Hongera Maulid Kitenge

Hongera Maulid Kitenge

huyu jamaa nimemwangalia sana kwenye hiyo clip lakini kuna vitu navitilia shaka sana,
kwanza bastola ipo kushoto na yeye anatumia mkono wa kulia na anavyoitoa anaonesha kasoro katika kutoa kwa sababu ipo kushoto na yeye anatumia mkono wa kulia.
pili katulizwa na mtu ambaye hana mazoea nae hata kidogo ingeleta maana kama ni wenzake waliomtuliza lakini sio wenzake na pia huyu jamaa alie vaa T-shirt nyeusi nae kashindwa cha kufanya so hawa naona kama ni kikundi cha mafia cha mtu ambacho kipo kati ya usalama na polisi pia unganisha dots......................................................
 
Nilishangaa yule ofisa anachomoa bastola Kwa mkono wa kushoto halafu anaishika Kwa mkono wa kulia.....nikajua moja Kwa moja jamaa hana mafunzo..... mmmmh
Tz ya vi.wonder=Tz ya vi.maajabu
 
Siku ya leo kumetokea tukio la kustaajabisha ktk tasnia ya siasa nchini tanzania. Tukio hilo limetokea dar es salaam wakati aliyekuwa waziri wa michezo na tamaduni Nape nauye akitaka kuongea na waandishi wa habari baada ya kuondolewa katika nafasi yake ya uwaziri. Nape ameondelewa leo hii katika nafasi yake baada ya mh rais kufanya marekebisho madogo katika wizara mbili.

Baada ya mh Nape kuwasili maeneo ya Pritoria hotel kulitokea tafrani baada ya watu walitambuliwa kuwa ni maafisa usalama kumzuia asiongee na waandishi na kumtaka arudi ndani ya gari. Wakati sakata hilo likitokea mmoja wa maafisa usalama alitoa bastola na kumtishia Mh Nape ambaye naye hakustuka . Afisa huyo aliirudisha silaha hiyo kiunoni kisha kuanza kumsukuma Mh nape kumrudisha ndani ya gari. Pasipo kutarajiwa kijana mmoja mtanashati aliyevaa koti jekundu alionekana kujongea kujua kinachoendelea baada ya kuona tafrani ikitokea.

Kijana huyo aliweza kutambuliwa kuwa ni mtangazaji maarufu Maulid Kitenge. Kijana huyoo aliweza kuingilia kati na kumtoa afisa usalama kwa nguvu eneo la tukio huku akimsukuma bila kuogopa. Hakika alifanikiwa akamuondoa eneo hilo na afisa huyo alitii bila shurti. Wengi tumeona na kustaajabu na hatuna budi kumpa hongera maulidi kitenge kwa ujasiri aliouonesha.

ILA
Nimejaribu kujiuliza kwa hali ya kawaida kuna raia wa kawaida anaweza kuwa na ujasiri wa namna hiyoo. Nikapata jibu inawezekana na yeye ni wale watu wanaovaa suti nyeusi(mashushu).mpaka sasa bado sijapata jibu sahihi .

Waungwana ninyi mnaonaje nawasilishaView attachment 485865View attachment 485866View attachment 485867View attachment 485868

Mkuu Jana Ilikuwa Birthday ya KITENGE na Gwajima alitembelea EFM na akampatia UPAKO wa UJASIRI safi sana maulid kitenge
 
Wewe umejuaje kama hakupitia mafunzo? Alijiamini ndio maana alisogea walikuwepo wengi pale lakini hawakuthubutu kusogea. Wewe unamjua maulid kama mwandishi wa habari ila humjui nje ya uandishi ni mtu wa aina gani. Kwako ni hatari yawezekana kwake ni kawaida tu

Kwa kumuheshimu Mwanamichezo na mwana Tasnia mwenzangu Maulid Baraka Kitenge naomba nisiseme kingine tena chochote juu yake na niseme tu naomba niishie hapa tafadhali.
 
Kitenge ni Muhuni wa Alharamain Secondary School , usikute alishapasha cha Shaurimoyo kabla ya kwenda kwny press conference halafu Ana hasira sana na Mke Mwenzie Janet aliefoji vyeti na majina
'Mke mwenzie' unamaana ipi?
 
Kwani kuna mtu asiyejua kwamba kitenge ni usalama. Yule yupo katika ivi vyombo vya habari kwa kazi maalum. Jezi nambari 9 mgongoni Maulidi mbaraka wa kitenge
Aliekuambia hilo ni nani ? Kwa kigezo kipi unauthibitishia uma yakua jamaa ni Usalama?
 
Unatengeneza movie ati unajiita mtoto wa mjini, kaaaaaa only Tz!
 
Daaa kumbe ni ww maulidi kazi nzuri sana kwa kuonyesha una jali wanojali kazi yk bigup sana
 
Tutayasikia mengi sana, ila Kitenge ni mtu wa kawaida tena mhuni wa mtaani hivyo haogopi kinachokuja wala kinachoenda!.
Pili: Maulid Kitenge hajaona ile bastola ndio maana alikuwa na ujasiri wa kumsukuma bila kuwa na uwoga wowote ule!
 
Tufanye kazi. Tuache maneno. Nchi hii ni tajiri sana tatizo watu wavivu.
nakubaliana na wewe mkuu, anaeongoza nchi hii ana kazi kubwa, kumechipuka udini, ukabila, na kujuana. namuombea mungu afanikiwe. ana safari ndefu na ngumu. siwezi au nashindwa kuelezea. mungu ilinde Tanzania...!! nawaza kwa sauti tu..!!!!!.
 
Afisa alijua Kitenge ni mtu wa sports jezi namba tisa Mgongoni sio wa kumchezea wakati yeye ni mtu wa bwax
Niwa kispoti bana usimchukulie poa.
Kitenge.JPG
 
Tutamuelewa mheshimiwa baada ya muda. Hao kina dkt. Machache wanafiki mno. Awamu wamebanwa kila kona. Hakuna kupenyeza kimemo ili kupata upendeleo. Hapa kazi tu
 
Hapo Maulid nilimkubali kishenz yaan, jamaa hakuwa mwoga kabsa.

Ila mdogo wangu Harmo rapper alilula kona ni hatari. Alipata kiboko yake pale
Hamorapa break ya kwanza chalinze.

Hichi kitoto mashauzi sana Nape alivyoshuks kikawahi mbele kutafuta kick kilivyoona bastora tu hata Filbert Bayi haoni ndani kwa mbio zile.
 
Back
Top Bottom