Huu uvaaji mwingine ni biashara mchana kweupe

Huu uvaaji mwingine ni biashara mchana kweupe

Mwanaume kuvaa mlegezo ni janga la taifa. Ni sawa na maradhi, umaskini, ujinga, rushwa etc

Mlegezo unakuja kwa
kasi sana huku Kiongozi wa kuuzui bado hajazaliwa ,sasa jiulize mpaka
siku kiuongozi wa kuthubutu akizaliwa Mlegezo utakuwa umefika
wapi?
 
Wananchi mda wote ni watu wa kuongozwa na kukumbushwa maadili ya mtanzania Je? Ni lini Mara ya mwisho umemsikia Waziri akiwakumbusha wananchi juu ya hayo? Swali anawaogopa? au yupo busy na katiba mpya au yupo busy akiwaza bajet na uchaguzi mwakani?

hahahaha unachekesha majukumu yote aliyonayo waziri akae anawakumbusha jinsi ya kuvaa watu wenye meno 32
 
Watanzania huwa ni wepesi ku-copy Utamaduni wa hovyo hovyo kuliko ku-kopy uchapa kazi ,sasa vijana wa siku hz wamepagawa na Milegezo kiasi kwamba hata utembeaji umebadilika,wavaa milegezo na Vinguo vya Ajabu ajabu sasa ni full Majanga ! Wabunge,mawaziri na Viongozi wote Wamegoma kuthubutu kulikemea hili,ipo siku tutashuhudia Milegezo sehemu tusizotarajia, chezea mlegezo wewe.......

Watakemeaje wakati na wao ni walewale tu?
 
sio uongo mkuu mie yameshanikuta ndio maana nimesema hivyo...
Acha uongo, mwanamke anaevaa kwa kujisitiri haitwi mshamba, anaitwa wife material. Jina zuri na lenye mvuto kabisa.

Huyo mwanamke anayejifanya mjanja kuanika viungo vyake hadharani ndio mshamba, kwa sababu hajui thamani ya mwili wake. Na huyo anaitwa kicheche.
 
lakini huko huko USA kuna majimbo yamepiga marufuku uvaaji wa hovyo

Nitajie jimbo moja tu ambalo limepiga maarufu "uvaaji wa hovyo". Nitajie jimbo moja tu.

hata Shirika la Ndege la America wameweka mabango kwenye ndege zao kupiga marufuku uvaaji wa hovyo kwa wasafiri wanatumia ndege zao,

Naomba source ya hili dai lako, tafadhali.
 
wewe mwenyewe mwanamke unaweka picha ya hivyo ya mwanamke mwenzio kweli!

Mkuu ng'wana ong'wa kulwa, samahani sana tena narudia tena samahani. Mimi ni Katibu wa #TeamWekaPicha ila sihusiki na picha iliyowekwa hapo nilipocomment.

Tafadhali sana rudi kwenye hiyo comment ustudy ufahamu ni nani aliyeweka hiyo picha, kisha urudi kunitaka radhi kwa kunikosea!

Asante
 
Last edited by a moderator:
Free economy!
Free country!

Tuna mengi sana ya msingi ya kutokomeza ambayo yangeweza kuleta/kuongeza GDP na GNP...!

Kama ni kuvaa tu, waacheni wavae! si wamenunua? sasa wewe unasema hawajalipa kodi unamaanisha nini mwandishi?

Kumbe uchumi huujui vizuri eenh? hizo nguo zimelipiwa kodi bwana mdogo, siku nyingine uchekeche kichwa kabla hujazungumza mambo ya kodi..!

Yani, hata wakitaka kutembea bila nguo, we waache tu!

- assume huoni..

-ukiona, fuata rule number one!
 
Tukivaa hijab masimango, tukionyesha tunayoyafichaga pia shida...
Wanaume hamridhiki....

kwasababu kunakila aina ya wanaume hivyo kila kundi linaeleza linachopenda
 
Akiliyako fupi kama maisha ya inzi, yaani ww unafikiri nchi ina duara moja tu la uchumi!!, hujui kuwa kuna mambo ya kijamii, mambo ya kisiasa, kisheria etc!! loh!!
Pili sikumanisha biashara ya nguo hailipiwi kodi, nilimaanisha watembea robo tatu uchi wanauza miili yao bila kulipa kodi. Wapigwe marufuku.

Free economy!
Free country!

Tuna mengi sana ya msingi ya kutokomeza ambayo yangeweza kuleta/kuongeza
GDP na GNP...!

Kama ni kuvaa tu, waacheni wavae! si wamenunua? sasa wewe unasema
hawajalipa kodi unamaanisha nini mwandishi?

Kumbe uchumi huujui vizuri eenh? hizo nguo zimelipiwa kodi bwana mdogo,
siku nyingine uchekeche kichwa kabla hujazungumza mambo ya kodi..!

Yani, hata wakitaka kutembea bila nguo, we waache tu!

- assume huoni..

-ukiona, fuata rule number one!
 
Walio wengi hasa vijaNA
Sio kosa lao,HAWAJAFUNDISHWA
Ndio Maana nimeanzisha taasisi ya Adili Tanzania ili kutoa elimu hiyo ,
Tovuti haijawa tayari kwa sasa tembelea ukurasa wangu wa facebook Adili Tanzania
hivi mtu anahitaji kufundishwa kusitiri mwili wake?
 
Bila shaka biashara yako ni ya kuuza hivyo vinguo ambavyo havina hadhi ya kuitwa nguo. Maana haviusitiri mwili bali vinaudhalilisha mwili.

Free economy!
Free country!

Tuna mengi sana ya msingi ya kutokomeza ambayo yangeweza kuleta/kuongeza
GDP na GNP...!

Kama ni kuvaa tu, waacheni wavae! si wamenunua? sasa wewe unasema
hawajalipa kodi unamaanisha nini mwandishi?

Kumbe uchumi huujui vizuri eenh? hizo nguo zimelipiwa kodi bwana mdogo,
siku nyingine uchekeche kichwa kabla hujazungumza mambo ya kodi..!

Yani, hata wakitaka kutembea bila nguo, we waache tu!

- assume huoni..

-ukiona, fuata rule number one!
 
Wauze tuu,demand and supply forces inaapply kila sehemu. Wewe sio mlaji achana nao.
 
Katika historia ya dunia,kila jambo lenye kuvunja/kubomoa jamii basi linaonekana ni maendeleo na litatetewa na watu wengi.Kuna siku watakuwa wakibadili pedi vituo vya mabasi.
Mmmmhhhhhh......huko mbali kaka km mbingu na ardhi
 
Akiliyako fupi kama maisha ya inzi, yaani ww unafikiri nchi ina duara moja tu la uchumi!!, hujui kuwa kuna mambo ya kijamii, mambo ya kisiasa, kisheria etc!! loh!!
Pili sikumanisha biashara ya nguo hailipiwi kodi, nilimaanisha watembea robo tatu uchi wanauza miili yao bila kulipa kodi. Wapigwe marufuku.

Nakwambia hii inaitwa mkuki kwa nguruwe
 
Apa mpige tu makelele!
Ole wenu rai ya uvaaji iingizwe kwenye katiba mpya!

Pambaf sana! Hamjui kama sie twasafisha macho pale?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom