Mrisho Gambo: Gharama ya Bando imepanda sana, majibu tunayopewa hayaendani na hali halisi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 52, leo Juni 21, 2023



Kulaza Shule za Bweni watoto wenye umri chini ya Miaka 5
Naibu waziri wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolijia Mhe. Omary Juma Kipanga (Mb) amesema kuwa kibali cha kulaza wanafunzi wa Bweni hutolewa kwa wanafunzi kuanzia darasa la 5 au kinaweza kutolewa kwa kibali maalumu kwa walio chini ya umri huo.

27010330.jpg

Omary Juma Kipanga, Naibu waziri wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolijia
Amebainisha kuwa Serikali itaendelea kudhibiti tatizo la watoto wenye umri chini ya miaka 5 kusoma shule za bweni kwa kuhakikisha inachukua inafanya ufuatiliaji wa mara kwa mara na shule itakayobainika kukiuka maelezo haya itachukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria ikiwemo kufutiwa usajili.

Kuuza Mazao nje ya Nchi
Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Serikali haijazuia uuzwaji wa mazao nje ya nchi bali imezuia watu kufanya biashara bila kufuata utaratibu wa kisheria.

DVLw0dEXcAA_5do.jpg

Hussein Bashe, Waziri wa Kilimo
Amesema "Haiwezekani mtu unanunua mahindi Songea, unapakia kwenye malori, huna business license ya aina yoyote, hata business name kusajili ambayo ni huduma inayotolewa, huna TIN, huna TAX clearance, huna export permit... halafu unataka nchi ikuruhusu kwenda kuuza nje mazao hayo."

Ameongeza, "Malipo hayaonekani katika mfumo rasmi wa fedha, hatuzipati data katika export statement zetu za nchi. Maelekezo ya Rais yako wazi, Mtanzania yeyote anayetaka kufanya biashara ya mazao kwa ajili ya kuuza nje ama kuuza ndani ya nchi akate leseni ya Biashara"

Amewaambia wafanyabiashara wa mazao kwenda kwenye Halmashauri kukata leseni za biashara na TRA kuchukua TIN certificate ili waingie kwenye mfumo rasmi wa biashara ya mazao ya kilimo. Nia ya Serikali ni kurasimisha shughuli za kilimo na shughuli za biashara za mazao ya biashara.

Kodi ya Tsh. 100 kwenye kila lita ya Mafuta
Mbunge wa Arusha Mjini Mrisho Gambo amesema hakubaliani pendekezo la kuongeza kodi ya Tsh. 100 kwa kila lita ya mafuta ya petroli na dizeli inayotaka kuanzishwa na Serikali kwenye Bajeti mpya ya mwaka 2023/24.

Screenshot-2023-04-13-at-11.15.17.png

Mrisho Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini
Amesema tayari kuna zaidi ya kodi 22 na kuongeza Tsh 100 nyingine ni kuongeza mzigo kwa mwananchi, hivyo kuongeza gharama ya maisha.

Eneo la mafuta huwagusa wananchi moja kwa moja hivyo serikali inapaswa kuongeza ubunifu kwa kutafuta vyanzo vingine vya mapato badala ya kumuumiza mtanzania wa kawaida.

Amesisitiza pia kuongeza gharama ya simenti ni kuwaumiza wananchi pia inakwenda kinyume na sera ya Serikali inayotaka watu wawe na makazi bora.

Mrisho Gambo: Gharama ya Bando imepanda sana, majibu tunayopewa hayaendani na hali halisi


Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo amesema gharama za bando zimepanda sana nchini.

"Katika kitu ambacho tunatakiwa tukiangalie vizuri ni gharama za bando zimepanda sana. Majibu tunayopewa hayaendani na hali halisi. Unaambiwa sijui zima app hii, sijui fanya hivi...hicho ni kitu kimoja, kitakupunguzia matumizi" amesema Gambo

Kupanda huku kwa gharama za bando kunapunguza ubunifu, udadisi na kujifunza pamoja na kuongeza gharama ya maisha.
 
Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo amelalamikia suala la Bei kubwa ya Bando za Intaneti huku Wananchi wakitakiwa kuzima baadhi ya 'App' ili kupunguza matumizi kitu ambacho hakina uhalisia wa gharama.

Gambo amesema Watoa Huduma (Mitandao ya Simu) wamepunguza kiasi cha Bando za Intaneti huku bei ikibaki kuwa kubwa ambapo mwaka 2020 Bando ya GB 10 iliuzwa Tsh. 15,000 (Tsh. 1,500 kwa GB1) lakini sasa ni Tsh. 15,000 unapata GB 7.2 (Tsh. 2,083 kwa GB1).

Amesema gharama hizo zinasababisha Wanafunzi kushindwa kusoma, zinapunguza Ubunifu na Udadisi pamoja na kuongeza gharama za maisha. Pia, ameshauri kutolinganisha Bei za Bando za Tanzania na Nchi nyingine .
 
Kama mambo hayaendi vizuri kwenye bando SI tuwaite warabu waje kuwekeza? Sababu ndicho tulichobakiza.
 
Tetesi: Takwimu zinaonyesha 75% ya bando hutumika kutazama picha chafu na mitandao kama tiktok, instlive na dating site. Serikali imejaribu kuzifungia ikashuka na kifikia asilimia 74%. Serikali imejionea bora ikusanye kodi sababu hakuna namna.
 
Hilo bunge lote halina maana kabisa, lineshindwa kulinda maslahi ya taifa huru Tanganyika kwenye ule mkataba wa hovyo wa bandari.
 
Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo amelalamikia suala la Bei kubwa ya Bando za Intaneti huku Wananchi wakitakiwa kuzima baadhi ya 'App' ili kupunguza matumizi kitu ambacho hakina uhalisia wa gharama.

Gambo amesema Watoa Huduma (Mitandao ya Simu) wamepunguza kiasi cha Bando za Intaneti huku bei ikibaki kuwa kubwa ambapo mwaka 2020 Bando ya GB 10 iliuzwa Tsh. 15,000 (Tsh. 1,500 kwa GB1) lakini sasa ni Tsh. 15,000 unapata GB 7.2 (Tsh. 2,083 kwa GB1).

Amesema gharama hizo zinasababisha Wanafunzi kushindwa kusoma, zinapunguza Ubunifu na Udadisi pamoja na kuongeza gharama za maisha. Pia, ameshauri kutolinganisha Bei za Bando za Tanzania na Nchi nyingine .
Nape anasema hawawezi kukimbiza wawekezaji ,
 
Network providers....wameunda cartel yao now bando n flat rate ....10k unapata 4920mb_4925mb.....hawa n wez kama walivo majangiri
 
Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo amelalamikia suala la Bei kubwa ya Bando za Intaneti huku Wananchi wakitakiwa kuzima baadhi ya 'App' ili kupunguza matumizi kitu ambacho hakina uhalisia wa gharama.

Gambo amesema Watoa Huduma (Mitandao ya Simu) wamepunguza kiasi cha Bando za Intaneti huku bei ikibaki kuwa kubwa ambapo mwaka 2020 Bando ya GB 10 iliuzwa Tsh. 15,000 (Tsh. 1,500 kwa GB1) lakini sasa ni Tsh. 15,000 unapata GB 7.2 (Tsh. 2,083 kwa GB1).

Amesema gharama hizo zinasababisha Wanafunzi kushindwa kusoma, zinapunguza Ubunifu na Udadisi pamoja na kuongeza gharama za maisha. Pia, ameshauri kutolinganisha Bei za Bando za Tanzania na Nchi nyingine .
Kabisa udadisi especially eneo la minyanduano.
 
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 52, leo Juni 21, 2023



Kulaza Shule za Bweni watoto wenye umri chini ya Miaka 5
Naibu waziri wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolijia Mhe. Omary Juma Kipanga (Mb) amesema kuwa kibali cha kulaza wanafunzi wa Bweni hutolewa kwa wanafunzi kuanzia darasa la 5 au kinaweza kutolewa kwa kibali maalumu kwa walio chini ya umri huo.

View attachment 2664160
Omary Juma Kipanga, Naibu waziri wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolijia
Amebainisha kuwa Serikali itaendelea kudhibiti tatizo la watoto wenye umri chini ya miaka 5 kusoma shule za bweni kwa kuhakikisha inachukua inafanya ufuatiliaji wa mara kwa mara na shule itakayobainika kukiuka maelezo haya itachukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria ikiwemo kufutiwa usajili.

Kuuza Mazao nje ya Nchi
Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Serikali haijazuia uuzwaji wa mazao nje ya nchi bali imezuia watu kufanya biashara bila kufuata utaratibu wa kisheria.

View attachment 2664157
Hussein Bashe, Waziri wa Kilimo
Amesema "Haiwezekani mtu unanunua mahindi Songea, unapakia kwenye malori, huna business license ya aina yoyote, hata business name kusajili ambayo ni huduma inayotolewa, huna TIN, huna TAX clearance, huna export permit... halafu unataka nchi ikuruhusu kwenda kuuza nje mazao hayo."

Ameongeza, "Malipo hayaonekani katika mfumo rasmi wa fedha, hatuzipati data katika export statement zetu za nchi. Maelekezo ya Rais yako wazi, Mtanzania yeyote anayetaka kufanya biashara ya mazao kwa ajili ya kuuza nje ama kuuza ndani ya nchi akate leseni ya Biashara"

Amewaambia wafanyabiashara wa mazao kwenda kwenye Halmashauri kukata leseni za biashara na TRA kuchukua TIN certificate ili waingie kwenye mfumo rasmi wa biashara ya mazao ya kilimo. Nia ya Serikali ni kurasimisha shughuli za kilimo na shughuli za biashara za mazao ya biashara.

Kodi ya Tsh. 100 kwenye kila lita ya Mafuta
Mbunge wa Arusha Mjini Mrisho Gambo amesema hakubaliani pendekezo la kuongeza kodi ya Tsh. 100 kwa kila lita ya mafuta ya petroli na dizeli inayotaka kuanzishwa na Serikali kwenye Bajeti mpya ya mwaka 2023/24.

View attachment 2664156
Mrisho Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini
Amesema tayari kuna zaidi ya kodi 22 na kuongeza Tsh 100 nyingine ni kuongeza mzigo kwa mwananchi, hivyo kuongeza gharama ya maisha.

Eneo la mafuta huwagusa wananchi moja kwa moja hivyo serikali inapaswa kuongeza ubunifu kwa kutafuta vyanzo vingine vya mapato badala ya kumuumiza mtanzania wa kawaida.

Amesisitiza pia kuongeza gharama ya simenti ni kuwaumiza wananchi pia inakwenda kinyume na sera ya Serikali inayotaka watu wawe na makazi bora.

Gharama za Bando
Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo amesema gharama za bando zimepanda sana nchini.

"Katika kitu ambacho tunatakiwa tukiangalie vizuri ni gharama za bando zimepanda sana. Majibu tunayopewa hayaendani na hali halisi. Unaambiwa sijui zima app hii, sijui fanya hivi...hicho ni kitu kimoja, kitakupunguzia matumizi" amesema Gambo

Kupanda huku kwa gharama za bando kunapunguza ubunifu, udadisi na kujifunza pamoja na kuongeza gharama ya maisha.

Wizara ina waziri asiye na AKILI unategemea nn, kuwa mshabiki tu wa CCM basi unapewa wizara na Elimu ya kuungaunga CCM inalikosea sana adabu Taifa hili.
 
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 52, leo Juni 21, 2023



Kulaza Shule za Bweni watoto wenye umri chini ya Miaka 5
Naibu waziri wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolijia Mhe. Omary Juma Kipanga (Mb) amesema kuwa kibali cha kulaza wanafunzi wa Bweni hutolewa kwa wanafunzi kuanzia darasa la 5 au kinaweza kutolewa kwa kibali maalumu kwa walio chini ya umri huo.

View attachment 2664160
Omary Juma Kipanga, Naibu waziri wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolijia
Amebainisha kuwa Serikali itaendelea kudhibiti tatizo la watoto wenye umri chini ya miaka 5 kusoma shule za bweni kwa kuhakikisha inachukua inafanya ufuatiliaji wa mara kwa mara na shule itakayobainika kukiuka maelezo haya itachukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria ikiwemo kufutiwa usajili.

Kuuza Mazao nje ya Nchi
Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Serikali haijazuia uuzwaji wa mazao nje ya nchi bali imezuia watu kufanya biashara bila kufuata utaratibu wa kisheria.

View attachment 2664157
Hussein Bashe, Waziri wa Kilimo
Amesema "Haiwezekani mtu unanunua mahindi Songea, unapakia kwenye malori, huna business license ya aina yoyote, hata business name kusajili ambayo ni huduma inayotolewa, huna TIN, huna TAX clearance, huna export permit... halafu unataka nchi ikuruhusu kwenda kuuza nje mazao hayo."

Ameongeza, "Malipo hayaonekani katika mfumo rasmi wa fedha, hatuzipati data katika export statement zetu za nchi. Maelekezo ya Rais yako wazi, Mtanzania yeyote anayetaka kufanya biashara ya mazao kwa ajili ya kuuza nje ama kuuza ndani ya nchi akate leseni ya Biashara"

Amewaambia wafanyabiashara wa mazao kwenda kwenye Halmashauri kukata leseni za biashara na TRA kuchukua TIN certificate ili waingie kwenye mfumo rasmi wa biashara ya mazao ya kilimo. Nia ya Serikali ni kurasimisha shughuli za kilimo na shughuli za biashara za mazao ya biashara.

Kodi ya Tsh. 100 kwenye kila lita ya Mafuta
Mbunge wa Arusha Mjini Mrisho Gambo amesema hakubaliani pendekezo la kuongeza kodi ya Tsh. 100 kwa kila lita ya mafuta ya petroli na dizeli inayotaka kuanzishwa na Serikali kwenye Bajeti mpya ya mwaka 2023/24.

View attachment 2664156
Mrisho Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini
Amesema tayari kuna zaidi ya kodi 22 na kuongeza Tsh 100 nyingine ni kuongeza mzigo kwa mwananchi, hivyo kuongeza gharama ya maisha.

Eneo la mafuta huwagusa wananchi moja kwa moja hivyo serikali inapaswa kuongeza ubunifu kwa kutafuta vyanzo vingine vya mapato badala ya kumuumiza mtanzania wa kawaida.

Amesisitiza pia kuongeza gharama ya simenti ni kuwaumiza wananchi pia inakwenda kinyume na sera ya Serikali inayotaka watu wawe na makazi bora.

Mrisho Gambo: Gharama ya Bando imepanda sana, majibu tunayopewa hayaendani na hali halisi


Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo amesema gharama za bando zimepanda sana nchini.

"Katika kitu ambacho tunatakiwa tukiangalie vizuri ni gharama za bando zimepanda sana. Majibu tunayopewa hayaendani na hali halisi. Unaambiwa sijui zima app hii, sijui fanya hivi...hicho ni kitu kimoja, kitakupunguzia matumizi" amesema Gambo

Kupanda huku kwa gharama za bando kunapunguza ubunifu, udadisi na kujifunza pamoja na kuongeza gharama ya maisha.

Nadhani hata Mrisho Gambo anajua kwamba wizara ya habari inaongozwa na kilaza tena very matured.
 
Back
Top Bottom