Hivi Watangazaji wa Clouds FM wana shida gani?

Hivi Watangazaji wa Clouds FM wana shida gani?

Ruge ni rafiki mkubwa wa January Makamba kila jambo la ikulu hupewa Ruge.
 
Rege yupo ccm na Joseph Kusaga yupo Ukawa kila mmoja ana Timu yake japo waziwazi hawajionyeshi lakini Gerard Hando huwa ni Ukawa ingawa huzuga kiaina kuwatetea ccm .

Huyu rege ni mjamaika au ni mtanzania mwenzetu mkuu?
 
SHIDA YAO WANA MASLAHI YA CHAMA,Bila kujari Maslahi ya NCHI. ''Lazima wakumbuke, na Wajue kuwa MUNGU NDIO ANAE TAWALA SIO CHAMA FULANI''. Hapo walikosea na hawana jipya
 
hawa watu wamegoma kusoma magazeti ya leo eti kisa yameripoti habari za lowassa.

Eti wanasema kilichotokea jana kila mtu alishughudia hivyo hakukuwa na haja magazeti kuripoti leo.

Kweli clauds?

Walichoamua eti bora tusome uhuru(jarida la ccm). Ambalo limeripoti ''magufuli ushindi wa tsunami''
kwa design hii waandishi wa clauds na media zenu wekeni wazi kuwa ninyi ni vyombo ya propaganda za ccm.

mkuu kwani hujui hilo? Hakuna tofauti kati ya clouds na uhuru fm. Lakini jambo la muhimu ni kuwa hawawezi kuzuia mafuriko kwa mikono.
 
Gerald yupo UKAWA wakuu. Anafanya hivyo ili kulinda kazi. Tusimlaumu sana makamanda.
 
Nasononeka kwani huwa mnajidai hamuisikilizi wala kuangalia clouds ila chochote msichokipenda mnakuja kulia lia kwan mna shida gani?.
 
SHIDA YAO WANA MASLAHI YA CHAMA,Bila kujari Maslahi ya NCHI. ''Lazima wakumbuke, na Wajue kuwa MUNGU NDIO ANAE TAWALA SIO CHAMA FULANI''. Hapo walikosea na hawana jipya

Ruge ni mtanzania ila ameamua kuuza utu wake kwa maCCM. naomba watanzania wote waisusie clouds media. waachieni maCCM na cloudCCM yao.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom