Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Mzee MKJJ hivi Serikali na EL wanaogopa nini ? Haya machapisho hayaendani na makatwa ya CCM na Serikali yake ama kuna nini ?
 
Mzee MKJJ hivi Serikali na EL wanaogopa nini ? Haya machapisho hayaendani na makatwa ya CCM na Serikali yake ama kuna nini ?


Mimi nadhani hapa kuna watu wanalinda maslahi binafsi....Halafu eti Serikali inasema imedhamiria kumkomboa Mtanzania. Haya mabango yanatakiwa yawekwenye kwenye kila ofisi ya kijiji/ kata/ mjumbe wa nyumba kumi na kituo cha basi na kwingineko. Huu ndio uwazi ambao jamii na serikali inapaswa kuunga mkono.

MJJ

Fanya uwaone HE tujue kulikoni..
 
Kuna Kitu Hapa Kinaendelea Ambacho Hakieleweki Kati Ya Serikali Na Haki Elimu. Watu Ambao Wana Nyeti Wazimwage Hapa Tafadhali, Hayo Uliyotuwekea Mkjj Naona Siyo.
 
Kuna Kitu Hapa Kinaendelea Ambacho Hakieleweki Kati Ya Serikali Na Haki Elimu. Watu Ambao Wana Nyeti Wazimwage Hapa Tafadhali, Hayo Uliyotuwekea Mkjj Naona Siyo.


Hapa hata mimi....I smell FISH. Either upande wa HakiElimu au Sirikali, somebody is hiding something.
 
Mwandishi Wetu




HII ni ndoto yangu. Ndoto hii niliiota siku nilipoamua kumrejea Mungu wangu wa kweli ambaye hakuna asiyemjua duniani, chini ya ardhi, juu ya ardhi hata angani.


Jina la Mungu wangu ni siri kuu. Ni siri ya siri kuu zote za dunia hii. Hivyo nimeona ni vyema nikawasimulia na wananchi wenzangu ili tujifunze yaliyowahi kuwatokea wenzetu waliotutangulia na kuona kama tutapata somo.


Kwa bahati mbaya au tuseme makusudi, Kaisari alipokuwa akishindana na wadogo zake juu ya urithi wa himaya yao Julius Mroma Augustus Kaizer (JMK), aliwadanganya Warumi kuwa angewatoa kwenye mateso yaliyokuwa yamefanywa na Kaisari Brutus Wilfrem Mkirene (BWM), aliyekuwa amemtangulia.


Wakati wa kampeni hizo za mwaka 2005 (KK), alitoa ahadi lukuki zinazoingia na kutoingia akilini. Katika ahadi zake zote, moja kuu iliwamotisha na kuwashawishi warumi hadi wakamchagua kwa kura nyingi. Ahadi hii si nyingine ni ile ya kuwapeleka Kanaani kwenye nchi ya maziwa na asali.


Warumi (Waisraeli) kwa mtazamo wa Kaisari, walikuwa utumwani Misri (BWM). Utumwa huu waweza kuelezwa kama ubabe, wizi, uzushi, kulindana, rushwa, matusi, unyang'au na mengine mengi kama hayo.


Kwa kuwa kwao Misri kwenye kiu na njaa, aliwaahidi kuwa atawapeleka Kanaani kwa msisitizo.


Aliwaahidi kuwavusha kwenye Bahari ya Sham (rushwa, wizi, ubadhirifu, kujuana, uzembe, umaskini, maradhi, ujinga na jinamizi lote la madhira kama hayo).


Warumi walidanganyika na kupewa matumaini hadi wakafikia kukufuru kwa kumlinganisha huyu Musa (Kaisari) wao wa bandia na Nabii yule (Julius Karneillo Nemesis au kwa kifupi JKN).


Ndimi zilianza kuwawasha wakikamia kugida maziwa na kumung'unya asali na manna (mafanikio, ukuaji wa uchumi, kuondoa rushwa, kurekebisha zoezi zima la uwekezaji na madhambi mengi yaliyokuwa yametamalaki).


Hamadi! Kumbe maskini Warumi hawakujua lugha za mafumbo tena ya kinyumenyume. Hawakujua na saa nyingine hawatajua wala kukengeuka kuwa walichochagua ni sawa na zile siku arobaini za Mwana wa Adam kujaribiwa na shetani!


Hawakujua kuwa walikuwa wakiandaliwa kutiwa mijeledi, kunyweshwa siki na hatimaye kusulubiwa. Na hii ingefanyika kwa kufungwa kamba na kuswagwa kama ng’ombe apelekwaye machinjioni.


Hakuchi hakuchi sasa kuchele. Matarajio yote kama tofali la barafu yalimomonyoka yasiache lau tuta!


Badala ya kuanza msafara kuelekea Kanaani na kuiacha Misri, kwa jeuri mpya na nguvu mpya na staili mpya, walichapa mguu kuelekea Misri kusini kwenye maeneo ya Ismailia na Aswan wakajenge mapiramidi mengine makubwa kuliko yale ya Giza (kutamalaki vitendo vya rushwa na wizi, kulindana kimtandao katika himaya ya Rumi wakati ule).


Amini usiamini firauni wa jana alianza kuonekana mzuri kuliko Musa bandia huyu na nduguye Haruni Losarius.


Hata wale wazee wa Mayahudi waliokuwa na busara waligeuzwa majuha watupu tena wa kujikomba kwa Musa Farao.


“Waisraeli walipoomba samaki walitupiwa nyoka, wanaomba maji wananyweshwa usaha, wanaomba mkate wanapewa mawe! Anayebisha aangalie washauri wa Musa bin Bandia.


“Angalia yanayojiri kwa sasa. Si kingine zaidi ya mapigo zaidi ya mia ya ndui, ukoma na magonjwa mengine hatari kuliko hata UKIMWI.” alinung’unika Mrumi mmoja baada ya kuona mambo si mambo.


Kulitokea ukoma na ndui na Musa, yaani Kaisari aliamua kujivua kushughulikia magonjwa kama haya akidai aliyeyasambaza ni mtangulizi wake.


Pili, kulizuka majipu na ngwengwe ya kuuzwa Roma kwa Magiriki na misafara ya wafanyabiashara wa Kiasia.


Pia kilizuka kifua kikuu cha Rumi kuingia mikataba ya vito vyake na magonjwa mengine ya zinaa kama vile kujuana, na dini mpya iliyoitwa webnization.


Mambo yalienda yakijirudia na kuongezeka. Kwani kulizuka na kashfa ya kununuliwa punda feki wa Musa kwa bei ya kulangua. Hata pesa ya Rumi kipindi kile ilianza kushuka thamani.


Iliporomoka kama inaharisha huku Kaisari akiwaambia Warumi “Mambo poa.”


Kwa upande mwingine Musa aliwaarika kina Delila wakachukua marimba, mabanjo, nyuta na kayamba zao kuwapumbaza Waisraeli ili waisahau ahadi kuu na agano kuu la kupelekwa Kanaani.


Angekuwa na uwezo angewaita hata wazaburi watumbuize Waisraeli ili waendelee kulala na kunajisiwa.


Taratibu ilianza kujitokeza tabia ya kujitengenezea sanamu ya ndama ifananayo na Musa na kuanza kuisujudia! Hasira za Mimi niko ambaye niko lazima zitawaangamiza Waisraeli.


Hebu zitazame dalili zote. Bahati mbaya wamejaa makahaba kila kona. Wako hata karibu na lilipowekwa agano kule Jerusalem (Roma hii ni kama Dodoma kwetu).
Walikuwamo hata kwenye madhabahu ya Bwana (wakuu wa mikoa na wilaya za Rumi).


Hata makuhani (viongozi wa dini), waandishi (vyombo vya habari), Mafarisayo (wasomi) na Masadukayo (watu maarufu) walinyweshwa kikombe hiki cha usaliti na uovu kiasi cha kuwa kwenye kundi moja na Firauni (Kaisari) mpya ambaye aliingia akiwa amejivika sura ya Musa.


Waisraeli badala ya kupelekwa Kanaani walikoahidiwa, wamewekwa rehani mikononi mwa Wagiriki majambazi (Waasiria) na kila aina ya utumwa.


Lile hekalu takatifu la Mungu (Ikulu ya Roma), taratibu liligeuka kuwa pango la wevi na watafuta ngawira. Hali iliharibika tangu alipoondoka nabii yule.


Hadithi hii ni ndefu mno. Leo tuishie hapa tukiwasalimia ndugu zetu waliopo kule Kaperanaum, Kahama ,Kaisaria, Mtwara, Krete, Tanga, Samalia, Mbeya, Galilaya, Biharamulo, Bethlehemu, Dumila, Idumea na Korintho.


Ni wenu Muisraeli aliyemo safarini kuelekea utumwani kusini mwa Misri.


Muhimu mtahadhali pigo hilo jipya la UKIMWI wa kiuchumi kutoka Asia Minor.

mmsemahovyo@yahoo.com Simu:0713260071



Source:http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/1/31/makala4.php
 
Duh!
Hiyo ndoto ni fumbo linaloendana na hadisi ya KUSADIKIKA.
 
There is nothing fishy here! Hapa issue ni serikali kuogopa demokrasia. Ni mazoea tu mabaya. Wenzetu wamezoea kusifiwa, sasa ikitokea mtu anawakosoa inakuwa shida. Serikali ya sisiem ni kama kikaragosi, wanataka uwasifie kuwa wanapendeza hata kama wamejifunga gunia. Hawa ni malimbukeni wa kutupa. Mtu atuambie katika matangazo ya Hakielimu, kitu gani ambacho sio cha kweli? Na ni kipi hicho ambacho kinakwenda kinyume na maslahi ya jamii?
 
Wana JamboForum,

Serikali kuifungia HakiElimu ni kwa sababu ya woga wa kuogopa kuvuli chake. Hii inadhihirisha serikali inajua kwamba utawala wao si bora, haukidhi hata robo ya shida za wananchi.

Kila mtanzania anapenda mwanae asome na aelimike ili baadae apate maisha bora yasiyokuwa tegemezi.


Sasa kauli mbiu ya HaElimu imekuwa inagonga vizuri msumari pale unapopaswa kugongwa, tena inagonga kwa kulenga na utaalamu hasa. Mfumo mzima wa elimu yetu ni shaghalabaghala, kuanzia mitaala ya sasa hivi, mazingira wanayosomea wanafunzi, mishahara ya waalimu na maswala mengi ya jamii ktk sekta hii.

HakiElimu kwa kutumia Radio na TV imejitahidi vizuri mno ktk kuanika uozo ndani ya sekta ya elimu na wanachi wanaanza kuamka na kuelewa na kugundua kuwa walikuwa wamo usingizini. Na hivyo basi ili wadanganyika wasiendelee kuamshwa serikali ya CCM (alianza waziri wa Elimu wa awamu ya tatu) imeamua kulifungia Shirika Lisilo la Kiserikali lililosajiliwa kihalali na halijawahi hata siku moja kutangaza matangazo yao kinyume na sheria za nchi.

SERIKALI YA CCM SASA IMEVAA MKANDA WA UKIDIKTETA

Jamani tuwaokoe wadogo zetu na watoto wetu, hao wa akina EL wanasoma Ulaya!!
 
kwa kweli hawa haki elimu ni moja ya tasisi ya kiraia isiyokuwa na chembe ya malengo ya kisiasa iliyobakia tumaini la watanzania sasa kama wameifungia ni uchinjaji wa demokrasia maana upinzani wameununua sasa hata na hizi taasisi za kiraia pia hawataki!!
kati ya jambo la mwisho wananchi kufikiri jk angefanya ni kuendelea kuionea haki elimu ,mkapa tulijua ni ubabe ,sasa jk tumuiteje,mnafiki?
 
Mtafaruku mwingine huo!,kila siku Drama mpya,tutafika kweli kwa mwendo huu!
 
Nashawishika kuamini kuwa kuna jambo kubwa zaidi ya hilo au hayo yanayoonekana kwa nje. Binafsi, kwa mfano, sioni kama hayo matangazo yana ubaya au kejeli kiasi kwamba hayavumiliki.

Nashawishika badala yake kutaka kuamini madai kuwa "wanatumiwa na majasusi" na wafadhili (ambao daima ni ndumila kuwili) kwa hiyo hizo ni harakati za kuwakatisha tamaa au kuwanyamazisha viongozi wake. Sitashangaa kama hao viongozi wake (wawili) wanaweza wakaambiwa siyo raia!

Nikilinganisha kwa mfano na magazeti binafsi au viongozi wa siasa wasio chama tawala, nadhani wanatoa maneno makali ambayo wakati mwingine unaweza kufikiri serikali itawaita "wahaini" lakini mbona hawafanyiwi mizengwe hivyo?
 
Nashawishika kuamini kuwa kuna jambo kubwa zaidi ya hilo au hayo yanayoonekana kwa nje. Binafsi, kwa mfano, sioni kama hayo matangazo yana ubaya au kejeli kiasi kwamba hayavumiliki.

Nashawishika badala yake kutaka kuamini madai kuwa "wanatumiwa na majasusi" na wafadhili (ambao daima ni ndumila kuwili) kwa hiyo hizo ni harakati za kuwakatisha tamaa au kuwanyamazisha viongozi wake. Sitashangaa kama hao viongozi wake (wawili) wanaweza wakaambiwa siyo raia!

Nikilinganisha kwa mfano na magazeti binafsi au viongozi wa siasa wasio chama tawala, nadhani wanatoa maneno makali ambayo wakati mwingine unaweza kufikiri serikali itawaita "wahaini" lakini mbona hawafanyiwi mizengwe hivyo?


True unachosema...ni ukweli ulio wazi kuwa bongo ukitaka kufanikiwa hata ikiwa business binafsi au NGO fulani ni lazima uwe na mpambe mmoja kwenye corridor za siasa ya bongo. Sasa, hapa HE na Serikali nadhani kuna mafahari 2 ambao wanashindwa kukaa meza moja. Sidhani kama tatizo ni ujumbe ambao HakiElimu wanatoa (hiyo ni sababu tu) bali kuna something deeper that what's on the surface.

Kwa maoni yangu...njia pekee ya kujua chimbuko la hii mizengwe ni kuangalia jinsi HakiElimu ilivyoanzishwa mpaka hapa ilipo sasa...nina uhakika tutakuta chanzo cha mizengwe. Pia, nina mashaka makubwa sana kwamba matatizo ya HakiElimu yanatokana na Suceess iliyopata. Mafanikio ya HakiElimu yanamtekenya mtu huko kwenye siasa za bongo...na nia ni kuifanya hakiElimu ibongoe ili mwana siasa fulani naye apate kipisi cha cake. Tukijua mchakato mzima uliopelekea HakiElimu kuanzishwa tutajua...nina uhakika 101% tatizo sio huo ujumbe wao...Just a tip Jenerali Ulimwengu yumo kwenye Bodi ya Wakurugenzi, pamoja na hawa ambao naweza kuwaita dream team....

Founder Members

Wilbert Kapinga, Member and Director, HakiElimu Board of Directors and Senior Partner, Mkono & Co.; former Dean of the Faculty of Law, University of Dar es Salaam.

Helen Kijo-Bisimba, Director, HakiElimu Board of Directors, human rights advocate and Executive Director, Legal and Human Rights Center (LHRC).

Demere Kitunga, Member, HakiElimu and writer, activist and Director,
E & D Publishers.

Elieshi Lema, Director, HakiElimu Board of Directors; author of children's books and fiction and Director, E & D Publishers.

Richard Mabala, Member, HakiElimu; Regional Advisor on HIV/AIDS, UNICEF; and writer, animator and activist on gender and youth.

Japhet Makongo, Member and Program Manager, Community Governance Program, HakiElimu: education and community development specialist.

Marjorie Mbilinyi, Member, HakiElimu; Professor of Education, Institute of Development Studies, University of Dar es Salaam; and Coordinator, Rural Food Security Program.

Elisabeth Missokia, Member, HakiElimu and Program Officer, Education, CARE International in Tanzania.

Martha Qorro, Member, HakiElimu and Head, Department of Foreign languages and Linguistics, University of Dar es Salaam.

Rakesh Rajani, Member, Founder and Executive Director, HakiElimu; child rights researcher, analyst, author and advocate.

Mary Rusimbi, Member and Chairperson of the HakiElimu Board of Directors, gender activist and Executive Director, Tanzania Gender Networking Program (TGNP).

Joseph Semboja, Member, HakiElimu; economist, policy analyst and Executive Director, Research on Poverty Alleviation (REPOA).

Suleman Sumra, Member and Senior Program Officer Research and Policy Analysis, HakiElimu; Associate Professor (retired), Faculty of Education, University of Dar es Salaam.

Illuminata Tukai, Member, HakiElimu; Project Officer, Education, UNICEF Tanzania and child rights advocate.

Jenerali Ulimwengu, Member, HakiElimu; independent thinker, journalist, publisher and Chairperson, Habari Corporation.

The problem is NOT the message that HakiElimu are bringing to the masses, I am so convinced it has something to do with they way it was founded/run...and may be amount of money they receive from the donors (somebody wants a piece of the cake...!!). Sooner or later we will know the truth, we just have to dig deeper past Gov childish excuses and allegations.

Well...that is why we are here...to uncover/separate the truth from the mizengwe.
 
daymn.. mbona hakuna hata Mbunge Mmoja? mashirika mengi na taasisi nyingi zina vingunge wa CCM...mbona Haki Elimu haina hata mmoja. Labda wamuombe mama Lowassa na Mama Kikwete kuwa memba, mambo yao yatawanyokea. Kisha nitajaribu kulichambua hili la Haki Elimu
 
Mwaka ule Serikali kwa agiza la waziri mkuu iliamua kuifuta NYF yaani Nationa Youth Forum alitumwa JK more than 2 times kuongea na wakurugenzi wake . JK aliwaita Dodoma na kusema , Wakubwa akiwemo Rais wakati huo BM analalamika kwamba kikundi hiki ni kikali ila hakina wazee wa kuwatunza . Mnaobwa kubadili na kuwa na wazee wachache toka Bungeni ama serikalini nk . Vinginenvyo mtafutwa.

HM alimjibu akasema Mh.JK hii ni NYF na mimi ni above 35 najiondoa wabakie vijana kwa mujibu wa Katiba . Lakini Lukuvi na Sumaye na JK wali hakikisha inafutwa kwa kuwa pia likuwa na machapisho makali .

NYF ilipigwa vita na Kitilya wa CCM , Nchimbi nk baada ya kuondoka wakidhani itakufa wakaanza kutumiwa na usalama wa Taifa nk. Leo hii sishangai HE kukaliwa kooni na mafedhuli hawa wanadhani Nchi walipewa wao wenyewe na si watanzania wote .
 
JK alisema "tutaendeleza mambo mazuri yote yaliyoanzishwa na Mkapa" . Msishangae hii ni moja ya ahadi imetimia.
 
NI LAZIMA KUISIFIA SERIKALI?
HakiElimu wanasema "Hapana"- Serikali inasema "Ndiyo"
Na. M. M. Mwanakijiji

Kwa wale ambao tulifikiri kuwa sakata la HakiElimu na Serikali ya Tanzania limekwisha tulikuwa tumeficha vichwa vyetu kwenye mchanga kama mbuni. Ukweli wa mambo ni kuwa serikali ya Rais Kikwete ikirithi toka serikali ya Rais Mkapa inaendeleza wembe ule ule wa kulazimisha watu au vikundi vya watu watoe maoni, mawazo, sifa, na hoja inayokubaliana nazo. Tuliona mwelekeo huu wa serikali kwenye mjadala kuhusu filamu ya "Darwin's Nightmare" na sasa tunayaona tena baada ya ofisi ya Waziri Mkuu kuwakumbusha watu wa HakiElimu kuwa agizo la wao kufungiwa kutangaza kwenye vombo vya habari na kujihusisha na masuala yoyote ya utafiti wa elimu katika shule zetu kama lilivyotolewa na aliyekuwa Waziri wa Elimu na Utamaduni wa wakati ule Bw. Joseph Mungai bado lipo na lina nguvu.

Kwa wale ambao hawajui hasa ni nini kinaendelea basi niwape historia fupi ya sakata hili. Shirika la Haki Elimu ambalo liliundwa kwa sheria ya Bunge limekuwa likijihusisha na shughuli mbalimbali za utafiti na uelimishaji jamii kuhusu masuala mbalimbali ya Elimu. Lilianza kazi zake vizuri hadi pale lilipoanza kurusha matangazo na vipeperushi ambavyo vilionekana vinakosoa mafanikio ya sera ya Elimu chini ya Rais Mkapa na kukejeli mafanikio hayo. Tarehe 29 August 2005 Waziri wa Elimu Bw. Mungai akizungumza kwenye mkutano wa mwaka wa Elimu kwenye Ukumbi wa AICC huko Arusha alitaka shirika hilo kusitisha matangazo na vipeperushi hivyo ama sivyo "litafutwa". Waziri Mungai akiizungumzia HakiElimu alinukuliwa akisema "Wizara yangu imegundua kuwa shirika hilo linaoongozwa na mtu ambaye hana taaluma ya elimu lakini anatumia mbinu ya uvumishaji wa taarifa potofu zenye lengo la kuombea fedha kwa wahisani ambazo anazitumia kuwakodisha wataalamu mamluki wamuandikie taarifa anazozitaka yeye kwa mtindo wa ’’He who pays the piper calls the tune"

Shirika hilo liliendelea na kazi zake kama kawaida. Ilikuwa ni mwanzoni mwa kwezi Septemba 2005 ilipojulikana kuwa serikali imepiga marufuku shirika hilo "kufanya nakuchapisha tafiti kuhusu shule za Tanzania". Barua ya kupigwa marufuku huko ilisainiwa na Afisa Elimu Mkuu katika Wizara hiyo Bw. Ricky Mpama. Baadaye mwezi wa Kumi Rais Mkapa alitetea uamuzi wa Wizara ya Elimu na kuapa kabisa kuwa kuwa HakiElimu "hairuhusiwi kukanyaga katika shule".

Hata hivyo mara baada ya uongozi mpya wa Rais Kikwete kuchukua madaraka, Waziri Mpya wa Elimu na Utamaduni mama Margaret Sitta aliapa kuwa Wizara ya Elimu chini ya uongozi wake haina mpango hata chembe wa kufungia asasi zisizo za kiserikali kwa vile tu hawakubaliani nazo.

Huo hata hivyo haukuwa mwisho wa hoja hiyo kwani tarehe 5/4/2006 swali juu ya kufungiwa HakiELimu lililetwa Bungeni na Mhe. Mgana Izumbe Msindai (Iramba Mashariki - CCM) ambaye alitaka kujua ni sababu zipi zilizosababisha HakiElimu kufungiwa na kama serikali ya awamu ya nne iko tayari kuifungulia taasisi hiyo badala ya kuacha mtu mmoja aifunge (akimaanisha Waziri Mungai). Akijibu maswali ya Mbunge huyo Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bw. Ludovick Mwananzila alidai kuwa shirika hilo lilitumia uhuru wa maoni "kuonesha hisia za kubeza, kudharau, na kudhihaki mafanikio ya Serikali yaliyopatikana kwa kushirikan na wananchi nchini Tanzania." Naibu Waziri huyo hata hivyo hakutaja ni mabezo gani, dharau gani au dhihaka zilizotolewa na shirika hilo.

Alipoulizwa ni kitu gani HakiElimu wafanye ili wafunguliwe (swali liliulizwa kama nyongeza na Mhe. Lazaro Nyalandu -Singida Kaskazini - CCM) Waziri huyo alijibu kuwa "HakiElimu, wakiri na waombe radhi ili waweze kupewa ruhusa ya kuendelea na shughuli zao. Wakiweza kutambua yale waliyoyafanya kwamba yalikuwa yanawakera Watanzania na kuandika barua kwa Waziri anayehusika wataruhusiwa na wataendelea na shughuli zao bila ya Matatizo" HakiElimu wamegoma kufanya hivyo.

Ni hivi karibuni HakiElimu walianza kurusha tena matangazo yao na kuchapisha na mojawapo ya matangazo hayo kwa mujibu wa asasi hiyo "Linaonesha adha anazozipata mwalimu wakati anaposafiri kwenda kuchukua mshahara unaocheleweshwa, kinyume na maagizo ya Rais ya mwaka 1998" na tangazo jingine likionesha "tofauti iliyopo kati ya hali ya maendeleo ya kichumi na hali halisi ya familia umaskini, ikionesha kuwa maenedeleo ya kiuchumi bado hayajaweza kuwafikia Watanzania wote". Watu wa HakiElimu wamesema kuwa waliandaa matangazo hayo "kama changamoto kwa Watanzania kutafuta majibu ya matatizo haya"

Ni baada ya matangazo haya ndipo serikali kupitia ofisi ya Waziri Mkuu hivi karibuni waliamua kuwakumbusha watu wa HakiElimu kuwa marufuku ile ya mwaka 2005 bado ipo. Hiyo ndiyo historia fupi ya sakala la HakiElimu na Serikali ya Tanzania.

Maoni yangu binafsi ni kuwa:

Kwanza, hakuna mahali popote katika Katiba yetu au sheria yetu panapomtaka mtu kuisifia serikali au kuikosoa serikali. Zaidi ya yote hakuna mahali panapomlazimisha mtu anapoikosoa serikali lazima pia aipe sifa. Kama mtu hataki kukupa sifa kwanini umlazimishe? Katiba yetu inapotambua haki ya raia kutoa maoni au mawazo haisemi hata chembe mawazo hayo yawe ya aina gani! Kitendo cha kulazimisha mtu au kikundi cha watu kutoa mawazo yanayoipendeza serikali na yenye kukubalika na serikali ni kitendo kinachopakana na utawala wa kiimla.

Pili, HakiElimu kama jumuiya ya Kitanzania hata kama inapokea misaada kutoka nje (kwani siyo kosa) ina haki ya kuchambua mambo na kuyatolea maoni bila kulazimishwa na serikali, chombo cha serikali, au maafisa wa serikali kutoa maoni ya aina fulani. Kama watu wa HakiElimu wanaonesha uozo au upungufu wa aina fulani na serikali inaona maneno hayo si ya kweli, au yana walakini, jukumu la serikali siyo kuifungia taasisi hiyo (isipokuwa kama inatuhumiwa Uhaini!) isipokuwa kusahihisha habari hizo. Kama HakiElimu wanatumia vyombo vya habari kusambaza "sumu" ya ujumbe wao, serikali wanao uwezo na nyezo za kutumia vyombo hivyo vya habari kusahihisha uongo huo. Hata hivyo itakuwa ni kuudanganya umma kujifanya kuwa serikali inahodhi habari sahihi kuhusu mambo yote yanayohusu elimu au utekelezaji wa sera ya elimu au mikakati mbalimbali ya elimu. Huu ni ukiritimba wa mawazo.

Tatu, serikali ya Tanzania haikuchaguliwa ili iwe baba na mama ya Watanzania! Kitendo cha Wizara ya Elimu na Ofisi ya Waziri Mkuu kutuamulia ni aina gani ya habari Watanzania wapate ni kitendo cha kizandiki, kibabe, na kisichojali haki za raia. Sisi siyo watoto wa Serikali ambao serikali lazima itulinde tusipotoshwe na "mamluki"! Watu wa Tanzania wana uwezo wa kuona na kuelewa uongo na ulaghai toka mbali, hatuhitaji "kiranja mkuu" wa kutuchambulia ni habari gani tunazisoma, au ni matangazo gani tunayaona. Serikali inaweza kusema ni habari gani haziweti kutangazwa katika hadhara gani, lakini kunyamazisha habari za uchunguzi wa kisayansi au utafiti ni utumiaji mbaya kabisa wa madaraka. Ukimya wa watu wetu haina maana ya udhaifu, na heshima yetu kwa viongozi isitafsiriwe kama ni woga! Hivi wanasiasa wanapotudanganya na kutupa maneno ya kilaghai kama ya sakata la Richmond mbona wao wenyewe hawajifungii ili tujue kweli wako makini kusimamia maoni na habari katika Tanzania?

Nne, kitendo cha HakiElimu ni kama kile cha yule mtoto aliyepiga kelele kwenye kadamnasi ya watu kuwa "Mfalme hajavaa nguo" na mtoto huyo kutoboa siri ile ambayo watu wengi waliiona lakini kwa kumuogopa mfalme hawakuthubutu kuisema. Tanzania siyo ufalme wa Kikwete na wala si himaya ya CCM! Na Ikulu yetu siyo kasri ya sultani! Uwezo na mamlaka ya viongozi wetu hutoka kwa watu na kwa watu pekee vitu hivyo vinabakia. Kitendo cha serikali kumlazimisha mtoto (HakiElimu) anyamaze asimuaibishe Mfalme kinaweza kumliwaza mfalme (rais) na wapambe wake (viongozi wengine), lakini hakiondoi ukweli kuwa mfalme hajavaa nguo (tuna tatizo katika sekta ya Elimu)! La maana ni kumsiriti mfalme siyo kunyamazisha sauti ya watoto!! Kama wakinyamazisha sauti hizo za watoto basi siku moja wasishangae "mawe(kina sisi) nayo yatapaza sauti zao"!

Tano, hatuna budi kujiuliza ni kwanini agizo hili la sasa limetolewa na ofisi ya Waziri Mkuu badala ya kutoka Wizara ya Elimu iliyotoa Agizo la awali la kufungia HakiElimu? Je inawezekana kuwa mama Sitta aliyeahidi kuwa Wizara yae haina mpango wa kufungia asasi za Serikali hajakubaliana na uamuzi huo na hivyo kuilazimisha Ofisi ya Waziri Mkuu kuingilia kati na kutoa kumbusho hilo? Kama hili ni kweli, basi Mama Sitta hana budi kuomba aondolewe wadhifa wake huo kwani viongozi wake wa juu hawako tayari kumuacha aongoze Wizara hiyo kwa manufaa ya Watanzania na kwa kiapo alichokula.

Sita, ni nani aliyesema kuwa raia wanalazimika kuisifia serikali hata kama haistahili sifa hizo? Waswahili wanakiita kitendo hicho ni "kuvikwa kilemba cha ukoka" na "kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa" Ni vipi watu waimwagie sifa serikali iliyoingia mikataba mibovu mibovu, inayolea uzembe na kutokuwajibika, yenye kuvumilia ufisadi na ubovu serikalini? Ni sifa gani watu waipe serikali ambayo imeshindwa kujibu hoja za HakiElimu na badala yake kutumia fimbo ya waziri kuinyamazisha? Kauli mbinu yangu ni "hoja hujibiwa kwa hoja" Kama serikali imeshindwa kushindana katika uwanja sawa wa fikra, ikubali yaishe! Hoja za serikali hazipati nguvu kwa vile wanauwezo wa kumfungia mtu au jumuiya! Aidha hoja zina nguvu zenyewe au hazina.

Saba, kwa upande wa HakiElimu, kitendo cha wao kuendelea kusubiri huruma ya serikali nacho kinakatisha tamaa, kinachochea matumizi mabaya ya madaraka, na kinalea viongozi wenye kutumia nguvu kujenga hoja. Kama wao HakiElimu wanaona kuwa haki yao ya Kikatiba ya kutoa maoni na kupata habari imeminywa na kunyimwa wamekaa kimya badala ya kwenda mahakamani kuilazimisha serikali kufuta agizo lake. Wakati umefika wa watu wa HakiElimu kuacha kuandika barua na kuomba idhini ya serikali, waende mahakamani ili serikali ilazimishwe kutetea hoja yake ya kwanini inawapiga marufuku wao HakiElimu.

Mwisho, ni nani aliyesema kuwa wananchi wa Tanzania ni lazima wacheze kila siku serikali ikipiga ngoma? Ni nani aliyesema kuwa kuipenda serikali ni lazima? Na ni nani aliyesema ni marufuku kuichukia serikali? Watu wakiipenda serikali wanaichagua kuwaongoza, wakiichukia wanaiondoa kwenye sanduku za kura. Wale wanaoipenda wana haki hiyo na wale wanaoichukia wana haki hiyo hiyo. Wale wananchi wanaoimwagia sifa serikali au viongozi wake wanafanya hivyo kwa haki kabisa, na wale wanaoikosoa na wanaokosoa viongozi wake wana haki hiyo hiyo pia. Tatizo linakuja pale baadhi ya viongozi wanapofikiri wao ni wana wa mfalme ambao wanaweza kutawala kwa maneno yao na kulazimisha watu kuwasifia! Hilo halina nafasi katikaTanzania na tunapinga kwa nguvu zetu zote hadi pumzi ya mwisho. Tanzania ni nchi huru, na itaendelea kuwa huru, hatumtumikii mfalme au wana wa mfalme, mapenzi yetu ni kwa jamhuri yetu na utii wetu wa kwanza ni kwa Katiba yetu. Aneyehoji uzalendo wa watu kwa vile mawazo yao hayaendani na yale ya serikali au kwa vile wanaikosoa serikali amefilisika kifikra na siasa haziwezi, bora aachie ngazi.

Katika utawala wa demokrasia (kama tunaojaribu kujenga) uhuru wa mawazo na maoni haonekani pale tunaporuhusu mawazo kama ya kwetu kutolewa, bali pale tunaporuhusu mawazo yanayopingana na mawazo yetu kutolewa na kuitetea haki ya wanaofanya hivyo kulindwa! Kitendo cha serikali kujifanya kuwa ndiyo pekee iliyo kisima cha habari sahihi ni uongo mwingine ambao hatuko tayari kuununua. Serikali ituachie tupate habari kokote tunakozipata, tuzilinganishe habari hizo, na tuzipime kama watu wenye akili, na tuzitolee maamuzi juu ya ukweli wake. Vinginevyo, serikali iamue kupitisha sheria mpya ya Habari Sahihi toka Serikalini Pekee ya Mwaka 2007 ili tujue kuwa hatimaye Tanzania tumeingia rasmi kwenye utawala wa kibabe wa serikali ya kiimla inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi. Kama sivyo, waifungulie HakiElimu bila ya masharti yoyote yale ili kazi ya ujenzi wa Taifa iendelee.
 
Wow!

Mwanakijiji naomba niiweke hii kauli/makala yako kwenye tovuti yangu. I like it mate. Ningeichukua bila hiari yako lakini nikubalie mkubwa. I promise, naandika kuwa mwandishi ni wewe!

Ruksa?
 
Back
Top Bottom