Huko kwenye viwanja vya Saba Saba hali ikoje?

Huko kwenye viwanja vya Saba Saba hali ikoje?

Sawa pia mkuu punguza matumizi ya chartgpt.
situmii hiyo kitu na sijui kuitumia. Na ikiwa ni kitu cha wazi, nadhani ikiwa kinaweza kukusaidia unaweza kukitumia tu gentleman,

Ila kwangu mimi,
ninafanya haya yote kwa Neema na Baraka za Mungu tu, gentleman sina cha kujivunia zaidi ya hilo humu jukwaani na nje ya jukwaa 🐒
 
In fact hata ninavyoreply comment yako niko viwanjani, umauti wa wananchi wanaoingia na kutoka kwenye maonyesho ni mkubwa pengine kuliko hata wakati uliopita licha ya kua kuna hali ya mawingu na mvua za hapa na pale.

halafu kupo shwari sana,
na utaratibu wa kuingia na kutoka umerahisishwa na kuboreshwa sana.

Nadhani bila unafiki na propaganda za vibaraka na mamluki wa mabwenyenye ya magharibi,
Tuwe wakweli tu,
maonyesho ya kibaashara ya kimataifa sabasaba kwa mwaka 2026 yamefanikiwa zaidi kuliko wakati mwingine wowote 🐒
Tutupie video gentleman
Nipaone 77 palivyo sahv

Ova
 
Ila mahudhurio ya watu ni hafifu. Kwa maneno marahisi maonyesho yamedoda.
Ila mahudhurio ya watu ni hafifu. Kwa maneno marahisi maonyesho yamedoda.
Sio yamedoda Tu Bali hakuna watu wameingia sabasaba, huku mitaa yetu ya temeke,mtongani Hadi mbagala vituo vya mafuta vya lake oil vimefungwa vyote ,Hali ya barabarani Leo ni ngumu Sana Kwa wananchi kwenda sababasa
 
Maeneo mengi nchini ni kama mwaka mpya kwani maduka yamefungwa watu wengi wameitikia wito wa maandamano kwa staili ya kipekee sana na ni pigo kubwa sana kwa serikali ambayo haina ridhaa ya wananchi.
Hapa kwangu nina jirani na rafiki yangu ana magari (mabasi ya abiria) TATA nne hivi hufanya safari za Kahama - Shinyanga - Mwanza. Nayaona leo yote yamepaki nyumbani kwake...

Nipo Kahama maeneo ya mitaa ya Majengo Mapya...
 
Back
Top Bottom