Hivi nani aliweza kuacha pombe kabisa?

Hivi nani aliweza kuacha pombe kabisa?

Binafsi nlikua nakunywa sana pombe lakini sikuwa naona faida yoyote. Nalewa...hangover kichwa kinauma. Nalewa....nikasema hivi napata faida gani.

Nikawakimbia marafiki wote walevi.

Sent using my NOKIA torch
Then ukawa tajiri...
 
Mimi kila siku napambana niache Pombe, hii vita nimeianza 2013 hadi Leo inanishinda ila sijakata tamaa, Mimi naweza kunywa Mara moja au mbili kwa wiki ila sasa nikinywa inanidrive hatari, naona kabisa hii ni destructive path ila inakuwa ngumu kuacha.
Baada ya maelezo yote hayo Leo Nina mwezi toka sijanywa, nataka kuquit kabisa this time

Sent using Jamii Forums mobile app

Mungu akusaidie katika safari yako ya matumaini, lakini kuacha pombe siyo rahisi hivyo, otherwise TBL ingekuwa ishafungwa kama kuacha kungekuwa rahisi
 
Mkuu INAWEZEKANA KABISA kama UKIAMUA.
Mimi nilianza kinywa pombe nikiwa na miaka 14,nilikunywa aina mbalimbali zza pombe,(za kienyeji na zenye TBS)
Unywaji ulikiwa ni wa Kiwango cha KULEWA.
Unywaji wangu ulichanganya na uvutaji sigara bangi.
Baada ya miaka 7 nikiwa na miaka 22, NILIACHA VYOTE NDANI YA SIKU MOJA.
Nilienda kwenye IBADA kanisa la WALOKOLE na mwishoni mwa IBADA waliita watu KUOKOKA,nikafanya hivyo.
Kuanzia hapo KIU ya vyote hivyo iliisha,leo ni mwaka wa16 nimeachana na ULEVI!
ASANTE YESU kwa muujiza huu.

So mkuu 22+16 ni 38?
 
Sijaacha pombe kabisa, so this is a little bit off.

Mimi niliweza kuacha pombe kwa mwakamzima mwaka juzi, na hata sasa nikiamua kuacha naacha.

Na nikiamua kuacha, sharti langu ni kwamba niwe na mizinga ya Scotch Whisky isiyopungua mitatu ndani, na bia ziwe kwenye friji.

Halafu naamua kuacha huku naziona hizo pombe kila siku.

Hapondipo najua nimeamuakuacha.

Nikiwa sina pombe ndani, halafu nasema nimeacha, nakuwa sina uhakika kama nimeacha kweli, au nimeishiwa pombe tu.

Mimi huwa natofautisha kuacha na kuchwa na pombe hivi,
kuacha: Ni pale uko na pesa au uwezo wa kupata pombe lakini Voluntarily unaamua kutokunywa
kuachwa: Ni pale uko na kiu ya kupiga monde na nia lakini kwa kuwa huna pesa/access na pombe basi unaacha/unaachishwa kunywa.
 
Mimi niliacha Pombe mwaka juzi siku hizi nakunywa tu bia. Kwangu bia sio pombe hazinileweshi.
 
Mimi huwa natofautisha kuacha na kuchwa na pombe hivi,
kuacha: Ni pale uko na pesa au uwezo wa kupata pombe lakini voluntary unaamua kutokunywa
kuachwa: Ni pale uko na kiu ya kupiga monde na nia lakini kwa kuwa huna pesa/access na pombe basi unaacha/unaachishwa kunywa.
Ndiyo maana nikasema nikiacha pombe ni lazima niwe na mizinga ya Scotch mitatu ndani, na bia za kutisha kwenye friji.

Najiridhisha kwamba nina access na pombe lakini naamua kutokunywa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dawa ya kuacha pombe ni maziwa freshi ya ng'ombe,
Dozi: kunywa vikombe 3 asubuh, na jioni vikombe 2 kabla ya kula, na kikombe kimoja baada ya kula (dinner) kila siku, after 7 days, hata ukilala TBL hunywi kamwe!
kuwa serious basi,una uhakika na hii tiba
 
Back
Top Bottom