Kuna tofauti kubwa kati ya Wakenya na Watanzania lakini kubwa ni kwamba wenzetu wanachapa kazi, sisi tumelala. Niliwahi kufika mpakani mwa Tanzania na Kenya, Isebania (Kenya) na Sirari(Tanzania) usiku wa manane natokea Nairobi kuja Tanzania. Sikiliza kioja. Upande wa Kenya haukuwa na umeme, sijui siku hizi, lakini Maafisa Uhamiaji wa Kenya walitumia taa za kandili kutugongea haraka passport zetu tukaingia Tanzania. Loo! kufika Tanzania, kwenye umeme tukakuta miafisa uhamiaji yetu imelala, siyo ofisini, bali majumbani mwao na ofisi imefungwa. Tulilazimika kuyasubiri mavivu yetu yajivute wakati kumekucha kabisa, napo taratiiibu na tukagongewa passport zetu. Tulikaa upande wa Tanzania kwa saa 5. Je, unaweza kujiuliza kwa kutuchelewesha pale ni watu wangapi walichelewa katika biashara zao? Haya, wakati Kenya usiku ndo wanafanya biashara nchi nzima, maana usafiri unaendelea, ati Tanzania waliambiwa na Ziraili kuwa ikifika saa 4 usiku mabus yasisafiri kuna ajali. Utalinganaje na Kenya, wakati wao usiku wanafanya kazi, Tanzania wanalala, na huenda ndo nchi pekee duniani ambayo huzuia watu wake kusafiri usiku. Wanatuzidi kwa mengi, tena yaliyo chini ya uwezo wetu! Utadhani tumeshushiwa laana! Kipindi hicho ili ufike Mwanza, ilibidi upitie Kenya, maana yake tulikuwa tunawapelekea uchumi. Kisa, barabara. Sitaki kuendelea ntalia bure.....