Hivi Wakenya wametushinda nini?

Ujamaa ulikuwa na faida nyingi sana kuliko unavyofikiri wewe. Hata kiswahili ni lugha inayotuunganisha. Tatizo hapa ni watu kukosa uzalendo. Hasa nyie mnaoenda nje ya nchi hamkumbuki nyumbani.
Mkuu hapa kwenye wanaoenda nje hawakumbuki nyumbani si kweli hata kidogo.
Nimekaa nje sana na ninaweza kukuhakikishia WaTZ ndiyo wanaokumbuka nyumbani kuliko waliotoka sehemu nyingine za Africa.
Tatizo kubwa sana ukishatua tu Dar, unaanza kunusa ubabe wa nchi.
Nitakupa kisa kimoja tu kilichomisibu rafiki yangu ambaye alitaka kuwekeza nchini kama miaka sita hivi illiyopita kwa kuanzia na tshs. 100mln. Akaenda Tanzania Invenstment TIC akazungumza na Bwana mmoja pale kuhusu nia yake. Akaelekezwa NHC, wakati huo wakiingia ubia na wananchi wenye nia ya kuwekeza na kima cha chini wakati huo ili kupewa support ya kuwekeza ilikuwa ni Mln 100 kwa Mtanzania. Walikuwa wanakupa kiwanja mahali penye jengo la zamani ili uweze kulibomoa na kujenga kitega uchumi. Kama sijakosea walikuwa wao wanachukua 25 ~ 30% ya mapato kama mambo yakishakubalika na kukamilika.
Alichagua mahali kutokana na orodha ya viwanja alivyoonyeshwa, na Arusha ndiyo mahali alichagua. Kabla ya kusaini mkataba ulitakiwa kuanza kutengeneza bussiness plan pamoja na michoro ya jengo. Ilimgharimu rafiki yangu fedha nyingi kufanya safari hadi Arusha kukagua eneo, kutengeneza bizi-plan na kuchora jengo. Alipofika kuwasilisha kama alivyotakiwa, mizengwe ikaanza. Wakubwa wakamwambia kwenye lile jengo akaongeze ghorofa mbili za kwao! Na hapo hawatodhubutu kujiandikisha wazi kuwa ni zao, watakuletea ndugu au mwanafamilia na kuwaandikisha kwenye mkataba.
yule Bwana ilibidi aachilie mbali, amekwenda kufanya mambo mengine kabisa.

Watanzania tunahitaji kubadilika na kuwapenda wenzetu waliobahatika na walio na nia kuja kuwekeza nchini siyo kuwakatisha tamaa.

Nimeona mengi sana kuhusu hili swala. Nikiamua kuyaandika hapa utadhani ninatunga. Kwanza kabisa watanzania na haswa viongozi, kuliko amsadidie mtanzania mwenzake kuendeleza au kuanzisha biashara yake ni afadhali amsaidie mgeni. Sijua huwaridhisha nini haswa ndani ya mioyo yao.

Binafsi niliwahi kwenda Wizara ya Hazina kwa mazungumzo ya aina hiyo tena baada ya kuomba appointment. Nilifika nikaingia ofisini kwa bwana mkubwa, nilipoingia tu akaanza kulalamika, Oh mama mkwe kafanyiwa operation nataka niende hospitali sasa hivi. Nikamwabia basi afadhali tupange siku nyingine nitakayoweza kukuona. Akasema hebu nileze kwa kifupi haswa nini ulikuwa unataka. Nikazidi kumsihi kuwa mazungumzo yatakuwa marefu kwani yalikuwa yanabidi apitie makaratasi fulani ili aweze kunielewa. Akaamka tukabidi tutoke tunaongea. Alipofungua ofisi akamwona kijana mdogo tu mwenye asili ya kiAsia. Akamsalimia kwa shangwe akarudi ndani ya ofisi, nilkaa pale nje ya ofisi kwa sekretari wake kama dakika nyingine arobaini ikabidi niondoke.

Hivi unafikiri uhusiano wa namna hiyo unajenga nia njema kwa walioko nje kuja kuwekeza?? Nadhani wapo wengi waliokumbwa na mambo kama haya na ni wakati umefika jambo hili likajadilliwa hata Bungeni. Wapo watanzania wengi sana nje ambao wangependa kuja kuwekeza lakini mambo kama haya yanakatisha tamaaa!.
 
Shida yetu kubwa, Sera nzuri kiasi, Watekelezaji wazembe. Kuoneana haya; mtu anafanya uharibifu unamwangalia kwa kuwa sisi ni ndugu. Kutoweza kukaripia matumizi mabovu na kukataa kuonewa kwa kutouliza maswali magumu. Kimsingi tunao uwezo mzuri na mkubwa, wakenya wana-mafyongo ila wanajificha katika mambo machache yakiwamo kujifanya kiingereza ndio elimu. Kwetu tukiweza sema ukweli pasipo hofu, kuwajibisha viongozi wajing, kuwaadibisha wananchi wasiotimiza wajibu wao, na mwishoni tukiweza kukataa fedha yetu kutumika kwa anasa, tutakuwa tumekaribia mwanzo wa maendeleo. TUNAWEZA
 
wanajamvi!
Tuseme ukweli wakenya wametuzidi kwa mengi. Wanajituma kwenye kazi, zaidi si spenders kama sisi(kuanzia serikali mpaka mtu binafsi mfano kwao waziri anapanda passat(saloon car),unaweza kukuta mkenya tajiri mwenye majumba kila kona na makampuni kadhaa anatembelea toyota probox. Tembea kenya hususani miji mikubwa (nairobi, kisumu, mombasa) uhesabu investments kubwa kubwa real estates,apartments,majengo makubwa,supermarkets,kampuni kubwa za insurance, constructions, media houses (tv stations, publishing), airlines, kampuni za mabasi yanayosafiri ndani na nchi jirani kwa aslimia kubwa yanamilikiwa na wakenya wenyewe na wameajiri wakenya wenzao(suala la kabila gani ndo wanaajiriwa usiniulize leo, mimi naanagalia wakenya ndo walioajiriwa). Sasa njoo tanzania serikalini matumizi ni makubwa kupitiliza magari ya kifahari, watanzania wa kawaida ni spenders mtu anatembelea toyota land cruiser v8 lakini hana investment ya maana. Zaidi watanzania ni wavivu kupitiliza, nenda hoteli hapa tanzania ukimka asubuhi ya saa 12 ukiuliza chai unaambiwa bado. Nenda kalale hoteli za kenya saa 12 kasoro chai tayari so unakunywa chai then kama unasafiri muda huo unaendelea na safari zako.

Kubwa kupita yote, kenya wanathamini elimu kuliko vitu vyote (nikisema elimu simaanishi elimu ya vyuo vikuu tu) kuanzia shule ya msingi, sekondari na kuendelea) kwao mpaka mtu wa saloon anasomea na ukienda saloon utaona tofauti na saloon za kibongo). Lugha ya kiingereza nayo imetufanya tujione wanyonge sana mbele yao. Wakenya ni wepesi kutafuta opportunities hapa usa wakenya wamejaa, ukienda uk ndo usiseme, saudi arabia, south sudan, tz, uganda, south africa ndo balaa na wakipata hela zao wanaenda ku-invest kenya. Ndio maana makaburu (south africa) wanashindwa/wanapata wakati mgumu kuinvest kenya maana competition kenya tofauti na tz hakuna competition na watz hawathamini bidhaa za kwao(tz).

point.
 
Na wewe unakiri kushundwa??. yaani huna confidence, una longo longo huwezi kudeliver??. Hakuna watu wenye longolongo kama wakenya,.
Hata kama ni hivyo mbona wametuzidi mambo mengi wakati tuna rasilimali nyingi kuliko wao bwana
 
Ndugu yangu tunatakiwa tubadilike, hii culture tuliyonayo tuiache kwa sababu haitatupeleka popote. Maneno mengi vitendo hakuna. Si ajabu hapa kwetu kuingia kwenye maofisi ukakuta wafanyakazi wazongoa huku watu wapo kwenye foleni wanasuburi huduma, Sisi tunaotembea tunapita mijini na vijijini unaona vijana wamekaa vijiweni asubuhi hadi jioni kisa eti hakuna ajira, jamani hii siyo sawa.
Ni vingumu kumpa mtanzania kashughuli, ukamwambia mimi ninao mtaji huu hapa, hebu simamia hii shughuli, haiwezekani kabisa, mashirika yote imeshindikana, mashirika mengine biashara ipo wazi na ya kufa mtu (Reli) lakini imeshindikana kabisa.
Kuna mmoja anasema Kenya ilijengwa na wakoloni, hapana, super highway unayoiona haijajengwa na mkoloni, flyover zinazojengwa hazijengwi na wakoloni, wenzetu wanakopa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, sisi tunakopa kwa ajili ya kulipana masurufu, hili siyo la ukoloni, hebu fikiria, nchi yenye uongozi bora unaweza leo, ukapanga kujenga Mandela road hivi inavyojengwa jamani, Kweli tunahitaji mapinduzi ya kifikra.
 
Wametushinda ujasili na uthubutu. Hawaogopi kudai haki zao
 
Tulishindwa kuweka misingi imara katika kila nyanja baada ya kupata Uhuru, kwa miaka 24 tumetawaliwa kidikteta nakila alichosema Rais tulilifata "blindly", maamuzi mengi yaliyofanywa wakati huo ndio yamekuwa chachu ya maporomoko ya kila kitu Tanzania.

Baada ya kugundua hilo tufanye nini maana miaka 24 unayosema ni ile ya baba wa Taifa ambapo mwisho wake ilikuwa 1984, na kutoka 1984 mpaka sasa ni miaka 28. Toka 1984 tumefanya nini kubalisha hiyo hali na tufanye nini baada ya kugundua tatizo hilo
 
Baada ya kugundua hilo tufanye nini maana miaka 24 unayosema ni ile ya baba wa Taifa ambapo mwisho wake ilikuwa 1984, na kutoka 1984 mpaka sasa ni miaka 28. Toka 1984 tumefanya nini kubalisha hiyo hali na tufanye nini baada ya kugundua tatizo hilo

Shule za Sekondari zaidi ya 5,000 kwa sasa (zilikuwa chini ya 500 wakati wa Nyerere (na zote za kurithi kwa mkoloni), wanafunzi vyuo vikuu zaidi ya 300,000 (wa ndani tu ya nchi) mbali wanaosoma kwa jitihada zao nje ya nchi.

Huu ni msingi mwema sana. Tumeshaanza kuona manufaa yake inabidi sasa tuongeze ufanisi kwa kuziboresha na kuziboresha kutaanza kuwa na maana pale tu tutakapo anza kupata waalim waliosoma ambao ndio hao tunawasomesha sasa..
 
Anyway, hilo li super highway wamejengewa na waChina. Kuanzia wazo mpaka kulijenga na kuchora hiyo mistari wamefanya wachina.

Ukweli ni kwamba hakuna namna mwaafrika atakaa awaze na kujenga barabara kama hilo. Na akijaribu, huo mradi hautafika mwisho kabla hela zote hazijaibwa. Hata umsimamie na mtutu wa bunduki haitasaidia
 
Shule za Sekondari zaidi ya 5,000 kwa sasa (zilikuwa chini ya 500 wakati wa Nyerere (na zote za kurithi kwa mkoloni), wanafunzi vyuo vikuu zaidi ya 300,000 (wa ndani tu ya nchi) mbali wanaosoma kwa jitihada zao nje ya nchi.

Huu ni msingi mwema sana. Tumeshaanza kuona manufaa yake inabidi sasa tuongeze ufanisi kwa kuziboresha na kuziboresha kutaanza kuwa na maana pale tu tutakapo anza kupata waalim waliosoma ambao ndio hao tunawasomesha sasa..

Safi sana mkuu kwa maneno mazuri ila hata hivi vyuo tulivyonavyo tunahitaji kuvitanua kwani idadi ya wanachuo in relation to facilities haiendeni, shule nyingi za msingi zina wanafunzi kuanzia 800 mpaka 1500 wakati sera inatuambia shule moja wanafunzi 560 ukienda shule za serikali za secondari nyingi ni double session yaani idadi ya wanafunzi waliopo nao ni kubwa kulinganisha na majengo. Nadhani kwa kuanzia si mbaya ila tunahitaji tukimaliza la waalimu nadhani bado kazi ya ujenzi wa shule na madarasa ya kutosha unahitajika ili darasa moja liwe na watu 40 kuanzia primary school to university. Kwa utaratibu huu wa wanafunzi wengi facilities chache mwisho wa siku tunapata wataalamu ambao si makini mfano mzuri siku hizi multiple choice questions in exams ni kuanzia primary school to university kwa kuwa walimu wana wanafunzi wengi hivyo anaona akitoa mtihani wenye maswali ya kupima general knowledge atapata wapi muda wa kusahihisha wakati ana wanafunzi 400 anafundisha kwa madarasa tofauti, mwisho wa siku tunapata wataalamu ambao hawajaumiza vichwa kufikiri hence poor performance, otherwise contribution yako nzuri.
 
Anyway, hilo li super highway wamejengewa na waChina. Kuanzia wazo mpaka kulijenga na kuchora hiyo mistari wamefanya wachina.

Ukweli ni kwamba hakuna namna mwaafrika atakaa awaze na kujenga barabara kama hilo. Na akijaribu, huo mradi hautafika mwisho kabla hela zote hazijaibwa. Hata umsimamie na mtutu wa bunduki haitasaidia

Lakini wamethubutu kwa kuwaachia wachina wajenge kwa niaba yao kwa kuwa wana amini hawawezi kujenga, je sie tuna huo moyo. Tukiletewa tu kocha wa mpira wa miguu tunataka tumchagulie wachezaji
 
Safi sana mkuu kwa maneno mazuri ila hata hivi vyuo tulivyonavyo tunahitaji kuvitanua kwani idadi ya wanachuo in relation to facilities haiendeni, shule nyingi za msingi zina wanafunzi kuanzia 800 mpaka 1500 wakati sera inatuambia shule moja wanafunzi 560 ukienda shule za serikali za secondari nyingi ni double session yaani idadi ya wanafunzi waliopo nao ni kubwa kulinganisha na majengo. Nadhani kwa kuanzia si mbaya ila tunahitaji tukimaliza la waalimu nadhani bado kazi ya ujenzi wa shule na madarasa ya kutosha unahitajika ili darasa moja liwe na watu 40 kuanzia primary school to university. Kwa utaratibu huu wa wanafunzi wengi facilities chache mwisho wa siku tunapata wataalamu ambao si makini mfano mzuri siku hizi multiple choice questions in exams ni kuanzia primary school to university kwa kuwa walimu wana wanafunzi wengi hivyo anaona akitoa mtihani wenye maswali ya kupima general knowledge atapata wapi muda wa kusahihisha wakati ana wanafunzi 400 anafundisha kwa madarasa tofauti, mwisho wa siku tunapata wataalamu ambao hawajaumiza vichwa kufikiri hence poor performance, otherwise contribution yako nzuri.

Ndio kwanza tumeanza kuweka misingi ambayo haikuwekwa na waliopewa madaraka mwanzoni, itatuchukuwa muda kuweka kila kitu sawa, ndio kwanza tunaanza kuwaelimisha raia wetu kwa kiwango cha juu, waliopewa madaraka mwanzoni waliishia kuwasomesha wengi kwa kiwango cha kujuwa kusoma magazeti na kuandika barua za kifamilia.

Sasa tunaona Serikali ya awamu hii, ikikazana kutuondoa huko na kutupeleka kwenye kisomo cha juu, ni hii miaka 7 tu iliyopita tumeona zaidi ya shule za sekondari 5,000 zikijengwa, vyuo vikuu vipya karibu viwili kila mwaka kwa miaka 7 sasa ya Kikwete.

Waliopita wangeyanfanya hayo, saa hizi tunaongea mingine. Tuna safari ndefu lakini ni vizuri kuw Kikwete kaanza kuifupisha hiyo safari.
 
Ndio kwanza tumeanza kuweka misingi ambayo haikuwekwa na waliopewa madaraka mwanzoni, itatuchukuwa muda kuweka kila kitu sawa, ndio kwanza tunaanza kuwaelimisha raia wetu kwa kiwango cha juu, waliopewa madaraka mwanzoni waliishia kuwasomesha wengi kwa kiwango cha kujuwa kusoma magazeti na kuandika barua za kifamilia.

Sasa tunaona Serikali ya awamu hii, ikikazana kutuondoa huko na kutupeleka kwenye kisomo cha juu, ni hii miaka 7 tu iliyopita tumeona zaidi ya shule za sekondari 5,000 zikijengwa, vyuo vikuu vipya karibu viwili kila mwaka kwa miaka 7 sasa ya Kikwete.

Waliopita wangeyanfanya hayo, saa hizi tunaongea mingine. Tuna safari ndefu lakini ni vizuri kuw Kikwete kaanza kuifupisha hiyo safari.

Mwanzo mzuri ila tuweke pia mkakati kwamba baada ya miaka 5 tuwe na wahadhiri wa kutosha maana kwa hali iliyopo wahadhiri wengi wanafanya consultancy work kila siku utakuta wiki hii ana kipindi Tumaini Iringa wiki ijayo ana kipindi SAUT Mwanza wiki ya tatu anarudi kituo chake cha kazi na wiki ya 4 anakwenda Makumira university Arusha. Hapa inaonyesha wahadhiri pia ni wachache ikiwezekana tuombe msaada nchi za wenzetu watusaidie kwa hili wakati tunaandaa wahadhiri wetu ktk kipindi cha miaka 5 ili kupunguza vijana wetu kufundishwa na vijana wenzao ambao wamemaliza just few months ago
 
fikra za ujamaa na uswahili mwingi. Maendeleo hayaji kwa lelemama, yanahitaji kujituma. Lets be serious, otherwise ni aibu tupu. Hivi nchi hii Mungu ametupa kila kitu tunaweza kumlaumu nani kwa umaskini na aibu hii. Nipo nje ya nchi na ninapokutana na watu ukiwaambia umetoka tz, they associate it na umaskini, what a shame. Leaders ndio kila wakati kuzurura kuombaomba wakati sisi ndio tungetakiwa kuombwa.

Kinachotokea tanzania ni kwamba kutakuwa na tabaka la wale walio matajiri kutokana na juhudi zao, na lile la umaskini wa kutisha ambao wataendelea kulaumu kila mtu kwa hali zao. And then there will be a fight between. Kwakuwa tabaka la juu litakuwa na nguvu, wajipanga kujihami kama ilivyo marekani, mabunduki kila mahali
Hapo kwenye red: "uswahili" mwingi. Uswahili si lugha tu bali ni utamaduni pia. Sisi watz tu waswahili si kwa kuwa tunaongea lugha (kiswahili tu) bali pia tu waswahili wa utamaduni licha ya wingi wa makabila yetu. Na moja ya sifa ya waswahili ni upigaji wa domo, soga bila kuwa siriaz kwenye kazi za maendeleo. Sifa hii imewajaa wengi. Tunakosa seriousness ktk kazi, kujiamini kudogo, kuridhika kwa sana kwa mafanikio kidogo, kukosa ambition ya maendeleo, kupenda vya dezo na starehe bila jasho. Kwa kifupi wengi ni dull. Ndiyo uswahili huo.
 
Hoja kami hizi ndio NEC ya CCM ingekua ianakaa na kuzichanganua ili kujua wapi warekebishe - lengo la CCM iwe kuipita KENYA kama itakua madarakani. Ikiipita Kenya, basi ifuate Angola, kisha tuipite S. Afrika.
 
Kenya wanachotuzidi ni kitu kimoja , kuwa na kiongozi mkuu bora, siasa ndio inayotawala nyanja zote za maisha. Na kwenye nchi zinazoendelea kingozi ndiye anayeongoza hizo siasa, Nenda Rwanda imebadirika ghafla sababu ya mzee Kagame mtu mwenye vision , Tanzania wakati wa Mkapa ilikuwa imeanza kupata mwelekeo na kusema kweli kama mzee Mkapa angeendelea kipindi cha miaka kama 10 zaidi tungekuwa mahali pengine sasa, Sasa kaja mweshimiwa wetu huyu Dr. kwanza hajui kwanini nchi ni maskini sasa atajuaje mwarobaini wa kuigeuza nchi hii iwe nchi ya maendeleo? Vision yake ni ipi ? alishasifika kwa kitu gani cha kujivunia,Hili nalo ni janga la kitaifa kwamba miaka 10 hii imepotea bure
 

Similar Discussions

21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom