SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 5,129
- 7,898
Jana nilipokuwa nafuatilia gemu ya Yanga, nilikuwa nasikia mahaba ya kupitiliza kwa timu ya Yanga kutoka kwa mtangazaji Baraka Mpenja na hii siyo mara ya kwanza kuliona hili.
Jana alikuwa anatoa kauli kama "upande wa pili nao watakuwa wakienda chooni wanasema Yanga kweli anapiga mpira mwingi" na kauli aliyokuwa anairudia mara nyingi ni "huu ni mpira wa kitabuni, siyo mpira wa papatu papatu". Ulikuwa unawalenga kina nani kwa kauli hizo?
Viongozi wa Simba nao waamke, hali iliyokuwepo msimu uliopita ya kuishi kinyonge haitaifikisha hii timu popote. Karibia media zote sasa hivi ziko kwenye payroll ili kuichafua Simba. Mnaweza kuyaona haya mambo ni madogo ila media ina nguvu sana inaweza kuupamba uongo hadi ukaonekana kweli.
Azam kiujumla ni kama wamekuwa na bifu na Simba ndiyo maana wanasimba wengi wanafurahi mnapofanya vibaya. Uwanjani mnaikamia Simba halafu Yanga wanajipigia wanavyotaka.
Mechi zinazochezwa uwanja wa Uhuru hawafanyi coverage nzuri, Camera ya muhimu inawekwa chini na muda wote unaona kwanza mabenchi na nguzo kabla haujawaona wachezaji waliopo uwanjani. Mechi za mikoani hawaweki camera za kuonyesha offside, matokeo yake minong'ono kuwa Simba inabebwa na marefa inakuwa na nguvu bila ushahidi wa kutosha. Inabidi wawepo watu ndani ya Simba kuhakikisha mechi zake hasa zile za nyumbani zinatangazwa ipasavyo.
Kwa ujinga huu ndiyo maana wengine ikifika makundi tu ya CAF tunaswitch DSTV. Watangazaji wa nje wanatoa facts siyo mahaba binafsi na pia hawatangazi mpira kama wako redioni.
Nimemaliza.
Jana alikuwa anatoa kauli kama "upande wa pili nao watakuwa wakienda chooni wanasema Yanga kweli anapiga mpira mwingi" na kauli aliyokuwa anairudia mara nyingi ni "huu ni mpira wa kitabuni, siyo mpira wa papatu papatu". Ulikuwa unawalenga kina nani kwa kauli hizo?
Viongozi wa Simba nao waamke, hali iliyokuwepo msimu uliopita ya kuishi kinyonge haitaifikisha hii timu popote. Karibia media zote sasa hivi ziko kwenye payroll ili kuichafua Simba. Mnaweza kuyaona haya mambo ni madogo ila media ina nguvu sana inaweza kuupamba uongo hadi ukaonekana kweli.
Azam kiujumla ni kama wamekuwa na bifu na Simba ndiyo maana wanasimba wengi wanafurahi mnapofanya vibaya. Uwanjani mnaikamia Simba halafu Yanga wanajipigia wanavyotaka.
Mechi zinazochezwa uwanja wa Uhuru hawafanyi coverage nzuri, Camera ya muhimu inawekwa chini na muda wote unaona kwanza mabenchi na nguzo kabla haujawaona wachezaji waliopo uwanjani. Mechi za mikoani hawaweki camera za kuonyesha offside, matokeo yake minong'ono kuwa Simba inabebwa na marefa inakuwa na nguvu bila ushahidi wa kutosha. Inabidi wawepo watu ndani ya Simba kuhakikisha mechi zake hasa zile za nyumbani zinatangazwa ipasavyo.
Kwa ujinga huu ndiyo maana wengine ikifika makundi tu ya CAF tunaswitch DSTV. Watangazaji wa nje wanatoa facts siyo mahaba binafsi na pia hawatangazi mpira kama wako redioni.
Nimemaliza.