Huyu dada nimfanye nini wadau?

Huyu dada nimfanye nini wadau?

Raha ya JF ukizingua raia hawakukawizi unapewa za uso fasta.
 
Tenda wema uende zako.Asa akifukuzwa utafaidika kitu gani
 
Kama kweli ww ni msomi uliye soma haupaswi kuwa na tabia mbovu kama iyo. Kikubwa fanya Kazi uliyoomba yy atabaki na aibu yake uyo secretary
 
Ukiona secretary ananyodo ujue Boss anapumzika pale.... Sasa uchague moja kumvunjia kaka yako mahusiano au kufanya kazi iliyo kupeleka hapo...
 
piga kofi tuu laap! ili uondoe stress akikuuliza why you slap me muulize km anakumbuka nyodo zake.
 
Fanya kilicho kupeleka hapo mkuu japo kwa ni mgongo wa bro!!!
 
Hiyo ni kawaida kwa baadhi wadada, wewe achana nae. Iyo ni moja kati ya dalili za kukuwa kaka. Uyo mpuuze tu, asikuletee kiza mwachie aharibike wewe tunza heshima yako ila ikiwa tabia yake haikuridhishi usimruhusu awe karibu na kazi zako. Usimfukuzishe
 
Wakuu habarini humu,

Kama wiki mbili zimepita kuna ofisi moja maarufu sana hapa Mji wa Mawe aka Roku city,kuna Brother wangu ambae hapo ni Meneja sasa nikafika kwa ajili ya Interview ila Secretary hakunipokea vizuri na hata aliponiuliza kama nafuatilia kazi sikumjibu ukweli nikamwambia ni mambo binafsi.

Sasa nashukuru nimepata hyo nafasi na bahati nzuri namimi nimepewa cheo,ambapo huy dada anakuwa chini yangu

Hiv najiuliza sijui nimfukuzishe kazi maana alinipokea kwa nyodo sana.

Mwaonaje wakuu?

Haukustahili hata kupata hiyo kazi jinsi ulivyo mpvmbavu! Umepewa kazi ukamfukuzishe yeye kazi??
 
Wakuu habarini humu,

Kama wiki mbili zimepita kuna ofisi moja maarufu sana hapa Mji wa Mawe aka Roku city,kuna Brother wangu ambae hapo ni Meneja sasa nikafika kwa ajili ya Interview ila Secretary hakunipokea vizuri na hata aliponiuliza kama nafuatilia kazi sikumjibu ukweli nikamwambia ni mambo binafsi.

Sasa nashukuru nimepata hyo nafasi na bahati nzuri namimi nimepewa cheo,ambapo huy dada anakuwa chini yangu

Hiv najiuliza sijui nimfukuzishe kazi maana alinipokea kwa nyodo sana.

Mwaonaje wakuu?

No wonder tunaitwa malofa, kazi yenyewe umepewa kwa undugu ndugu unajifanya kampuni ya baba yako badala ya kumpa somo la customer care ulete mabadiliko ndani ya kampuni, unaanza umbea hata kazi hujaanza, siku ya kuripo vaa sidiria kabisa wajue chaumbea kaja
 
Kwanza hata wewe hukumjibu vizuri alipokuuliza shida yako. Badala yake ukajibu shida binafsi.. Ulitaka akufanyeje? Kukuuliza tu alikuwa na utayari wa kukusaidia ila wewe ukasema shida binafsi. Hujasema kama alikutusi..ila aliamua kukupotezea baada ya wewe kuwa na shida binafsi wakati pale ofisini. Maana shida binafsi haziji ofisini..zinaishia nje ya ofisi. Jitafakari maana na wewe unaonekana ulienda na mbwembwe baada ya kuahidiwa favor ya kazi.
 
Wote mlikutana mna nyodo mwanaume mitabia hiyo haipendeze acha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom