Hospitali ya Taifa Muhimbili-Lloganzila kuanza kupandikiza figo

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Baada ya uwekezaji na uwezeshaji mkubwa kutoka Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila inatarajiwa kuingia katika historia tarehe 13/04/2023 kwa kuwa miongoni mwa Hospitali zinazotoa huduma ya kupandikiza Figo hapa nchini Tanzania.

Awali Hospitali hiyo ilikuwa ikitoa huduma ya Kusafisha damu (Dialysis) pamoja na kutoa huduma ya matibabu ya kuvunja mawe kwenye Figo na mfumo wa mkojo kwa njia ya mawimbi mshtuko/mtetemo bila kumpasua mgonjwa ambapo mgonjwa anaweza kutibiwa wa siku moja akisubiria mawe hayo yapasuke na kutoka kwa njia ya haja ndogo.

Hapa nchini Hospitali kadhaa ikiwemo Hospitali ya Taifa Muhimbili-Dar es Salaam na Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma ni miongoni mwa Hospitali zinazotoa huduma ya kupandikiza figo.

Pia Hospitali hiyo ya Muhimbili-Mloganzila ipo katika hatua za mwisho katika kuanza kutoa huduma ya kupandikiza Kizazi na Ini.
Mloganzila1.jpeg
 
Hospitali hii huku mikoani inajulikana kama chinja chinja
Kwa vile hawafahamu ni magonjwa gani yanatibiwa hapo. Hiyo sio Hospital ya maralia fikiria wagonjwa wa figo, stroke, ini, na mengine kama hayo internal medicine halafu linganisha na zinazotibu maralia
 
..tujielekeze kwenye kujikinga na magonjwa makubwa-makubwa yanayohitaji huduma za gharama kubwa.

..tuwaelimishe wananchi kuhusu VYAKULA / VINYWAJI wanavyotumia na athari za kiafya wanazoweza kuzipata.
Wizara ya Afya inatakiwa ipambane na matumizi holela ya energy drinks.
 
Ni habari njema na ni hatua kubwa katika sekta ya afya.

Shida ya mloganzila bado kuna matatizo kwenye utendaji,

kulingana na unyeti wa hospitali hiyo nashauri uongozi na hata wizara lazima wahakikishe watumishi katika hospitali hiyo wanakidhi sifa weledi na uadilifu,

maana kuna wakati unakutana na madaktari. Wanafunzi ndio wanatoa huduma bila hata ya usimamizi wa mtaalamu aliye fuzu.

Tuache kabisa kuharibu taswira ya hospitali ya Taifa Mloganzila, ifahamike kuwa ni hospitali muhimu na nyeti sio tu kwa watanzania bali hata kwa mataifa mengine JIRANI hivyo lazima tujenge hiyo credibility.
 
Back
Top Bottom