Hongera sana Jerry Silaa. Naona mwanzo wa nchi yetu yote kupimwa na kupangwa chini yako

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Kama kuna jambo linalonifanya kila siku niseme inawezekana nchi yetu tulilaaniwa ni namna ambavyo nchi yetu imejengwa vibaya bila mpangilio. Yaani namna watu wanavyojijengea hovyo hovyo tu bila mpangilio na kupangwa.

Kila siku tumekuwa tukiandika humu na kusema humu huku titicaca Serikali ichukue hatua ila kwa muda ilikuwa ni kama kumpigia mbuzi gitaa.

Kwa namna Waziri Jerry Silaa alivyoanza kulishughulikia hili jambo napenda kumwambia kwa akili zangu zote kuwa ametufurahisha sana watu wenye akili tuliokuwa tunalipigia kelele hili jambo.

Najua watanzania wanapenda sana uholela na najua kwa wengi kuishi eneo lililopangwa na kupimwa vizuri wanaona ni kama kitu kigeni na cha kitajiri sana hivyo kutopenda.

Nichachopenda kuwaambia watanzania kila mtu ana haki na kustahili kuishi katika eneo lililopangwa na kupimwa vizuri. Hii sio haki ya watu wachache kama wanavyodhani hivyo ili nchi yetu kuwa na mpangilio mzuri ni lazima sasa waiunge mkono Serikali kuhakikisha nchi yetu yote inapimwa na kupangwa vizuri ili tuondokane na takataka za ujenzi holela.

Mwisho kwa Jerry Silaa naomba usiishie kutoa matamko tu. Sasa uje na mpango na utekelezaji wake katika kuhakikisha nchi yetu yote inapimwa na kupangwa vizuri. Weka fedha, weka mfumo tuondokane na aibu za kuishi kama wadudu na nchi yetu kuwa ya hovyo. Unaenda vizuri na kuanzia sasa nitazidi kukuombea ili usiondolewe katika Uwaziri wa Ardhi na tutimize ndoto ya nchi yetu kupimwa na kupangwa yote.
 
Kama kuna jambo linalonifanya kila siku niseme inawezekana nchi yetu tulilaaniwa ni namna ambavyo nchi yetu imejengwa vibaya bila mpangilio. Yaani namna watu wanavyojijengea hovyo hovyo tu bila mpangilio na kupangwa.

Kila siku tumekuwa tukiandika humu na kusema humu huku titicaca Serikali ichukue hatua ila kwa muda ilikuwa ni kama kumpigia mbuzi gitaa.

Kwa namna Waziri Jerry Silaa alivyoanza kulishughulikia hili jambo napenda kumwambia kwa akili zangu zote kuwa ametufurahisha sana watu wenye akili tuliokuwa tunalipigia kelele hili jambo.

Najua watanzania wanapenda sana uholela na najua kwa wengi kuishi eneo lililopangwa na kupimwa vizuri wanaona ni kama kitu kigeni na cha kitajiri sana hivyo kutopenda.

Nichachopenda kuwaambia watanzania kila mtu ana haki na kustahili kuishi katika eneo lililopangwa na kupimwa vizuri. Hii sio haki ya watu wachache kama wanavyodhani hivyo ili nchi yetu kuwa na mpangilio mzuri ni lazima sasa waiunge mkono Serikali kuhakikisha nchi yetu yote inapimwa na kupangwa vizuri ili tuondokane na takataka za ujenzi holela.

Mwisho kwa Jerry Silaa naomba usiishie kutoa matamko tu. Sasa uje na mpango na utekelezaji wake katika kuhakikisha nchi yetu yote inapimwa na kupangwa vizuri. Weka fedha, weka mfumo tuondokane na aibu za kuishi kama wadudu na nchi yetu kuwa ya hovyo. Unaenda vizuri na kuanzia sasa nitazidi kukuombea ili usiondolewe katika Uwaziri wa Ardhi na tutimize ndoto ya nchi yetu kupimwa na kupangwa yote.
Alhaj kuwa mkweli kaka, hilo lingewezekana kwa collective responsibility si kwa waziri pekee, Chama chetu ndicho kimeongoza Awamu zote hizi, sote Twajua Mkoloni (wa kijerumani na wa kiingereza) aliacha plan nzuri sana katika miji yetu, nini kilitusibu baada ya kupewa uhuru? Tuko serious kweli wakili? Umemshauri vyema kwenye paragraph ya mwisho
 
Kama kuna jambo linalonifanya kila siku niseme inawezekana nchi yetu tulilaaniwa ni namna ambavyo nchi yetu imejengwa vibaya bila mpangilio. Yaani namna watu wanavyojijengea hovyo hovyo tu bila mpangilio na kupangwa.

Kila siku tumekuwa tukiandika humu na kusema humu huku titicaca Serikali ichukue hatua ila kwa muda ilikuwa ni kama kumpigia mbuzi gitaa.

Kwa namna Waziri Jerry Silaa alivyoanza kulishughulikia hili jambo napenda kumwambia kwa akili zangu zote kuwa ametufurahisha sana watu wenye akili tuliokuwa tunalipigia kelele hili jambo.

Najua watanzania wanapenda sana uholela na najua kwa wengi kuishi eneo lililopangwa na kupimwa vizuri wanaona ni kama kitu kigeni na cha kitajiri sana hivyo kutopenda.

Nichachopenda kuwaambia watanzania kila mtu ana haki na kustahili kuishi katika eneo lililopangwa na kupimwa vizuri. Hii sio haki ya watu wachache kama wanavyodhani hivyo ili nchi yetu kuwa na mpangilio mzuri ni lazima sasa waiunge mkono Serikali kuhakikisha nchi yetu yote inapimwa na kupangwa vizuri ili tuondokane na takataka za ujenzi holela.

Mwisho kwa Jerry Silaa naomba usiishie kutoa matamko tu. Sasa uje na mpango na utekelezaji wake katika kuhakikisha nchi yetu yote inapimwa na kupangwa vizuri. Weka fedha, weka mfumo tuondokane na aibu za kuishi kama wadudu na nchi yetu kuwa ya hovyo. Unaenda vizuri na kuanzia sasa nitazidi kukuombea ili usiondolewe katika Uwaziri wa Ardhi na tutimize ndoto ya nchi yetu kupimwa na kupangwa yote.
Tunamwomba mh. Samia Rais wetu ampatie kila support inayohitajika ikiwepo rasilimali fedha. Wizara ya Ardhi ndio kila kitu, ndio maisha. Kila kitu kipo kwenye ardhi iwe juu ya ardhi au chini ya ardhi. Nnatamani kuona naibu waziri mkuu anakuwa waziri wa Ardhi kwa mujibu wa Katiba.
 
Ametoa mkakati wa kuipima nchi hii? Lini? Kwa fedha zipi?

Hata ule mradi wa bilioni 350 kuimarisha miundombinu ya ofisi za ardhi hauongelei, hagawi vifaa vya upimaji, wapimaji hajawapa malengo ya upimaji ardhi kwa mwaka. Na hasemi hizo hela ziko wapi mpaka sasa, na mradi unaanza lini.

Anachofanya yeye ni kuzurura na vipisi vya migogoro ili kujipatia umaarufu wakati yeye anatakiwa kusimamia sera, ili sera ijitafsiri katika kumaliza kero za ardhi.

Hii nchi kubwa, utatembelea wangapi? Kama mifumo ina shida, mtu wa level ya waziri ndio kazi yake, asuke mifumo,


Anataka wananchi wakanunue viwanja kwa maafisa ardhi, ametoa takwimu hao maafisa ardhi wana stock ya viwanja vingapi? Ndio hivyo viwanja vikitangazwa ni 1000, maombi ya wananchi 80000
 
Back
Top Bottom