Uhalisi wa bei za bando la internet dhidi ya wastani wa kipato cha mwezi cha kila Mtanzania

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Jul 7, 2020
6,328
8,243
Kwanza kabla ya yote naomba kusema kwamba nchi ya Tanzania ndio yenye bei ya chini zaidi ya bando za internet katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Pili ukichukua wastani wa mshahara wa kila mwezi, inaonekana watanzania ndio wanalipa asilimia kubwa zaidi ya mapato yao katika kununua bando la internet.

Sheet_01 (1).png


Bei za data kwa Tanzania ni dolla za kimarekani 0.75 ($0.75), Uganda ni dolla 1.56 ($1.56) na Kenya ni dolla 2.25.

Wastani wa mapato ya kila mwezi ya kila mtanzania ni dolla 174 ($174), Uganda ni $1291 na Kenya ni $738.

Kikawaida gharama ya bando la GB 5 haipaswi kuzidi asilimia mbili (2%) ya wastani wa mapato ya kila mwezi ya mtanzania, ambayo inapaswa kufikiwa kabla ya 2026.

Kwasasa gharama ya internet bando ni kubwa zaidi kuliko ya asilimia mbili (2%) ya wastani wa kipato cha kila mwezi kwa GB 5.

Bei ya wastani ya GB5 ni Shilingi za Kitanzania 40,960 (USD17.57), ambayo ni asilimia 10 ya mapato ya wastani ya Shilingi za kitanzania 410,147 (USD176).

Ukipiga hesabu bei hiyo ni mara tano zaidi ya bei ya asilimia mbili (2%) ya wastani wa mapato ya kila mwezi.

Na kitakwimu hii bei inawaumiza zaidi wanawake na wakulima.

Ukijaribu kuchambua taarifa zilizowekwa katika jedwali linaonyesha wastani wa mapato na bei za bando la internet kulingana na sekta.

Table_01 (1).png

Jedwali linaonyesha gharama za bando ni kubwa zaidi kwa watu wakulima wadogo, ambapo ni asilimia ya ishirini na moja (21%) ya mapato yao.

Bei zilizoorodheshwa zinatokana na takwimu za Septemba 2022. Mwaka 2020, mtu angeweza kununua bando la data la GB 10 kwa Shilingi 10,000 za kitanzania ambayo ni sawa na dolla za kimarekani 4.3 (USD4.3).

Lakini kwa sasa, 9.8GB inauzwa kwa Shilingi za Kitanzania 20,000 (USD8.6), ambayo ni bei mara mbili ndani ya miaka miwili tu.

Kumbe tukifanya bei za bando ziwe nafuu kulingana na kiwango cha maisha cha mtanzania kutaongeza kushiriki na ufikiaji wa habari kwa urahisi.

Imeandikwa na: bandg.editors@gmail.com
 
Average monthly salary Uganda ni $1291?? Kweli?

Hapa kuna kitu hakiko sawa

"Wastani wa mapato ya kila mwezi ya kila mtanzania ni dolla 174 ($174), Uganda ni $1291 na Kenya ni $738."

GDP per capita, yani mapato ya mtu mmoja kwa mwaka, kwa mwaka wa 2022 kwa mujibu wa Benki ya Dunia, yalikuwa hivi.

Kenya $2,099 / 12 = $ 175 per month
Uganda $ 1,085 /12 = $ 90 per month
Tanzania $ 1,191 / 12 = $ 99 per month
 
Hapa kuna kitu hakiko sawa

"Wastani wa mapato ya kila mwezi ya kila mtanzania ni dolla 174 ($174), Uganda ni $1291 na Kenya ni $738."

GDP per capita, yani mapato ya mtu mmoja kwa mwaka, kwa mwaka wa 2022 kwa mujibu wa Benki ya Dunia, yalikuwa hivi.

Kenya $2,099 / 12 = $ 175 per month
Uganda $ 1,085 /12 = $ 90 per month
Tanzania $ 1,191 / 12 = $ 99 per month
Naunga mkono hoja
 
Sawa ila why ununue bando Kila siku ?
Ununuaji wa bando unategemeana na kipato cha mtu. Watanzania wametofautiana vipato.

Hivyo wapo wengine wanauwezo wa kununua bando la kiwango kama chakwako wengine wananunua kila siku kidogokidogo. Lakini mwisho wa siku wote wanakutana mtandaoni.

Kwa hiyo mkuu kama wote wakinunua bando la unlimited ni nani atakayenunua hilo la limited. Mitandao ya simu imetengeneza mabando ya aina mbalimbali kulingana na kila mtanzania anavyoweza kuafford.

Mwisho hili bandiko lipo kwaajili ya kuelimishana.
 
Ununuaji wa bando unategemeana na kipato cha mtu. Watanzania wametofautiana vipato.

Hivyo wapo wengine wanauwezo wa kununua bando la kiwango kama chakwako wengine wananunua kila siku kidogokidogo. Lakini mwisho wa siku wote wanakutana mtandaoni.

Kwa hiyo mkuu kama wote wakinunua bando la unlimited ni nani atakayenunua hilo la limited. Mitandao ya simu imetengeneza mabando ya aina mbalimbali kulingana na kila mtanzania anavyoweza kuafford.

Mwisho hili bandiko lipo kwaajili ya kuelimishana.
Ok
 
Back
Top Bottom