Hongera Maulid Kitenge

El'son

JF-Expert Member
Jun 3, 2012
380
324
Siku ya leo kumetokea tukio la kustaajabisha ktk tasnia ya siasa nchini tanzania. Tukio hilo limetokea dar es salaam wakati aliyekuwa waziri wa michezo na tamaduni Nape nauye akitaka kuongea na waandishi wa habari baada ya kuondolewa katika nafasi yake ya uwaziri. Nape ameondelewa leo hii katika nafasi yake baada ya mh rais kufanya marekebisho madogo katika wizara mbili.

Baada ya mh Nape kuwasili maeneo ya Pritoria hotel kulitokea tafrani baada ya watu walitambuliwa kuwa ni maafisa usalama kumzuia asiongee na waandishi na kumtaka arudi ndani ya gari. Wakati sakata hilo likitokea mmoja wa maafisa usalama alitoa bastola na kumtishia Mh Nape ambaye naye hakustuka . Afisa huyo aliirudisha silaha hiyo kiunoni kisha kuanza kumsukuma Mh nape kumrudisha ndani ya gari. Pasipo kutarajiwa kijana mmoja mtanashati aliyevaa koti jekundu alionekana kujongea kujua kinachoendelea baada ya kuona tafrani ikitokea.

Kijana huyo aliweza kutambuliwa kuwa ni mtangazaji maarufu Maulid Kitenge. Kijana huyoo aliweza kuingilia kati na kumtoa afisa usalama kwa nguvu eneo la tukio huku akimsukuma bila kuogopa. Hakika alifanikiwa akamuondoa eneo hilo na afisa huyo alitii bila shurti. Wengi tumeona na kustaajabu na hatuna budi kumpa hongera maulidi kitenge kwa ujasiri aliouonesha.

ILA
Nimejaribu kujiuliza kwa hali ya kawaida kuna raia wa kawaida anaweza kuwa na ujasiri wa namna hiyoo. Nikapata jibu inawezekana na yeye ni wale watu wanaovaa suti nyeusi(mashushu).mpaka sasa bado sijapata jibu sahihi .

Waungwana ninyi mnaonaje nawasilisha
IMG_20170323_181605_974.jpg
IMG_20170323_181605_975.jpg
Screenshot_2017-03-23-17-53-58.jpeg
Screenshot_2017-03-23-17-53-44.jpeg
 
Yaani maulid angekuwa afisa usalama angepandishwa cheo suala sio nguvu ushawishi tu. Ndio maana proceedure za polisi zipo wazi anajitambulisha anakueleza kosa anakuomba muelekee kituoni.

Ukikataa bado harusiwi kutumia nguvu na ikibidi kutumia nguvu sio kutoa au kutumia silaha.
 
Mambo yakusema uyo alietoa silaha ni usalama ni uongo akuna kitu kma icho uyo sio usalama akuna usalama pumbavu kma uyo usalama wanatumia akiri na nguvu inakuja baada yaa
hahaahah kwa kuwa kazi zao wanafanya kwa siri basi tumejenga picha ni watu wenye akili za hali ya juu, kumbe ukiwaleta hadharani ni ma bashite sana. amini mkuu ndo hao vilaza
 
Mambo yakusema uyo alietoa silaha ni usalama ni uongo akuna kitu kma icho uyo sio usalama akuna usalama pumbavu kma uyo usalama wanatumia akiri na nguvu inakuja baada yaa

Usalama bongoooo??!! Nenda zako hukooo!

Mbona Usalama wenye gwanda zao kabisa zile Mpauko walivamia Clouds lakin Hakuna aliekumbuka kuomba clip ya CCTV camera na kufuta sehemu ya Uvamizi iliyoonekana?
 
Siku ya leo kumetokea tukio la kustaajabisha ktk tasnia ya siasa nchini tanzania. Tukio hilo limetokea dar es salaam wakati aliyekuwa waziri wa michezo na tamaduni Nape nauye akitaka kuongea na waandishi wa habari baada ya kuondolewa katika nafasi yake ya uwaziri. Nape ameondelewa leo hii katika nafasi yake baada ya mh rais kufanya marekebisho madogo katika wizara mbili.

Baada ya mh Nape kuwasili maeneo ya Pritoria hotel kulitokea tafrani baada ya watu walitambuliwa kuwa ni maafisa usalama kumzuia asiongee na waandishi na kumtaka arudi ndani ya gari. Wakati sakata hilo likitokea mmoja wa maafisa usalama alitoa bastola na kumtishia Mh Nape ambaye naye hakustuka . Afisa huyo aliirudisha silaha hiyo kiunoni kisha kuanza kumsukuma Mh nape kumrudisha ndani ya gari. Pasipo kutarajiwa kijana mmoja mtanashati aliyevaa koti jekundu alionekana kujongea kujua kinachoendelea baada ya kuona tafrani ikitokea.

Kijana huyo aliweza kutambuliwa kuwa ni mtangazaji maarufu Maulid Kitenge. Kijana huyoo aliweza kuingilia kati na kumtoa afisa usalama kwa nguvu eneo la tukio huku akimsukuma bila kuogopa. Hakika alifanikiwa akamuondoa eneo hilo na afisa huyo alitii bila shurti. Wengi tumeona na kustaajabu na hatuna budi kumpa hongera maulidi kitenge kwa ujasiri aliouonesha.

ILA
Nimejaribu kujiuliza kwa hali ya kawaida kuna raia wa kawaida anaweza kuwa na ujasiri wa namna hiyoo. Nikapata jibu inawezekana na yeye ni wale watu wanaovaa suti nyeusi(mashushu).mpaka sasa bado sijapata jibu sahihi .

Waungwana ninyi mnaonaje nawasilishaView attachment 485865View attachment 485866View attachment 485867View attachment 485868

Mazoezi ya Efm jogging club yao yanamdanganya dogo na kuna siku atakuja kukutana na wenyewe wenyewe wa kweli hicho Kibwenzi chake kitaoteshwa Ulimini.
 
Back
Top Bottom