Huu ni Ukweli wa Dr Slaa??

Yah lakini kinachonifurahisha zaidi na Dr Slaa ni kushindwa uzalendo na huo upadri...je mnajua wakati alipokuwa Padri aliamua kumweka mwanamke kinyumba?

safi sana...ukisikia mtu rijali ndio huko

Nani alokwambia kuwa padri ni uzalendo?Kwa sie wakatoliki,upadre unahitaji wito.Kipi kingekufurahisha kati ya haya mawili:Slaa kuendelea na upadre ilhali dhamira yake inamsuta kuhusu "wito" wake au kuamua kuwa mkweli katika dhamira yake kwa kuachana na daraja la upadre na kuishi maisha ya kawaida?
 
Hiyo ya mapadri kuwa na wanawake haiwezi kuwa issue hata kidogo. Kwa sababu kuna mapadri wengi tu wanawatoto na wengine wanavimwana kama mchezo. Hiyo hata Vatican ipo, kwa hiyo kama mtu anataka kuleta hoja hiyo atashindwa tu. Mapadri wa namna hiyo naweza kusema ni ma realist kwa sababu they are responding to the call of nature created by God.
 
I don't think his PhD or MSc matters at this point, we have alot of PhD holders from Ivy legue in the Bunge today, but are they worth even sumni? Not at all, they are butch of yes sir, no sir CCM slaves. They worry about their Land crusers and big houses across Masaki and mikocheni, they can't even ask why for anything. So, when people like Dr Slaa jump in and challange JK non sense government decisions, sorry people like this one challange his credentials. What the point of having LLB at Harvard while you cant think straight? Does it make sense to graduate at Colombia while you cant even ask why someone sign contract at the hotel?
Ni kweli kabisa, tuna viongozi wengi serikalini wenye Harvard degrees lakini wamegeuka kuwa Hazard kwenye maamuzi yao mbalimbali.
 
Mimi nampenda DR SLAA kwa sababu jamaa ni mtu honest
Alikuwa anatembea na mke wa mtu wakati ni padre na uzalendo ulipomshinda na huo upadre kawarudishia hao wakatoliki then yeye kaamua kuendelea kula NYAMA ...safi sanaa yaani i can relate naye zaidi kuliko JK na wanafiki wenzie akina LOWASA
 
suala ni kwa nini viongozi wa dini, wafanyabiashara, matapeli, majambazi,wauaji,watangazaji,waandishi wa habari, na watu wenye fani nyingine tofauti woooote wakimbilie kwenye siasa ? kuna nini huko tuambiane na mie nikimbilie huko !
 
suala ni kwa nini viongozi wa dini, wafanyabiashara, matapeli, majambazi,wauaji,watangazaji,waandishi wa habari, na watu wenye fani nyingine tofauti woooote wakimbilie kwenye siasa ? kuna nini huko tuambiane na mie nikimbilie huko !

Mmmmmhhhh.. jibu simple tu,
Kwasababu wao ndo wahusika wakuu wa kugawa ka SUNGURA hivyo hupata nafasi ya kujipendelea kuondoka na minofu na firigisi wakituachia mifupa kwi kwi kwi
 
Slaa na PHD yake!
Katika pitia pitia yangu kule kwenye tovuti ya Bunge nilivutiwa kuangalia CVs za waheshimiwa wetu..nikavutiwa zaidi kuangalia PHD ya Mh Slaa. Mshtuko nilioupata nikuwa ..kumbe Daktari yule aliweza kufanya PHD akiwa ni just a Cerificate holder! Tena lakushtua zaidi alikuwa akifanya Advanced Diploma tena ya mwaka mmoja huku akiwa tayari ameshaanza PHD yake! Swali la kujiuliza hii inawezekana?au ndio zile PHD zetu za Malecturer wa Mzumbe?!. Apart from that nakubaliana na hoja zake Bungeni maana zimesimama vizuri na ni mchapa kazi….kwa wanaofahamu waniwekee wazi Slaa na PHD yake!

Mheshimiwa Kingwele nimependa jinsi ulivyoangalia CV ya Mbunge na katibu Mkuu wa Chadema, Dr Slaa,nafikiri ulikuwa na wasiwasi na PHD yake!,naomba uigeuze Shilingi upande wa pili na omba CV ya Mbunge na katibu Mkuu wa CCM iwekwe hapa,ili watu wapate kuichambua.
 
Nyie waswahili mnaoongea phd hii elimu ile, yaelekea bado mna mawazo ya kikikoloni (mental slavery ya aina fulani towards 'western education')hizo digrii sio muhimu cha muhimu ni kiongozi mwaminifu,common sense n.k.Hao wenye ma phd wamewapeleka wapi kama sio kula tu sungura zenye minofu kama Mwami Rwabugiri kigeri V {joke mzee) alivyogusia?

Wake up and stop talking this nonsense about degrees,talk about real issues!!!
 
Na mimi nadhani kwa vile suala la PhD ya Mh. Slaa limeshawekwa wazi, naunga mkono tupate pia wasifu binafsi wa katibu mkuu wa CCM hapa tuweze kuona kiwango chake cha elimu kikoje hadi anaongoza chama kinachotawala nji?
 
Kwa jinsi navyofahamu viongozi wa kanisa katoliki, ukiona ameamua kujitenga na wito wa upadre au hata uaskofu, ujue ana kitu kinachomsumbua katika nafsi yake. Tunamifano mingi, lakini ya hivi karibuni ni ya Askofu Milingo - Zambia, Askofu Ncube- Zimbabwe na hata kina Privatus Karugendo.Badhi wameamua kupambana na mfumo wa kanisa hasa dhana ya useja na wengine kuigeukia jamii na hasa watawala katika kujaribu kuwawajibisha. Kwa hiyo simshangai Dr. Slaa hata kidogo kwa sababu ndiyo hasa anachotakiwa kufanya kama kiongozi aliyefuzu katika kanisa Katoliki.
 
tujikite sana katika jambo lililopelekea hoja hii. it is no good to attack one's personality.
 
Slaa na PHD yake!
Katika pitia pitia yangu kule kwenye tovuti ya Bunge nilivutiwa kuangalia CVs za waheshimiwa wetu..nikavutiwa zaidi kuangalia PHD ya Mh Slaa. Mshtuko nilioupata nikuwa ..kumbe Daktari yule aliweza kufanya PHD akiwa ni just a Cerificate holder! Tena lakushtua zaidi alikuwa akifanya Advanced Diploma tena ya mwaka mmoja huku akiwa tayari ameshaanza PHD yake! Swali la kujiuliza hii inawezekana?au ndio zile PHD zetu za Malecturer wa Mzumbe?!. Apart from that nakubaliana na hoja zake Bungeni maana zimesimama vizuri na ni mchapa kazi….kwa wanaofahamu waniwekee wazi Slaa na PHD yake!

Baada ya Form Six, wanasoma Falsafa kwa miaka 2 au mitatu; na baada ya hapo wanasoma Theolojia kwa miaka 5 au 6, rigorously, si kwa ubabaishaji. Hakika wanakuwa na elimu sawa na wasomi wa level ya Masters, ingawa wanapewa "vyetu" tu. Wanapokwenda kuongeza elimu vyuo vya nje (Ulaya na Marekani) wanapokelewa moja kwa moja postgraduate courses kulingana na choice ya msomi mwenyewe. Wanaomjua Dk Slaa na kuchuguza intellectual abilities zake hawawezi kutilia shaka PhD yake. Ni mara 10zaidi ya hizo za vijana wetu wa hapo mlimani. Sizungumzii wa Western Pacific University...Na kama wasemavyo wajumbe hapa, usomi haina maana kama hauambatani na umakini na uzalendo.
 
Sina uhakika kama unafahamu kwamba Dr Wilbroad Slaa alikuwa Padri wa Kanisa Katoliki, na kwa miaka 10 au zaidi alikuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC). Hiyo PhD aliyo nayo ni ya sheria za Kanisa (Canon Law). Ukifuatilia hatua za kupata upadri katika Kanisa Katoliki utakubaliana nami kwamba Kanisa hili lina utaratibu wa kujikusanyia hazina kubwa ya watu wenye uwezo mkubwa kiakili, na wote wanaofikia hatua ya kuwa Padri wana uwezo wa kufanya PhD na zaidi. Masomo wanayofanya katika Seminari Kuu (Philosophy na Theology) ni sawa kabisa na universities kwa shahada ya kwanza na ya pili, ingawa baadhi ya seminari hizo huwa haziwapi shahada hizo (kwa sababu za ukiritimba na kuogopa kuwa wakipata sifa kubwa watatoroka, labda). Sababu nyingine za kuwanyima shahada japo wamesoma sawa na (au zaidi ya) wenye shahada ni lile dai la kwamba kitu cha muhimu kwa Padri ni lile daraja/sakramenti ya upadrisho ambayo hutolewa na Askofu, na wala si cheti kikubwa! Na kwa kuwa mapadri huweka nadhiri (vows) ya utii, inabidi wakubaliane na hali hiyo. Lakini akishafanya kazi na kuaminiwa zaidi na Askofu, basi hapo Padri anaweza kupewa nafasi ya kwenda kupata shahada zake, na huwa wanafanya masomo kuendana na kipaji chake na mahitaji ya Kanisa kwa wakati huo kama itakavyoamuliwa na Askofu, na ndipo atakaposoma hadi kufanya hizo PhD nk. Kwa kufuata nadhiri ya utii, Padri hata mwenye PhD anaweza kupangiwa kazi yoyote na Askofu wake, na haruhusiwi kukataa. Kwa mfano, Askofu anaweza kumpangia padri huyo kazi ya kutunza accounts, na kama atasema hana taaluma hiyo, atatumwa akasome(ndio maana unaweza kumkuta Padri mwenye umri wa miaka 50 au zaidi, anasomea cheti cha accounts technician, na usishangae ukakuta huyo ana PhD ya fani fulani, labda Lingustics au Sociology) .

Hiyo inaweza kuwa possible explanation ya Dr Slaa kusoma Advanced Diploma (sijui ya nini) wakati alishafanya PhD. Wanaomfahamu zaidi (au yeye mwenyewe) wanaweza kutoa maelezo specific zaidi, lakini mimi nimetoa maelezo ya jumla yanayowahusu watu walioko au waliopitia mkondo huo wa Upadri katika Kanisa Katoliki. Natumaini kwa kiasi fulani nimekidhi kiu ama shauku yako ndugu Kingwele.

Mkuu Kithuku,

Heshima mbele mkuuu, na SALUTE!

Yes, hii ndio tunaita kumkoma nyani giladi, case closed!
 
Jamani hii nimeipata kwenye e mail na naona inazunguka hapa sijaongeza chochote nawasiliasha hoja


Tarehe 11/10/2007 katika kituo kimoja maarufu cha runinga kulionyeshwa kipindi kimoja cha vichekesho ambacho sasa kimezua jambo ndani ya chama maarufu cha CHADEMA.(Maoni yangu ilikuwa ZE COMEDY)

Katika kipindi hicho, baadhi ya vitendo vichafu vya Dr. WILBROD SLAA vilianikwa hadharani. Awali watazamaji wengi hawakutilia maanani yaliyosemwa kwenye kipindi hicho kwani walidhani ni vichekesho vya kawaida. Lakini sio hivyo tena baada ya hali ya kisiasa isiyotarajiwa kufahamika ndani ya chama cha CHADEMA.

Katika siku za karibuni Dr. SLAA amejichotea sifa nyingi baada ya kutoa hadharani tuhuma alizoziita za kifisadi na kutaja majina ya watu aliowaita mafisadi. Ingawaje Dr. SLAA mwenyewe amekiri miongoni mwa marafiki zake kwamba tuhuma zake hazina hata chembe ya uthibitisho lakini amepata furaha ya mshangao kuona jinsi ambavyo tuhuma zake zimempa sifa lukuki ndani na nje ya nchi.

Habari toka ndani ya chama cha CHADEMA zinasema kuwa ingawaje kwa juu juu MBOWE na ZITTO KABWE wanaonekana kufurahia umaarufu wa Dr. SLAA lakini wote hao wawili kwa sababu zao tofauti wameelezwa kuumia sana kwani wanaona Dr. SLAA anawapiku umaarufu wa kisiasa na kwamba huenda akaamua kugombea urais mwaka 2010 kwa tiketi ya CHADEMA.

Mhe. MBOWE na ZITTO KABWE wameapa kummaliza kabla hajafika mbali. Ati MBOWE anaona Ikulu inamwita na njia ni nyeupe lakini sasa anaibuka mtu anaitwa SLAA anataka kumnyang誕nya kilicho chake!

Ni kwa msingi huo, sasa MBOWE na ZITTO wameamua kuanika madhambi ya Dr. SLAA ili wananchi wajionee kwani wanaamini madhambi yao wao hayajulikani maana wameshatumia mamilioni ya pesa kuyazika madhambi hayo. Ili kutimiza lengo lao wameamua kusambaza baadhi ya vioja vya Dr. SLAA. Hivi wanadai ni baadhi tu kwa vile orodha ni ndefu na wataitoa kwa awamu. Wameanza na nyepesinyepesi. Haya ndiyo wameyaanika kwa sasa:

MJUE DR SLAA

Mpaka sasa SLAA hana nyumba huko Karatu, badala yake hulala kwa rafiki yake ambaye inadaiwa ni shoga.

Tangu mwaka 1977 hadi 1991, SLAA alikuwa Padre wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbulu. Aliachishwa Upadre baada ya kukosa uaminifu na kuendekeza tabia ya ufuska na wake za waumini. Hali hiyo ilimpelekea kupata watoto wawili wakati akiendelea kutoa huduma za kiroho. Watoto hao ni EMILIANA aliyezaliwa 18/06/1987 na LINUS aliyezaliwa 23/09/1988. Dr. SLAA alimuoa ROSE, mmoja wa waumini wake mwaka 1991 ndipo kanisa likamfukuza Upadri. Wakati huo ROSE alikuwa mchumba wa mweka hazina wa Kanisa ambaye miaka michache baadaye alikufa kutokana na mfadhaiko.

Uchunguzi umeonesha kwamba, Dr. SLAA ni fuska aliyebobea, na anayo tabia ya kufanya mapenzi na wake wa marafiki zake hata baada ya kuoa. Kwa mfano Diwani wa Kata ya Baray wilayani Karatu LAZARO TITUS MASSAY (CHADEMA) aliwahi kupeleka malalamiko katika uongozi wa juu wa CHADEMA kuhusu tabia ya SLAA ya kufanya mapenzi na wake za watu wakiwemo hata wake za Madiwani Jimboni Karatu. Aidha, tarehe 01/11/2004, SLAA alifumaniwa na mkewe katika chumba kimojawapo cha Hotel 56 mjini Dodoma akiwa anafanya mapenzi na msichana aitwaye NJARI. SLAA aliruka dirishani bila nguo na wahudumu wa hoteli wakamsetiri kwa shuka na kumficha hadi mke wake alipoondoka kwa hasira kali baada ya kupambana na 僧wizi・wake sawasawa - tukio hilo lilinaswa kwenye mkanda wa simu ya mkononi ya mhudumu na umehifadhiwa kwa matumizi katika wakati muafaka.

Dr. SLAA anasumbuliwa na 爽gonjwa mkubwa・ Amekuwa akienda kutibiwa mara kwa mara nchini Afrika Kusini. Mwezi Oktoba hadi Desemba, 2006, SLAA alilazwa katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam akitibwa 組onjwa moja hatari sana ・

Dr. SLAA amewahi kula mamilioni ya fedha za vilema ambazo zililetwa na wafadhili toka Ujerumani. Ushahidi upo kama atafanya ubishi.

Alihongwa nyumba Ujerumani na hawara yake wa Kijerumani ambaye sasa ni marehemu na Dr. SLAA anategemea kuhamia huko. Inasemekana Dr. SLAA na hawara yake ambaye ni marehemu walishirikiana kumuua mume halali wa mama huyo aliyejulikana kwa jina la 全imbosh・

Dr. SLAA alikuwa kachero wa Idara ya Usalama wa Taifa kama alivyo LYATONGA MREMA na alikuwa anaendelea kulipwa kiasi kikubwa cha fedha. Baadaye Idara hiyo nyeti iligundua fedha hizo anapeleka kwa hawara zake hivyo ikasitisha malipo hayo hali ambayo imemuudhi na akaanza kuipaka matope kwa kuituhumu na taarifa za kughushi anazodai amezipata. Vyanzo vya kuaminika vimebaini SLAA alipewa taarifa ya kughushi na akainunua kwa bei mbaya. Baada ya kubaini hivyo sasa anamsaka mbaya wake aliyemwingiza mjini.

Ujumbe huu ambao inaaminika MBOWE na ZITTO KABWE wanausambaza kwa kasi umemtia hofu Dr. SLAA kwani anajua yapo mengi yanayomhusu ambayo asingependa yajulikane. MBOWE na ZITTO wanaungwa mkono na chama cha CUF ambacho nacho kinadhani CHADEMA imekipiku katika umaarufu wa upinzani. Sera ni jino kwa jino.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom