Cos101
JF-Expert Member
- Sep 16, 2020
- 446
- 1,015
Hongera Mkuu.View attachment 1628751
Naam, miaka 4 ya nenda - rudi kortini imehitimishwa leo baada ya hukumu ya mwisho kusomwa mahakamani.
Nachukua fursa hii kumshukuru Mungu kwa ulinzi wake katika safari hii; nawashukuru ndugu na familia kwa kuwa nami bega kwa bega katika kesi hizi na kunitia moyo; nawashukuru uongozi na watendaji wote wa JamiiForums kwa kuwa nami katika kila hatua; asanteni marafiki mliokuwa nami bila kunitupa na kuniombea kila mara; nawashukuru watanzania wote ambao kila mlipokutana nami (na wengine humu mitandaoni) mlisisitiza nisitetereke mpo nami; nawashukuru wanasheria mliokuwa nami mwanzo hadi mwisho na pia nawashukuru wadau wote wa habari na #UhuruWaKujieleza ambao mmekuwa mkitupa ushirikiano kwa namna moja ama nyingine.
Hakuna kesi ndogo, yamepita mengi lakini nikiri safari hii imekuwa na mafunzo mengi kwangu. Imekuwa safari ngumu lakini yenye faida kubwa kwani nimepata marafiki wa kweli, nimepata uelewa mpana zaidi na nimekuwa imara zaidi ya awali.
Sipendi kuongelea content ya kesi, ila niseme tu: Safari itaendelea, maisha yataendelea na hakuna kurudi nyuma. Milima, mabonde, mitikisiko n.k. havina budi kutokea - tutapimwa mwishoni kwa kusimama imara kwetu katika mawimbi haya. Asitiwe yeyote hofu, JamiiForums will always be JamiiForums! Niwaombe wadau wote kuzingatia mwongozo wa ushiriki katika Majukwaa, ni vipengele 16 muhimu sana.
Kwa wadau wengine wa Uhuru wa Kujieleza: Tunajenga nyumba moja, tusigombanie fito!
KISUTU, DAR: Maxence Melo akutwa bila hatia shtaka la Kikoa. Apewa 'Conditional Discharge' kwenye shtaka la kutotoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi
Hukumu ya kesi namba 458 ya 2016 ya Jamhuri dhidi ya JamiiForums inatarajiwa kusomwa leo Novemba 17, 2020 katika Mahakama ya Kisutu Katika shauri hili lenye mashtaka mawili, watuhumiwa wanashtakiwa kuendesha mtandao ambao haujasajiliwa kwa kikoa cha DO-TZ Katika shtaka la pili, Polisi ilimtaka...www.jamiiforums.com
God has been good.
Sent using Jamii Forums mobile app