Hivi Wakenya wametushinda nini?

Labda ndio madhara ya kuuwa ukabila ndio yametufanya hivyo....... Hakuna competitiveness kati yetu.......tumebaki kulumbana dini gani wako wengi zaidi ya wengine......
 
Ukikutana nao nje ya nchi wana confidence za kufa mtu. wakiwa kwao hawataki longo longo na kama hawaelewani watapigana mikwaju kisha wanadeliver

Tazama KTN au KBC picha ziko clear, news zimetulia, watangazaji wametulia

Soma gazeti la NATION au Standard...huwezi fananisha na lile gazeti la Michuzi (daily nyuz) au lile la copy and paste (guardian)

sisi tuna watu wengi zaidi, rasili mali nyingi zaidi, wanasiasa wengi zaidi, vyama vya siasa vingi zaidi, magazeti mengi zaidi, JF ndio zaidi, cabinet yetu kubwa kuliko ya kwao, katiba yao (na mahakama ya kadhi ndani) ndio walipitisha, sasa kwa nini hawa wana deliver na sisi hatuna kitu?

I've tried to hate them lakini nimeshindwa, cant hate their ambition esp based on their national interest.

Halafu wao kujenga li Superhighway kama hili ili iweje?

ahh sisi hata kuthubutu tunashindwa sijui kwa nini

7293527580_6750ff3295_b.jpg
Nchi yetu imetoa kipaumbele kwa siasa na wanasiasa toka zamani!! Na siasa ikachukuliwa kama longo longo na uswahili mwingi. Unafiki ni wa hali ya juu TZ na siasa iliyokuwa inasisitiza kuwa serikali italetea maendeleo watu wake! bila kujibidisha. Hiyo mentality imekuwepo hadi leo. Kenya toka zamani ulikuwa uchumi huria na ukicheza kidogo unakufa njaa. Hakuna urafiki wa kusaidiana wala kuoneana huruma. Niko kwao kikazi na hadi sasa sijui jirani yangu wa nyumba ya karibu anafananaje mwaka wa pili huu!! Hakuna kuombana chumvi hapa. Usipohangaika unakufa kweli hakuna utani. Hapo nyumbani tunaelekea huko toka tuingie uchumi huria. Dalili zote zipo wazi. Chama tawala bado kinataka wananchi wasifanye uchambuzi!! lakini njaa inapozidi wote wataamua kufanya kazi siyo mchezo
 
Ukitaka kuendelea lazima uwe na roho mbaya. Wametuzidi roho mbaya na utu hawana kabisa, Pesa mbele utu nyuma.

halafu ni corrupt sana, na wakiiba wanafanya investment kwao na hawatoroshi nje ya nchi kama akina chenge, na investment zao zinatengeneza ajira kwa wakenya wenzao, ila watz wakiiba kama hawatapeleka nje ya nchi basi wataishia kujenga nyumba na kununua viwanja, kuhonga, na kununua magari kwa sifa
 
Kuna tofauti kubwa kati ya Wakenya na Watanzania lakini kubwa ni kwamba wenzetu wanachapa kazi, sisi tumelala. Niliwahi kufika mpakani mwa Tanzania na Kenya, Isebania (Kenya) na Sirari(Tanzania) usiku wa manane natokea Nairobi kuja Tanzania. Sikiliza kioja. Upande wa Kenya haukuwa na umeme, sijui siku hizi, lakini Maafisa Uhamiaji wa Kenya walitumia taa za kandili kutugongea haraka passport zetu tukaingia Tanzania. Loo! kufika Tanzania, kwenye umeme tukakuta miafisa uhamiaji yetu imelala, siyo ofisini, bali majumbani mwao na ofisi imefungwa. Tulilazimika kuyasubiri mavivu yetu yajivute wakati kumekucha kabisa, napo taratiiibu na tukagongewa passport zetu. Tulikaa upande wa Tanzania kwa saa 5. Je, unaweza kujiuliza kwa kutuchelewesha pale ni watu wangapi walichelewa katika biashara zao? Haya, wakati Kenya usiku ndo wanafanya biashara nchi nzima, maana usafiri unaendelea, ati Tanzania waliambiwa na Ziraili kuwa ikifika saa 4 usiku mabus yasisafiri kuna ajali. Utalinganaje na Kenya, wakati wao usiku wanafanya kazi, Tanzania wanalala, na huenda ndo nchi pekee duniani ambayo huzuia watu wake kusafiri usiku. Wanatuzidi kwa mengi, tena yaliyo chini ya uwezo wetu! Utadhani tumeshushiwa laana! Kipindi hicho ili ufike Mwanza, ilibidi upitie Kenya, maana yake tulikuwa tunawapelekea uchumi. Kisa, barabara. Sitaki kuendelea ntalia bure.....

Like mkuu! Natumia simu,
 
Wametushinda vingi ikiwemo jana kupitisha sheria kwamba wabunge lazima wawe na angalau degree ya kwanza ili waweze kutoa hoja zenye mashiko badala ya jazba!

Natamani Bunge hili mwaka ujao lipitishe sheria kama hiyo ili wabunge wenye wasiokuwa na angalau shahada ya kwanza waende shule kwanza.

Ikipitishwa naona kama makundi kwa makundi ya wabunge wakienda kusoma BBA jioni pale UDOM!
 
Wametushinda vingi ikiwemo jana kupitisha sheria kwamba wabunge lazima wawe na angalau degree ya kwanza ili waweze kutoa hoja zenye mashiko badala ya jazba!

Natamani Bunge hili mwaka ujao lipitishe sheria kama hiyo ili wabunge wenye wasiokuwa na angalau shahada ya kwanza waende shule kwanza.

Ikipitishwa naona kama makundi kwa makundi ya wabunge wakienda kusoma BBA jioni pale UDOM!

Hivi wanao wabunge wa KUTEULIWA kama wetu?
 
Historia ndio kikwazo kwa watanzania kwani historia inatufundisha kuwa kutokuwa na ukabila kunadumaza maendeleo.pili kutokuwa na migongano pia ni tatizo kubwa kwani watu wataishi kama watoto wa baba mmoja na kutofikiri mbele zaidi.na ndio matatizo yatukumbayo watanzania wengi sana,ki ukweli kenya wanatuzidi miundombinu lakini so case kivile mpaka tujione hatufai mbele yao.mimi kubwa naloliona ni tatizo tukijilinganisha nao ni kuhusu elimu hasa ukianzia sekondari,watanzania hatuumizi vichwa kwa kutaka elimu mteremko na ya kuibiaibia ndio sababu unapokuwa na mkenya ktk kutafuta kazi lazima ataonekana anajiamini kwa hilo na kuthaminiwa zaidi kwenye ajira.tuondokane na dhamira ya uwoga na kujua vitu sio kufatilia siasa zaid,miziki vitu ambavyo havimjengi mtu kupambana kimataifa,badala yake kufanya kile ambacho kinaushindani zaidi ili kukabiliana na haya yote.ni mtazamo tu waungwana
 
Nyie wavivu sana kufanya kazi, nenda kwenye mashirika yenye wakenya hapa Tanzania utakuta wabongo wanalia lia eti wanaonewa! mmekalia uvivu tu

Hii imesababishwa na kurithi culture ya Waarabu,kuendekeza uswahili na makao makuu ya nchi kuwa Pwani yaani Dar es salaam.
 
Ukikutana nao nje ya nchi wana confidence za kufa mtu. wakiwa kwao hawataki longo longo na kama hawaelewani watapigana mikwaju kisha wanadeliver

Tazama KTN au KBC picha ziko clear, news zimetulia, watangazaji wametulia

Soma gazeti la NATION au Standard...huwezi fananisha na lile gazeti la Michuzi (daily nyuz) au lile la copy and paste (guardian)

sisi tuna watu wengi zaidi, rasili mali nyingi zaidi, wanasiasa wengi zaidi, vyama vya siasa vingi zaidi, magazeti mengi zaidi, JF ndio zaidi, cabinet yetu kubwa kuliko ya kwao, katiba yao (na mahakama ya kadhi ndani) ndio walipitisha, sasa kwa nini hawa wana deliver na sisi hatuna kitu?

I've tried to hate them lakini nimeshindwa, cant hate their ambition esp based on their national interest.

Halafu wao kujenga li Superhighway kama hili ili iweje?

ahh sisi hata kuthubutu tunashindwa sijui kwa nini
ndio mana nimejiunga nao kukamilisha ule usemi wa "IF YOU CANT BEAT THEM JOIN THEM".nakwenda nao sambamba aye for an aye,tooth for a tooth.[h=3][/h]
 
Mwanzo nilikuwa nikiwachukia wakenya kwa tabia yao ya ujivuni, lakini kuna kipindi nilisoma nao hawa jamaa wako very aggressive kwenye kutafuta maendeleo yaani hawakubali kushindwa, kuna kipindi nilikwenda kutembelea ofisi za shirika moja la kimataifa la uhifadhi wa ndege linaitwa BirdLife International pale Cambridge UK, coordinator wa project za afrika ni mkenya, nilimuuliza kwanini wakenya wenigi ndio wanapata funds kwa ajili ya projects au ni vile uko hapa! alinipa jibu ambalo limekuwa nguzo yangu kuu katika kupigania maendeleo alisema, " My friend, success is lying at the far end corner of failure" Wakenya wamefundishwa kutokukata tamaa! kuanzia pale nimetokea kuhusudu sana juhudi zao! hii inanikumbusha jamaa mmoja aliniambia, "Tatizo la sisi watanzania ni kuwa tunataka pesa bila kufanya kazi, hebu ona waenzetu wachina wanafanya kazi bila kujua pesa itatoka wapi, matokeo yake pesa inakuja!
 
kwa kifupi mafanikio 'sustainable' huja kwa KAZI. Udhaifu wetu kimataifa unatokana na ubabaishaji mwingi, hasa mashuleni na vyuoni na kupenda shortcuts. ELIMU kwetu ni cheti tu. KAZI kwetu ni kutegea na kukinga mwisho wa mwezi. WaTZ kwa kiasi kikubwa hawajui jinsi uchumi unavyofanya kazi. Lazima tuchemshe tu.
 
nchi yenye Form 1 ALIYEFAULU huku hajui kuandika jina lake is simply DOOMED! Hakuna maajabu hapo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom