Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,400
Ni wazi kuwa serikali ya sasa imeamua kuchukua maamuzi ambayo yamekosa ushauri na mwongozi sahihi.
Kuna masuala kadhaa:
1. Mkataba wa bandari za Tanzania Bara na kampuni ya kimataifa ya DP world umewahishwa sana. NI wazi kuwa kulikuwa na mijadala kuhusu "terms" za mkataba hadi umauti ulipomfika hayati Magufuli.
2. Leo tumesikia (ingawa haijathibitishwa) kwamba mswaada wa kurekebisha sheria ihusuyo Rasilimali za Taifa utapelekwa Bungeni ili kuruhusu umiliki wa ardhi kwa wageni.
3. Sheria nyingi ambazo zilirekebishwa kwa manufaa ya nchi na watanzania ikiwemo sheria hii ya Rasilimali za Taifa MWAKA 2017 ndizo hizohizo zimeanza kurekebishwa na kuwa kinyume.
Kwa mfano, mgeni yoyote asie raia wa Tanzania, haruhusiwi kumiliki ardhi ya Tanzania isipokuwa kama atakuwa na mwenza (Partner) au kupitia ubia kati ya raia wa Tanzania na huyo mgeni.
Ukibadilisha sheria ya Rasilimali za Taifa hiyo yamaanisha kwamba hata wale watanzania ambao wana uraia pacha nao sheria hiyo mpya itakapokuwa yatumika, nao watakuwa na haki ya kumiliki ardhi ya Tanzania ukiondoa mambo mengine kama kupiga kura na kugombea nafasi za kisiasa.
Pia ni wazi kuwa sheria nyingi ambazo zilipitishwa mwaka 2017 chini ya wanasheria nguli kama Profesa Kabudi na kupitishwa Bungeni kisha kuidhinishwa na aliekuwa raisi wa Tanzania John Magufuli, sasa yaonekana kuwa sheria hizo ndizo zinobadilishwa lengo lake kuu likiwa ni kuhakikisha kwamba mali za nchi zina "access" kwa watu wa nje.
Iliwahi kuandikwa huko nje katika vyombo vya habari kwamba moja ya sababu kubwa ya kuchukiwa kwa hayati John Magufuli ilikuwa ni kuwanyima "access" raia na wawekezaji wa kigeni ambao wengi ni wale wanotaka kumiliki ardhi kwa kutumia kama mashamba au kwa kujenga mahoteli makubwa ya kitalii.
Itakumbukwa kuwa hayati Magufuli aliwahi kutembelea eneo la mbuga ya Selous ambapo alilala katika hoteli moja ambayo gharama za kulala hapo kwa usiku mmoja ni zaidi ya dola 3,000. Hayati Magufuli alikuwa akitembelea eneo ambalo ndipo pajengwa bwawa la umeme la Mwalimu Nyerere.
Twarudi tena na tena kwamba mali au "assets" za nchi ni mali za watanzania wote bila kujali ni mtanzania Bara wala Mtanzania Zanzibar. Hakuna cha huyu mBara wala yule mZanzibara kwani wote tuliungana na kuwa Tanzania.
NIkisema mali au "Assets" ni ardhi, miundombinu, mashirika ya umma na taasisi zote, mabenki, mahospitali, bandari zote, shule, njia za reli, mbuga za hifadhi za vilivyomo vyote, misitu, mito, maziwa, bahari na vingine voye ambavyo vyatambulika kuwa ni mali zake.
Watanzania Bara na watanzania Zanzibar huko nje ni watu wamoja ambao hukutana na kujumika pamoja kama ndugu na pia hukutana nayakti za sikukuu na shughuli zingine za majumuiko, hivyo hakuna suala la wazi kubaguana kwa misingi ya ubara na uzenji.
Lakini maamuzi ya miezi ya hivi karibuni kuhusu nchi yetu ya Tanzania yaonekana ni kama vile mtu kaamua kugawa karanga kwa mafungu kwa misingi ya Ubara na Uzanzibara kwa kuamua kuingia mikataba uhusuyo rasilimali na mali za nchi bila ridhaa ya wananchi wake. Tayatu kumefanyika mambo mazito huko Loliondo na sasa yamefikia haya ya DP World ambao watakuwa na "access" na badari zetu zote bila masharti magumu.
Kwanini ufanyike uchaguzi mkuu kabla ya 2025?
Serikali yoyote iliopo chini ya chama tawala (kupitia raisi) huweza kujiuzulu khasa pale ambapo chama hichi tawala kina imani ya asilimia 100 kwamba wananchi wana imani nacho. Hivyo kwa kuitisha uchaguzi mapema ni katika kuhakikisha chama hicho chapata kura nyingi ambazo zitakipa chama hicho haki sahihi (mandate) ya kutekeleza mipango yake na pia kurekebisha pale ambapo wamekosea.
Pili, vyama vya upinzani pia vitapata nafasi ya viti bungeni hivyoi kuweza kufikisha hoja za wananchi hususan masual kadhaa yahusuyo mikataba kama huu wa sasa wa DP Wordl ambao serikali imeingia na nchi ya Kifalme wa Imirati.
Tatu, nchi itakuwa imepata bunge jipya na serikali mpya na huo utakuwa ni mwanya kwa serikali hiyo kurekebisha mambo yote ambayo yana kasoro na kuanza upya kama si kuimarisha mipango yake hususan katika maeneo mengine kama afya, elimu, uchumi na miundombinu. Vilevile vyama vya upinzani vitakuwa na uwezo wa kupiga kura ya kutokuwa na imani kwa serikali iliyopo endapo vitaona kuwepo kwa mashinikizo kwenye kupitisha baadhi ya miswaada yenye utata.
Nne, uchaguzi mpya utaiweka serikali kwenye imani na wananchi ambao mpaka sasa wameondoa imani kwa serikali yao kutokana na aina ya maamuzi ambayo yachukua. Ingawa serikali haiwezi kuona hii imani ndogo iliyopo mitaani na katika mitandao ya kijamii, lakini imesahau kwamba wananchi wa nchi hii walizoea kuiona serikali ikizunguka kuzungumza nao na kusikiliza shida zao, jambo ambalo kwa sasa halipo.
Hivyo imani kwa wananchi itaonekana wazi kupitia sanduku la kura za mapema (early election) na hivyo kuifanya serikali hiyo kusimama kifua mbele (mandate) kufanya shhughuli zake bila wasiwasi.
Mwisho, nchi yetu ipo kwenye njia panda na kuna haja ya kufanyika mabadiliko makubwa ambayo yatatoa mwelekeo sahihi wa taifa letu. Nchi nyingi zimefanya haya Uingereza, Italia na juzijuzi Ugiriki wamefanya wamebadilisha au kufanya uchaguzi mapema ili kupata serikali ambayo itafanya kazi yake kwa usahihi unotakiwa. Uingereza wao wamebadilisha mawaziri wakuu 5 ndani ya miaka zaidi ya 10 kuanzia bwana Cameron, Theresa May, Johnson, Liz Truss na sasa Rishi Sunak.
Hii si kwa kucheza mchezo wa kupokezana vijiti bali ni wale walopewa dhamana ya kuongoza nchi kushindwa kufanya hivyo kutokana na kutokuwa na mipango sahihi na washauri sahihi.
CCM yapaswa kubadilika kwa lazima na kusema (lets forget about the sins of the past) na kufanya mabadiliko makubwa ndani yake (major reforms) na kuachana na mawazo ya kimazoea na kwamba eti CCM ina wenyewe. Ni kweli CCM ina wenyewe lakini hao "Wenyewe" ni watu sahihi.
Wazee kama Phillip Mangula ni watu muhimu sana kwenye kutekeleza hili na akijitokeza kutoa kauli za kutaka mabadilikoi ndani ya chama ataeleweka na kuungwa mkono kwa asilimia 101 kuliko mtu mwingine yoyote ndani ya kamati kuu ya chama hicho. Tukumbuke maneno ya hayatio baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwamba upinzani wa kweli utatoka ndani ya CCM yenyewe.
Waandishi wa habari nao wana wajibu mkubwa wa kupasha habari na kuilimisha jamii juu ya masuala mbalimbali na kuondoa tabia ya kuegemea upande mmoja katika kazi zake na hivyo kujisahau wajibu wao. Vyombo vya habari vingi vya Tanzania vimepokwa kazi yake ni vyombo vidogovidogo vya habari ambavyo sasa vyatumia mtandao wa YouTube kupasha, kuchambua habari na hata kuweka mijadala muhimu ihusuyo hali ya nchi yetu.
Waandishi hao wakumbuke kauli ya hayati Baba wa Taifa katika kitabu chake cha Uongozxi wetu na Hatma ya Tanzania alisema, “Kukubali kufanywa vikaragosi vya viongozi ni dalili ya woga si dalili ya heshima ………kujenga mazoea ya kutii viongozi hata katika mambo haramu ni dalili ya woga ni kukaribisha udikteta”.
Hivyo waandishi wetu wa habari wana wajibu mkubwa wa kuwa wakosoaji na waelimishaji wakubwa kwa jamii ya watanzania.
Hivyo bila kupoteza mtiriko wa mada hii naomba nitoe hoja ya kwamba serikali ichukue uamuzi mgumu wa kuitisha uchaguzi mkuu mapema (early Election) ili tuweze kuipata serikali mpya yenye kuhakikisha maslahi ya Tanznaia na watanzania yazingatiwa na kulindwa kwa namna yoyote ile.
Mungu Ibariki Tanzania.
Kuna masuala kadhaa:
1. Mkataba wa bandari za Tanzania Bara na kampuni ya kimataifa ya DP world umewahishwa sana. NI wazi kuwa kulikuwa na mijadala kuhusu "terms" za mkataba hadi umauti ulipomfika hayati Magufuli.
2. Leo tumesikia (ingawa haijathibitishwa) kwamba mswaada wa kurekebisha sheria ihusuyo Rasilimali za Taifa utapelekwa Bungeni ili kuruhusu umiliki wa ardhi kwa wageni.
3. Sheria nyingi ambazo zilirekebishwa kwa manufaa ya nchi na watanzania ikiwemo sheria hii ya Rasilimali za Taifa MWAKA 2017 ndizo hizohizo zimeanza kurekebishwa na kuwa kinyume.
Kwa mfano, mgeni yoyote asie raia wa Tanzania, haruhusiwi kumiliki ardhi ya Tanzania isipokuwa kama atakuwa na mwenza (Partner) au kupitia ubia kati ya raia wa Tanzania na huyo mgeni.
Ukibadilisha sheria ya Rasilimali za Taifa hiyo yamaanisha kwamba hata wale watanzania ambao wana uraia pacha nao sheria hiyo mpya itakapokuwa yatumika, nao watakuwa na haki ya kumiliki ardhi ya Tanzania ukiondoa mambo mengine kama kupiga kura na kugombea nafasi za kisiasa.
Pia ni wazi kuwa sheria nyingi ambazo zilipitishwa mwaka 2017 chini ya wanasheria nguli kama Profesa Kabudi na kupitishwa Bungeni kisha kuidhinishwa na aliekuwa raisi wa Tanzania John Magufuli, sasa yaonekana kuwa sheria hizo ndizo zinobadilishwa lengo lake kuu likiwa ni kuhakikisha kwamba mali za nchi zina "access" kwa watu wa nje.
Iliwahi kuandikwa huko nje katika vyombo vya habari kwamba moja ya sababu kubwa ya kuchukiwa kwa hayati John Magufuli ilikuwa ni kuwanyima "access" raia na wawekezaji wa kigeni ambao wengi ni wale wanotaka kumiliki ardhi kwa kutumia kama mashamba au kwa kujenga mahoteli makubwa ya kitalii.
Itakumbukwa kuwa hayati Magufuli aliwahi kutembelea eneo la mbuga ya Selous ambapo alilala katika hoteli moja ambayo gharama za kulala hapo kwa usiku mmoja ni zaidi ya dola 3,000. Hayati Magufuli alikuwa akitembelea eneo ambalo ndipo pajengwa bwawa la umeme la Mwalimu Nyerere.
Twarudi tena na tena kwamba mali au "assets" za nchi ni mali za watanzania wote bila kujali ni mtanzania Bara wala Mtanzania Zanzibar. Hakuna cha huyu mBara wala yule mZanzibara kwani wote tuliungana na kuwa Tanzania.
NIkisema mali au "Assets" ni ardhi, miundombinu, mashirika ya umma na taasisi zote, mabenki, mahospitali, bandari zote, shule, njia za reli, mbuga za hifadhi za vilivyomo vyote, misitu, mito, maziwa, bahari na vingine voye ambavyo vyatambulika kuwa ni mali zake.
Watanzania Bara na watanzania Zanzibar huko nje ni watu wamoja ambao hukutana na kujumika pamoja kama ndugu na pia hukutana nayakti za sikukuu na shughuli zingine za majumuiko, hivyo hakuna suala la wazi kubaguana kwa misingi ya ubara na uzenji.
Lakini maamuzi ya miezi ya hivi karibuni kuhusu nchi yetu ya Tanzania yaonekana ni kama vile mtu kaamua kugawa karanga kwa mafungu kwa misingi ya Ubara na Uzanzibara kwa kuamua kuingia mikataba uhusuyo rasilimali na mali za nchi bila ridhaa ya wananchi wake. Tayatu kumefanyika mambo mazito huko Loliondo na sasa yamefikia haya ya DP World ambao watakuwa na "access" na badari zetu zote bila masharti magumu.
Kwanini ufanyike uchaguzi mkuu kabla ya 2025?
Serikali yoyote iliopo chini ya chama tawala (kupitia raisi) huweza kujiuzulu khasa pale ambapo chama hichi tawala kina imani ya asilimia 100 kwamba wananchi wana imani nacho. Hivyo kwa kuitisha uchaguzi mapema ni katika kuhakikisha chama hicho chapata kura nyingi ambazo zitakipa chama hicho haki sahihi (mandate) ya kutekeleza mipango yake na pia kurekebisha pale ambapo wamekosea.
Pili, vyama vya upinzani pia vitapata nafasi ya viti bungeni hivyoi kuweza kufikisha hoja za wananchi hususan masual kadhaa yahusuyo mikataba kama huu wa sasa wa DP Wordl ambao serikali imeingia na nchi ya Kifalme wa Imirati.
Tatu, nchi itakuwa imepata bunge jipya na serikali mpya na huo utakuwa ni mwanya kwa serikali hiyo kurekebisha mambo yote ambayo yana kasoro na kuanza upya kama si kuimarisha mipango yake hususan katika maeneo mengine kama afya, elimu, uchumi na miundombinu. Vilevile vyama vya upinzani vitakuwa na uwezo wa kupiga kura ya kutokuwa na imani kwa serikali iliyopo endapo vitaona kuwepo kwa mashinikizo kwenye kupitisha baadhi ya miswaada yenye utata.
Nne, uchaguzi mpya utaiweka serikali kwenye imani na wananchi ambao mpaka sasa wameondoa imani kwa serikali yao kutokana na aina ya maamuzi ambayo yachukua. Ingawa serikali haiwezi kuona hii imani ndogo iliyopo mitaani na katika mitandao ya kijamii, lakini imesahau kwamba wananchi wa nchi hii walizoea kuiona serikali ikizunguka kuzungumza nao na kusikiliza shida zao, jambo ambalo kwa sasa halipo.
Hivyo imani kwa wananchi itaonekana wazi kupitia sanduku la kura za mapema (early election) na hivyo kuifanya serikali hiyo kusimama kifua mbele (mandate) kufanya shhughuli zake bila wasiwasi.
Mwisho, nchi yetu ipo kwenye njia panda na kuna haja ya kufanyika mabadiliko makubwa ambayo yatatoa mwelekeo sahihi wa taifa letu. Nchi nyingi zimefanya haya Uingereza, Italia na juzijuzi Ugiriki wamefanya wamebadilisha au kufanya uchaguzi mapema ili kupata serikali ambayo itafanya kazi yake kwa usahihi unotakiwa. Uingereza wao wamebadilisha mawaziri wakuu 5 ndani ya miaka zaidi ya 10 kuanzia bwana Cameron, Theresa May, Johnson, Liz Truss na sasa Rishi Sunak.
Hii si kwa kucheza mchezo wa kupokezana vijiti bali ni wale walopewa dhamana ya kuongoza nchi kushindwa kufanya hivyo kutokana na kutokuwa na mipango sahihi na washauri sahihi.
CCM yapaswa kubadilika kwa lazima na kusema (lets forget about the sins of the past) na kufanya mabadiliko makubwa ndani yake (major reforms) na kuachana na mawazo ya kimazoea na kwamba eti CCM ina wenyewe. Ni kweli CCM ina wenyewe lakini hao "Wenyewe" ni watu sahihi.
Wazee kama Phillip Mangula ni watu muhimu sana kwenye kutekeleza hili na akijitokeza kutoa kauli za kutaka mabadilikoi ndani ya chama ataeleweka na kuungwa mkono kwa asilimia 101 kuliko mtu mwingine yoyote ndani ya kamati kuu ya chama hicho. Tukumbuke maneno ya hayatio baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwamba upinzani wa kweli utatoka ndani ya CCM yenyewe.
Waandishi wa habari nao wana wajibu mkubwa wa kupasha habari na kuilimisha jamii juu ya masuala mbalimbali na kuondoa tabia ya kuegemea upande mmoja katika kazi zake na hivyo kujisahau wajibu wao. Vyombo vya habari vingi vya Tanzania vimepokwa kazi yake ni vyombo vidogovidogo vya habari ambavyo sasa vyatumia mtandao wa YouTube kupasha, kuchambua habari na hata kuweka mijadala muhimu ihusuyo hali ya nchi yetu.
Waandishi hao wakumbuke kauli ya hayati Baba wa Taifa katika kitabu chake cha Uongozxi wetu na Hatma ya Tanzania alisema, “Kukubali kufanywa vikaragosi vya viongozi ni dalili ya woga si dalili ya heshima ………kujenga mazoea ya kutii viongozi hata katika mambo haramu ni dalili ya woga ni kukaribisha udikteta”.
Hivyo waandishi wetu wa habari wana wajibu mkubwa wa kuwa wakosoaji na waelimishaji wakubwa kwa jamii ya watanzania.
Hivyo bila kupoteza mtiriko wa mada hii naomba nitoe hoja ya kwamba serikali ichukue uamuzi mgumu wa kuitisha uchaguzi mkuu mapema (early Election) ili tuweze kuipata serikali mpya yenye kuhakikisha maslahi ya Tanznaia na watanzania yazingatiwa na kulindwa kwa namna yoyote ile.
Mungu Ibariki Tanzania.