Hii ndio inaitwa kuupiga mwingi, gharama za bando zimepanda tena

The Assassin

JF-Expert Member
Oct 30, 2018
4,355
17,321
Ndani ya kipindi kifupi gharama ya bando/bundle ya internet imepanda kwa zaidi ya 45%.

Sisi watumiaji wa Vodacom tulikua tunanunua kifurushi cha Mwezi kwa shilingi elfu 50 na kupata GB 50.

Haikukaa muda kifurushi kikapanda gharama badala ya kupata GB 50 tukapewa GB 37. Mwezi March/April mwaka huu kikapanda tena ama kwa maana nyingine thamani ya shilingi ikashuka tena tukapata GB 32.

Leo nimejaribu kununua kifurushi kile kile kwa Elfu 50 nimepata GB 28.

Hii kiuchumi ni kwamba ndani ya mwaka mmoja thamani ya fedha yetu imeshuka kwa 45% ama gharama za maisha zimepanda kwa 45%. Maana yake ni kua kitu ulichokua unaweza kukinunua kwa elfu 50 leo utakipata kwa elfu 80.

Rais wetu kitu kinachoitwa mfumuko wa bei kimemshinda kabisa kudhibiti. Wafanyabiashara na watoa huduma wanajiamulia bei wanayotaka. Tunaoumia ni sisi walaji.

Tanzania kwa sasa hakuna consumer protection, bei zinapanda kila uchwao. Kufikia December mwaka huu GB 1 itakua elfu 5.

Gharama za bando na maisha kwa ujumla kwa miaka 5 ya Magufuli zilikuwa ni zile zile pamoja na janga la Covid, ila ndani ya mwaka mmoja wa Serikali ya kuupigwa mwingi kila kitu kimepanda bei.

Mama endelea kuupiga mwingi.
Screenshot_20220717-173156_Phone.jpg
 
Maisha yanasonga mbele baharia, hayarudi nyuma. Mbona watumishi wamepadishiwa mishahara?

Na wewe pandisha bei kile unachokifanya. Iwe biashara ama huduma.

Ukiwa huna kabisa cha kupandisha bei, basi pandisha bei ya unyumba kwa mwenzi wako.
 
Maisha yanasonga mbele baharia, hayarudi nyuma. Mbona watumishi wamepadishiwa mishahara?

Na wewe pandisha bei kile unachokifanya. Iwe biashara ama huduma.

Ukiwa huna kabisa cha kupandisha bei, basi pandisha bei ya unyumba kwa mwenzi wako.
Tumia akili ndogo tu uliyonayo. Tunaongelea maisha kupanda bei wewe unaongelea watumishi kupandishiwa mishahara, kwani umesikia kila mtu Tanzania ni mtumishi anaesubiri kulipwa mshahara?
 
Tumia akili ndogo tu uliyonayo. Tunaongelea maisha kupanda bei wewe unaongelea watumishi kupandishiwa mishahara, kwani umesikia kila mtu Tanzania ni mtumishi anaesubiri kulipwa mshahara?
Hakuna kitu hakijapanda bei. Wakulima wamepandisha bei ya mazao yao

Wakulima wamepandisha bei ya bidhaa zao

Wafanyakazi mishahara imepanda.

Ngoma droo. Sasa kelele za nn?
 
Ndani ya kipindi kifupi gharama ya bando/bundle ya internet imepanda kwa zaidi ya 45%.

Sisi watumiaji wa Vodacom tulikua tunanunua kifurushi cha Mwezi kwa shilingi elfu 50 na kupata GB 50.

Haikukaa muda kifurushi kikapanda gharama badala ya kupata GB 50 tukapewa GB 37. Mwezi March/April mwaka huu kikapanda tena ama kwa maana nyingine thamani ya shilingi ikashuka tena tukapata GB 32.

Leo nimejaribu kununua kifurushi kile kile kwa Elfu 50 nimepata GB 28.

Hii kiuchumi ni kwamba ndani ya mwaka mmoja thamani ya fedha yetu imeshuka kwa 45% ama gharama za maisha zimepanda kwa 45%. Maana yake ni kua kitu ulichokua unaweza kukinunua kwa elfu 50 leo utakipata kwa elfu 80.

Rais wetu kitu kinachoitwa mfumuko wa bei kimemshinda kabisa kudhibiti. Wafanyabiashara na watoa huduma wanajiamulia bei wanayotaka. Tunaoumia ni sisi walaji.

Tanzania kwa sasa hakuna consumer protection, bei zinapanda kila uchwao. Kufikia December mwaka huu GB 1 itakua elfu 5.

Gharama za bando na maishakwa ujumla kwa miaka 5 ya Magufuli zilikua ni zile zile pamoja na janga la Covid, ila ndani ya mwaka mmoja wa serikali ya kuupigwa mwingi kila kitu kimepanda bei.

Mama endelea kuupiga mwingi.View attachment 2294351
Hii ni bad news kwangu pia. Bye bye kifurushi pendwa changu. Nilipoanza kukitumia nilikuwa natoa 35,000 napata 25G, kikashuka nikapata 22 Gb nikasikitika, leo 20Gb sijui nilie! Naomba alternative wadau niichome moto line ya Voda!
 
Hakuna kitu hakijapanda bei. Wakulima wamepandisha bei ya mazao yao

Wakulima wamepandisha bei ya bidhaa zao

Wafanyakazi mishahara imepanda.

Ngoma droo. Sasa kelele za nn?
Tuache propaganda, tusiwe kama mashetani, hii Nchi imejengwa na Watanzania wa hali ya chini sana .


Kwa Sasa Tunazungumzia INFLATION , hili ni tatizo Kwa Mtanzania .

Serikali inapokua Dhaifu kiasi Cha kushindwa kuwaongoza WAFANYABIASHARA, matokeo yake ni Bei , holela holela.

Inflation Kwa Sasa ni our Common Problem tunayeshea Watanzania wote.

Ikiwa hatua madhubuti hazichukuliwi, basi huwezi KAMWE kujivunia Nyongeza ya 23% ili hali Maisha yako na yanaendelea kua juu.

Kwa hiyo mwaka 2023, 2024 nakuendelea ,wawe wanazidi kuongeza mishahara kama nafuu Kwa wafanyakazi, wakati Masikini wa Nchi hii akitaabika??


VIJANA, HII NCHI INAJENGWA NASISI, TUACHANE NA SIASA MAJITAKA, SIASA ZA UPUMBAVU NA UBWABWAJIKAJI MIDOMO.


HAUPASWI KUA KIPOFU WA PATRIOTISM KIASI KWAMBA USHINDWE KUFACE THE REALITY.
 
Ni kweli alikua mbovu kama unavyosema wewe ila bei ya bidhaa zilibakia zile zile kwa miaka 6.

Rais wetu mzuri ndani ya mwaka mmoja gharama za maisha zimepanda kwa asilimia 45 ama zaidi.

Sijui kama akili yako inaweza kutofautisha vitu kama hivyo.
Kuna kipindi bei ya unga wa ugali ilipanda balaa..sio sahihi kusema vitu havikupanda bei.
 
Back
Top Bottom