Hoteli ya kitalii Arusha hali tete

Hoteli ya kitalii Arusha hali tete

Mh Mkuu wrong track vyumba 300 na high season hii? Utalii ume shuka Sana,Kigwangalla anajua utalii ni anti porching tuu maana naona yeye na majangili tuu sioni jitihada zake kuufufua utalii,au sio kipaumbele cha awamu hii
wizara nyeti kama ile umakwenda kumpa kigwangwala !!! nikulivunjia nidhamu taifa
 
Kwa Arusha ni kawaida kabisa,maana hapa nchini tuna hotel 11 ambazo ni Five Star,ambapo 6 kati ya hizo ziko jijini Arusha,4 ziko Zanzibar na 1 iko Dar-es-salam.

Hope so, nimeshatajiwa Ngurdoto mkuu.

Ila issue ya kuwa 5-Star hairelate na idadi ya vyumba mkuu.
 
Inawezekanaje mtu unafanya biashara ya hotel au lodge unashindwa kuniweka kwenye standard ya kimataifa nilala lodge moja mkoa mmoja niling'atwa na kunguni hata baada ya kubadilishiwa chumba niling'atwa na kunguni tena . Hawa wenye haya ma biashara ya hotel na lodges wakishindwa kuziendesha waziuze au wapangishie.Hyatt Regency Arusha arusha ikifunguliwa tena hao jamaa si watasaulika.
 
Hiyo hoteli tangu mmliki wake afariki imekuwa shamba la bibi... Hakuna kiendacho sawa.. Tusiweke siasa kwenye hili wenyewe wameshindwa kuiendesha. Huduma mbaya!!
Si waikodishe au waiuze, huduma nzuri na murua ndio utambulisho na kioo cha biashara.
 
Idadi ya vyumba na namba za vyumba ni vitu viwili tofauti Mkuu.

Wakisema mia tatu wanamaanisha vyumba mia tau hata kama utakutana na room namba 702, 810 n.k.
Mimi nilifanya kaz hotel.hio 11 yra ago, ni kweli ina vyumba 300, tena huyo manager katoa idadi ya vyumba vya kawaida. Nikimaanisha standars rooms and delux rooms,,,kuna presidential rooms pale ambazo ziko 7, ni za marais tuu na huwa hawa shei
 
Kuwekeza kunahitaji zaidi ya yote kusoma nyakati, hasa mazingira ya kisera (policy environment) ya Chama Tawala na Serikali yake.

Rais Magufuli alipoingia madarakani anatimiza ahadi yake wakati wa kampeni kuwa nchi ni Tajiri ila fedha za Serikali zinaliwa/kuchezewa na wachache. Kauli yake ya kwanza alipoingia madarakani alisema wazi kuwa kuna watu wanafanya biashara kwa fedha za Serikali badala ya kufanya biashara kwa kwa fedha yao wenyewe inayozalishwa kibiashara.

Hoteli hiyo, naamini ilijengwa wakati shughuli nyingi za Serikali na Taasisi zake, hasa kubwa, zilifanyika Arusha, na ikawa ndiyo mahala pa Wakubwa kujinafasi.

Wakati ukuta, mwenye hoteli anapaswa kurudi kwenye meza ya mipango ajipange upya, kwa miaka 8 iliyobaki ya utawala wa Serikali inayoongozwa na Dr Magufuli.

Mwekezaji, wala mashabiki wa kisiasa wasije na lawama, kwa kuwa uamuzi wa kuwekeza ni wa mwekezaji na siyo Serikali. Serikali huweka mazingira rafiki ya uwekezaji.o
Mbona Magufuli yeye anafanya biashara ya korosho kwa kutumia fedha za serikali? Ina maana ameanza kula matapishi yake?
 
Nimemuona na kumsikia Meneja wa moja ya Hoteli kubwa na maarufu ya Kitalii ya Arusha kwenye taarifa ya habari usiku huu anasema/anajitetea kwa Maofisa wa Serikali kuwa Hoteli ile ina vyumba mia tatu (300) na hakuna Mgeni hata mmoja pale ndani.

Sasa nimejiuliza ni kwamba wao ndio hawapo kwenye right track ama?

Hoteli ya Kitalii inakuwaje na isiyo ya Kitalii inakuwaje..?
 
Muwe mnasoma reviews kujua kwanini biashara inaanguka.. Meneja anayejua kazi angekaa chini kwanza na kuangalia yasiyo sawa hotelini na sio kulalamika huku hoteli imejaa majanga..
Kama ni wewe jiongezeni huko.. msilaumu yasiyo huku chanzo ni hapo hotelini..
Reviews nyingi za trip advisor huwa ni negative, kwa Hotel nyingi sana utapata hivyo.

Isitoshe mpaka Mgeni aingie kule ku comment ni baada ya kuchafuka, ni mara chache Wanaofurahia kuingia huko.
 
Mh Mkuu wrong track vyumba 300 na high season hii? Utalii ume shuka Sana,Kigwangalla anajua utalii ni anti porching tuu maana naona yeye na majangili tuu sioni jitihada zake kuufufua utalii,au sio kipaumbele cha awamu hii
aisee kumbe umeona,jamaa sijaona plan zake katika kuitangaza utalii,japo analofanya ni jema
 
Hotel nyingi Arusha,Moshi hazina wageni hasa hizi za kitalii,hali ni mbaya sana.

Kuna baadhi zinapata wageni kumi kwa wiki,unalipa mishahara kwa wafanyakazi,kodi,maji,umeme,NSSF na kwingineko,kwa nini wasifunge hizo hotel?
 
Hotel nyingi Arusha,Moshi hazina wageni hasa hizi za kitalii,hali ni mbaya sana.

Kuna baadhi zinapata wageni kumi kwa wiki,unalipa mishahara kwa wafanyakazi,kodi,maji,umeme,NSSF na kwingineko,kwa nini wasifunge hizo hotel?
Sasa utashangaa Waswahili wanakimbilia kusoma reviews za Trip Advisor kuhalalisha hali mbaya ya uwepo wa Watalii/Wageni.

Ili hali Hoteli hiyo hiyo imekuwa na sifa zote muhimu za kupokea Wageni miaka michache iliyopita.
 
Meku hata pale naura hawana hivyo vyumba mkuu. Mount meru hawazid 100 na kitu. Hiyo yenye vyumba 300 itakuwa ya kona ipi jomba?
Ila jana ilionekana ITV wakati watu wanaoshughulikia mambo ya Vibali vya kazi hasa kwa wageni,walipotembelea hotel husika,Meneja pamoja na mambo mengine aliyohojiwa akagusia kwa kusema Hotel yake ina vyumba 300 na kwa wakati huo hakukua na mteja hata mmoja.
Source ITV News-Saa 2 usiku(13-11-2018)
 
Back
Top Bottom