Hivi nani aliweza kuacha pombe kabisa?

Hivi nani aliweza kuacha pombe kabisa?

Raha Banana wanaiita Nax. Ile ya Ulomi ya miaka ya 2000 hivi mpaka 2004 chini ya chupa lazima ukute uji na majani ya mgomba
kweli mkuu banana za 2000-2004 zilikuwa kali sana ukipigaa 3 aisee we kiboko unafungua banana dakika kama kumi hivi maana ukikosea unakuta nusu chupa
 
hiyo ni roho mbaya inakutesa sasa
Amua mwenyewe kuwa hutaki tena kunywa pombe, epuka mazingira yanayokupelekea au yanayokushawishi kunywa pombe, pia muombe Mungu akusaidia kushindana na hiyo kiu ya pombe
 
Wazee wenzangu (mabibi na mabwana),
Natumain mko wazima kabisa..

Mim Mwanaume, na Nafikisha miaka 30 this year,.

Unajua kwenye maisha kuna mambo meng tunafanya kwa kukusudia yawe mazuri au mabaya, ila mara nyingi tunajutia yale mabaya...

Najuta sana kuwa addicted na Bia, na ninaona kabisa ni adui yangu ila haipit siku bila kuuweka, this hurts Me sana...

Kuna aliyeweza kuacha bia kabisa na aliwezaje?. Nataman niachee, chaah! this too Much

NB: ushaur wa kukaa mbali na vishawishi au mbali na washkaj nishajarib na haujafaa, maana kiu ya bia hatar sana,. Hata ukikaa.mwenyewe utaitafuta.
Mimi hapa. Nilipokuwa chuo nilikuwa cha pombez sana... yaan mim kuwa bwax ni kawaida. Kabla ya kumaliza chuo kuna tukio lilinipata.. lilinivuruga akili, kisaikologia nikapoteza hamu ya pombe kabisa kabisa. Yaan nikaona kama vile haina ladha tena.
Nimeacha mpaka leo.

Nadhani mtoa mada hujawi kukutana nao sababu reference umejitolea mfano wewe. Watu hawako sawa, wapo walio amua na wakaweza. It is down to maamuzi japo si rahis
 
Dawa ya kuacha pombe ni maziwa freshi ya ng'ombe,
Dozi: kunywa vikombe 3 asubuh, na jioni vikombe 2 kabla ya kula, na kikombe kimoja baada ya kula (dinner) kila siku, after 7 days, hata ukilala TBL hunywi kamwe!

Mhuuuu ya kweli haya? Nsije poteza pesa zangu za bia bure kwa kutaka kuipa taraka pombe in a wrong way. Na pombe ikihisi unataka kuiacha hahahaha utaisom namba, mpaka binti mlokole anaweza kukupa ofa
 
Brother, mtu anahitaji concrete solution..mimi mwenyewe nimeshafanya hivo.
Kukaa mbali na wana,kujikaza kisabuni..Ila dah
Najikuta nakaa mwenyewe mara kabaam..nishasukutua na castle lite 2 baridi..
Ahaaa... Yataka moyo.. Ukivikimbia vishawishi itakua hujaweza kujipima juu ya maamuzi yako..
 
Nilipumzika miaka miwili ila nilivyowasha gari tena ni balaa,hapa naandika hii post nna hangover hatari hadi job nmeshindwa kwenda! NAMI NATAMANI KILA SIKU NIACHE ILA NAJIKUTA NSHAKUNYWA.

Teh teh! Wewe kiboko, ila kama uliweza miaka miwili ilipaswa uache kabisa dakika hii. Naona umeingia na nguvu mpya
 
Nilipumzika miaka miwili ila nilivyowasha gari tena ni balaa,hapa naandika hii post nna hangover hatari hadi job nmeshindwa kwenda! NAMI NATAMANI KILA SIKU NIACHE ILA NAJIKUTA NSHAKUNYWA.

Dah nimecheka sana, kuna kipindi nilipambana na hali yangu kuacha pombe ila nilipopata pesa tu, nkajikuta mkononi nko na Safari baridi
 
Dawa ya kuacha pombe ni maziwa freshi ya ng'ombe,
Dozi: kunywa vikombe 3 asubuh, na jioni vikombe 2 kabla ya kula, na kikombe kimoja baada ya kula (dinner) kila siku, after 7 days, hata ukilala TBL hunywi kamwe!

Ngoja niijaribu hii weekend ya leo
 
ukiamua unaweza....wewe mwenyewe kuamua......wala usikwepe kwenda maeneo.....weka moyoni mwako....sinywi pombe tena....full stop...
 
Duh pole sana....mbona bia sio issue....unaweza kaa hata miaka miezi etc.
 
Nakushauri ubadili id yako kwanza jiite hata mwanakondoo wa bwana hakika utaacha tu

Nakutakia mafanikio mema
 
Back
Top Bottom