Bado mtoa mada ana hoja nzri. Ni mda sasa kuzuia ujenzi holela jijn Dar. Yaani usmamizi wa maendeleo ya ardhi ni very poor. Unakuwa a squatters Dar kwa ukosefu a ardhi na mipango miji wakati mkoa jrani wa Pwani kuna ardhi ya kutosha. Kinahotakiwa ni kupima maeneo ya kutosha tena kuanzi SQM 1000, mji upanuke kwa ukisasa. Hata tuungae na MORO mradi miundobinu iwpo tu.
Mkoa wa Pwani ugawanywe
Kibaha, Bagamoyo, Kisarawe na Mkuranga ziunde jiji la Dar Es Salaam.
Rufiji, Kilwa, Mafia na Kibiti ziunde Mkoa wa Pwani/Rufiji/Kilwa.
Mikoa miwili ya Tanzania bara yaani Morogoro na Tabora iwe mikoa ya Viwanda vikubwa/vizito zaidi na technologia ya majeshi yetu na taasisi nyingine kama za matibabu.
Hapa naamanisha Viwanda vizito vyote visiendelee kujengwa Mkoa wa Pwani tena bali vielikezwe Morogoro na Tabora na Viwanda vyepesi viendelee kujengwa Mkuranga kama eneo la rasmi la Viwanda, huku Bagamoyo, Kibaha na Kisarawe yawe makaazi tu lakini serikali ipime maeneo hayo yote ili kuepuka ujenzi holela wa makaazi, hii inalenga upanuzi wa Jiji la Dar Es Salaam.
Serikali ichore ramani mpya ya Dar Es Salaam ikiunganisha Halmashauri hizo katika miundombinu ya Barabara za kisasa, Reli, umeme, Maji, pia serikali itenge eneo kubwa zaidi kule Kisarawe kwa ajili ya ujenzi wa uwanja mwingine wa ndege, yawezekana miaka 50 mpaka 70 ijayo kutoka leo uwanja wa ndege wa Mwalimu Julias Nyerere utazidiwa kutokana na maendeleo makubwa na upanuzi wa miundombinu ya usafiri wa Anga.
Viwanda vyote ambavyo vimejengwa tayari Mkoa wa Pwani vibakie hivyo hivyo na/au vinaweza kuhamishwa hasa vile vizito na kuelekezwa Morogoro na Tabora.
Morogoro iwe sehemu ya kilimo cha kimkakati na Viwanda vikubwa/vizito ikiwemo na taasisi za utafiti wa kisayansi za majeshi yetu na technologi nyingine zielekezwe Morogoro na Tabora.
Na,
Nicolas J Clinton Gabone