Hivi nani aliweza kuacha pombe kabisa?

Hivi nani aliweza kuacha pombe kabisa?

Mkuu Acha Ujinga, Uache Pombe Uende Kwenye Nini! FUTA HILO WAZO!
 
maana kiu ya bia hatari sana. Hata ukikaa mwenyewe utaitaf

Screenshot_2018-08-27-23-11-11-1.png
 
Wazee wenzangu (mabibi na mabwana),
Natumaini mko wazima kabisa.

Mimi ni mwanaume, na nafikisha miaka 30 this year.

Unajua kwenye maisha kuna mambo mengi tunafanya kwa kukusudia yawe mazuri au mabaya, ila mara nyingi tunajutia yale mabaya.

Najuta sana kuwa addicted na Bia, na ninaona kabisa ni adui yangu ila haipiti siku bila kuuweka, this hurts me sana.

Kuna aliyeweza kuacha bia kabisa na aliwezaje?. Natamani niache, chaah! this too much.

NB: Ushauri wa kukaa mbali na vishawishi au mbali na washkaji nishajaribu na haujafaa, maana kiu ya bia hatari sana. Hata ukikaa mwenyewe utaitafuta.
Ukitaka kuacha, anza kwa kubadili user name. Jiite hata novida mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni uamuzi tu!
Mimi nilikuwa nikiona tangazo la bia kwenye tv koo linaita ile mbaya!
Nilifanya maamuzi ya kuacha baada ya kuona maisha yangu yanaelekea kubaya,yani ukijenga imani kuwa unaacha ni rahisi tu sasa hivi ni mwaka wa saba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kuushinda Moyo wako tu.

Yaani inawezekana sana
 
Anza na kubadili ID yako.

Kataa kujitambulisha kama pombe!!
Majina huwa hayana kitu juu yetu iwapo tu tumeyabebesha maana ya KUTUTAFSIRI!!

Unakunywa kila siku.
Unaamini kuacha pombe hakuwezekani.
Unakosa utashi wa kutokutamani.
Unajitambulisha kwa jina la pombe.

ANZIA HAPO KWANZA!!
 
Ilikuwaje?interesting na.mnanipa Moyo
INAWEZEKANA!!
.kila mwanadamu ana URAIBU wake.
Watu wanapigana na URAIBU mbalimbali na wanafanikiwa.

Wengine tunapigana na kuacha sigara.
Wengine tunapigana na kuacha ngono.
Wengine tunapigana na kuacha madawa ya kulevya.
Wengine tunapigana na kuacha kuchat
Wengine tunapigana na kuacha ulawiti

So my dear!!
KUBALI KUWA INAWEZEKANA!!
WEKA NIA.!!
ANZA KUFANYIA KAZI!!

BE BLESSED!!
 
Mimi kila siku napambana niache Pombe, hii vita nimeianza 2013 hadi Leo inanishinda ila sijakata tamaa, Mimi naweza kunywa Mara moja au mbili kwa wiki ila sasa nikinywa inanidrive hatari, naona kabisa hii ni destructive path ila inakuwa ngumu kuacha.
Baada ya maelezo yote hayo Leo Nina mwezi toka sijanywa, nataka kuquit kabisa this time

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wazee wenzangu
(mabibi na mabwana),
Natumaini mko wazima kabisa.

Mimi ni mwanaume, na nafikisha miaka 30 this year.

Unajua kwenye maisha kuna mambo mengi tunafanya kwa kukusudia yawe mazuri au mabaya, ila mara nyingi tunajutia yale mabaya.

Najuta sana kuwa addicted na Bia, na ninaona kabisa ni adui yangu ila haipiti siku bila kuuweka, this hurts me sana.

Kuna aliyeweza kuacha bia kabisa na aliwezaje?. Natamani niache, chaah! this too much.

NB: Ushauri wa kukaa mbali na vishawishi au mbali na washkaji nishajaribu na haujafaa, maana kiu ya bia hatari sana. Hata ukikaa mwenyewe utaitafuta.
Mkuu hata Mimi napitia the same situation naeza kaa wiki nsinywe ila nikirudi balaa yani nakuwa kama nimejiunga bando la konyagi la mwezi mzima inaniumiza sana
 
Ukitaka kuacha Pombe tafuta Mdizi uchane katkat utakuta kile kama kamrija iv kaponde ponde iv alaf yale majimaji yake yanywe fanya ivo kwa siku tatu asubuh na jion na kuanzia hapo ukinywa pombe utatapika kupindukia na kuanzia hapo pombe itakua Basi. Sitanii wakuu mtu afanye hvo then arud hapa kutoa shuhuda

Sent using Jamii Forums mobile app
Like serious?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi nilianza kunywa pombe (beer) mwaka 2001 baada ya kupata ajira kwenye taasisi moja ya kiserikari,hii ilitokana na kuambatana na marafiki ambao walikuwa mapampula.Ila nilikuwa na matatizo yafuatayo: nikilewa nakuwa mkorofi kupindukia,pia nikishalewa nashindwa kuvuka barabara hii ya kigogo pale landa bar pamenitesa sana hasa usiku gari iko kigogo mwisho ikinipiga mwanga tu hata nipo katikati ya barabara nitarudi kuanza upya,mwisho asbh nilikuwa nikiamka kichwa kinauma hatari naambiwa dawa yake nikazimue tena pombe. Nikafikiria mwisho nikaamua kuachana na marafiki pampula na kuanza maisha kivyangu mpaka bia naiona kama tako la mama mkwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
Haaahaaa....kwenye kuvuka barabara umenifurahisha[emoji23] [emoji23] [emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom