Pasco alimuuliza Dr Slaa kuhusiana na hili na akamjibu vizuri jinsi utaraatibu ulivyokuwa...ila naelewa ni kwa ajili ya kuuza magazeti ndio maana waandishi wa habari lazima waandike hivyo..
 
Kuna thread kama tatu ama nne mfululizo zenye kuhusu this topic zilianzishwa almost in a simultaneous fashion, lakini naona mods nao wako very fast!lol
 
Asante pia kwa kutafuta na kupata ufafanuzi. Kuna gazeti leo limeripoti haya mambo ya JK na Dr Slaa kukwepana. Sijui ni lini haya magazeti yataitumia Jf kama source ya habari zao kwa uwazi na kuitaja bila kificho.


Kwani huko msibani mwandishi wa habari alikuwa ni Pasco tu?
 
Kumbukeni yaliomkuta DK. MWAKYEMBE katika maeneo kama hayo ya ujirani mwema. DK. Slaa lazima uwe mbali na adui, tena kuwa makini sana.
 
Slaa,
Moto ni huo huo. Ole wako nikuone siku moja unakutana na mwizi wetu wa kura. Tunajua JK katumia msiba wa Regia kujipaisha umaarufu wake wa kisiasa ambao umeporomoka kwa kasi ya kutisha!
 
Kwa wale wanaofikiria Dr Slaa anamuogopa JK nawashangaa! Iwapo mawaziri wake hawamuogopi JK kwa udhaifu wake wanajichotea mali za umma bila kuwa na ubavu wa kuwakemea, sembuse Dr Slaa?

Sana sana Dr Slaa amemsaidia JK kutokaa karibu naye maana JK angekuwa unease kutokana na aibu ya madhambi aliyo nayo kwa Watz akiwa karibu na mpambanaji wa ukweli wa ufisadi!

Dr Slaa -- usikubali kukaa na mtu huyo anayenuka ufisadi mtupu, anaweza kukuambukiza!
 
Yaani waandishi wa habari banaa hii yote ni kwa ajili wauze gazeti tu yaani kilichoandikwa hapa na nilichoona Ifakara ni vitu viwili tofauti Dk Slaa alipangwa kukaa jukwaa jingine na Kikwete jukwaa jingine sasa watu walikuwa wanataka kwamba Slaa anyanyuke ndio akamsalimie JK yaani mimi sijaona mantiki yoyote kwenye hili suala zaidi ya watu kulifanya kubwa ili wauze magazeti yaani ukiwa haupo kwenye eneo la tukio waandishi wa habari wanaandika vitu vya ajabu na uwongo tu ili wauze magazeti.

Yaani mtu umepangwa kukaa jukwaa la kushoto kama ilivyokuwa kwa Dr Slaa halafu Kikwete ndio kakaa jukwaa kuu ambapo alikuwa pamoja na Mbowe, Zitto, Makinda, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Job Ndugai na wengineo sasa mtu unataka kuniambia Dr Slaa atoke jukwaa la kushoto ili tu akamsalimie JK jukwaa kuu naona ndio mawazo ya watu yalivyo ikumbukwe pia kiprotokali pia ilikuwa imepangwa hivyo tulipokutana na Slaa, Pasco alimuuliza Dr Slaa kuhusiana na hili na akamjibu vizuri jinsi utaraatibu ulivyokuwa...ila naelewa ni kwa ajili ya kuuza magazeti ndio maana waandishi wa habari lazima waandike hivyo..

Hapana Dr.Slaa amemjibu kuwa amepangiwa kiti cha nyuma na sio kuwa majukwaa tofauti. Hapa kuna walakini
 
Hapana Dr.Slaa amemjibu kuwa amepangiwa kiti cha nyuma na sio kuwa majukwaa tofauti. Hapa kuna walakini
Gaijin ngoja nikuwekee picha ili uone vizuri watu wasije wakafikiri napotosha hapa ndio utajua kama Slaa alikuwa kweli kiti cha nyuma na sio jukwaa tofauti
 
Gaijin ngoja nikuwekee picha ili uone vizuri watu wasije wakafikiri napotosha hapa ndio utajua kama Slaa alikuwa kweli kitu cha nyuma na sio jukwaa tofauti

Hapana Finest, wewe unasema ulichokiona, na Pasco ameeleza alichojibiwa na Dr.Slaa

Sasa apparently hivyo vitu havi match at all. Alipangiwa kiti cha nyuma na kuamua kukaa jukwaa jengine au alipangiwa jukwaa jengine na kukaa huko lakini akasahau na kusema alipangiwa kiti cha nyuma? Au yote siyo?
 
Ok then The Finest, tuwekee the fine evidence lol!
 
DSC_0699.JPG

Hili ni Jukwaa alilokuwa amekaa Dr Slaa na huyo nyuma ni bodyguard wake pia kwenye jukwaa hili walikuwa wamekaa Lema, Josephine na wabunge wengine wa vyama vya upinzani sasa anayesema kuwa alipangiwa kiti cha nyuma aeleze vizuri
 
Yaani waandishi wa habari banaa hii yote ni kwa ajili wauze gazeti tu yaani kilichoandikwa hapa na nilichoona Ifakara ni vitu viwili tofauti Dk Slaa alipangwa kukaa jukwaa jingine na Kikwete jukwaa jingine sasa watu walikuwa wanataka kwamba Slaa anyanyuke ndio akamsalimie JK yaani mimi sijaona mantiki yoyote kwenye hili suala zaidi ya watu kulifanya kubwa ili wauze magazeti yaani ukiwa haupo kwenye eneo la tukio waandishi wa habari wanaandika vitu vya ajabu na uwongo tu ili wauze magazeti.

Yaani mtu umepangwa kukaa jukwaa la kushoto kama ilivyokuwa kwa Dr Slaa halafu Kikwete ndio kakaa jukwaa kuu ambapo alikuwa pamoja na Mbowe, Zitto, Makinda, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Job Ndugai na wengineo sasa mtu unataka kuniambia Dr Slaa atoke jukwaa la kushoto ili tu akamsalimie JK jukwaa kuu naona ndio mawazo ya watu yalivyo ikumbukwe pia kiprotokali pia ilikuwa imepangwa hivyo tulipokutana na Slaa, Pasco alimuuliza Dr Slaa kuhusiana na hili na akamjibu vizuri jinsi utaraatibu ulivyokuwa...ila naelewa ni kwa ajili ya kuuza magazeti ndio maana waandishi wa habari lazima waandike hivyo..

TF nakubaliana nawe hii habari imetiwa chumvi kama walivyofanya jana kuhusu Kafulila, wanatafuta mauzo!
 
View attachment 45697

Na huyo ni JK aliyekuwa amekaa Jukwaa kuu kulia kwake alikuwa amekaa Anna Makinda na kushoto kwake alikuwa amekaa mkuu wa mkoa wa Morogoro akifuatiwa na Mbowe halafu Zitto Kabwe, nyuma ya Kikwete kulikuwa kuna hao watu wa Usalama wa Taifa kama unavyoona sasa anayesema Slaa alikaa kitu cha nyuma atueleze vizuri
 
Hivi hawa waandishi wameshindwa kuipa uzito kwa mfano habari za mgomo wa madaktari? Kwanza hii si habari ni swala linalofaa kuandikwa kama makala ili ifanyiwe uchambuzi! magazeti yetu kazi ipo!
 
Back
Top Bottom