Tlaatlaah
JF-Expert Member
- May 18, 2023
- 36,413
- 30,966
Gentleman,Huwa najiuliza, viongozi wa hii nchi wana akili timamu kweli? Yaani wanajua kabisa raia wao wengi hawana elimu na wamejirundika Dar es Salaam kwa ajili ya jina. Kwanini wasiifanye wilaya ya Kibaha kuwa ndani ya Dar es Salaam ili watu wasambae kujenga huko?
Maana naona kutoka Kibaha mpaka Mbezi Magufuli ni karibu kuliko kutoka Kariakoo mpaka Mbezi Magufuli, ambapo ndio kituo kikubwa cha mabasi Tanzania. Aisee, namuomba Rais wetu Samia aipanue Dar es Salaam kwa kuchukua ardhi ya Kibaha, maana hata daladala zinapandisha nauli kila siku kwa kigezo cha Kibaha kuwa mkoa mwingine, wakati unakuta umbali ni mdogo tu.
kibaha, mkuranga na kisarawe vitaendelea kua sehemu ya mkoa wa Pwani kimkakakati ili kusogeza huduma za kijamii karibu zaidi na wananchi na kupunguza msongamano wa wananchi ndani ya jiji la Dar es salaam, lakini pia kuchochea na kuongeza shughuli na fursa za kiuchumi maeneo hayo na kupanua zaidi mkoa wa Pwani uweze kushikamana na Morogoro na hatimae Dar-Moro kue karibu zaidi kuliko dar-mkuranga kimkakati zaidi 🐒