Hivi nani aliweza kuacha pombe kabisa?

Hivi nani aliweza kuacha pombe kabisa?

Soma nimejibu nini kijana mdogo!
Kuna watu wengi nawajua wameacha pombe kabisa!
Binadamu akinuia kitu lazima atakipata!
AKINUIA!
That’s all
Binadamu wengi..!! wangapi kama sio 3 kati ya 100,000?

Acha kudanganya watu hapa, ukishakuwa mlevi mbwa ndio hivyo tena ni nadra sana kurudia hali yako ya awali.
 
Mimi hapa.

Kwa sasa huwa nakunywa chupa moja ya ciroc kila mwezi.
 
Wazee wenzangu (mabibi na mabwana),
Natumaini mko wazima kabisa.

Mimi ni mwanaume, na nafikisha miaka 30 this year.

Unajua kwenye maisha kuna mambo mengi tunafanya kwa kukusudia yawe mazuri au mabaya, ila mara nyingi tunajutia yale mabaya.

Najuta sana kuwa addicted na Bia, na ninaona kabisa ni adui yangu ila haipiti siku bila kuuweka, this hurts me sana.

Kuna aliyeweza kuacha bia kabisa na aliwezaje?. Natamani niache, chaah! this too much.

NB: Ushauri wa kukaa mbali na vishawishi au mbali na washkaji nishajaribu na haujafaa, maana kiu ya bia hatari sana. Hata ukikaa mwenyewe utaitafuta.
Sijui Kama nimeacha lkn huu ni mwaka wa tisa bila kunywa
 
Ukifanikiwa kuacha nakupa zawadi ya kret moja..mimi nipo kwenye mpango mkakati wa kufanya upembuzi yakinifu wa kuandaa mpango kazi wa namna gani ya kuishi bila kunywa
ntakutafuta Mkuu, kabla ya mwaka kuisha, Ila kreti liwe la maji na Soda, Challenge accepted
 
Mimi ni mmoja wa waioacha pombe . Kila nikipata pesa naweka heshima bar , ila kuna soku nilishukiwa na roho wa bwana akaniambia kila ninapokunywa niandike kumbukumbu . Nilipoona kiasi cha pesa kwa mwezi nimeacha kabisa hata harufu yake siipendi .

Sent using Jamii Forums mobile app
Nalo hili nilifanya,
Mim nilijidai sina hela kwa zaid ya wiki 3, na nina matatizo ya kifedha nione kama ile kampan ya bia itanisaidia,.ila kwenye watu 10, akanisaidia mmoja,.nikaona haina haja kuwa nao, nikawa siend maskan nikitoka Job ni Home, nikaanzisha Hobbies nyingne , na bia nakunywa ijumaa tu, na nimeweza
 
Wazee wenzangu (mabibi na mabwana),
Natumaini mko wazima kabisa.

Mimi ni mwanaume, na nafikisha miaka 30 this year.

Unajua kwenye maisha kuna mambo mengi tunafanya kwa kukusudia yawe mazuri au mabaya, ila mara nyingi tunajutia yale mabaya.

Najuta sana kuwa addicted na Bia, na ninaona kabisa ni adui yangu ila haipiti siku bila kuuweka, this hurts me sana.

Kuna aliyeweza kuacha bia kabisa na aliwezaje?. Natamani niache, chaah! this too much.

NB: Ushauri wa kukaa mbali na vishawishi au mbali na washkaji nishajaribu na haujafaa, maana kiu ya bia hatari sana. Hata ukikaa mwenyewe utaitafuta.
Ukitaka kuacha Pombe tafuta Mdizi uchane katkat utakuta kile kama kamrija iv kaponde ponde iv alaf yale majimaji yake yanywe fanya ivo kwa siku tatu asubuh na jion na kuanzia hapo ukinywa pombe utatapika kupindukia na kuanzia hapo pombe itakua Basi. Sitanii wakuu mtu afanye hvo then arud hapa kutoa shuhuda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom