Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Hapa ndipo ninapo uliza ukweli na usafi wa JK . Je ahadi zake za mikataba kuwa bayana ndiyo hizi ama bado anamalizia Kampeni ?
 
Ujinga huu.

Yaani nchi yetu haina checks and balances. Serikali inaweza kujifanyia lolote bila kuogopa wananchi wanataka nini? Nilitegemea kuwa bunge letu lina Kamati inayoaangalia mambo ya serikali (Government Affairs). Kamati hii ilitakiwa iwe inapata taarifa zote za maamuzi ya serikali na kuangalia kama maamuzi hayo yana masilahi kwa wananchi. Inapoonekana kuwa hakuna masilahi ya wanachi basi wana haki ya kuleta maauzi hayo yajadiliwe bungeni, na hivyo bunge kuishauri serikali maamuzi mbadala.

Inaelekea kuwa serikali yetu ni ya miungu!!
 
Kwa hiyo nchi zinazopitisha baadhi ya mikataka bungeni huwa wanakosea. Mbona hata hiyo rada tuliyouziwa imepitishwa bungeni Uingereza kutolewa kwa kibali itakuwaje sisi. Ndio hawa wasomi wa Bongo maanake elimu zao zimekomea mwisho wa kurasa za kitabu...They can't think beyond that.
Dk. Juma Ngasongwa, hana exposure ya mambo yanavyokwenda duniani na kwao maana ya Uongozi ni Kutawala.
Huduma za bandari kutopewa UAE tulizisikia ktk vikao vya congress Marekani na mkataba kufutwa hawa wote hawafahamu utaratibu wa mikataba?
Hii ndiyo ukisikia serikali kuendesha nchi bila ridhaa ya wananchi.. Huu ni udikteta!... hamuwezi kutuvalisha nguo tusizopenda kuvaa.

Ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni. Kisichowezekana duniani kote kinawezekana Tanzania tu.
 
Huu ni uhuni, wabunge inabidi wasikubali kuburuzwa na Serikali. Haiwezekani mtu mmoja akasema ati mikataba haiwahusu wabunge, wanaficha kitu gani hapa? Wabunge ni lazima walivalie njuga hili swali mpaka kitu kieleweke.

Hivi kweli kwenye 21st century bado mtu anaweza kujibu namna hii kwenye Bunge? Mbona analifedhehesha bunge namna hii, wabunge wanalindwa kusema chochote bungeni na ndio wawakilishi wa wananchi sio viongozi wa kuteuliwa na rais. Sio huyu EL aliyewanyamazisha wabunge na sasa anaongelea swala hilohilo la Richmond na kuundiwa kamati, what is the difference na wabunge kuhoji mikataba? THIS GUY IS A FAILURE AND HE SHOULD BE REMOVED.
 
Kikwete afichua siri wakati akificha siri



na Mwandishi Wetu


MAZUNGUMZO aliyoyafanya Rais Jakaya Kikwete na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari katikati ya wiki hii, yamefungua ukurasa mpya wa mwenendo wa Serikali ya Awamu ya Nne iliyodumu madarakani kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.


Kikubwa kilichofungua ukurasa mpya katika mazungumzo hayo, ni kauli nzito alizozitoa rais wakati wa mazungumzo hayo, kwa namna ambayo katika hali ya kawaida zinaweza kuonekana zisizo na maana kubwa.


Miongoni mwa mambo mazito aliyofichua ni kauli aliyoitoa kwa mara ya kwanza sasa kwamba, miongoni mwa orodha za walarushwa alizotumiwa, ziko zilizochezewa kwa malengo ambayo yeye mwenyewe hakuyaweka bayana.


Akijibu swali la mwanahabari mmoja aliyetaka kujua iwapo alikuwa ameshawahi kupata orodha ya walarushwa hasa ikizingatiwa kuwa katikati ya mwaka jana alikaririwa akisema anawafahamu watu hao kwa majina, Kikwete alitoa kauli zilizoibua maswali mengi mengine.


Kwanza, rais hakufanya kabisa juhudi zozote za kutoa ufafanuzi wa matamshi hayo aliyoyatoa na badala yake akasema kwamba amekuwa akipokea majina ya walarushwa kupitia katika ujumbe wa maandishi (SMS) anaoupata kutoka katika simu yake ya mkononi.


Kauli hiyo ya rais imekuja miezi kadhaa baada ya Waziri Mkuu, Edward Lowassa kueleza kwamba, Kikwete alikuwa akipokea SMS nyingi ambazo naye alikuwa akizielekeza (akizi-forward) kwake kwa ajili ya kufanyiwa kazi.


Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa na gazeti hili unaonyesha kwamba, Rais Kikwete hajawahi hata mara moja kuweka bayana namba yake ya simu anayosema ndiyo anayotumia kupokea ujumbe wa maandishi.


Kikubwa katika hilo ni kwamba, viongozi kadhaa wa serikali waliowasiliana na gazeti hili ili waeleze iwapo walikuwa wakiijua nambari hiyo iliyo wazi ya rais, wote walionekana kutojua jambo hilo.


Aidha, waandishi wa habari kadhaa waandamizi ambao wamekuwa wakiandika habari zinazohusu serikali, nao kwa nyakati tofauti walishindwa kuwa na namba hiyo ya rais.


Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili kwa siku kadhaa sasa, unaonyesha kwamba, nambari ya zamani ya simu ya mkononi ya Rais Kikwete iliyokuwa kichwani mwa waandishi wengi wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, hivi sasa haipatikani kabisa inapopigwa.


Utata wa pili ulioibuka wakati wa mazungumzo ya Kikwete na wahariri, ulitokana na kauli yake ya kushindwa kuipinga moja kwa moja taarifa iliyotolewa na Taasisi ya Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKURU) hivi karibuni, ingawa kimantiki alionekana kutokubaliana nayo.


Wakati TAKURU katika taarifa yake waliyoisambaza magazetini walisema Kikwete alikuwa hajawahi kupokea orodha yoyote ya walarushwa, yeye mwenyewe alikuwa ana mtazamo tofauti na huo.


Kwanza, alikiri kupokea taarifa yenye orodha ndefu ya majina ya walarushwa iliyokuwa na mihuri ya Kijapani ambayo hata hivyo alipoanza kuihakiki akimshirikisha Jaji Joseph Warioba aliyedaiwa kuiandaa, ilionekana kuwa na hitilafu kadhaa.


Pamoja na kugundua hitilafu kadhaa, Kikwete bila ya kumtaja mtu kwa jina, alisema kwamba miongoni mwa watu waliokuwa wametajwa kuwamo katika orodha hiyo ya walarushwa ni watu wakubwa ndani ya vyombo vya habari.


Ingawa hakuwa tayari kuingia katika undani wa suala hilo, Kikwete alikuwa akirejea habari iliyoandikwa katika gazeti moja la kila siku mwaka jana kuhusu orodha hiyo ya walarushwa, ambayo kwa mara ya kwanza ilielezwa ilikabidhiwa mwaka 1999 kwa aliyekuwa rais wakati huo, Benjamin Mkapa.


Mbali ya orodha hiyo, Kikwete alikiri kupokea majina mengine ya walarushwa kupitia ujumbe wa maandishi katika simu ambayo hadi hivi sasa nambari yake imeendelea kubakia kitendawili majina ambayo alikuwa akiyatuma PCB.


Majibu hayo ya Kikwete kwa kiwango kikubwa yalithibitisha kuwa, taarifa ya PCB kukanusha kwa niaba yake kwamba, alikuwa hajawahi kupokea ‘orodha yoyote’ ya walarushwa, ilikuwa na walakini au ilitolewa kwa malengo ya kisiasa zaidi.


Utata wa tatu katika majibu ya rais, ulikuwa pale aliporejea kwa kujiamini kauli yake aliyowahi kuitoa huko nyuma kwamba, urais wake ulikuwa hauna ubia na mtu mwingine yeyote.


Alipoulizwa hiyo juzi iwapo kauli hiyo ilikuwa ama ikiwalenga wasaidizi wake kadhaa aliowaona wakinyemelea wadhifa huo, Kikwete aliweka chumvi zaidi kwenye kidonda, pale alipoifanyia marekebisho kidogo.


“Niliposema maneno hayo sikuwa na wasiwasi wowote. Kwanza niseme kwamba ni mimi tu na Makamu wa Rais wenye ridhaa ya wananchi. Wengine wote tumewakusanya ili watusaidie kazi,” alisema Kikwete ambaye alisisitiza alikuwa haoni tabu kuirejea tena kauli hiyo aliyoielezea kwa Kizungu kuwa ni ‘Statement of fact’ (kauli thabiti).


Wanasiasa kadhaa waliozungumza na Tanzania Daima, wakiwamo watu waliokuwa karibu na mchakato wa kumuunga mkono katika harakati zake za urais, wameielezea kauli hiyo kuwa iliyokuwa na lengo la kujenga uhasama miongoni mwa viongozi wa juu serikalini.


Tangu rais alipotoa kauli hiyo, watu mbalimbali wamekuwa wakiamini kuwa ilikuwa ikiwalenga wasaidizi wake wakuu na kundi la wanamtandao lililoongoza harakati zake za kuingia Ikulu.
 
HakiElimu wameitwa kukutana na PM dodoma. Natumai HakiElimu watatumia nafasi hiyo kumuelewesha mpendwa kiongozi wetu kuhusu kazi wazifanyazo na nini mipaka yake ili next time kusiwe na migongano.

I hope pia HakiElimu hawata tetemeka wala kuchemsha kwa kuitwa kwao huko na PM.

Wakumbuke tu, majadiliano yoyote mazito hufanyika Dodoma....toka enzi hizo za akina marehemu Kolimba nadhani ( sina hakika sana na hilo jina).
Kazi kwenu HakiElimu.

Soma habari kamili hapo chini


Lowassa awaita HakiElimu Dodoma

*Ni kuhusu matangazo yake
*Atakutana nao kesho

Na Mwandishi Wetu @ Mwananchi Communications Ltd


SUALA la serikali kufungia matangazao na machapisho ya shirika lisilokuwa la kiserikali la Hakielimu, limechukua sura mpya baada ya Waziri Mkuu, Edward Lowassa kuamuru viongozi wa shirika hilo kukutana naye Dodoma kesho.

Taarifa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, zinaeleza kuwa katika mkutano huo viongozi wa Hakielimu watajieleza mbele ya Lowassa kuhusu matangazo na machapisho hayo.

Hatua ya waziri mkuu kutaka kukutana na Hakielimu imekuja siku chache baada ya watu mbalimbali wakiwamo, wasomi, wanasheria na wadau mbalimbali kulaani hatua ya serikali kuifungia shirika hilo.

Januari 30 mwaka huu, Ofisi ya Waziri Mkuu ilipiga marufuku machapisho na matangazo yanayotolewa na HakiElimu kupitia vyombo vya habari na kutishia kulichukulia hatua kali za kisheria iwapo litakiuka amri hiyo.

Hata hivyo, hatua hiyo imeelezwa na shirika hilo kuwa ni ya ukandamizaji inayolinyima haki ya kikatiba ya uhuru wa kutoa maoni na kujieleza.

Hii ni mara ya pili kwa serikali kutoa tamko la kupiga marufuku HakiElimu kufanya au kuchapisha tafiti kuhusu shule, kuandaa na kurusha filamu au matangazo katika redio na televisheni na kusambaza machapisho mashuleni.

Onyo la awali lilikuwa limetolewa na aliyekuwa Waziri wa Elimu na Utamaduni, katika serikali ya awamu ya tatu, Joseph Mungai, Septemba 8, 2005.

Baadhi ya machapisho na matangazo yatolewayo na Hakielimu yanakosoa baadhi ya watendaji katika sekta ya elimu kujihusisha na rushwa hasa katika ununuzi wa vifaa vya elimu kwa njia za rushwa, ucheleweshaji wa mishahara ya waalimu na matumizi mabaya ya viboko kwa wanafunzi.

Matangazo hayo pia yanaelekea kukubalika na kueleweka vizuri kwa umma mkubwa wa wananchi kutokana na kuwatumia wasanii maarufu ambao pia huonkena katika maigizo mbalimbali ya tamthilia.

Kwa kiasi kikubwa matangazo ya Hakielimu yameonyesha mafanikio kwa serikali kuondoa baadhi ya kero ambazo zimetajwa katika matangazo hayo ambayo hufanyiwa tafiti za kitaalam kabla ya kurshwa katika vyombo mbalimbali vya habari.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa HakiElimu, Elieshi Lema alikaririwa akisema kwamba wameshangazwa na barua hiyo ya ofisi ya Waziri Mkuu kwa kuwa imekuja wakati wanafanya juhudi za kukutana ili kufanya maridhiano na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Helen Kijo Bisimba ambaye pia ni mjumbe muanzilishi wa HakiElimu hivi karibuni alikaririw akisema kwamba maonyo hayo yanapingana na mpango mzima wa serikali ya Awamu ya Nne unaosisitiza suala la uwajibikaji.
 
Juzi Jk amesema swala la kufungiwa HE amelisikia akiwa ziarani Ethiopia.

Kumbuka hapo kama sikosei EL ndo alikuwa "acting president" hivyo akachukua hatua mara moja kama kawaida yake kukurupuka.

Sasa JK amesema atalifuatilia kwa kina.....Ndio hivyo siajabu EL kaambiwa awaite Ddm, nadhani hapa wanazuga tuu....kitakachofanyika HE itaruhusiwa kuendelea na shughuli zake KAMA KAWAIDA...kwa kisingizio ati wameomba msamaha......kwani kuwaruhusu hivihivi EL ameogopa aibuuuuu....

YOU'LL TELL ME...just wait!
 
Watawala waoga lazima hupenda kusifiwa .Lakini kila lenye mwanzo huwa lina mwisho . Tunawasifu huku kashfa zinakuja nje .Hii ni kama ile ya mtu kutaka kuzuia mvua isinyeshe Tanzania ama Duniani . Yatatoka tu .Wacha tungoje Dodoma itakuwaje .
 
Serikali yatoa masharti mapya HakiElimu

chanzo:-Mwananchi

WAZIRI Mkuu, Edward Lowassa, amesema serikali itaondoa amri walizopewa taasisi isiyo ya kiserikali ya HakiElimu kuhusu matangazo na machapisho yao kwa makubaliano kuwa taasisi hiyo itazingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi.

Mwandishi wa Waziri Mkuu, Said Nguba, alimkariri Lowassa akiyasema hayo jana baada ya kikao alichokiitisha ofisini kwake mjini Dodoma, kufuatia maombi ya taasisi hiyo inayojishughulisha na masuala ya elimu ya kutaka kuonana naye.

Alisema kwamba licha ya kuzingatia sheria, kanuni na taratibu, taasisi hiyo katika matangazo na machapisho yao pia izingatie heshima na utu wa Watanzania katika kujiletea maendeleo hayo.

Mazungumzo hayo ambayo yalikuwa ya kindugu na kirafiki yalitawaliwa na dhana kwamba “nchi ni yetu sote na tusaidiane kupata maisha bora kwa kila Mtanzania”.

Kwa upande wao HakiElimu, hawakuwa tayari jana kuzungumza chochote kilichotokana na mkutano huo, wakisubiri kwanza serikali itoe taarifa yake kwanza, jambo linaloashiria kuwa huenda hakukuwa na maelewano, na mahusiano baina yao bado ni ya kuwindana mithiri ya paka na panya.

Taarifa ya Nguba kwa gazeti hili ilileza kuwa ilikubaliwa katika mkutano kuwa katika kufuata sheria, kanuni na taratibu, kwa mfano, ili kusambaza shuleni vitabu vya kuelimisha, makala mbalimbali au katika kufanya utafiti kuhusu elimu, HakiElimu inabidi kwanza kupata kibali cha Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Katika utoaji wa matangazo kwenye televisheni, redio na magazeti HakiElimu inabidi ihakikishe kuwa kunakuwepo na uwiano wa maudhui yaliyomo kwenye matangazo yenyewe.

Ilikubaliwa pia kuwepo na mawasiliano ya kutosha baina ya maofisa wa serikali na HakiElimu ili kufanikisha utekelezaji wa lengo la kuendeleza sekta ya elimu nchini.

Mkutano huo ulihudhuriwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Margaret Sitta; Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Muhammed Seif Khatib, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Joseph Mungai na Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana, Dk Emmanuel Nchimbi.

Kwa upande wa HakiElimu waliohudhuria ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Elieshi Lema, Mjumbe wa Bodi, Jenerali Ulimwengu na mwanachama wa taasisi hiyo Helen Kijo-Bisimba na Mkurungenzi Mtendaji, Rakesh Rajani.

Serikali ilitoa amri (Government Notice No. 373) ya tarehe 11 Novemba mwaka 2005 ikipiga marufuku HakiElimu kutoa, pamoja na mambo mengine, matangazo yote ambayo yalionekana yanakwenda kinyume na maslahi ya jamii.

Katika hatua nyingine, Irene Lipende anaripoti kuwa,
MTANDAO wa Elimu Tanzania (TEN/MET), umetoa tamko la kupinga hatua ya serikali kuzuia kutangazwa kwa machapisho na matangazo ya HakiElimu katika vyombo vya habari kwa madai kuwa yanaharibu taswira ya elimu nchini.

Tamko hilo lililotolewa kwa vyombo vya habari na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TenMet, Antoine Gizenga, jijini Dar es Salaam, jana liliitetea taasisi ya Hakielimu kuwa ina lengo la kuhumiza utawala bora na uwajibikaji katia sekta ya elimu.

Alisema kuzuiwa taasisi hiyo kufanyakazi zake, ni sawa na ukandamizwaji wa haki za uhuru wa kujieleza na usambazaji wa habari ambazo wananchi wamehakikishiwa katika katiba ya nchi na kutozingatiwa kwa kanuni za utawala wa kidemokrasia.

“Maisha ya umma, ushiriki wa umma na nguvu ya umma ndiyo msingi hasa wa utwala wa demokrasia. Zaidi ya hayo mojawapo ya majukumu ya asasi za kiraia yaliyokubaliwa katika MMEM ni kukusanya na kusambaza taarifa za elimu kutoka na kwenda mashukleni, katika jamii, serikali na wadau wengine” alisema Gizenga

Alisema katika nchi za kidemokrasia majukumu ya asasi za kiraia ni pamoja na kuchambua mapungufu yaliyomo katika sera za serikali na utekelezaji wake ili kurekebishana na kujenga nchi kwa pamoja.

Katika hatua nyingine asasi zisizo za kiserikali za TEN/MET na Policy Forum, zimelaani hatua ya serikali ya kulifungia shirika lisilo la kiserikali la HakiElimu kutoa matangazo na machapisho zikisema kuwa, inatishia uwepo wa asasi hizo nchini.

Mbali na hilo, asasi hizo zimesema hatua hiyo pia inalenga kukandamiza uhuru wa kujieleza na usambazaji wa habari, pia inaonyesha namna serikali isivyokuwa tayari kukubaliana na fikra kinzani, kutokuzingatia kanuni za utawala wa kidemokrasia na kupunguza fursa ya kushiriki kwa asasi za kiraia katika maendeleo ya sekta ya elimu na sekta nyingine nchini.

Hayo yamo katika taarifa ya pamoja iliyotolewa na asasi hizo kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TEN/MET, Antoine Gizenga na Mratibu wa Policy Forum, Getrude Mugizi, ilieleza kuwa wanachama wa asasi hizo wameguswa na kushangazwa na hatua iliyochukuliwa na serikali dhidi ya HakiElimu ambayo ni mwanachama wa asasi hizo.

"Kwa ufahamu wetu, kazi ya HakiElimu ambayo kwayo imesajiliwa, inalenga katika utawala na uwajibikaji, haki za binadamu, demokrasia na haki za kijamii...kuzuiliwa kwa HakiElimu ni sawa na kugandamizwa kwa uhuru wa kujieleza na usambazaji wa habari, ambao wananchi wamehakikishiwa katika katiba yetu," ilieleza taarifa hiyo.

Wakati asasi hizo zikieleza hayo, Chama cha Wananchi (CUF) nacho kimesema kimesikitishwa na hatua ya serikali ya kuizuia HakiElimu kuzungumzia mipango yoyote inayohusiana na Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) na Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES).

Taarifa ya CUF kwa vyombo habari iliyosainiwa na Kaimu Mkurugenzi wake wa Haki za Binadamu na Mahusiano na Umma, Mbaralah Maharagande, imeielezea hatua hiyo ya serikali dhidi ya HakiElimu kuwa ni ya uvunjaji wa katiba ya nchi inayotoa uhuru na haki kwa kila raia kutoa maoni na kupewa taarifa.

CUF, kimesema hatua hiyo pia inathibitisha ukweli kuhusu madai dhidi ya serikali ya kutaka kuvibana vyombo vya habari kupitia rasimu ya muswada wake wa habari na imelenga kukwepa utekelezajiwa nidhamu ya uwajibikaji pale inapokosolewa
 
Komaeni wana HE the tumwagieni nyeti huyo mtu wa Richmonduli ana matatizo gani
 
Serikali yatoa masharti mapya HakiElimu

chanzo:-Mwananchi

Alisema kwamba licha ya kuzingatia sheria, kanuni na taratibu, taasisi hiyo katika matangazo na machapisho yao pia izingatie heshima na utu wa Watanzania katika kujiletea maendeleo hayo.


Jamani hapa wana maana gani...mimi nadhani walitaka kusema wazingatie matakwa ya Serikali.

Taarifa ya Nguba kwa gazeti hili ilileza kuwa ilikubaliwa katika mkutano kuwa katika kufuata sheria, kanuni na taratibu, kwa mfano, ili kusambaza shuleni vitabu vya kuelimisha, makala mbalimbali au katika kufanya utafiti kuhusu elimu, HakiElimu inabidi kwanza kupata kibali cha Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.


Hii kama process ya kuomba kibali ni nzuri itahakikisha wanafunzi wetu hawapewi makala za kuwa-brain wash na utombo ...mf makala za kisiasa, dini, kikabila n.k Hofu yangu inakuja pale ambao kibali ndio kitachukuliwa kama nyenzo ya unyanyasaji...kusambaza mamba ambayo Serikali inataka kusambazwa na si vinginevyo.


Ilikubaliwa pia kuwepo na mawasiliano ya kutosha baina ya maofisa wa serikali na HakiElimu ili kufanikisha utekelezaji wa lengo la kuendeleza sekta ya elimu nchini.


Positive move...ila huko serikali kila kitu kinafanywa kwa urasimu sijui kama watawezana.
 
Serikali yatoa masharti mapya HakiElimu

chanzo:-Mwananchi
Katika utoaji wa matangazo kwenye televisheni, redio na magazeti HakiElimu inabidi ihakikishe kuwa kunakuwepo na uwiano wa maudhui yaliyomo kwenye matangazo yenyewe.


Msaada....Hii ina maana gani, sijui ni kushindwa kuelewa lugha au nina mambo mengi akilini...!!
 
Komaeni wana HE the tumwagieni nyeti huyo mtu wa Richmonduli ana matatizo gani


Tatizo lake ni dogo sana; analinganisha u-PM na U-morani; basi akishakula
lodwaa antimka kama hana akili na kufanya maamuzi ya nchi kama yuko nyumbani kwake vile.. na hivi ameshambuliwa na Richmonduli basi anatafuta scapegoat
He is such a waste...mpaka atoke kwenye u-morani si leo, ni aondolewe tu kinamna
 
Lifuatalo ndugu zangu ni tamko la Haki Elimu kufuatia mazungumzo yao na serikali. Kwa maoni yangu, Serikali ilishindwa kuhalilisha kitendo chake, na haki elimu wameibuka washindi!
 

Attachments

Mzee wa Kijijini asante sana kwa tamko hili . EL anajiona uchi mbele za watu na Tanzania . Hivi ana washauri huyu Mzee ama anakurupuka tu ? Tanzania ya leo si tanzania ya akina Sokoine na Mwalimu ati !
 
Juzi Jk amesema swala la kufungiwa HE amelisikia akiwa ziarani Ethiopia.

Kumbuka hapo kama sikosei EL ndo alikuwa "acting president" hivyo akachukua hatua mara moja kama kawaida yake kukurupuka.

Sasa JK amesema atalifuatilia kwa kina.....Ndio hivyo siajabu EL kaambiwa awaite Ddm, nadhani hapa wanazuga tuu....kitakachofanyika HE itaruhusiwa kuendelea na shughuli zake KAMA KAWAIDA...kwa kisingizio ati wameomba msamaha......kwani kuwaruhusu hivihivi EL ameogopa aibuuuuu....

YOU'LL TELL ME...just wait!
Kwani Muheshimiwa huyu EL si waziri mkuu???sasa anapo act president kwani makamu wa raisi hayupo???au katiba imebadilika huko bongo????
 
Back
Top Bottom