Hotuba za Rais kila mwezi

Hotuba za Rais kila mwezi

Je unaridhika na hotuba za Rais Kikwete?

  • Ndio

    Votes: 13 15.5%
  • Hapana

    Votes: 71 84.5%
  • SIJUI

    Votes: 0 0.0%
  • Sina jinsi

    Votes: 1 1.2%

  • Total voters
    84
  • Poll closed .
Jk alipewa uwanja wa kimataifa lakini hakuwa anajiandaa kujibu misimamo yetu Wantanzania kulingana na matukio ya kimataifa, hata hivi sasa im afraid hali yake haijabdilika (inabidi apigwe msasa kwa hilo), kuna jamaa wawili (Wabongo) kule South Africa wakati wa discussion na BBC, walisaidia kufunika mepesi yaliyozungumzwa na JK, hao jamaa wampige msasa JK. Pia humu bodini kuna watu smart sana JK aweza kuwatumia pia (some free of charge!!)
 
Wanabodi,
Je, Kuna uwezekano kuwa VIONGOZI wetu lazima wawe wasaniii ili kukubalika kwa wananchi?
Nimepata baadhi ya Interview za Mkapa... Zinavutia sana lakini kama kweli kuna MSANII basi huyu hakuwa mbali na Bolywood..
Ukitazama interviews zake utakuta kwamba kayafanya mengi sana ambayo yeye mwenyewe alikuwa hakubaliani nayo ktk hotuba zake. na matokeo yake yamekuwa vile vile alivyokuwa akisema kupinga maendeleo ya nchi zetu maskini.
Mkapa na Elimu ya Kitabu kusema kweli alikuwa mzima sana!
Tazameni site hii:- http://www.pbs.org/wgbh/commandingheights/shared/minitextlo/int_benjaminmkapa.html
 
Of course jamaa alikuwa/ni mzima kwenye interviews. Kwenye matendo ndio hayo sasa uliyosema, kama alivyosema yeye haweki matendo kwenye mdomo wake.
 
Oh ya!, alikuwa very goood kwenye interviews lakini akashindwa kujenga hata nyumba kwao Masasi, na hata baada ya kustaafu akajenga Lushoto Tanga kwa marafiki zake kina Ngwiliz na Kigoda,

Badala ya kujenga kwenye mizimu ya mababu zake, Masasi, je tulitegemea nini kutoka kwa huyu msomi as far as taifa is concerned?
 
Oh ya!, alikuwa very goood kwenye interviews lakini akashindwa kujenga hata nyumba kwao Masasi, na hata baada ya kustaafu akajenga Lushoto Tanga kwa marafiki zake kina Ngwiliz na Kigoda,

Badala ya kujenga kwenye mizimu ya mababu zake, Masasi, je tulitegemea nini kutoka kwa huyu msomi as far as taifa is concerned?




MANENO YAKO NI MAZITO SANA NDUGU YANGU


halafu usisahau tunavyokumbushwa jinsi gani alivyokuwa MSOMI na JK hasomi

sasa whats the point ya kusoma?
 
Oh ya!, alikuwa very goood kwenye interviews lakini akashindwa kujenga hata nyumba kwao Masasi, na hata baada ya kustaafu akajenga Lushoto Tanga kwa marafiki zake kina Ngwiliz na Kigoda,

Badala ya kujenga kwenye mizimu ya mababu zake, Masasi, je tulitegemea nini kutoka kwa huyu msomi as far as taifa is concerned?

mzee%20mkapa2.JPG

Wednesday, 22 November 2006
RAIS Jakaya Kikwete na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa wakibadilishana mawazo kijijini Lupaso ambako JK alikwenda kumtembelea juzi akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Mtwara. (Picha na Godfyre Baluah)

Source: gazeti la Uhuru, and http://jambotanzania.net/v2/index.php?option=com_content&task=view&id=896&Itemid=2
 
Tusichanganye mambo.
Kuwa 'intellectual' na kuwa kiongozi mzuri ni mambo mbalimbali.
'Intellectual' haina maana mtu si mpokea rushwa. Tuseme 'intellectual' anaweza kuwa na uwezo mzuri wa kuyachambua mambo na kuyawasilisha; kwa mfano kwa kutoa hotuba zenye nasaha. Kwa hiyo tupime u-intellectual wa viongozi wetu hawa kwa mantiki ya hotuba zao walizozitoa, na sio kwa kigezo cha uzuri wa uongozi wao.

Mnhh!! hao wasanii si ma-intellectual jamani tusidanganyane!
 
Kumbe hoja ni Simba na Yanga!!!!!!!!!!!!

Kuweni wakweli kwa faida ya JF na wazalendo,angalieni wanetu watarithi nini kutoka ktk maandiko ya hawa wakubwa.

BM alishutumiwa sana alipoanza kazi ya urais 1995 kuwa anapenda kusoma hotuba;mlisema JKN na AHM waliweza kuzungumza pasipo kusoma na kuivuta hadhira,baada ya 10 yrs yake JMK alianza kwa kusoma pale bungeni na nyote mkasisimka kwa uzito wa hotuba yake.
Sasa leo haya kusema rushwa na blabla zake zinahusianaje na namna mahiri ya kufikisha ujumbe kwa njia ya hotuba?!!!!!!

ES!!! Kwani Mkapa alikufanyia kitu gani kiasi cha kutamani umtoe roho?!! Maana sasa nakuona umezidi kupoteza mwelekeo wako kama ilivyoonyeshwa kwa mtandao ule wa mwanzo.
JF ni open book ,acheni ubinafsi kwani tushausoma zamani sana kinachotakiwa ni hoja ijibiwe kwa namna ilivyoletwa.

Tupe way forward na siyo way back kwa chuki binafsi,haitusaidii.
 
Nadhani suala la hotuba ni la utashi wa rais mwenyewe kujua anataka kuongelea jambo gani. Hebu tufikirie JK alikuwa Waziri wa Mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa kwenye kipindi cha mkapa kwa miaka 10, na alikuwa mwakilishi mzuri tu wa Rais kwenye vikao vya nje kiasi cha kwamba mkapa vikao vingine alikuwa anamwachia amwakilishe bila wasiwasi, mfano: wakati mkapa alikuwa amelazwa hospitali akiuguza mguu wake huko nje, kulikuwa na vikao vingi tu vilifuata ambapo mkapa yeye mwenyewe alipotoka hospitali alikiri kuwa JK amefanya kazi yake ipasavyo na kiwango alichokitaka. Kwa hiyo suala la speech ni utashi wa mtu na marais wengi tu wanatoa speech kwa wao waonavyo, tusimlaumu JK ila kufanya hivyo ni kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi iliyomuweka madarakani.
 
I think we have a tendency to use concepts very loosely. Mimi nadhani tuwe very careful with this. Ni vizuri kuchimbua maana ya concept, na kuitendeaa haki katika kuitumia!

Intellectualism sio usomi, na kumtambua ama kum-brand mtu kuwa ni intellectual sio jambo dogo hata kidogo! Sio mtu kubebwa na nafasi na katika kutekeleza majukumu yake ya msingi basi anakuwa intellectual. This shows kuwa scale zetu za expectations kwenye Presidency kama an institution ziko very low. Zaidi sana one cross-cutting feature ya intellectuals ni kuwa hiyo identity anaibeba yeye binafsi, kwa uwezo, passion, jitihada na outstandingness yake kama an individual.

Ukitaka kujua academic ama theoretical use ya concept 'intellectual' you may need to be familiar with works kama za kina Antonio Gramsci...discussing aspects za Ideological hegemony na role ya intellectuals katika ku-create counter hegemony. Pia you may need to understand kazi za Karl Mannheim katika 'Ideology and Utopia'discussing the role of intellectuals. Ni vizuri pia ukaelewa kiasi kazi za Georg Lukacs ama katika an African context Frantz Fanon, katika issues za national conscisouness. After this it might be possible kui-tailor na kui-apply concept kwa a particular individual on the basis of comparisons with an ideal intellectual.

Naomba kuwakilisha!
 
Mimi sijaona tofauti kati ya hotuba za Mkapa na Kikwete ila kikwete huzungumza kwa ulaini na Mkapa alikuwa kama mbogo.kama utamu wa hotuba basi Nyerere alikuwa akijua kuzungumza an kuwa na mvuto zaidi.Katika masuala ya uongozi hotuba nzuri tu pia haitoshi kwani nakumbuka hotuba za mwalimu zilivyokuwa tamu na watu wakicheka na kutabasamu lakini wakirudi majumbani njaa kali ilikuwa ikiwasubiri.Binadamu kama kawaida tunasahau haraka madhila baada ya faraja kupiga hodi.Nani ana haja na hotuba za ujamaa na kujitegemea za miaka ya sabini na themanini?Matatizo ya umaskini na njaa hayakidhiwi kwa lugha za vichekesho.
Hotuba za Kikwete zina ubaya gani katika nyakati zetu ukilinganisha na zile za zama za ulanguzi na bei za kuruka?Wanaomsakama Rais hawana hata vigezo.Vigezo gani vya kulinganisha hotuba ya Kagame na mgeni wake Kikwete na ile ya Kagame kuonekana bora?Mwalimu alikemea wale wanaokimbilia ikulu na kuuliza kuna nini ikulu,lakini hakuna aliyemuuliza mbona wewe uliishi ikulu kwa zaidi ya miaka 20? kwa hotuba Mwalimu alikuwa best lakini vitendo?
 
MWANASIASA

JK -JANUARY MAKAMBA ARUDI SHULE ''FIELD'' IMEISHA ONE YEAR
Ndiyo sababu hotuba zote mwaka mmoja zimekuwa mbaya ''alikuwa field''
Kapoteza marafiki ana wakumsaidia
Boss wake amemchoka
Ni kati ya wanao msifia JK

CCM-mtandao ilikuwa kwenye kampeni ya muh. huyu nchi nzima ilisisikia wanavyo panga mipango yao jinsi walivyo kuwa watu wa muhimu wakati wa kampeni kuanzai tareha 21 dec,2005 simu zote

za waliopewa nafasi za kazi zilibadilika kuwa PRIVATE NUMBER, nyingi zilibadilishwa, nyinge ukipiga hazipokelewi ,basi hawakujua yatatokea hayo lakini wamejifunza kitu, kama kunakijana ambaye ni kiherehere basi JANUARY MAKAMBA kafuzu

kuanzia kipindi chote cha kampeni hadi sasa, atakikuona mtu anaongea au kumsalimia muh.JK anafukuza watu mbele ya MUH. na kuwaambia ondokeni mumesha msalimia.lakini wakati wa kampeni watu walikuwa na uhuru wa kuongea na kucheka ambayo nitabia ya muh. kukaa na watu.

sasa basi baadaya ''k'' huyo kupewa kazi ya kuwa mzaidizi upande wa Hotuba za Rais ana act kama PERSONNEL SECRETARY

ninafikiri huyu ''K'' awezi atakumshauri boss wake jinsi ya kuandika HOTUBA yeye pale anajifunza anaandaliwa 2010 kuwa mwandishiwa Rais HOTUBA Muh.rais usimtegemee sana huyu kijana, kama ni kujifunza inatosha sasa arudi shule alikuwa yuko ''field'' watu wazuri wako kama ilivyo zungumzwa kwenye forum hii.

au waondowe wote wawili wana kuletea aibu, ninaomba wengine wanao mfahamu kijana huyu ''kabla na baada''



Mzee Makamba mwenyewe anachemsha sana huko CCM. kumbukeni pia alipohojiwa na wanahabari baada ya mtoto wa Jk kuchukua formu za NEC!

huyu mzee makamba aliwatukana watanzania na kusema kuwa mtto wa dreva atabaki kuwa dreva na kamwe hawezi kuwa mwanasiasa au kiongozi! Kwake mtoto wa rais ni rais! Je ni kweli???

huyu mzee pamoja na mwanae ninaona wanachemka kweli kweli!

Iko kazi mpaka mtakaposema NO NO, NO WAY! KOMENI KUTUDANGANYA.
HATA MTOTO WA MKULIMA ANAWEZA KUWA KIONGOZI WA NCHI HII NA AKATAWALA VIZURI TU KAMA WALIVYOFANYA WENGINE!
 
Hotuba ya Mnazi Mmoja (14 Julai) kwenye uzinduzi wa kampeni ya kupima UKIMWI ilikuwa nzuri...

alipoharibu ni pale alipokuwa akizungumzia tabia ya baadhi ya watu kujinufaisha kwa mgongo wa waathirika, akatumia maneno "Hiyo ndiyo Bongoland". Hapo aliua uzito wa hoja yake katika kuonyesha ubaya wa hao watu wanaojinufaisha. Kwangu, ni kama vile alionyesha kuwa suala hilo si baya, au tatizo, na hasa kwa vile alitumia maneno hayo kimzaha huku akicheka. Badala yake, angepaswa kukemea kwa ukali!
 
Intellectual
From Wikipedia, the free encyclopedia
Jump to: navigation, search
"Literati" redirects here. For the Yahoo! game, see Literati (game).
An intellectual is one who tries to use his or her intellect to work, study, reflect, speculate on, or ask and answer questions with regard to a variety of different ideas.
There are, broadly, three modern definitions at work in discussions about intellectuals. First, 'intellectuals' as those deeply involved in ideas, books, the life of the mind. Second, 'intellectuals' as a recognizable occupational class consisting of lecturers, professors, lawyers, doctors, scientist, engineers, etc. Third, cultural "intellectuals" are those of notable expertise in culture and the arts, expertise which allows them some cultural authority, and who then use that authority to speak in public on other matters.
 
Nadhani suala la hotuba ni la utashi wa rais mwenyewe kujua anataka kuongelea jambo gani. Hebu tufikirie JK alikuwa Waziri wa Mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa kwenye kipindi cha mkapa kwa miaka 10, na alikuwa mwakilishi mzuri tu wa Rais kwenye vikao vya nje kiasi cha kwamba mkapa vikao vingine alikuwa anamwachia amwakilishe bila wasiwasi, mfano: wakati mkapa alikuwa amelazwa hospitali akiuguza mguu wake huko nje, kulikuwa na vikao vingi tu vilifuata ambapo mkapa yeye mwenyewe alipotoka hospitali alikiri kuwa JK amefanya kazi yake ipasavyo na kiwango alichokitaka. Kwa hiyo suala la speech ni utashi wa mtu na marais wengi tu wanatoa speech kwa wao waonavyo, tusimlaumu JK ila kufanya hivyo ni kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi iliyomuweka madarakani.

Mkapa ni mtu mstaarabu na mwana diplomasia. Kama JK ameharibu hawezi kutoka hospitali akasema hadharani kuwa Kikwete ameharibu ukizingatia wote ni mafisadi. Kwahiyo, Mkapa kumsifia JK kuwa amefanya kazi nzuri, haina maana kuwa JK alifanya kazi nzuri.
 
Watanzania Nimewasoma,

Viongozi wetu hawa wawili wako tofauti kabisa; Mh. Ben kwa kweli watu walioenda shule walimwelewa sana, maana hata Kiswahili chacke kilikuwa cha kitabuni, ilikuwa ni nadra sana Mh. Ben asiboreshe hotuba yake kwa medhali etc... Ila Mh., Ben alikuwa anawatoa wananchi knock out na hotuba zake kwa upande mwingine msisahau hili.

Upande mwingine Mh. Jakaya yeye anaongea lugha ambayo mwananchi wa Manzeshe kwa mfuga mbwa wanamuelewa,,, kwa bahati mbaya makundi haya mawili (wasomi na wanakijiji) kuyatosheleza ni kazi kweli kweli, aliweza Mh. Julius tu ambaye well ni kichwa kingine kabisa... Africa inalifahamu hili.

Ila naomba kuwakumbusha kidogo kwamba Mh. Jakaya ni Muungwana, nakumbuka Mh. Jakaya kwenye hotuba ya mwisho au karibu na mwisho ya Kampeni 2005 pale Jangwani,,, alisema "leo nimeshauriwa niandike hotuba maana nimeambiwa nina tatizo la kuelezea jambo moja kwa muda mrefu sana...."

Mh. hili analifahamu and with time, atajirekebisha after all, sio priority ya nchi...

Kwa maana nyingine jamani utamaduni wa hotuba kuandikwa alituletea Mh. Ben na tunamshukuru kwa hili, ingawa kwa ukasuku wetu hotuba zinaandikwa siku hizi hata za kusema shukrani,kipa imara nk. wakati kitu kama shukrani ni jambo lilokugusa moyoni hivyo hata usipoandika unatakiwa uweze kutamka...

Wote wawili sio maintelectual,,, in short kama Mh. Ben alikuwa interlectual tungemwona mwenyewe kabla ya Mh. Hayati nyerere kumpiga stop Mh. John. kugombea...

Nawasilisha
 
Watanzania Nimewasoma,

Ila Mh., Ben alikuwa anawatoa wananchi knock out na hotuba zake kwa upande mwingine msisahau hili.

Upande mwingine Mh. Jakaya yeye anaongea lugha ambayo mwananchi wa Manzeshe kwa mfuga mbwa wanamuelewa,,, kwa bahati mbaya makundi haya mawili (wasomi na wanakijiji) kuyatosheleza ni kazi kweli kweli, aliweza Mh. Julius tu ambaye well ni kichwa kingine kabisa... Africa inalifahamu hili.

Yaani watanzania na huu utamaduni wa "MHESHIMIWA"..Hivi JK si alikataa kuitwa mheshimiwa na ndio maana hata katika picha zake alisisitiza itumike Ndugu? Na Nyerere pia mnamwita mheshimiwa?

Kama inakuwa ngumu huko kwenye ukadalization basi angalao hapa katika bunge letu tukutu jitahidini kupunguza haya maneno ya kibwanyenye. Tukiyamiss tutembelea kweny vikao vyetu vya ulaji ambako heshima za kinafiki zimejigubika.

Acheni hizo. jifunzeni kujiamini kidogo.

Tanzanianjema
 
Naomba kunukuu hotuba ya rais Kikwete aliyoitoa bungeni tarehe 30/12/2005. Nanukuu ukurasa wa tatu na wa nne kidogo ili tuweze kujadili kama alikuwa anaanisha alichokuwa anakisema ama ilikuwa ni siasa ama usanii kama usanii mwingine wowote ule.

Nimeona niweke hapa hili kutokana na jinsi Zitto na Dr. Slaa walivyotendwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania,ndani ya mwaka mmoja na nusu .

Nanukuu,

Mheshimiwa Spika,
Nawapongeza wabunge wote waliochaguliwa.Ninyi ,waheshimiwa wabunge ,ndio macho na masikio ya wananchi.Mmeaminiwa na kuheshimiwa .Naomba kila siku mnapoingia au kutoka katika bunge hili ,mnapozungumza humu ndani au mnaposikiliza wengine wakizungumza,mnapokuwa macho au mnapofumba macho kutafakari kwa kina ,kila mara mkumbuke imani na heshima hiyo kubwa mliyopewa na wananchi.

Nakupongeza sana wewe mwenyewe ,mheshimiwa spika,kwanza kwa kuchaguliwa kuwa mbunge,na pili kwa kuchaguliwa kuwa spika wa bunge hili tukufu. Umepata kazi ya heshima kubwa sana ,yenye wajibu mkubwa sana .Unao uwezo na uzoefu wa kuifanya.Hivyo sina shaka utaimudu vema kazi hiyo,na utaliongoza bunge hili kwa hekima na busara,ukiwatendea haki wabunge wote,na upande wa serikali pia. Ninakutakia kila la kheri,na ninakuhakikishia ushirikiano kamili katika kazi zako.

Je? maneno hayo ya busara alikuwa akimaanisha ama alikuwa akisema tuu mdomoni bila kuyaweka moyoni?

Naomba kutoa hoja ili ijadiliwe na wadau kwani matukio yanayotokea hapa nchini yananifanya niweze kurudi nyuma na kuanza kusoma ahadi na hotuba za viongozi wetu.

Wabunge wanastahili kuendele kuaminiwa na kuheshimiwa na wananchi?

Spika anatumia busara na hekima kwenye kuliendesha bunge?

Wabunge wote wanatendewa haki?
 
SALAMU ZA MWAKA MPYA ZA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TAN ZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, KWA WATANZANIA,
TAREHE 31 DESEMBA, 2007

Utangulizi

Ndugu Wananchi;

Leo imefikia siku ya kuuaga mwaka 2007 na kuukaribisha mwaka 2008. Naungana na Watanzania wenzangu tuliobahatika kufika siku hii ya leo kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa wema na rehema zake kwetu. Kwanza, tunamshukuru kwa kutujaalia uhai hivyo kutuwezesha kumaliza mwaka 2007 salama. Wapo wenzetu wengi hawakupata bahati hii. Pili, tunamshukuru kwa kuendelea kuijaalia nchi yetu amani, umoja na utulivu. Ametuvusha salama hata katika nyakati ambazo nchi yetu ilipitia katika mazingira magumu na tete. Tumuombe aijaalie nchi yetu baraka na neema tele mwaka ujao wa 2008.
Ndugu Wananchi;
Binafsi yangu, namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa mambo mawili. Kwanza, kwa kunijaalia uhai na afya njema, mimi na familia yangu. Pili, namshukuru kwa kuniongoza vizuri na kuniwezesha kuitumikia nchi yetu na nyinyi Watanzania wenzangu kwa salama na kwa uwezo wangu wote.
Napenda pia kuitumia fursa hii kuwashukuru tena wananchi wenzangu wote wa Tanzania kwa imani yenu kubwa kwangu na kwa kuendelea kuiunga mkono Serikali yetu. Uelewa wenu mzuri wa mambo mbalimbali ya nchi yetu, msaada wenu na ushirikiano wenu mzuri ndivyo vilivyotuwezesha kuzikabili vyema changamoto mbalimbali zilizoikabili nchi yetu katika mwaka huu tunaoumaliza leo. Naomba tuendelee hivyo katika mwaka 2008.

Mapitio ya Mwaka 2007 na Matarajio kwa Mwaka 2008
Ndugu Wananchi, Watanzania Wenzangu;
Mwaka tunaoumaliza leo kama ilivyokuwa mwaka jana 2006 ulikuwa na mambo mengi mazuri na ya mafanikio. Pia ulikuwa na magumu yake na changamoto zake. Napata faraja moyoni mwangu kwamba mambo mengi tuliyokusudia kuyafanya mwaka huu tumeweza kuyafanya tena mengi tumeyafanya kwa ufanisi wa kiwango cha kuridhisha.
Changamoto kuu nyingi nilizozizungumza katika hotuba yangu ya mwaka wa jana zimepatiwa ufumbuzi. Bahati mbaya changamoto moja ambayo haijapata ufumbuzi ni suala la bei kubwa ya mafuta ya petroli. Bei kubwa ya mafuta imekuwa chanzo kikubwa cha kuongeza ugumu wa maisha nchini. Siyo tu kwamba hatujapata ufumbuzi wake lakini ukubwa na ukali wa tatizo umekuwa mbaya zaidi sasa kuliko ilivyokuwa Desemba, 2006. Bei ya mafuta Desemba, 2006 ilikuwa dola 62.3 kwa pipa na mwezi huu wa Desemba, 2007 ni dola 97.12 kwa pipa. Bahati mbaya hatuna uwezo wa kuzifanya bei hizo zipungue. Lakini, lililo baya zaidi ni kuwa bei kubwa ya mafuta ndicho kichocheo kikubwa cha kuongezeka kwa gharama za maisha.

Hali ya Chakula
Ndugu Wananchi;
Mwaka huu hali ya chakula ilikuwa nzuri. Mavuno yalikuwa mazuri karibu nchi nzima na ilipatikana ziada ya nafaka. Sehemu ya ziada hiyo imenunuliwa na Hifadhi ya Chakula ya Taifa (SGR). Hadi kufikia tarehe 11 mwezi huu (Desemba) SGR ilikuwa na akiba ya tani 142,295.981 za chakula zikiwemo tani 135,129.646 za mahindi na tani 7,166,335 za mtama. Kazi ya ununuzi wa nafaka bado inaendelea katika baadhi ya mikoa yetu ikiwemo Iringa, Ruvuma na Dodoma.
Hali ya Mvua za Vuli
Ndugu Wananchi;
Hatuna budi kuwapongeza wakulima kwa kazi nzuri waifanyao. Kadhalika tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia mvua nzuri zilizoleta tija hii katika kilimo mwaka huu. Tuendelee kumuomba atujaalie mvua nzuri mwaka ujao 2008. Bahati mbaya mwaka huu mvua za vuli ambazo hunyesha kuanzia mwezi Oktoba hadi Desemba hazikuwa nzuri katika mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Pwani, Morogoro na Dar es Salaam. Hali hiyo itasababisha mazao ya vuli kuwa kidogo au kukosekana kabisa katika baadhi ya maeneo.
Aidha, inaashiria hatari ya kuwepo tatizo mwakani hasa iwapo mvua za masika nazo hazitakuwa nzuri katika mikoa hiyo. Hivyo tumuombe Mwenyezi Mungu ajaalie mvua za masika ziwe nzuri mwaka ujao. Napenda pia kutumia nafasi hii kuwasihi wakulima kutokukata tamaa kwa sababu ya kukosekana kwa mvua za vuli bali wajiandae kwa kilimo cha mvua za masika. Inshaalah Mwenyezi Mungu atujaalie rehema zake ili mwakani mvua ziwe nzuri.

Hali ya Uchumi
Kwa ujumla hali uchumi ilikuwa tulivu. Ni matarajio yetu kuwa lengo la uchumi kukua kwa asilimia 7.3 tutalifikia na kwamba mwaka ujao 2008 tutafikia asilimia 7.7 au zaidi. Mwelekeo wa ukusanyaji wa mapato ya serikali ni mzuri na wa kutia moyo. Bila ya shaka malengo yetu ya mwaka wa fedha 2007/08 tutayafikia. Thamani ya safari yetu imeendelea kuimarika. Mfumuko wa bei hata hivyo bado ni tatizo. Una mawimbi. Mfumuko wa bei umeongezeka kutoka asilimia 6.2 Novemba, 2006 hadi 7.3 Novemba, 2007. Kukabiliana na mfumuko wa bei bado ni changamoto kubwa ya kushughulikia mwaka 2008 ili gharama za maisha ziwe nafuu.
Natambua ugumu uliopo hasa kwa vile bei za mafuta ziko juu na dalili ya kushuka ni ndogo. Hata hivyo hatuna budi kuhakikisha kuwa uzalishaji wa chakula na bidhaa nyingine hapa nchini unaongezeka ili uhaba wake usije ukachangia kupanda kwa mfumuko wa bei kama ilivyokuwa kwa bei ya saruji hivi karibuni.

Maendeleo ya Elimu
Ndugu Wananchi;
Mwaka 2007 umeendelea kuwa mzuri kwa upande wa elimu. Elimu ya msingi tumefikia asilimia 97 ya watoto wenye umri wa kwenda shule kuwa darasani kutoka asilimia 96 mwaka 2006. Taarifa ya watoto kutofanya vizuri mtihani wa darasa la VII imenifadhaisha. Nakubaliana na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi kuwa tufanye uchunguzi wa kina na makosa yarekebishwe.
Kata nyingi nchini zimeendelea kutekeleza mpango wa ujenzi wa shule za sekondari za kata. Kwa ajili hiyo shule mpya 1,090 zimesajiliwa na jumla ya watoto 448,448 wameweza kujiunga na elimu ya sekondari kote nchini. Idadi hii ambayo inajumuisha wanafunzi katika shule za Serikali na binafsi ni kubwa kuliko ya mwaka 2006 ambayo ilikuwa 345,441.
Wakati tukiwapongeza wananchi na viongozi kwa mafanikio haya, napenda kuahidi kuwa Serikali inatambua wajibu wake kuhusu upatikanaji wa walimu, vitabu na vifaa vya maabara na vingine vya kufundishia. Tunaahidi kuwa tutaendelea kutimiza wajibu wetu katika mwaka ujao 2008 kama tulivyofanya mwaka huu. Kubwa zaidi ni makusudio yangu kufanya tathmini ya mpango mzima wa upanuzi wa elimu ya sekondari nchini kwa kushirikisha wadau. Lengo la tathmini hiyo ni kupima mwendo wetu: tulipo sasa na kule tuendako ili tuwe na mikakati na mipango bora zaidi.
Kwa upande wa elimu ya juu, nafurahi kwamba chuo Kikuu cha Dodoma kimeanza. Bado tunayo kazi kubwa ya kukijenga. Tutaendelea kwa kasi zaidi mwaka ujao. Katika mwaka ujao pia ni makusudio yetu kulifuatilia kwa karibu suala la mikopo ya wanafunzi kwa nia ya kurekebisha kasoro zilizopo.

Huduma ya Afya
Ndugu Wananchi;
Mwaka ujao tunatarajia kuanza utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi. Mpango ambao shabaha yake ni kusogeza huduma ya afya karibu na wanapoishi watu. Utekelezaji wake utaongeza zahanati vijijini na vituo vya afya katika Kata. Kufanikiwa kwa mpango huu kunategemea ushirikiano wa wananchi. Nawaomba wananchi wenzangu tutumie maarifa yale yale tuliyoyatumia kufanikisha ujenzi wa Sekondari kufanikisha mpango huu.

Hali ya Kisiasa
Ndugu Zangu, Watanzania Wenzangu;
Tunaumaliza mwaka 2007 nchi ikiwa tulivu kisiasa na hali ya amani na usalama imeendelea kutawala. Nawashukuru viongozi na wanachama wenzangu wa vyama vya siasa kwa kudumisha utamaduni wa kushindana bila kupigana. Huo ndiyo msingi mama wa demokrasia ya vyama vingi. Kukingiana ngumi, kupigana au kufanya ghasia ni matendo yaliyo kinyume na misingi ya demokrasia. Tuzidi kumuomba Mungu aendelee kutuwezesha kudumisha utamaduni huo na nchi yetu iendelee kuwa kisiwa cha amani barani Afrika.
Nachelea kutukanana, kupakana matope na kudhalilishana kusije kuwa sehemu ya utamaduni wa siasa za Tanzania. Tutakuwa tumejifikisha mahali pabaya na kuifanya shughuli ya siasa kukosa thamani. Siasa ni shughuli tukufu lazima iendeshwe kwa misingi hiyo. Kutukanana ni kinyume cha utukufu huo.
Ndugu Wananchi;
Kama nilivyoahidi katika salamu zangu za mwaka mpya mwaka jana, tumedhamiria katika mwaka 2008 kuendelea kujenga mahusiano mazuri ya kisiasa na kijamii ili kuimarisha umoja, maelewano na mshikamano miongoni mwetu. Kwa sababu za msingi kabisa karibu mwaka wote huu tumeutumia kwa mazungumzo kati ya CCM na CUF. Nia yetu ni kumalizia haraka pale paliposalia katika mazungumzo hayo. Aidha, baada ya hapo tuwe na mawasiliano ya karibu na vyama vingine vya siasa. Yapo mengi ya kuzungumza kwa maslahi ya nchi zetu na vyama vyetu.

Hali ya Usalama
Ndugu Zangu, Wananchi Wenzangu;
Hali ya usalama wa nchi yetu nayo imeendelea kuwa nzuri. Navipongeza vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwa kazi kubwa na nzuri waifanyayo ya kulinda mipaka na uhuru wa nchi yetu pamoja na mali ya raia wa Tanzania. Vita dhidi ya ujambazi imeimarika na mafanikio yanazidi kupatikana. Ingawa bado kuna matukio ya ujambazi ya hapa na pale lakini Jeshi la Polisi sasa limejenga uwezo mzuri wa kukabiliana na uhalifu huo.
Katika mwaka tunaouanza kesho tumedhamiria kuimarisha zaidi Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya dola katika mapambano dhidi ya ujambazi, biashara ya madawa ya kulevya, rushwa na vitendo vingine vyote vinavyotishia amani na usalama wa watu wetu.
Ndugu Wananchi;
Miongoni mwa mambo yaliyonisikitisha sana mwaka huu ni ongezeko la makosa ya ubakaji, mauaji na ajali za barabarani. Hadi Novemba, 2007 makosa ya ubakaji yalikuwa yameongezeka na kufikia 8,000 kutoka 3,946 mwaka 2006. Makosa ya mauaji yaliongezeka kutoka 2,309 mwaka 2006 hadi 3,144. Makosa ya ajali za barabarani yaliongezeka kutoka 15,560 mwaka 2006 hadi 15,650 mwaka 2007.
Ubakaji
Chanzo kikuu cha makosa ya ubakaji ni mmong’onyoko wa maadili mema ya kijamii kuhusu mapenzi. Wakati mwingine ni imani za ushirikina hasa imani za kipuuzi ati mfanyabiashara ukifanya mapenzi na watoto wadogo au akiwa na viungo vya mtoto au albino anaongeza utajiri. Tatizo la kuongezeka kwa ubakaji na mauaji kwa imani za kishirikina ni mambo ambayo yanahitaji mkakati maalum wa kijamii kukabiliana nayo. Sheria zilizopo zina adhabu kali za kutosha kwa makosa yote mawili. Pengine elimu itakayoondoa imani potofu hizi itasaidia. Shime sote, wanawake kwa wanaume, wazee kwa vijana, tufanye kila tuwezalo kuelimisha jamii kuhusu ubaya na ukatili wa vitendo vya ukabaji.

Mauaji
Kwa upande wetu, kuhusu mauaji yanayotokana na imani za ushirikina, Jeshi la Polisi litafanya kazi ya kutambua mitandao ya uhalifu huu kwa nia ya kuivunja. Mkakati huu unalenga kutambua waganga wa kienyeji wanaopotosha watu wanapofiwa au kuuguliwa kuhusu kurogwa kwa wagonjwa wao na kutambua wachawi wao. Aidha, kutambua waganga wanaodai kuwa na uwezo wa kuwaongezea watu utajiri au bahati kwa njia ya kuua watu wa aina fulani katika jamii au kupata baadhi ya viungo vya wanadamu. Kadhalika mkakati huo unalenga kutambua na kuvunja mitandao au makundi ya watu wanaokodishwa kuua watu wengine.
Ajali za Barabarani
Ndugu Wananchi;
Ajali za barabarani ni nyingi mno na hasara yake ni kubwa kwa taifa. Katika mwaka ujao tuchukue hatua thabiti zitakazosaidia kupunguza ajali za barabarani hasa zinazosababishwa na uzembe wa madereva, magari mabovu yasiyostahili kuwa barabarani na usimamizi usioridhisha kwa upande wa wahusika. Miongoni mwa hatua ambazo hatuna budi kuchukua ni pamoja na zifuatazo:

(a)Kuhakikisha kuwa mtu anayepewa leseni ya kuendesha gari amepata mafunzo stahiki katika taasisi au vyombo vinavyotambulika. Tuache udereva wa kubahatisha.
(b)Madereva wazembe na wale wenye kumbukumbu za kuwa wakosaji sugu wafutiwe leseni za udereva wanapokutwa wamefanya kosa. Namtaka Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mkuu wa Jeshi la Polisi walifanyie kazi agizo hili. Kama hapana budi sheria za sasa zifanyiwe marekebisho au sheria mpya itungwe.
(c)Kuhakikisha kuwa magari yanayotembea barabarani yana kiwango stahiki cha uzima. Magari mabovu na yasiyokuwa na sifa stahiki yasiruhusiwe kutembea barabarani.
(d)Wahusika na usimamizi wa sheria za usalama barabarani na uendeshaji wa shughuli za usafirishaji watimize ipasavyo wajibu wao. Hapa nina maana ya kwanza, Polisi wa Usalama Bararani (Traffic Police) wawe wakali, waache mazungumzo na madereva wazembe na wahalifu nyuma ya magari. Wanaofanya hivyo wachukuliwe hatua mara moja. Pili ni SUMATRA watimize ipasavyo wajibu wao kuhusu usalama wa vyombo vya usafirishaji wa abiria na mizigo. Na tatu, TANROADS wahakikishe ubora wa barabara hasa katika maeneo ambayo ajali hutokea mara kwa mara.

Mapambano Dhidi ya UKIMWI
Ndugu Zangu, Watanzania Wenzangu;
Napenda kuelezea furaha na shukrani zangu kwa jinsi watu walivyoitikia Kampeni ya Upimaji Virusi vya UKIMWI kwa hiari. Hadi kufikia tarehe 15 Desemba, 2007 kwa nchi nzima watu 3,004,701 walikuwa wamepima, kati yao wanaume ni 1,365,926 na wanawake ni 1,638,775. Hii inaamaanisha kuwa asilimia 72 ya lengo limefikiwa. Jambo la kutia moyo ni kuwa watu wanazidi kujitokeza. Inaelekea ujumbe sasa umewafikia wengi.
Matokeo ya upimaji yametupa taarifa nzuri kuhusu hali ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI nchini. Taarifa inaonyesha kuwa kiwango cha maambukizi ni asilimia 4.9 badala ya asilimia 7 ya mwaka jana. Hili ni jambo jema lakini bado asilimia 4.9 ya Watanzania kuwa wameambukizwa virusi vya UKIMWI ni kubwa mno. Hatuna budi kuendelea kuwa makini na kuchukua tahadhari stahiki.
Nawaomba ndugu zangu tuazimie kuwa katika mwaka ujao tutazidisha mapambano dhidi ya maradhi haya. Kwa wale ambao hawajapima wajitokeze kupima. Pili, kwa wote kuamua kwa dhati kuepuka kupata maambukizi. Bado naamini na napenda sote tuamini hivyo kuwa Tanzania Bila UKIMWI inawezekana.

Uhusiano wa Kimataifa
Ndugu Wananchi;
Mwaka 2007 ulikuwa mwaka wa mafanikio makubwa kwa Tanzania katika medani ya kimataifa. Tumeshuhudia Watanzania kadhaa wakipata nafasi za juu katika vyombo vya kimataifa. Tulianza mwaka vizuri kwa kushuhudia dada yetu Dr. Asha-Rose Migiro akiteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na kuchukua nafasi yake Februari, 2007. Ilikuwa fahari kubwa kwa nchi yetu na heshima kubwa kwake na taifa letu. Tuendelee kumuombea na kumuunga mkono afanikiwe. Mpaka sasa mambo yanakwenda vizuri. Anaibeba vizuri heshima ya Afrika na Tanzania.
Ndugu Wananchi;
Uhusiano wetu na wabia wetu wa maendeleo uliendelea kuimarika. Imani yao kwa Serikali na nchi kwa ujumla iliendelea kuwa nzuri. Tumepata mafanikio ya kutia moyo kwa upande wa misaada ya maendeleo na msamaha wa madeni. Ukilinganisha na mwaka 2006 misaada ya maendeleo imeongezeka kutoka shilingi trilioni 1.9 hadi shilingi trilioni 2.5 mwaka huu wa fedha 2007/2008.
Kwa upande wa Marekani tunafurahi kwamba mchakato uliotuchukua miaka miwili ulikamilika Desemba 12, 2007, baada ya Bodi ya Mfuko wa Milenia wa Serikali ya Marekani kufanya uamuzi wa mwisho na kuafiki Tanzania ipate msaada wa dola 698 milioni. Kinachosubiriwa sasa ni Bunge la Marekani kutenga fedha hizo ili Januari, 2008 zipatikane na utekelezaji uanze wa miradi iliyokusudiwa ya miundombinu ya barabara, maji na umeme. Msaada huo utatusaidia sana kutatua matatizo ya barabara mikoa ya Ruvuma, Rukwa, Tanga na Zanzibar. Pia itatumalizia tatizo la umeme Kigoma na Kasulu. Vile vile itatupunguzia matatizo ya maji katika miji na maeneo kadhaa.
Ndugu Wananchi;
Kwa upande wa misamaha ya madeni nafurahi kusema kuwa mwaka huu umekuwa mzuri. Juhudi zetu za kupata misamaha ya madeni tunayodaiwa na baadhi ya nchi au taasisi zimeweza kuzaa matunda ya kutia moyo. Tumepata msamaha mkubwa wa madeni kutoka Serikali ya Japani pale Januari 30, 2007 walipoamua kutusamehe deni la karibu shilingi bilioni 595.5.
Tatizo kubwa kwa upande wa kutafuta msamaha wa madeni ambalo bado tunalo ni kwa nchi na taasisi za nchi ambazo si wanachama wa Paris Club. Nchi hizo ni Iran, Iraq, Algeria na Brazil ambazo kwa pamoja wanatudai kiasi kinachofikia dola bilioni moja.
Ni makusudio yangu na wenzangu Serikalini kuwa mwaka ujao tuelekeze nguvu zetu za mazungumzo katika nchi hizo kutafuta nafuu ya madeni hayo. Kwa hakika ni makubwa mno na uwezo wetu wa kulipa ni mdogo.

Wenyeji wa Mikutano ya Kimataifa
Ndugu Wananchi;
Kutokana na sifa na heshima tuliyojijingea, mwaka 2008 nchi yetu imepata heshima ya kuwa mwenyeji wa mikutano mitatu mikubwa na muhimu ya kimataifa. Mikutano hiyo ni:

(a)Mkutano wa Uzinduzi wa Shughuli za Mwaka wa Sayari Dunia kwa Bara la Afrika.
(b)Mkutano wa Utalii wa Bara la Afrika; na
(c)Mkutano wa Nane wa Sullivan.

Mikutano hiyo kufanyika hapa nchini ni jambo la faraja kubwa. Mikutano hiyo ina hadhi kubwa kimataifa, inashirikisha watu wengi na kuvutia macho na masikio ya dunia pamoja na vyombo vya habari vya kimataifa pale inapofanyikia. Hivyo basi kwetu sisi ni fursa nzuri ya kuitanganza nchi yetu kwa utalii na uwekezaji. Pamoja na hayo ni ukweli kwamba watu wapatao 4,000 watakaoshiriki wanaongeza mapato ya utalii kwa taifa letu.
Napenda kuitumia nafasi hii kuwaomba Watanzania wenzangu kujiandaa vyema kuwapokea wageni wetu hao. Watanzania tunayo sifa ya ukarimu, naomba tuendelee kuionyesha kwa wageni wetu hawa. Tunatarajia ushiriki wa Wakuu wa Nchi na Serikali katika shughuli ya Uzinduzi wa Mwaka wa Sayari Dunia na Mkutano wa Nane wa Sullivan.
Mkutano wa Sullivan ni jukwaa linalokutanisha Waafrika walioko Barani Afrika na ndugu zao wenye asili ya Kiafrika walioko Marekani. Katika mikutano ya Sullivan washiriki huzungumzia masuala ya kuinua maendeleo ya Bara la Afrika kwa uwekezaji, biashara, elimu na teknolojia. Mwaka huu agenda kuu ni kuendeleza utalii, miundombinu na hifadhi ya mazingira, mambo ambayo yana umuhimu wa aina yake kwa maendeleo ya Tanzania.

Mwaka wa Sayari Dunia
Ndugu Wananchi;
Mwaka 2005 Umoja wa Mataifa ulitanganza kuwa mwaka 2008 utakuwa Mwaka wa Sayari Dunia kufuatia uamuzi uliofanywa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa katika kikao chake cha 60 mwezi Desemba, 2005. Chimbuko la uamuzi huo ni pendekezo la Tanzania lililowasilishwa na kukubaliwa kwanza na Mkutano Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) mapema mwaka 2005 na baadaye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Uzinduzi wa shughuli za Mwaka wa Sayari Dunia utafanyika kwa awamu mbili. Awamu ya kwanza itakuwa ni uzinduzi wa kimataifa utakaofanyika Paris, Ufaransa kwenye Makao Mkuu ya UNESCO mwezi Februari, 2008. Awamu ya pili itakuwa ni kwenye ngazi ya kanda. Kwa kanda ya Afrika nchi yetu Tanzania imeteuliwa kuwa mwenyeji wa shughuli hiyo kunako Mei, 2008.
Ndugu Wananchi;
Sisi Watanzania tunao wajibu maalum katika jambo hili. Kwanza kwamba sisi ndiyo tuliobuni wazo hili na wenzetu wakatukubalia. Isitoshe Rais Mstaafu Mheshimiwa Benjamin Mkapa ndiye Mlezi wa Mwaka wa Sayari Dunia. Pili, sisi tumepewa dhamana ya kuwa wenyeji wa sherehe maalum za uzinduzi wa Mwaka wa Sayari Dunia. Kwa sababu hizo lazima Watanzania tuwe mstari wa mbele katika utekelezaji wa malengo ya Mwaka wa Sayari Dunia. Aidha, tuhakikishe kuwa shughuli ya uzinduzi wa Mwaka wa Sayari Dunia kwa Kanda ya Afrika itakayofanyika hapa kwetu inakuwa na mafanikio makubwa.

Madhumuni ya Mwaka wa Sayari Dunia
Ndugu Wananchi;
Madhumuni ya kuwa na Mwaka wa Sayari Dunia ni kutoa fursa kwa mwanadamu kuichambua na kuitafakari kwa kina hali ya dunia tunayoishi kwa nia ya kujiweka tayari kuchukua hatua za kuifanya kuwa mahali salama na bora pa kuishi. Lengo la kufanya uchambuzi na tafakuri hizo ni kwanza, kutambua kwa ufasaha mazuri, mabaya na changamoto zilizopo. Na pili, kutafuta njia muafaka ya kukabili changamoto hizo kwa maana ya kudumisha na kuendeleza mazuri upande mmoja na kurekebisha kasoro upande mwingine.
Ni ukweli usiofichika kwamba hali ya sasa ya mazingira ya dunia hairidhishi na muelekeo wake si mzuri hata kidogo. Mazingira yamechafuka sana. Kama hatua madhubuti za kurekebisha mambo hazitachukuliwa sasa, hali itakuwa mbaya zaidi katika miongo michache ijayo. Wanadamu na viumbe vingine watakosa mahali palipo salama pa kuishi na hata uhai wao unaweza kutoweka. Ukweli ni kwamba baadhi ya viumbe tayari vimeshatoweka.
Ndugu Wananchi;
Matendo yetu na shughuli zetu wanadamu ndicho chanzo cha madhara ya kimazingira yanayoisibu dunia yetu leo. Mwanadamu hana budi kubadilika. Aache tabia na matendo yake mabaya na kuchukua hatua za kurekebisha makosa na kuboresha mazingira ya Sayari Dunia. Matumizi ya maarifa ya sayansi dunia yamesisitizwa katika kufanya uamuzi na utekelezaji wake.
Kutakuwepo na programu maalum ya kuelimisha jamii inayolenga pia wanasiasa na watu walioko kwenye nafasi za kutoa maamuzi. Lengo ni kuwapa maarifa ya elimu ya sayari dunia na jinsi ya kuitumia kujiletea maendeleo na kuinua kiwango cha ubora wa maisha ya wananchi. Mafunzo maalum yatatolewa kwa waandishi wa habari na walimu kuhusu mambo yahusuyo Sayari Dunia na mazingira ili wao wasaidie kuelimisha jamii pamoja na vijana mashuleni.
Mabadiliko ya Tabia-Nchi
Ndugu Wananchi;
Miongoni mwa mambo muhimu yatakayochambuliwa na kutafakariwa katika Mwaka wa Sayari Dunia ni suala la mabadiliko ya tabianchi (Climate Change) au mabadiliko ya hali ya hewa kama wengi tulivyozoea. Nafurahi kwamba suala hili litapewa uzito unaostahili kwani unapozungumzia uharibifu wa mazingira kielelezo chake na kiini chake pia ni mabadiliko ya tabianchi.
Ndugu zangu, Wananchi Wenzangu;
Hakika mabadiliko ya tabianchi ni tishio kubwa kwa maisha na uhai wa mwanadamu. Walio hatarini zaidi ni sisi katika nchi maskini kwa sababu ya uwezo mdogo wa rasilimali, utaalamu na teknolojia za kukakabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Lakini hata hizo nchi zilizoendelea nazo ziko mashakani kwani hata kwao majanga ya asili yameongezeka. Isitoshe duniani tunategemeana: athari ya upande mmoja hugusa upande mwingine.
Ndugu Wananchi;
Chanzo kikuu cha mabadiliko ya tabianchi ni kuongezeka kwa joto duniani. Kuongezeka kwa joto duniani kunasababishwa na kuongezeka kwa gesijoto (greenhouse gases) kwa kiwango kikubwa mno kuliko kinachohitajika kuwezesha uhai na mifumo ya dunia kuwa katika hali yake ya asili.
Gesijoto husika hapa hasa ni gesimkaa (carbon-dioxide), methani (methane) na nyinginezo ambazo zinatokana na shughuli za mwanadamu katika kujiletea maendeleo. Shughuli kuu zinazohusika kuzalisha gesijoto kwa wingi ni viwanda, vyombo vya usafirishaji, ufyekaji misitu, uchomaji moto ovyo (mioto kichaa) na kilimo kisichoendelevu. Ili kuinusuru dunia na madhara ya mabadiliko ya tabianchi, mwanadamu hana budi achukue hatua za kuzuia kuongezeka zaidi kwa gesijoto duniani na kupunguza kiasi cha gesijoto kilichopo sasa ili kirejee kwenye viwango salama.
Huo ndiyo wajibu wa nchi zetu na watu wote duniani. Kufanya hayo ndiyo madhumuni na maagizo makuu ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (The UN Framework Convention on Climate Change) wa mwaka 1992 na Itifaki ya Kyoto (Kyoto Protocol) ya mwaka 1997.
Ndugu Wananchi;
Athari za mabadiliko ya tabianchi na sisi tumezipata na tunaendelea kuzipata. Misimu ya mvua haitabiriki siku hizi. Majanga ya mafuriko na ukame yameongezeka. Tunazikumbuka athari za mafuriko ya mvua za El-Nino za mwaka 1997/98. Tunakumbuka adha ya ukame wa 1993/94 na wa 2005/06 ambao ulikuwa mkali kuliko wowote uliowahi kuikumba nchi yetu kwa miaka mingi.
Theluji katika kilele cha Mlima Kilimanjaro inazidi kupungua. Wataalamu wanasema kuwa mlima wetu huo umepoteza asilimia 80 ya theluji yake katika kipindi kifupi cha miaka 50 iliyopita. Kina cha maji katika Ziwa Victoria kimepungua kwa mita 2.57 kati ya mwaka 1965 na 2006. Kisiwa cha Maziwe katika pwani ya Pangani kimezama kutokana na kuongezeka kwa usawa wa bahari.
Aidha, visima vya maji baridi katika baadhi ya maeneo ya Pwani kama vile Bagamoyo havitumiki tena kwa sababu ya kuongezeka kwa maji ya bahari. Maradhi ya malaria sasa yameenea hata katika maeneo ya milimani na yenye baridi kama vile Lushoto, Amani, Rungwe na Kitulo ambako zamani hayakuwepo. Sababu ni ongezeko la joto linalowezesha mbu kuishi.
Ndugu zangu;
Orodha ya mambo yanayodhihirisha athari za mabadiliko ya tabianchi hata hapa kwetu ni ndefu itoshe leo kutaja hayo. Lakini la muhimu ni kuwa tunao wajibu na sisi kama walio nao wenzetu wa mataifa yaliyoendelea wa kuchukua hatua za kuzuia ongezeko la joto na kupunguza kiasi cha joto kilichopo. Tunao wajibu wa kuzuia uharibifu wa mazingira na kuboresha palipo haribika.
Mengi ya yale tunayowajibika kufanya yamo katika maudhui ya nyaraka kuu tatu:

(a)Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004;
(b)Mpango wa Taifa wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (National Adaptation Programme of Action) 2006; na
(c)Mkakati wa Kuhifadhi Mazingira ya Ardhi na Vyanzo vya Maji (2006).

Hivi sasa Serikali iko mbioni kuandaa Waraka wa nne yaani Mkakati wa Hatua za Haraka za Kuhifadhi Mazingira ya Ukanda wa Pwani, Maziwa, Mito na Mabwawa.
Mimi naamini tukitekeleza ipasavyo yaliyoagizwa katika mipango na mikakati hiyo Tanzania itakuwa nchi salama kuishi sisi na vizazi vijavyo. Haya shime tutekeleze. Wakati ni huu. Hatuna muda zaidi wa kupoteza. Napenda kusisitiza kuwa katika kufanikisha malengo ya Mwaka wa Sayari Dunia tuazimie kuwa huo uwe ndiyo mchango wetu mkubwa.
Hitimisho
Ndugu Wananchi; Watanzania Wenzangu;
Napenda kuhitimisha salamu zangu za mwaka mpya kwenu kwa kuwashukuru tena nyote kwa imani yenu kubwa kwangu na kwa serikali ninayoiongoza. Mimi na wenzangu serikalini tunafarijika sana kwa ushirikiano mkubwa mnaotupa katika utekelezaji wa jukumu letu la msingi la kuwatumikia.
Tunapouanza mwaka mpya kesho, nataka kuwahakikishia tena kuwa tumedhamiria kwa dhati kuwatumikia kwa moyo wetu wote na nguvu zetu zote. Tutajitahidi kwa kadri ya uwezo aliotujaalia Mwenyezi Mungu kushirikiana nanyi katika kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa matatizo yanayolikabili taifa letu na kuimarisha kasi ya kuleta maendeleo nchini mwetu. Naamini kwa pamoja tutashinda.
Baada ya kusema hayo, nawatakieni nyote heri na fanaka ya mwaka mpya 2008. Sote tusherehekee kwa amani na utulivu.

Mungu Ibariki Afrika;
Mungu Ibariki Tanzania.
Asanteni kwa kunisikiliza.
 
Back
Top Bottom