Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Dr. Moshi,
I agree with the gist of your posting. But it would be a dream to expect Kenyan factories to employ Tanzanians while the unemployment in Kenya is very high. I think the opposite is more true--more Kenyans in Tanzania job market.
 
Jasusi,

The labor market in Tanzania consists mostly of civil servants, shop assistants and farm hands. There was a time when we had factories, but that was then. We hardly have any factories now, and we have put in place an energy and water policy that will keep it that way for a long time to come.

I do not see the Civil Service Commission filling our government offices with Kenyans and I would not mind seeing lots of Kenyans cutting sisal, and generally working the land for us. That leaves only the shop assistants, but that is not really a concern, as we have fewer than ten supermarkets. The rest of the shops are small family outfits; jobs in these will continue to be assigned to family members.

The most significant sector of our civil service consists of teachers. Are you against employing teachers from Kenya? But we need more teachers than we can train! If Kenya has spare teachers who would be willing to work under our conditions then we should be very happy to have them. After all they do have a good command of the English language, and that would be very advantageous.

Augustine Moshi
 
Nashangaa kwa nini kiingereza kinakuwa ni jambo la ufahari na kijivunia wakati ni sawa na lugha nyingine yeyote. kweli ukitaka kuwa na biashara ya kimataifa lazima ufahamu lugha kwa ajili ya mawasiliano lakini tuna wenzetu wengi tu ambao wanaendelea kutumia lugha zao. Japan, China, korea, France,Spain, Italy n.k.

Hawa walimu unaoongelea ni wakufundisha kiingereza au kitu gani? Hebu tuanze kujivunia lugha yetu tuachane na hii kasumba ya kiingereza.

Kuwa na idadi kubwa kwenye jumuiya sio kwamba basi tutaendelea, Nigeria ndio wengi zaidi Afrika na wana mafuta mbona mpaka leo wako kwenye kundi letu?

Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi kama majirani zetu ni sawa lakini muungano sidhani hapa tunajifunza kitu chochote kile, nchi ambazo tungetaka kuungana nazo ni zile ambazo ni marafiki wa kweli i.e. SADC ambao kwa muda mrefu tumekuwa tunaelewana katika nyanja za kimataifa etc. kulikuwa na maana gani kweli kupigania uhuru ambao hivi sasa tunataka kuwagawia wale washiriki wa waliokuwa wanatutawala? nani hasa alikuja na wazo hili la muungano? Viongozi wetu ambao wako madarakani kama wameshindwa kuongoza waachie madaraka; hili la muungano haliingii hata akilini na kama ndio hivyo kwa nini basi tulalamike Kenya wanasema Kilimanjaro na Serengeti ni za kwao? Kwa nini tusifute jina Tanzania leo hii na tukubaliane tuite nchi yetu Kenya? NAANZA KUAMINI KIDOGOKIDOGO KWELI NI KICHWA CHA MWENDAWAZIMU.
 
I'm telling you alichokifanya Idd Amini Dada hakina tofauti na hichi cha hawa Wakenya! Mamaaaa....yaani hapa Msabaha ni chalii na uprofesa wake akipepewa na wabongo wake....! Chama Cha Mfukoni (CCM mpooo?) Kweli TZ ni mwanamke tena MAMAHURUMA hapa keshafixiwa!

Hapo bado EAC/EAF haijaanza rasmi, na ikianza rasmi watakuwa wameshafika Mtwara! Wote twasherehekea KEnyata na MOi DAY! M7 nawe amka babaupara!

__________________
"U Can't Change The Nature"



Wakenya waanzisha shule bubu Tanzania

Na Samson Chacha, Tarime

WALIMU zaidi ya 40 wanaodaiwa kuwa ni wahamiaji kutoka nchi jirani ya Kenya, wameanzisha shule bubu kwenye nyumba za kuishi watu, ambazo hutumia mitaala ya Kenya kufundishia watoto.

Waandishi wa habari waliotembelea baadhi ya shule hizo, katika mji mdogo wa Sirari, mpakani mwa Tanzania na Kenya Januari 25, mwaka huu waliwakuta walimu hao, wakiwafundisha watoto kwa kutumia mitaala ya Kenya.

Kaimu Mratibu Elimu Kata ya Sirari, Omari Masese na Afisa Mtendaji wa Sirari, Samwel Philipo, alithibitisha kwepo kwa shule hizo na kwamba zina wanafunzi zaidi ya 1,000 ambao hulipa Sh5000 kwa mwezi, kila mmoja.

Naye Afisa Uhamiaji wa Kituo cha Sirari, alikiri kupokea malalamiko juu ya walimu hao na kwamba wanawafuatilia.
 
Ni hatari, hatari ya kunyanyaswa nchini kwetu na wahamiaji. Mfumo wa utawala wetu una kasumba ya kuabudu mtu ambaye si mtanzania hasa linapokuja swala la ajira (ajira - kazi yoyote mtu ajishughulishayo nayo ili kukidhi mahitaji yake ya kila siku, awe ameajiriwa rasmi au kajiajiri mwenyewe). Kwao Mtanzania hata awe amesoma vipi yeye ni kalaghabaho ikiwa sio mwana CCM..., kwanza ndo anakuwa adui.

Watakuja hawa wakenya na michanganuo yao mizuri ya miradi na wafungue makammpuni ya kilimo halafu watapewa mikopo na taasisi zetu hizi hizi za fedha, na faida yoote watakimbiza kwao Kenya. Mtz huwezi kupewa mkopo wa aina hiyo.

Hivi hawa viongozi haweoni kuna kuburuzwa? Ni nini itakuwa hatma ya Zanzibar katika muungano huu?
 
Washawasha unalaumu tena ? Usilaumu bwana maan ni Serikali ambayo unasema imefanya mema mengi ndiyo inatuingiza huku kwa interest zao na si za Watanzania. Unalaumu nini yaani nawe umeanza kulaumu kama sisi na wakati kuna mada umefungua unasema tuachane na lawama. Ama ulikuwa unaongelea Serikali gani Mzee ? Umesema tuwape muda sasa mbona unalaumu badala ya kuacha tuwape muda watuingize huko waliko dhamiria kutupeleka kwa mabavu yao ?
Si ni serikali hii hii ama au mimi sijakuelewa ?
 
Dua,

Shukran mshikaji, hili swala nimewahi kulizungumza na ndugu yangu Augustine Moshi kule Bcstimes, kwa zaidi ya mwaka mzima...

Mimi binafsi sioni tatizo kabisa kufundishwa lugha ya kiingereza na sio kiingereza kuwa lugha ya kufundishia. Hapa ndipo napogomba na hawa jamaa. Kwa mfano nchi zote ulotaja hapo juu wanafundisha lugha ya kiingereza.. yaani kiingereza kama lugha lakini vipindi vyao vyote vinafubdishwa kwa lugha zao tena wao hadi Chuo kikuu. Na bado wanao wataalam wa lugha ya kiingereza na watumishi wanaozungumza kiingereza kulingana na sehemu zinazohitaji lugha hiyo.
Sisi leo tunataka kiingereza kifundishwe toka chini sio kwa sababu ya lugha ila kwa sababu ya kuelewa (knowledge). Lakini kinachochekesha ni kwamba tunapofikia matumizi ya knowledge hiyo inabidi mtu azungumze kiswahili kuwaelekeza watu maanake wanaohudumiwa hawafahamu kiingereza.
Hapa ngoma kubwa maanake kuna watu maprofesa wanashindwa kabisa kuwaelekeza watu kwa kiswahili. Ukienda benki matatizo, yet viongozi wanashindwa kuelewa kwa nini benki zetu zote zina account chini ya millioni 1 ktk nchi yenye watu zaidi ya millioni 10 wana mapato ya ajira, ukulima ama biashara.
Na kibaya kuliko yote ni kwamba ktk ulimwengu huu wa utandawazi tumeshindwa kwanza kuangalia nafasi yetu ktk soko hilo. maanake ukitazama hata wafanya biashara wetu. Kutokana na umaskini wetu wamelazimika kuzungumza lugha za wengine na sio kiingereza. Vijana wanaokwenda China wamelazimika kuzungumza Kichina, Thailand -Kithailand, Ujerumani -Kijerumani, Ufaransa - Kifaransa n.k. Ama nje ya hapo lazima uwe na contact na mtu anayezungumza kiingereza na huyo ndiye atakuwa mkarimani wako. Hapa nazungumzia hata hizo Conferences, trade shows n.k. Wote wanatumia lugha zao ktk biashara achana na wahudumu wa uwanja wa ndege ambao wanazungumza kiingereza kama lugha kusaidia wasafiri, hawa wahudumu hawana elimu ya biashara hizo.
Tumeshindwa kabisa kutofautisha kati ya elimu ya lugha (matumizi yake) na elimu dunia (knowledge).
Ndio maana utakuta hata benki zetu zinaajiri Mkenya anayezungumza kiingereza hali mtu huyu hana shahada ya Benki na kumwacha Mtanzania mwenye shahada toka chuo cha benki kwa sababu tu anayezungumza kiswahili kama lugha yake ya kwanza. Na kibaya zaidi ni kwamba wateja tunaowategemea benki wengi watapendelea kuelekezwa mifumo ya uwekaji fedha benki kwa kiswahili zaidi ya kiingereza. Tena acha kuwa wanapendelea kiswahili, wengi hutoka benki hawafahamu kile walichoelekezwa.. Mara kibao nimeona watu wakibeba jamaa mkarimani kuja fungua account ama kuwekesha fedha zake.

Kwa hiyo hadi leo sielewi kabisa hao wanaopigania kiingereza toka shule za msingi hali wao wanapomaliza vyuo vikuu wameshindwa kuwaongoza wananchi ktk uzalishaji kwa kiswahili, then nini maana ya elimu zao!..
Ni kweli kiswahili hakijitoshelezi na ndio maana kiswahili kinatumika darasani ktk msingi wa elimu yetu hadi pale inajitosheleza.

Na matokeo yake ndio siku zote yametupa watu kama Augustine na wachangiaji wote humu..sote tumesoma kupitia mfumo huo na kuna kila hali ya kujivunia maanake watu wanaweza kujieleza kwa lugha zote!.. mwambie Mkenya aandike hapa kwa kiswahili kama sio matusi matupu.

Mimi nasisitiza zaidi kuwepo na somo la kiingereza kila darasa na pengine vipindi viwili kwa siku toka shule ya msingi ikiwa kiingereza ni big deal. Leo hii kuna vijana kibao wananambia eti hawaelewi kiswahili na wengine hata kuchapia Kiswanglish!..bado tunaendelea kudai kiswahili hakiwezi kufa! Subiri Wakenya, waganda, Wanyarwanda waingi mtaanza kuzungumza kama wao. Hii imeisha kuwa proven kuwa mwenyeji mara nyingi huigiza mgeni kuliko mgeni kujifunza matamshi fasaha ya lugha, Wataanza kupitisha Mkora sii muda kama ni kiswahili safi.
 
Washawasha unalaumu tena ? Usilaumu bwana maan ni Serikali ambayo unasema imefanya mema mengi ndiyo inatuingiza huku kwa interest zao na si za Watanzania. Unalaumu nini yaani nawe umeanza kulaumu kama sisi na wakati kuna mada umefungua unasema tuachane na lawama. Ama ulikuwa unaongelea Serikali gani Mzee ? Umesema tuwape muda sasa mbona unalaumu badala ya kuacha tuwape muda watuingize huko waliko dhamiria kutupeleka kwa mabavu yao ?
Si ni serikali hii hii ama au mimi sijakuelewa ?
Mzee mimi lawama ambazo sizitaki ni kwamba mtu hajanywa chai bac anailaumu serikali,sasa wakuletee mkate ama?ila kama nilivyosema Roma haikujengwa kwa siku moja ,hivyo basi kuna vitu vingine wanaudhi sio siri,hasa ambavyo wanaweza kuvifanya ila ni kiburi chao na umelo wa madaraka,ni hayo tu kaka
 
Dr.Moshi,
Mbali na serikali, mwajiri mwingine nchini Tanzania ni sekta ya huduma.Hapa pia nasikia wawekezaji wanapendelea zaidi kuajiri Wakenya kuliko Watanzania kwa kisingizio cha Kiingereza. Yaani hata mfagiaji wa hoteli na yule anayebadilisha mashuka lazima ajue Kiingereza? Hapa Marekani hivi sasa kazi hizi zinafanywa na ndugu zetu kutoka kusini: Latin America. Na hawa hawajui Kiingereza lakini wameweza kuajiriwa.
 
Jasusi,

The labor market in Tanzania consists mostly of civil servants, shop assistants and farm hands. There was a time when we had factories, but that was then. We hardly have any factories now, and we have put in place an energy and water policy that will keep it that way for a long time to come.

I do not see the Civil Service Commission filling our government offices with Kenyans and I would not mind seeing lots of Kenyans cutting sisal, and generally working the land for us. That leaves only the shop assistants, but that is not really a concern, as we have fewer than ten supermarkets. The rest of the shops are small family outfits; jobs in these will continue to be assigned to family members.

The most significant sector of our civil service consists of teachers. Are you against employing teachers from Kenya? But we need more teachers than we can train! If Kenya has spare teachers who would be willing to work under our conditions then we should be very happy to have them. After all they do have a good command of the English language, and that would be very advantageous.
Augustine Moshi

Mwl Moshi,
Hivi kweli Kenya wamejitosheleza kwa walimu mpaka sisi tuchukue ziada? Walimu karibu duniani kote sasa hivi ni bidhaa adimu kwelikweli iweje Wakenya wao wawe na ziada ya kutupa sisi? Lililo wazi ni kuwa tunaowaona si walimu hata kidogo, hawakusomea Ualimu, hawana ethics za ualimu na hawana utaalamu wowote zaidi ya Kiingerza tena nacho siyo perfect kama tunavyoaminishwa. Kwa kifupi ni kuwa hawa ni watu wasioweza kupata ajira nchini mwao kwa sababu hawana sifa ndio maana wanakimbilia kwetu.
 
Tabasamu
Nikiwa majuu miaka kama 4 nyuma niliwahi kuitwa kenye mkutano mmoja hapo The Hague na NGO moja kubwa ambayo ilimwamini sana Mkapa na akawapa muda na mambo mengi TZ. Mara ya mwisho kabla hajamaliza muda wake walimwita Uholanzi kwenda kusema na wanafunzi wa ISS kile chuo .

Nasema niliyo yaona kule si kawaida . Waliletwa wanafunzi wa degree ya kwanza wakiwa kati ya miaka 20 na 24 kuja kufundisha Capacity Building . Niliwaka sana kwenye mkutano na nikasema haya ni matusi . Wakiwa Tanzania watakutana na Bob Mkandara na Jasusi . Wazee hawa wana miaka mingi kazini wake na watoto wanao wa manage . Hiyo ndiyo Capacity building iinako anzia . Hawa watoto Ulaya wanakaa kwa Baba na Mama wanaomba pesa na ku share ka room na mwenzake na hata kuosha vyombo hawawezi wanagombana leo anakujja TZ kama Expert . Nikasema no .

Nilizua kasheshe wakashangaa . Tabia hii ni mbaya sana na sisi tuna angalia . Hawa wazungu wengi ni vilaza ndiyo wanao kuja Tanzania hawana kazi kwao na hawawezi kupata .All they do ni kwamba wanaanza vi project baadaye wanaomba pesa serikalini kwao kwa jina la umasikini wa Africa na sisi kutokuwa makini wanakuja kutanua .

Wanakuwa na wamasai kibao nje na kuwadhalilisha wakati kwao Ulaya wanaishi maisha ya kijinga . Tuamke tuseme hapana . Wababaishaji hao .Ila wana idea ya job creation na wanakuwa supported na serikali yao basi tunawapigia magoti . Nasema it is time to say NO.
 
Lunyungu wale wanaitwa SNV ndiyo walio mkandia Mwalimu kwamba alikuwa na sera wakiwa wamekaa TZ miaka 30 wanaiba mali zetu .
 
I decided to put this artical here although it has more to do with EAC federation and business but those who remember very well when Tanzanians used to travel to Kenya for cheaper goods and now its viceversa.

The Nation (Nairobi)
January 27, 2007
Posted to the web January 26, 2007
Nation Team
Nairobi

When sickness strikes and death stares in the face of Kenyans living in Taveta, they have an easy solution: They take their sick to Mawenzi Hospital in Moshi, Tanzania, or Dr Minja's clinic in the same town.
And on bright days, freelance photographer James Kyalo Mutua waits for customers at the border town and secures enough business, before hopping into a bus to Arusha where the cost of processing pictures is cheap and services fast. Then he returns to Kenya to deliver his orders.
Mr Mutua says he also prefers seeking services in Arusha rather than Voi due to the poor state of the Taveta-Voi road.

Similar considerations drive small-scale traders to Tanzania where grain prices are lower and milling even cheaper. But they usually return to Taveta which offers a robust market where they retail their wares in 2-kg tins popularly known as goro goro.

Fish in abundance

The trend is not confined to Taveta. It is replicated in other border towns across Kenya, from Busia, where soap and confectioneries from neighbouring Uganda are cheaper than in Kenya, to Isebania, the town on the Kenya-Tanzania border that provides fish in abundance.
But Tanzanians seem to esteem Kenyan education as many students cross the border seeking schools and colleges. On their part, Kenyan students are registering in big numbers in Ugandan institutions where many attend Form Five and Six - courses that were long-scrapped in Kenya. Others join private universities in Kampala.
These social and economic activities defy the territorial boundaries that separate Kenya, Uganda and Tanzania.

But it is on the business front that small-scale traders are displaying versatility and resilience to take advantage of opportunities wherever they are to be found. Not even national borders can hold them back.
Services are cheaper
"Milling services are cheaper in Tanzania and most traders cross the border to mill their grains and return to Taveta to sell the flour," said Mr Kephas Rayasi, a Taveta businessman.
And for those who want to wind down with a cold beer, Holili trading centre in Tanzania is the place to go as it is only 20 minutes away by boda boda (bicycle taxi). There, one can also sample the popular Tanzanian gin, Konyagi.
"Most of the services and goods we enjoy here come from the other side of the border in Tanzania," said Mr Rayasi, as he dusted seats in his barber shop, ready to serve his next customer.
Mr Rayasi's Pare community occupies both sides of the Kenya-Tanzania border. His siblings live on the other side of the border, where he occasionally visits them.
"Life is a bit difficult here," he says, alluding to what may have prompted his siblings to migrate to Tanzania.

Like Taveta, the Kenya-Tanzania border towns of Isebania and Sirare are melting pots of cultures, where money-changers prowl the streets day and night, hoping to make a deal.
There is unrestricted movement of people on both sides of the border, and area residents fear this could have contributed to crime in the area. Gangsters routinely prey on motorists in Migori and Homa Bay districts, and disappear to Tanzania. They usually target saloon cars which are then dismantled and sold as spare parts, according to a top CID officer in Nairobi.
According to him, several cars have disappeared in Migori without a trace.
"We suspect there is collusion between criminals in Kenya and Tanzania. It is very difficult to recover stolen vehicles once they are driven across the border," said Mr Joseph Nyapete, whose saloon car was stolen recently in Migori Town.

Traders determined to evade paying tax also resort to smuggling using panya (illegal) routes, which are used to traffic contraband from one country to another.
Although it is reported that most of the bhang consumed in Kenyan schools and colleges is brought in from Tanzania where it is grown on a large scale, Tanzanian authorities are yet to crack down on the drug barons who operate from Mara Province.

"The drug trade will end when Kenyans stop providing a ready market for it," a Tanzanian official in Tarime told the Saturday Nation.
Incidents of cross border cattle rustling have also been reported between members of the Kuria communities on either side of the border, giving rise to vigilante groups known as sungu sungu.
Cross-border prostitution has also been on the rise in the area.
Some operate as barmaids by day and prostitutes by night, a situation that has led to a rise in Aids cases in Migori and Kuria districts.
But there is a unique trend in Busia and Teso districts on the Kenya-Uganda border. Here, family ties run deep. Some have relatives across the border, although one would expect all blood relatives to share a nationality.

Ugandan politics

One example is the Awori family. Kenya's Vice-President Moody Awori has a brother, Mr Aggrey Awori, who is also in the thick of Ugandan politics. The Ugandan Awori has been a leading opposition politician for many years.
Some people living near the border have sold their properties in their country of birth to start a new life in a neighbouring country. Mr Joash Wesonga is one of them.
The 50-year-old Kenyan from Nambale Division now lives in Iganga village in Uganda only a few kilometres from the Kenya-Uganda border town of Busia.
Mr Wesonga said he does not regret selling his unproductive land in Kenya to migrate with his family to Uganda in 2001.

"My family and I are enjoying our stay in Uganda and I do not intend to return to Kenya. I am engaged in commercial farming and it is paying off," he said. He is even trying to get his other relatives to join him there.
His mother, Mrs Truphena Bunyasi, 71, said that even though she was opposed to her son moving to another country, she was glad that he had put his land to proper use. But she was concerned about the fighting in Gulu, northern Uganda. However, she is now convinced that her son is safe since the area is no longer rocked by insurgency.
A number of people have also been engaged in cross-border marriages that have spawned a generation of "children of two worlds".

Ms Zainabu Lutta is a Kenyan married to a Ugandan for the last 14 years. She carries on with her business in Kenya but returns to her home in Uganda every evening.
"When I got a partner in Uganda I moved there but later I came back into the country to do business," she said.
And Mr Victor Lupia, 33, from Funyula division in Busia District has half brothers in Uganda.
They, too, meet annually in either country to catch up on what has happened over the year.

Sharing experiences

There is not just sharing of experiences, but also in the distribution of grains when there is crop failure in one country but their relatives have bountiful harvests in the other.
Neither is it unlikely to have Kenyan students seeking education in Uganda accommodated by their relatives there and vice versa.
"Those who seek Ugandan education and have relatives in Uganda do not incur huge living expenses," said Ms Winnie Natabona, whose relatives attended school in Uganda.
But it is not always smooth sailing.
"If one is found in Uganda without proper travel documents you are arrested for tax evasion," said Lupia.
Ugandans pay a tax commonly known as musolo, failing which one is arrested.
Lupia said that such arrests instil fear among the relatives who may wish to spend more time together.
"When one wants to share his harvest with relatives in another country during famine but is arrested in the process, this hinders sharing and local barter trade," he said.

Trade in timber

On the other side of the Kenya-Tanzania border, trade in timber also thrives. Most of the timber used for construction in Taveta is imported from Tanzania.
But for Mama Musimi, a Tanzanian second-hand clothes dealer, it's just business that keeps her in Taveta. Her family lives in Moshi and she occasionally travels there to meet them.

For Salim, who is newly arrived in Taveta from Rombo in Tanzania, the dusty town is still mysterious.
"I am currently trying to raise the capital for my business by selling bananas and other foodstuff," he said.

A boda boda operator who only identified himself as Tommy said he crosses the border up to Holili in Tanzania, about two kilometres from Taveta.
On this stretch, one need not produce a passport as it is considered as no-man's land.
Tommy is among the few boda boda operators who have embraced motorcycle taxis. "It cost me TSh900,000 (Sh50,000) to acquire this boda boda motorcycle but I am confident that it's rendering invaluable services to commuters," he said.
But he was unhappy with the border police whom he said often harass taxi operators.
"Most of the time, we are required to strictly adhere to traffic regulations for the two-wheel taxis such as wearing helmets and keeping current insurance documents," he said. Those who do not comply are arrested and taken to Rombo police station in Tanzania.
When and if the East African Community embraces political unity, these border communities are likely to celebrate and welcome the legalisation of the life that they have lived as though there were no borders.
- Reports by Pascal Mwandambo, Elisha Otieno and Ouma Wanzala
 
Ilani ya Uchaguzi 2005 -2010 ya Chama cha Mapinduzi. said:
Chama Cha Mapinduzi kinatambua kwamba ardhi wanayomiliki wananchi ni mtaji wao wa msingi wa kutegemewa katika kuwapatia ajira, kuwaondolea umaskini na kuwaletea ustawi wa jamii pale walipo."



Barua ya Wakazi wa Kurasini kwa Mheshimiwa Jakaya Kikwete, Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania​

(Aione Mheshimiwa Jakaya Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania)


Mheshimiwa,

Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania uliahidi (wakati wa awamu ya tatu) kuwa wananchi wote tuliojenga kwenye maeneo yasiyopimwa hasa mijini tutapimiwa maeneo ya nyumba zetu na kupewa hatimiliki ili kutuwezesha kuweka dhamana ya nyumba zetu tunapotaka mikopo kwenye benki zinazokopesha.

Sisi wananchi wa Kurasini Shimo la Udongo tunakukumbusha ahadi hiyo, na kukuomba SITISHA tafadhali uamuzi wa sisi kuondoshwa kwenye makaazi yetu mpaka pale utakapotoa uamuzi wa mwisho.

Mheshimiwa Rais, mwaka huu (2006), Machi 28 Bungeni Dodoma, Mheshimiwa Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Rita Miaki (MB), alikariri ahadi ya kuyatambua maeneo yaliyojengwa bila kupimwa na kuwapa wananchi wanaomiliki leseni za makazi (Residential License).

“Kazi ya kuwatambua wakazi waliojenga kwenye maeneo yasiyopimwa imefanyika katika Jiji la Dar es Salaam ambapo jumla ya miliki 210,000 zilitambuliwa na leseni za makazi 20,000 zimetolewa kwa wamiliki wa maeneo hayo," alisema Mheshimiwa Waziri Miaki alipokuwa akijibu swali la Mheshimiwa Masolwa Cosmas Masolwa, Mbunge wa Bububu (CCM).

Mheshimiwa Rais, hi kwa nini makazi yasiyopimwa Kurasini yasijumuishwe kwenye mpangiho huo? Sisi watu wa Kurasini tumelikosea nini taifa letu mpaka tulazimishwe kuyaacha makazi yetu, tofauti na ahadi uliyotupa Mheshimiwa Rais? Kwa mujibu wa Mheshimiwa Waziri Mlaki, ni baadhi tu ya nyumba zitakazoondolewa ili kupisha ujenzi wa MIUNDOMBINU kwenye makazi kama yetu kama vile barabara na mifumo ya majitaka au wale waliojenga kwenye maeneo hatari kama vile mabondeni. Hivi Mheshimiwa Rais unayo habari ya mambo haya?

Sababu tunayoambiwa ni "kupisha upanuzi wa bandari". Mheshimiwa Rais, sisi wananchi wa Kurasini haturidhiki na sababu hiyo, kwa vile watakokuja kuchukua maeneo yetu Si Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), kwa matumizi ya Bandari, bali ni "wawekezaji" ambao wanataka kuwa na "matumizi yanayoelekeana na bandari" hapa Kurasini.

Hili Mheshimiwa Rais lina tofauti ipi na ubaguzi wa rangi ("ethnic cleansing") -- kwamba sisi wazawa hatustahili kuwepo Kurasini? Je, makazi yabinadamu siyo matumizi yanayoelekeana na bandari?

Huku kwenye makazi yetu wanajenga gati namba ngapi? Hata TPA yenyewe ingekuwa ndiyo inahitaji maeneo ya huku Kurasini, bado Si sawa kutumia utaratibu wa kutunyang'anya ardhi uliyorasimisha tutumie, wakati ambapo sera iliyoko ni ya ardhi kuwa na thamani, na kwamba sekta binafsi (ambayo TPA ni mojawapo, au itakuwa hivi karibuni) inatakiwa kutumia nguvu ya soko kujipatia ardhi.

Serikali yako Mheshimiwa Rais ilijitoa kufanya biashara muda sasa. Ni kwa nini tena serikali itutoe kwa nguvu kwenye ardhi, halafu yenyewe ifanye biashara ya kuuza viwanja vyetu kwa 'wawekezaji'? Ikiwa serikali inaona hatuitumii ardhi ipasavyo, ni kwa nini isituagize tutumie kwa matumizi inayoona vyema?

Ulisema Mheshimiwa Rais kwamba uwekezaji siyo lazima uwe ugenisishaji. Hata ilani ya uchaguzi iliyotufanya tukupigie kura inasema "Chama Cha Mapinduzi kinatambua kwamba ardhi wanayomiliki wananchi ni mtaji wao wa msingi wa kutegemewa katika kuwapatia ajira, kuwaondolea umaskini na kuwaletea ustawi wa jamii pale walipo.

" Ilani hivo inaahidi "Kuanza utekelezaji wa Mkakati wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara Tanzania (MKURABITA) kwa lengo la kuwawezesha Watanzania kurasimisha ardhi na nyumba zao ili waweze kuzitumia kupata mikopo ya mabenki na miluko mingine ya fedha inayokopesha" ndani ya miaka mitano 2005 - 2010.

Sisi tulipo hapa Kurasini kwa nini tuondolewe, licha ya ahadi zako zote hizo? Kwa mujibu wa sheria za Ardhi, Mheshimiwa Rais unaweza kunyang'anya umiliki wa ardhi "kwa maslahi ya taifa". Je, kutoa umiliki kwa mtu mmoja binafsi, na kuuleta kwa mtu mwingine au taasisi nyingine binafsi, ni maslahi ya taifa?

Je ulituambia tufanye wanachotaka kukifanya hao watu wengine kwenye ardhi hii tukashindwa? Nini nafasi ya MKURABITA, MKUKUTA na mikakati mingineyo ikiwa Si kutuwezesha sisi wananchi kumiliki uchumi na makazi ya nchi yetu?

Au mikakati hiyo ni ya kwenye makaratasi tu? Kwa maelezo ya Mheshimiwa Waziri Mlaki, "Kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999 kifungu Na. 23 Halmashauri nchini zinayo mamlaka ya kutambua wananchi waliojenga nyumba kwenye maeneo yasiyo hatari na kutoa leseni za makazi." Sisi tunaoishi Kurasini hatupo kwenye maeneo ya hatari.

Tunakuomba Mheshimiwa Rais uturasimishie makazi yetu kama ambavyo ulituahidi kwenye ilani ya uchaguzi na kwenye nyaraka za serikali iii tuweze kuendelea kujenga taifa letu.

Kana kwamba uchungu wa kunyang'anywa ardhi yetu Si kitu, Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, inatutaka kubomoa nyumba zetu ndani ya siku 14 baada ya kupewa fidia zenye utata kwa hundi ambazo huiva ndani ya siku saba ambapo ni sawa na kwamba tumepewa siku saba za kuondoka katika eneo hilo.

Hata utawala wa Makaburu wa Mrika Kusini katika kilele cha ubaguzi wa rangi haukufanya hivyo! Ikiwa wamachinga walipewa miezi sita kuondoka katika maeneo yasiyoruhusiwa, vipi wakazi ambao tumeishi kwa miaka hadi 40 tupewe siku 14 kuondoka wakati tuna familia? Utawezaje kujenga nyumba ya kuishi kwa siku 14?

Maafisa wa Wizara ya Ardhi walituahidi kuwa wangetupa viwanja katika eneo la Kibada kujenga nyumba mpya, fedha za usafiri, fedha za miaka mitatu kwa ajili ya kutuwezesha kupanga nyumba, pamoja na kulipwa fidia kulingana na thamani ya nyumba ya mwaka huu, lakini hadi sasa hakuna lolote lililokwisha kutekelezwa.

'Fidia' yenyewe ambayo Wizara imelipa inakiuka misingi ya sheria za Ardhi Tanzania, Taaluma ya Tathmini ya Ardhi na haki za binadamu. Nyumba 46 za Kurasini Highway zimethaminiwa, lakini hazikufidiwa ipasavyo: Hamna "valuation reports" malipo yanayotolewa hayaonyeshi unalipwa kwa ajili ya nyumba ipi; hamna uwazi kwenye tathmini wala ripoti; hata viwanja vilivyopimwa vinanyang anywa bila kufuata taratibu; na hamna mchanganuo wa mazingira (EIA) uliofanywa kabla ya mradi huu wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi kutekelezwa.
 
Kwa Barua hii, sisi wakaazi wa Kurasini tunakuomba Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano mambo yafuatayo:

1.Rasimisha makaazi yasiyopimwa ya Kurasini kwa sisi wakaazi wa Kurasini kama ulivyotuahidi. Tuko tayari kurudisha pesa zozote za 'fidia' tulizolipwa.

2.Ikiwa wataalam wako watakuambia ni lazima ardhi ya Kurasini itumike kwa 'matumizi ya upanuzi wa bandari' au Kiswahili kinachofanana na hicho, na kisha wewe, Mheshimiwa Rais, ukakubaliana nao, basi tunakuomba Uturuhusu sisi wakaazi wa Kurasini kutumia MKUKUTA na MKURABITA kubadili makazi yetu kuwa uwekezaji "unaofanana na bandari" kama ambavyo wanakuambia wataalam wako.

'Ubinafsishaji siyo ugenisishaji': ndiyo mantiki ya sera ya uwezeshaji kama ulivyosema

Mheshimiwa Rais.
Uiamuru Wizara ya ardhi ilipe fidia ya nyumba kwa nyumba, siyo pesa -wizara ikajenge nyumba kwenye maeneo yaliyopimwa, na yenye miundombinu muhimu kama iliyoko Kurasini, kisha ituhamishie huko. Pesa za fidia Si zinatosha kujenga makazi mapya?

Suala la ujenzi wa nyumba ni la kitaaluma - tukipewa pesa tutajenga tena kwenye maeneo yasiyopimwa yenye miundombinu angalau, na kisha Wizara itakuja tena kutuondoa akitokea mtu mwenye pesa anayetaka kumiliki ardhi yetu.

Ikiwa kabisa hata wewe waridhia kwamba hatustahili kuitumia ardhi ya Kurasini, na kwamba tuondoke mbio kana kwamba tumezingirwa vitani, basi twakuomba zoezi la tathmini lirudiwe kwa kuzingatia taaluma ya Tathmini na Miliki, Sheria za Ardhi na Misingi ya Haki za Binadamu.

Tunaomba ukumbuke kuwa sisi pia ni binadamu kama watu wengine, binadamu kama wale walioko Wizarani au hao wanaotaka 'kuwekeza'.

Wasalaam, Ni sisi

WAKAAZI WA KURASINI (SHIMO LA UDONGO)

MABORESHO: Wakati tunaenda mitamboni, Wizara ya Ardhi imeweka wazi kwamba hamna upanuzi wowote wa bandari, ila wizara inafanya mradi wa kupata faida ya pesa kutokana na kutunyang’anya Ardhi ya makazi yetu. Badala ya kusimamia sera, sheria, kanuni na taratibu za ardhi, wizara imekuwa mfanyabiashara wa ardhi na huduma zinazoambatana na masuala ya ardhi, kama vile upimaji, tathmini, na nyinginezo.


//Viambatanisho
1. Kumbukumbu za Bunge (‘Hansard’)
2. Tangazo la Wizara ya Ardhi la Kufanya Biashara ya Kuuza Makazi yetu
3.Nakala


Part Questions » Principal Question(s)

Honourable Masoiwa Cosmas Masolwa [ CCM ] Bububu Constituency

To the Ministry of LAND AND HUMAN SETTLEMENTS Human Settlement/Land 28 Mar 2006

Kwa kuwa Mheshimiwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu aliahidi kuwa wananchi wote waliojenga kwenye maeneo yasiyopimwa hasa mijini watapimiwa maeneo ya nyumba zao na kupewa hatimiliki ili kuwawezesha kuweka dhamana ya nyumba zao wanapotaka mikopo kwenye benki

zinazokopesha: -

(a)je, zoezi hito limefikia wapi na nini kinachoendelea sasa?

(b) 3e, Serikali itachukua hatua gani kwa wananchi ambao hawatakuwa na hatimiliki za nyumba zao kwenye maeneo husika?

(c) je, kama mtu anataka kuifanyia ukarabati nyumba yake kwenye maeneo hayo au kujenga nyuma npya katika eneo lake akiwa tayari anayo hati miliki, atatakiwa kufuata hatua zipi kabla ya kuanza kazi hiyo?

ANSWERS TO PRINCIPAL QUESTION # 9 SESSION # 3 Answer From Hon. Rita Louise Mtaki LAND AND HUMAN SETTLEMENTS NAIBU WAZIRI alijibu:*Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Masotwa Cosmas Masotwa, Mbunge wa Bububu, lenye sehemu (a), (b) na

(c) kama ifuatavyo: -

(a) Mheshimiwa Spika, Serikali iliahidi kuyatambua maeneo yaliyojengwa bila kupimwa na kuwapa wananchi wanaomitiki leseni za makazi (Residential License). kazi ya kuwatambua wakazi waliojenga kwenye maeneo yasiyopimwa imefanyika katika uji la Dar es Salaam ambapo jumla ya miliki 210,000 zilitambuliwa na leseni za makazi 20,000 zimetotewa kwa wamitiki wa maeneo hayo. Pia kazi kama hiyo imefanyika ujini Mwanza, Manispaa ya Dodoma na itaendelea mijini katika mikoa mingine nchini kutingana na upatikanaji wa fedha.

(b) Mheshimiwa Spika, Serikali itatoa hatimiliki kwa wananchi wanaostahili kwenye maeneo yasiyopimwa mijini baada ya kukamilika kazi ya kuyatambua maeneo hayo na urasimishaji (regularization). Hata hivyo, mpango wa kutoa hati za kumiliki ardhi haukuwa kwa watu wote watiojenga kwenye maeneo yasiyopimwa kama ilivyoetezwa na Mheshimiwa Mbunge. Baadhi ya nyumba zitaondolewa ili kupisha ujenzi wa Miundombinu kama barabara na mifumo ya majitaka na wananchi wakaoondolewa watapatiwa viwanja kwenye maeneo mengine. Pia wananchi waliojenga kwenye maeneo hatari kama vile mabondeni hawatanufaika na mpango huu.

(c) Mheshimiwa Spika, mabadiliko yoyote yaliyokusudiwa kufanywa kwenye nyumba yenye hatimiliki na iliyotolewa kibali cha ujenzi, ni lazima yafuate taratibu zitizowekwa na Halmashauri za Miji na Wilaya.

Nakala

1. TIVEA - Chama cha watalaam watharnini Tanzania

2. Waziri wa Ardhi.

3. Mhe. John Magufu1i

4. Tume haki za Binadamu

5. UN-HABITAT

6. UN-HABITAT(HQ)

7. WORLD BANK

8. Wor1d-Bank (Washington) - HQ

9.. Vyombo vya Habari:

REUTERS
BBC
Deutche welle (DW) - Ujerumani
AFP

Vyombo vya habari Tanzania

~ BCS Times - Majira/Dar Leo

~ IPP Media -~Nipashe/Alasiri

~ Free media - Tanzania Dairna

~ Mwananchi Comm. - Mwananchi

~ Habari Corporation – Mtanzania\
~ HabariTanzania.com

- Vyombo vingine vya habari

Mkuu wa Mkoa.

Mkuu Wa Wilaya

Mheshimiwa Diwani

Mtendaji kata ya kurasini
 
hiii mbona kali

hizo CC si mchezo na inaonekana kuwa mumefanya kazi yenu ya kutosha sasa sijui response itakuwa vipi toka serikalini
 
JK aliulizwa swali kule NY juu ya zile Familia za Tarime ambazo nyumba zao na mashamba yao imegunduliwa kuwa na madini mengi maeneo yale. Akaulizwa na mtoto wa Mzee ambaye anahamishwa pale lwa maguvu kwamba Serikali inasemaje juu ya kuwaondoa kwa maguvu watu wale ambao wamekaa pale miaka yote hadi sasa ? Je kuna fidia nk . JK alijibu kama vile hakuelewa maana na thamani ya maisha ya watu wa Tarime na familia zao akasema . Kama kuna madini basi bora waondoke ba madini yachimbwe bila ya kusema watahamnishiwa wapi na loyalty italipwa nk .

Watu wa kurani mlismika mabendera ya CCM na kuwapiga mawe wapinzani kwa jina kasi mpya nk .Leo mnalia nini ? Kila muosha maiti huoshwa . Mlitoa kejeli kwa Wapinzani na hata kuwapiga sasa mnaoshwa kwa kuondolewa wawekezaji wakae. Kazi kwenu.
 
Mkandara ,

Siwezi kukubalina na wewe zaidi , ni kweli tumeshindwa kutofautisha matumizi ya lugha . Ni jambo la kushangaza kuona ya kuwa kiingereza kinakuwa ni kigezo kikubwa katika kumpatia mtu kazi katika maofisi mbali mbali hapo Tanzania wakati huo huo 90 % ya wateja wao wanazungumza kiswahili . Mimi najiuliza who are they catering to ?

Pili kuhusu hili suala la federation ni jambo zuri kama wananchi wa pande zote wataelimishwa na wataruhusiwa kwa utashi wao kufanya maamuzi , kazi kubwa ya serikali ni kuwaelimisha na kuacha demokrasia ifanye kazi yake na sio kujaribu kuwalazimisha watu wakubaliane na mawazo ya wachache. Ni lazima tutambue maamuzi tunayotaka kufanya yataathiri vizazi vingi vijavyo kwa hiyo ni lazima tuwe waangalifu.

Kitendo cha marais kukutana na kuamua ya kuwa Rwanda na Burundi kujiunga na jumuia bila idhini ya bunge speaks for itself "dharau". Jamani ni lazima tuwe waangalifu sio tujump tuu katika bandwagon bila ya kuwa na sababu za msingi . Ukiangalia kwa undani utaona Tanzania mpaka sasa hatujui tunataka nini , tunataka kuwepo kwenye SADC na wakati huo huo tupo kwenye EAC ..two incompatible systems .

Na hili suala la kusema watanzania wanaogopa ni cheap shot . Watu wowote makini na wanaojali maslahi ya nchi yao ni lazima wahoji kwa undani maamuzi nyeti kama hayo. Mbona hakuna mtu aliyesema wafaransa na wadachi waoga walipoipiga chini katiba ya ulaya? Cha msingi ni kujiliza ni kwa nini watanzania wanakuwa waoga katika kujiunga na jumuia ?
 
Hili la EAC kweli lilihitaji muda... hadi sasa hivi mimi binafsi sielewi kinachoendelea kabisa!
Chini ya marehemu Mchonga ningeweza kusema twende, itajulikana mbele kwa mbele maanake mwalimu alikuwa na vision ya kipekee kabisa.
Lakini leo hii sina hata la kusema zaidi ya kutazama muungano wa nchi ambazo karibu zote zina matatizo ya ndani. hata hiyo jumuiya ya Ulaya ilizitaka nchi zinazotaka kujumuika ziweze kurekebisha kwanza siasa zao za ndani. nchi kama Norway, Switzerland zilishtuka kutokana na baadhi ya policy ambazo wao hazingeweza kuwasaidia.

Tuna safari ndefu sana!....
 
Serikali yainyamazisha tena HakiElimu

Na Leon Bahati

OFISI ya Waziri Mkuu imepiga marufuku machapisho na matangazo yanayotolewa na Shirika lisilo la Kiserikali la HakiElimu kupitia vyombo vya habari na kutishia kulichukulia hatua kali za kisheria iwapo litakiuka amri hiyo.

Hatua hiyo imeelezwa na shirika hilo kuwa ni ya ukandamizaji inayolinyima haki ya kikatiba ya uhuru wa maoni na kujieleza.

Onyo la kutishia kuichukulia hatua kali za kisheria HakiElimu pamoja na Mkurugenzi wake Mtendaji, Rakesh Rajani, limo katika barua iliyoandikwa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Vincent Mrisho, Desemba 5 mwaka jana.

"Tumekuandikia kukukumbusha kwa mara nyingine tena kwamba machapisho na matangazo yako ambayo yamekuwa yakitolewa kwenye redio, televisheni na vyombo vingine vya habari yalipigwa marufuku na serikali kwa kuwa kinyume na maslahi ya jamii," inaeleza sehemu ya barua hiyo ikionya kuwa hatua kali zitachukuliwa kwa ukiukwaji wa amri hiyo.

Hii ni mara ya pili kwa serikali kutoa tamko la kupiga marufuku HakiElimu kufanya au kuchapisha tafiti kuhusu shule, kuandaa na kurusha filamu au matangazo katika redio na televisheni na kusambaza machapisho mashuleni.

Onyo la awali lilikuwa limetolewa na aliyekuwa Waziri wa Elimu na Utamaduni, katika serikali ya awamu ya tatu, Joseph Mungai, Septemba 8, 2005.

Akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa HakiElimu, Elieshi Lema, alisema kwamba wameshangazwa na barua hiyo ya ofisi ya Waziri Mkuu kwa kuwa imekuja wakati wanafanya juhudi za kukutana ana kwa ana, ili kufanya maridhiano na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Alisema kwamba HakiElimu imefanya mawasiliano ya barua pamoja na mawasiliano ya simu kwa zaidi ya mara 100 na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi tangu 2005 kuomba kufanya mazungumzo ya kumaliza tofauti zao, hivyo barua ya Ofisi ya Waziri Mkuu imekuwa kama msumari wa moto kwenye kidonda.

"Hatua hizi ni sawa na ukandamizaji. Zinaididimiza na kuinyima HakiElimu haki yake ya kikatiba ya uhuru wa maoni na kujieleza," alisema Lema na kufafanua:

"Siku zote tunaamini kuwa mjadala huru ukiongozwa na sheria na misingi ya demokrasia, utasaidia serikali na HakiElimu kufikia ufumbuzi na maelewano."

Alisema kuwa HakiElimu haijakata tamaa na wakati wote ipo tayari kukaa meza moja na serikali kwa kuwa lengo lao ni kutoa mchango wake wa kuisaidia serikali kuiboresha elimu nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Helen Kijo Bisimba ambaye piya ni mjumbe muanzilishi wa HakiElimu alisema kwamba maonyo hayo yanapingana na mpango mzima wa serikali ya Awamu ya Nne ya unaosisitiza suala la uwajibikaji.

"Kuna mkanganyiko kwa sababu wakati Rais (Jakaya) Kikwete alisisitiza hataki mtu ampake mafuta kwa mgongo wa chupa na badala yake akitaka akosolewe wakati wengine tunazibwa pumzi, hii inatoa ujumbe gani?" alihoji Bisimba.

Mjumbe mwingine, Mary Lusimbi, alisema kuwa kinachoonekana sasa ni kwamba serikali inaingilia uhuru wa mashirika yasiyo ya kiserikali.

Jenerali Ulimwengu ambaye pia ni mjumbe mwanzilishi wa HakiElimu, alisema kwamba mtiririko wa matukio ya kulifungia shirika hilo yanaweza kumfanya mtu kutafsiri kuwa serikali inaongozwa kwa mtindo wa kifashisti na kidikteta.

Ulimwengu alisema elimu ni suala nyeti katika nchi na kwamba wananchi wakipatiwa elimu bora ni jambo la muhimu katika maendeleo ya nchi, jambo ambalo HakiElimu inalipigania.

Alisema suala la kuboresha elimu hapa nchini limekuwa likizingatia zaidi ujenzi wa madarasa na madawati, lakini ukweli ni kwamba "maana ya shule ni kile kinachotendeka kati ya mwalimu na mwanafunzi."

Tangu kuibuka kwa mgogoro huo kati ya HakiElimu na serikali wadau na wananchi mbalimbali walionekana kuipinga serikali kwa uamuzi wake na kuiunga mkono taasisi hiyo, wakisema inachofanya ni kuonyesha ukweli katika masuala mbalimbali hasa yanayoihusu elimu.

Hivi karibuni, HakiElimu ilisitiza matangazo yake mawili yaliyokuwa yanapigania kucheleweshwa kwa mishahara ya walimu baada ya serikai kutangaza kuwalipa kila tarehe 23 kila mwezi.

(Mwananchi)

Baada jana hata hivyo, shirika la Haki Elimu lilitoa majibu yake kwa serikali angalia nimeambatanisha majibu yao na jinsi wanavyolichukulia suala hili. Tutajaribu kuwapata kesho ili tuhojiane nao. Hili suala la Elimu ni suala nyeti na uhuru wa watu kupata habari na kutoa habari ni muhimu katika utawala wa Demokrasia.

Vifuatavyo ni baadhi ya vikaragosi vinavyochapishwa na HE ambavyo kama agizo la serikali likisimama basi ujumbe wake hautawafikia wananchi wengi.
poster5.jpg

poster2.jpg

poster6.jpg


Ili kuweza kuelewa majukumu ya Haki Elimu tembelea tovuti yao hapa: http://www.hakielimu.org
 

Attachments

Back
Top Bottom