Skyline ya jiji la Dar es Salaam imepanuka sana

Skyline ya jiji la Dar es Salaam imepanuka sana

Traxtion

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2021
Posts
7,604
Reaction score
15,535
Miaka ya nyuma, skyline ya Dar es Salaam ilikuwa simple sana, majengo machache marefu, mengi yakiwa ya kati tu. Lakini leo hii, mji umebadilika kwa kasi kubwa ajabu.

Maeneo kama Posta, Upanga, Masaki na Kariakoo yameanza kujazwa na majengo ya kisasa (high-rise buildings), mengi yakiwa na ofisi, hoteli na apartments za kisasa.

Miradi mikubwa kama commercial towers, shopping complexes na mixed-use buildings imechangia sana kuibadilisha sura ya jiji.
Infrastructure nayo imeboreshwa, barabara, BRT, na huduma zingine nk na hii imefanya maeneo mengi yawe attractive kwa maendeleo ya majengo marefu.
Kwa sasa, skyline ya Dar imeshazidi miji mingi mikubwa Africa, na bado ukuaji unaendelea.
Kwa hiyo inapaswa tukaze buti kuhakikisha tunatatua changamoto za jiji hili kadri tuwezavyo ili lianze kuwa na hadhi za kimataifa

Shukrani kwa YouTube channel ya Bertin, kuendelea kuionesha Tanzania watu wapate kuona upande mwingine wa Tanzania apart from Safari, Zanzibar beaches na CCM

1. Dar es Salaam City Centre
Screenshot_20260325-123905.png
Screenshot_20260325-123954.png
Screenshot_20260325-124023.png


2. Kariakoo
Screenshot_20260325-124049.png


3. Upanga
Screenshot_20260325-124121.png
Screenshot_20260325-124354.png


4. Old Dar es Salaam
Screenshot_20260325-124142.png


5. Silicon Dar es Salaam
Screenshot_20260325-124206.png


6. Ilala
Screenshot_20260325-124231.png


7. Msasani Peninsula
Screenshot_20260325-124246.png


8. Morocco
Screenshot_20260325-124304.png


9. Sam Nujoma Road
Screenshot_20260325-124325.png
 
Dar Salaam bado ya hovyo, chafu sana na yenye mabanda mengi tu ya kutu na nyumba kama magofu.
Ukianzia Ubungo, Mwenge na Tazara kuelekea upande wa mikoani ni aibu tupu. Zaidi sana tatizo hata sio ukosefu wa maghorofa bali mpango mji mbovu, makazi yako shaghalabagala.
 
Dar Salaam bado ya hovyo, chafu sana na yenye mabanda mengi tu ya kutu na nyumba kama magofu.
Ukianzia ubongo, mwenge, Tazara kuelekea upande wa mikoani ni aibu tupu.
Nilikuwa naongelea skyline ya hayo maeneo niliyopost hapo juu
Hayo maeneo mengine unayotaja ni bad side of Dar, na uwepo wake still hauondoi skyline ya Dar niliyopost
Dar ni kubwa na haiwezi kuwa perfect kila sehemu. Chill
 
Dar Salaam bado ya hovyo, chafu sana na yenye mabanda mengi tu ya kutu na nyumba kama magofu.
Ukianzia ubongo, mwenge, Tazara kuelekea upande wa mikoani ni aibu tupu. Zaidi sana tatizo hata sio ukosefu wa maghorofa bala mpango mji mbovu, makazi yako shaghalabagala.
hapa nchinin kwetu hata sisi raia ustaarabu wetu upo wa kiwango cha chini sana achilia mbali ufuatiliaji wa mamlaka
 
Skyline ndio rubbish gani ?, ukimbukeni na ushamba .Miji kama Frankfurt ni miji misafi imepangika na Ina miundombinu ya kisasa na inavutia watu kuishi kuliko hizo shitholes zenu mnazoita majiji ,DAR no uozo na taka taka tupu ,haina hata hadhi ya kuitwa jiji ,total rubbish .Mji usio hata na drainage system mji gani huo ,mvua kidogo tu mafuriko ya mavi na mikojo + matope na takataka barabarani ,majengo ndio usiseme , takataka na uvundo na harufu mbaya
 
Dar Salaam bado ya hovyo, chafu sana na yenye mabanda mengi tu ya kutu na nyumba kama magofu.
Ukianzia ubongo, mwenge, Tazara kuelekea upande wa mikoani ni aibu tupu. Zaidi sana tatizo hata sio ukosefu wa maghorofa bala mpango mji mbovu, makazi yako shaghalabagala.
Hao ndio waTZ na ndio uchumi wao. Ukikua wataboresha.

Huwezi kupamba JIJI kwa kuficha masikini.
 
Nilikuwa naongelea skyline ya hayo maeneo niliyopost hapo juu
Hayo maeneo mengine unayotaja ni bad side of Dar, na uwepo wake still hauondoi skyline ya Dar niliyopost
Dar ni kubwa na haiwezi kuwa perfect kila sehemu. Chill
Skyline haina maana sana, kwa wakazi wengi wa mji, hiyo skyline inawahusu watatu chache sana wa Dar.
 
Uzuri wa mji sio maghorofa ya kilofa takataka hayo yaliyojengwa bola tata standards ,tembea duniani muone watu wanavyoishi na jinsi miji ilivyopangika na Kuwait na standards na kuvutia
Taja mji mmoja huko duniani
 
Skyline ndio rubbish gani ?, ukimbukeni na ushamba .Miji kama Frankfurt ni miji misafi imepangika na Ina miundombinu ya kisasa na inavutia watu kuishi kuliko hizo shitholes zenu mnazoita majiji ,DAR no uozo na taka taka tupu ,haina hata hadhi ya kuitwa jiji ,total rubbish .Mji usio hata na drainage system mji gani huo ,mvua kidogo tu mafuriko ya mavi na mikojo + matope na takataka barabarani ,majengo ndio usiseme , takataka na uvundo na harufu mbaya
Nimeona hii kitu kwa Watanzania, ni tofauti na Wakenya kidogo. Ukikuta post inasifia Kenya basi wakenya watakuja kuipamba nchi yao kwenye comments section lakini post za kusifia Tanzania, wabongo hawataki kabisa wanaanza kupondea in comment section as if kila kitu Tanzania ni kibaya
Mfano hapa, there's nothing wrong with having a good skyline lakini for unknown reason imekukasirisha kuiona
Mada inahusu skyline, sio siasa wala kitu chochote
Lazima kuna psychological reason for this. So nimeuliza ChatGPT kwa nini Watanzania wanapenda kupondea nchi yao kwa kila kitu
Baada ya kusoma majibu nimeelewa


1. Frustration ya maisha ya kila siku
Watu wengi wanakutana na matatizo kama miundombinu mibovu, foleni, uchafu, au huduma mbovu. Hivyo wanatoa hasira zao kwa kuikosoa nchi yao, kama ilivyo kwa mfano wa Dar es Salaam kwenye hiyo post.

2. Kulinganisha na nchi zilizoendelea
Watu wakiona miji kama Frankfurt ilivyo safi na organized, wanaanza kuona kwao hakuna kitu kizuri. Lakini mara nyingi wanalinganisha bila kuzingatia tofauti za historia, uchumi, na mipango ya muda mrefu.

3. Inferiority complex (kujiona duni)
Baadhi ya watu wanaamini kila kitu cha nje ni bora kuliko cha nyumbani. Hii inafanya hata maendeleo yaliyopo yasionewe thamani.

4. Culture ya kulalamika mtandaoni
Mitandao imefanya iwe rahisi sana ku-criticize kuliko kusifia. Negative posts hupata attention zaidi, hivyo watu wanaendelea kuandika hivyo.

5. Ukosefu wa uelewa wa progress
Watu hawafuatilii mabadiliko taratibu. Mfano, skyline ya Dar imekua sana miaka ya karibuni, lakini kwa mtu anayekaa kwenye matatizo ya kila siku, hilo halionekani muhimu.
 
Dar Salaam bado ya hovyo, chafu sana na yenye mabanda mengi tu ya kutu na nyumba kama magofu.
Ukianzia ubongo, mwenge, Tazara kuelekea upande wa mikoani ni aibu tupu. Zaidi sana tatizo hata sio ukosefu wa maghorofa bala mpango mji mbovu, makazi yako shaghalabagala.
Mpiga picha amejitahidi sana sana sana kupiga picha hizo picha ungekua wewe usingeweza kutoa vizuri hivyo ungeenda kupiga mabati yenye kutukutu kule Tandale Shimoni na kuzipost na kuwaambia hii ndio Dar-es-Salaam sio ile yenye maghorofa marefu
 
Mpiga picha amejitahidi sana sana sana kupiga picha hizo picha ungekua wewe usingeweza kutoa vizuri hivyo ungeenda kupiga mabati yenye kutukutu kule Tandale Shimoni na kuzipost na kuwaambia hii ndio Dar-es-Salaam sio ile yenye maghorofa marefu
Sehemu kubwa ya Dar es Salaam inafanana na Tandale shimoni.
 
Skyline haina maana sana, kwa wakazi wengi wa mji, hiyo skyline inawahusu watatu chache sana wa Dar.
Sawa hiyo skyline inahusu wachache lakini ni nzuri. Mada inahusu hiyo skyline, sio maisha ya wakazi wa Dar es Salaam
Sio kila kitu kinahusu maisha ya watu, siasa nk. Kuna watu wengi wanapenda skyline na mada specific for skyline zipo. Sikatai madai yako lakini ni nje ya mada
 
Dar takataka inazidiwa hata na Kigali , vi nchi masikini lakini vinajitahidi kupangilia miji yao na kuifanya kustaarabika,kuvutia na mahali panapofaa mtu kuishi,Miji ya Tanzania ni mazizi ya ng'ombe na nguruwe
 
Back
Top Bottom