Mcanada
JF-Expert Member
- Jun 8, 2020
- 982
- 1,904
Habari ya ijumaa wadau wa JF muda huu nimejiunga na azam max hapa nitazame mechi ya fainali ya mapinduzi cup huku nikiendelea na kazi but nimepata ukakasi kwa kile nilichokuwa nakisikia mara kwa mara kutoka kwa mtangazaji Gharib Mzinga kwa namna anavyopenda kutumia neno "madhambi" kwenye matangazo ya mchezo wa mpira wa miguu na si huyu tu kuna baadhi ya watangazaji wa azam tv pia wanapenda kutumia neno madhambi wanapotangaza mechi za mpira wa miguu..
Swali langu kwanini baadhi ya watangazaji hawa wanapenda kutumia neno hilo ikiwa mpira wa miguu si mchezo mtakatifu/msafi (kiuhalisi mpira wa miguu ni mchezo mchafu) vipi wewe mtangazaji useme mchezaji "Bubu" kamchezea "Madhambi" Mchezaji "Kijeba" ikiwa unaweza kutumia neno Faulo ukimaanisha mchezaji kumchezea ndivyo sivyo/kinyume cha sheria mchezaji mwingine? nyinyi watangazaji wa kizazi cha low IQ ndio chanzo cha king'amuzi chenu kudharaulika .. Badilikeni!!
Swali langu kwanini baadhi ya watangazaji hawa wanapenda kutumia neno hilo ikiwa mpira wa miguu si mchezo mtakatifu/msafi (kiuhalisi mpira wa miguu ni mchezo mchafu) vipi wewe mtangazaji useme mchezaji "Bubu" kamchezea "Madhambi" Mchezaji "Kijeba" ikiwa unaweza kutumia neno Faulo ukimaanisha mchezaji kumchezea ndivyo sivyo/kinyume cha sheria mchezaji mwingine? nyinyi watangazaji wa kizazi cha low IQ ndio chanzo cha king'amuzi chenu kudharaulika .. Badilikeni!!