Hotuba za Rais kila mwezi

Je unaridhika na hotuba za Rais Kikwete?

  • Ndio

    Votes: 13 15.5%
  • Hapana

    Votes: 71 84.5%
  • SIJUI

    Votes: 0 0.0%
  • Sina jinsi

    Votes: 1 1.2%

  • Total voters
    84
  • Poll closed .
Kweli tatizo ni JK mwenyewe. Hata kama ukimpa asome hotuba alizowahi kutoa Mkapa au Nyerere bado atachemka tu. Utoaji hotuba sio uzuri na nguvu ya maneno unayotumia tu bali pia jinsi uitoavyo(delivery). Delivery ya JK ni mbovu.
 
Namshauri JK apitiepitie hapa JF, kuna waandishi wazuri sana, wapo akina kulikoni, kichuguu, mlalahoi, DrWHO, MM Mwanakijiji, ni waandishi wazuri, awape kazi ataona tofauti.
 
Unajua wenzetu wanapokaribia kushika wadhifa kama huu hupewa darasa maalum la jinsi ya kuzungumza, body language na hata jinsi ya kutumia mikono yako kusisitiza kitu sio kuigandisha ktk meza ama kusimama kama askari. Sura yako kuonyesha unaelewa unachozungumza na sio kutafuta majawabu ama kukumbukia ulichokusudiwa kusema. Tatizo la JK ni kwamba hakupewa darasa hilo kwani wapo watu wa mtaani wanaoweza kuzungumza vitu vizito na hawana elimu hivyo.. mfano mkubwa alikuwa Kawawa.
Pili, kuzungumza ni kipaji fulani pia kwani wapo wasomi ambao hujigonga sana inapofikia ku-face umma wa watu ama wataalam wengine. Kazi hii ni sawa kabisa na Uongozi ktk dini Ma -Padre, Ualimu ama Utangazaji utaweza kutofautisha uwezo wa kila mmoja wao kwa sababu ya uzungumzaji wao. hata kama wote wanazungumzia kitu kimoja..
Mwandishi mzuri wa magazeti anaweza kabisa kuchemsha akipelekwa luninga. Mazoezi ni muhimu kama mcheza soccer, usidhani ukisha jua kukipiga basi hakuna haja ya mazoezi.
Kwa hiyo, swala la JK sio kutokuwa na hotuba nzuri iliyotayarishwa ila jinsi ya ku- deliver. Aliweza bungeni kwa sababu hoituba ile alitayarishwa vya kutosha na wapo wazee waliosema - Hawajaona rais baada ya Nyerere akizungumza vitu kwa mpangilio kama JK. Freeman nae kawatisha watu wengi na kikubwa Freeman nadhani hakosi mazoezi yake na wachambuzi wake babu kubwa.
 
Tatizo Mkandara viongozi wetu wanaamini ukishakuwa kiongozi unajua kila kitu na kuliko wote. Kwa hivyo hilo la JK kuingia darasa la kutoa hotuba sahau. Tutaendelea kuumbuka tu mpaka mwisho wa safari na wasaidizi wake wataendelea kumsifia. Maana mimi kabla sijaiangalia ile hotuba yake ya St. Thomas University nilishakutana na wasaidizi wake wakaniambia JK alitoa hotuba kali mpaka wazungu walishangaa pale. Sasa baada ya kumsikiliza then naelewa kwa nini wale wazungu walishangaa! Bila shaka hawakushangaa ubora wa speech bali how did he get elected with that level of intellect!
 
Bado hajachelewa sana, kuna njia nyingi za kutumia ili kuboresha uwezo wake wa kutoa hotuba. Kwanza kabisa atengeneze studio humo mwenye kasri lake la magogoni. Studio hiyo iwe ya nusu duara kwa mbele pamoja na audio na video recording system. Sasa kule kwenye nusu duara awe anaweka picha kubwa za kuonyesha mazingira mbalimbali ya hotuba: mikutano ya ngazi ya chini kama ile ya hadhara ambayo nadhani anaijua vizuri zaidi, mikutano ya ngazi ya kati kama kwenye za kitaifa, mikutano ya ngazi za juu kama kwenye kukutana na waandishi wa habari na kuhutubia formal setting kama kwenye vyuo vikuu, umoja wa mataifa nk. Hapa awe na maswali yaliyotayarishwa randomly na ajifunze pia jinsi ya kujibu maswali asiyojua majibu yake kwa njia ya kuridhisha.

Baada ya kuwa na maandalizi hayo, awe na PREP kila jioni kati ya saa mbili na saa nne jioni kama tulivyokuwa tukifanya huko sekondari boarding. Awe anapractice kutoa hotuba na kujirekodi mwenyewe, kisha ajitazame na kujilinganisha na vipanga wengine wa hotuba kama Nyerere. Kila atakapofanya hivyo atagundua weaknesses zake na atarekebisha kwa vile nina imani anao uwezo wa kujirekebisha. Akifanya hivyo, itamchukua miezi mitatu au minne tu kwa yeye naye kuwa kipanga wa kutoa hotuba.
 
jk jifunze kuwa makini katika kazi yako impression ya mwanzo watu watakujaji unavyo jieleza.na uelewe umebeba maisha ya watanzania 34million,please acha mzaa katika utendaji kazi.ikiwezekana tumia muda mwingi kufahamu mada zipi unaenda kuzitoa mbele za watu'kama uwezi jifanye unaumwa tuma vijana wakuwakilishe.wapo vijana wakuingia front
 
Bado hajachelewa sana, kuna njia nyingi za kutumia ili kuboresha uwezo wake wa kutoa hotuba. Kwanza kabisa atengeneze studio humo mwenye kasri lake la magogoni. Studio hiyo iwe ya nusu duara kwa mbele pamoja na audio na video recording system. Sasa kule kwenye nusu duara awe anaweka picha kubwa za kuonyesha mazingira mbalimbali ya hotuba: mikutano ya ngazi ya chini kama ile ya hadhara ambayo nadhani anaijua vizuri zaidi, mikutano ya ngazi ya kati kama kwenye za kitaifa, mikutano ya ngazi za juu kama kwenye kukutana na waandishi wa habari na kuhutubia formal setting kama kwenye vyuo vikuu, umoja wa mataifa nk. Hapa awe na maswali yaliyotayarishwa randomly na ajifunze pia jinsi ya kujibu maswali asiyojua majibu yake kwa njia ya kuridhisha.

Baada ya kuwa na maandalizi hayo, awe na PREP kila jioni kati ya saa mbili na saa nne jioni kama tulivyokuwa tukifanya huko sekondari boarding. Awe anapractice kutoa hotuba na kujirekodi mwenyewe, kisha ajitazame na kujilinganisha na vipanga wengine wa hotuba kama Nyerere. Kila atakapofanya hivyo atagundua weaknesses zake na atarekebisha kwa vile nina imani anao uwezo wa kujirekebisha. Akifanya hivyo, itamchukua miezi mitatu au minne tu kwa yeye naye kuwa kipanga wa kutoa hotuba.

Kichuguu ushauri wako mzuri sana, lakini unafaa kwa mtu aliye makini siyo JK. Imeshadhihirika huyu jamaa ni mbambaishaji wa hali ya juu. Shida yake ilikuwa naye siku moja awe Rais na ameshakuwa. Angeweza kufuata ushauri huo kama tu hilo lingekuwa kikwazo kuupata Urais. Kwa sasa ameshachelewa hawezi kujifunza maadamu maneno anayosikia ni ilikuwa hotuba nzuri sana, makofi kwa sana hata kama anaongea utumbo na mandamano ya kuunga mkono alichosema hata kama ni pumba tu.
Akina Nyerere hawakuwa watoaji wa hotuba nzuri hivihivi tu la hasha ni watu waliokuwa wanapenda kupata maarifa kwa kujisomea na kuandika, huyu wa kwetu ni ziara tu, warsha, kufungua gereji bubu na magenge kwa jina la super markets, sasa hapo atapata wapi uwezo wa kujenga hoja nzito?
 
mkandara,mwanasiasa,kichuguu,muta,
jk hana mpango kujiongezea ujuzi wa aina yoyote ule zaidi ya kucheza GOLF!!hilo ndilo lengo la jk kuanzia sasa hivi kwenda mbele.
 
Juzi TVT waliweka hotuba ya Mwalimu wakati anastaafu na baadae wakaweka hotuba ya JK siku ya kuadhimisha miaka 45 ya Uhuru.It was like an echo!
 
Jamani we should know that Mzee mkapa ni intellectual fulani ,lakini Bwana jk,amejaa sifa ,nakutaka kuonyesha watu alioenda nao shule na kazi mbalimbali ni lazima awafadhili bila kujari kwamba anendesha taifa,linalo takiwa initiative and intellectual ili kujikwamua na umasikini.we were doing very well economically twelve months ago
 
fine


unajua mimi sikualiani na hili la kutaka kumfananisha JK na MKAPA kwa sababu kila mmoja alikuwa na style yake a oungozi


lakini naona humu ndani mijadala ya kumkosoa JK imekaa ma SNOBISH ambao wanamlaumu eti rais hasomi,rais haendi Lirary,rais sijui hivi sijui vile....kundi hili ndio lile linalomlinganisa BUSH na CLINTON sasa hawa ni watu wawili tofauti na wanastyle tofauti ya Ladership na mnajua kuwa no matter what peope say BUSH won 4 elections pamoja na watu kudai kuwa interlect yake ni ndogo

sasa kama tutadiscuss issues then lets do that lakini sio ku question interlect ya JK

Maana kuna watu humu wanataka wamuimpeach wengine wanaquestion sanity yake.

tuache kudhaau watu jama
 
DrWHO,
Bush won only one election. The second one. The first one alipitishwa na Supreme Court ambayo majority ya majudges walichaguliwa na Republicans. Clinton alishinda 2 terms legally and above board. Na hivi leo niandikavyo opinion polls za Marekani zinampa Clinton 60% popularity wakati Bush ni 36%.
 
fine


unajua mimi sikualiani na hili la kutaka kumfananisha JK na MKAPA kwa sababu kila mmoja alikuwa na style yake a oungozi


lakini naona humu ndani mijadala ya kumkosoa JK imekaa ma SNOBISH ambao wanamlaumu eti rais hasomi,rais haendi Lirary,rais sijui hivi sijui vile....kundi hili ndio lile linalomlinganisa BUSH na CLINTON sasa hawa ni watu wawili tofauti na wanastyle tofauti ya Ladership na mnajua kuwa no matter what peope say BUSH won 4 elections pamoja na watu kudai kuwa interlect yake ni ndogo

sasa kama tutadiscuss issues then lets do that lakini sio ku question interlect ya JK

Maana kuna watu humu wanataka wamuimpeach wengine wanaquestion sanity yake.

tuache kudhaau watu jama

I disagree with all who say Bush's intellect is under par. Bush is just as smart as anyone else out there. Just because he didn't pronounce a few words correctly during the 2000 campaign or just because he has the propensity to stumble when he talks doesn't make him any less intelligent than Clinton, Gore, or Kerry. He's just not a good talker. He doesn't have what they call the gift of the gab.

Bush held his own during the 2000 presidential debates against Al Gore (who was supposedly smarter than him and was expected to totally annihilate him). Gore just kept on sighing and sighing and in the end he came across as too condescending.

Jasusi, for your information, Bush has never lost any election since the late 70's when he ran for congress. He has always been underestimated. Even when he ran against Ann Richards in '94, the so called pundits said he had no chance in hell beating the then popular governor. But guess what, he won. In 2000, he won that election. People shouldn't blame the supreme court. The only person to blame is Al Gore who couldn't win his own state of Tennessee. Gore didn't need Florida. How can anyone not even win their home state??? Even Walter Mondale won Minnesota (his home state) in the '84 election when Reagan won all 49 states and the district of Columbia.
 
Tutalia sana, hadi hiyo miaka 10 iishe kuna kazi. Wengine humu mtameza chupa zilizosagwa!


MWANASIASA

JK -JANUARY MAKAMBA ARUDI SHULE ''FIELD'' IMEISHA ONE YEAR
Ndiyo sababu hotuba zote mwaka mmoja zimekuwa mbaya ''alikuwa field''
Kapoteza marafiki ana wakumsaidia
Boss wake amemchoka
Ni kati ya wanao msifia JK

CCM-mtandao ilikuwa kwenye kampeni ya muh. huyu nchi nzima ilisisikia wanavyo panga mipango yao jinsi walivyo kuwa watu wa muhimu wakati wa kampeni kuanzai tareha 21 dec,2005 simu zote

za waliopewa nafasi za kazi zilibadilika kuwa PRIVATE NUMBER, nyingi zilibadilishwa, nyinge ukipiga hazipokelewi ,basi hawakujua yatatokea hayo lakini wamejifunza kitu, kama kunakijana ambaye ni kiherehere basi JANUARY MAKAMBA kafuzu

kuanzia kipindi chote cha kampeni hadi sasa, atakikuona mtu anaongea au kumsalimia muh.JK anafukuza watu mbele ya MUH. na kuwaambia ondokeni mumesha msalimia.lakini wakati wa kampeni watu walikuwa na uhuru wa kuongea na kucheka ambayo nitabia ya muh. kukaa na watu.

sasa basi baadaya ''k'' huyo kupewa kazi ya kuwa mzaidizi upande wa Hotuba za Rais ana act kama PERSONNEL SECRETARY

ninafikiri huyu ''K'' awezi atakumshauri boss wake jinsi ya kuandika HOTUBA yeye pale anajifunza anaandaliwa 2010 kuwa mwandishiwa Rais HOTUBA Muh.rais usimtegemee sana huyu kijana, kama ni kujifunza inatosha sasa arudi shule alikuwa yuko ''field'' watu wazuri wako kama ilivyo zungumzwa kwenye forum hii.

au waondowe wote wawili wana kuletea aibu, ninaomba wengine wanao mfahamu kijana huyu ''kabla na baada''
 
Wale ambao tumekuwa pamoja siku nyingi, mtakumbuka vizuri kwamba wakati wa kutafuta nani awe mgombea kwa tiketi ya CCM, nilikumbushia mara kadhaa jambo lifuatalo:

Wakati BWM amelazwa Ulaya na nchi za Jumuia ya Madola zinatafakari juu ya Zimbabwe, waandishi wa habari walimuuliza JK: Msimamo wa Tanzania kuhusu hatua gani zichukuliwe dhidi ya Zimbabwe ni upi? Alijibu kwamba tutasubiri tuone nchi nyingine zinafanya nini ndio tuamue.

Mtu anayesubiri kuona nchi nyingine zinafanyaje sio kiongozi. Wengi hamkuelewa wakati ule, lakini sasa nadhani mnaona ukweli unavyojitokeza.

Augustine Moshi
 
Back
Top Bottom