Hebu jikumbushie 'Siku ya Gulio Katerero'

Hebu jikumbushie 'Siku ya Gulio Katerero'

Ile kwaya ya Kana Primary School Tanga.....naikumbuka sana..

Mtama wa baba waliwa,
Mtama wa baba waliwa na ndege,
Wakiumaliza tutafanya nini eeh...
Fumbo muhimu sana mwaka 1981 leo tunashuhudia ukweli

Umeliwa na mbayuwayu?
 
Dada Asha sikiliza
Maneno ya kupendeza
Azimio laondoa giza
Azimio la Arusha.

Arusha umeitaja
Sijui inavyokuja
kulijua nina haja
Azimio Kitu gani?

Azimio la Arusha
Lilizaliwa Arusha
......................
..........................
 
shule za msingi ( upe )category:common interest - historydescription:
Ushawahi kusoma shule za kukimbia mchakamchaka, kwenda na kidumu cha maji na mfagio mkononi? Kama ndio basi kundi (group) hili linakufaa.

Hebu jikumbushie haya:

1. Bulicheka na nduguze
2. Mr. & mrs. Daudi
3. Fikiri na sadiki
4. Linda amwokoa kapilima
5. Siku ya gulio katerero
6. Tola anakula gizani
7. Twende tukawinde ngedere
8. Kibanga ampiga mkoloni
9. Nanzoge anapika.
10. Mafuriko ya mto rufiji
11. Pazi na jogoo

waweza ongezea na wewe.

Kama ulisoma academy school, huambulii...
Lazima ujifunze:

1. Sayansi kimu
2. Uraia
3. Sanaa

wakati wa mapumziko lazima ucheze,

1. Mpira (chandimu, one touchi, mputo)
2. Netboli na rede
3. Mdako
4. Bong'oa
5. Kula m'bakishie baba
6. Kubanjua gololi

msosi wakati wa mapumziko.

1. Mihogo ya kukaanga na chachandu
2. Aishiklimu
3. Barafu
4. Kashata
5. Bagia (za walimu)

6. lusi na damasi
 
Karudi Baba mmoja toka safari ya mbali,
kavimba yote mapaja
na kutetemeka mwili
 
Wakati wa mapumnziko, Bumunda la ufuta na alizeti zilizokaangwa, bila kusahau embe lenye pilipili. Wee !!!
 
Ikifika saa tisa kwenda kwenye kazi..ole wako kama hauna fyekeo,jembe,kotama au o'rwabyo ni mboko..
Madirisha yalikuwa wazi ikipigwa kengele tunaruka jirani kulikuwa na mahandaki tunaenda kujificha mpaka mida ya kutoka..
 
Kwenye menu ya mchana, sisi wengine tulikuwa tunakunywa uji usio na sukari !, Sukari ni kujitegemea. Na uji huo unatokana na mahindi yaliyovunwa toka shamba la shule. Ila wakati wa njaa "burga" toka kwa watu wa Marekani ili sevu sana kupunguza utapiamlo.
 
kuna mwalimu alikuwa anauza ndizi za kuchemsha kengele ya break ikilia hamtoki mpk mnunue ndizi zake ziishe vinginevyo anafanya zoezi la kusahisha madaftari drsn.
Halafu kulikuwa na style ya kuchapwa unaambiwa kodisha chumba unaingiza vichwa mpk maeneo ya kiuno nchini ya meza halafu makalio unayainua (unabong'oa) unapewa viboko vya uhakika huwezi kushika wala kukimbia
Halafu kungiza
 
hivi kweli hakuna uwezekano wa kuvichapisha hivyo vitaabu hivyo, ? maana nakumbuka sana vitabu hivyo,kwa sisi tuliosoma hapa Dar es salaam, kama hukuweza kukariri maneno aliyoyasema Umslopagasi wakati analinda ngazi kuu , wewe ulikuwa unahesabiwa kama wakuja, maneno yenyewe ni kama yafuatayo naomba mutanisamehe kwani kipindi kirefu kimepita na baadhi yake nimeyasahau, Alisema hivi, ''mimi gota gota,mimi muuaji,mimi mwenya mbio, mimi mwenye damu ya mfalme Chaka,nasikia harufu ya damu, nani anataka kulibusu shoka langu?''' SASA MANENO MENGI NIMEYASAHAU MWENYE KUKUMBUKA TUKUMBUSHANE, pia palikuwa na vitabu vinginevyo kama safari za Gulliver, Elisi katika nchi ya ajabu, Alfu lela u lela, Animal Farm,nk:redfaces::redfaces::redfaces::redfaces::redfaces::redfaces::redfaces:
 
Naona wenzangu mlisomea mjini, sie tuliosomea kijijini haf shule ilikuwa umbali wa kilomita sita, kwanza kuingia darasa la kwanza mpaka uwe na miaka zaidi ya 12 ndo utaweza kutembea, kumbuka kipindi kile hata baiskeli zilikuwa zinamilikiwa na watu wachache pale kijijni mfano mwenyekiti wa kijiji au mwalimu mkuu. Nakumbuka tulikuwa tunabeba chakula ambacho tulikuwa tunaita kipolo, kwa hiyo wakati wa mapumziko ya chakula cha mchana tulikuwa tunakula.
Nakumbuka mada moja ya darasa la kwanza katika kitabu cha kwanza cha kusoma ilikuwa inaitwa MKUBWA WETU! kitabu kilikuwa kinaeleza watu walikusanyika na kufanya kikao wamtafute mkubwa wao ambaye
awashinde wote kwa urefu
awashinde wote kwa watoto
awashinde wote kwa mali
awashinde wote kwa akili
awashinde wote kwa vyote
mwisho mwandishi alihitimisha kwa kusema atakayekuwa na sifa zote huyo ndo mkubwa wetu
Nakumbuka wanafunzi wengi walijibu Nyerere
kwa kweli nimekumbuka mbali sana!
 
Juma na Rosa
Safarri ya Chalinze
Mr. all of you
Cha wote
Sizitaki mbichi hizi
Karudi baba mmoja
Ahadi 10 za MwanaTANU (Std. III)




1. Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja
2. Sitapokea wala kutoa rushwa
3. Nitajitolea nafsi yangu....................
4. ............
5. ............
6. ............
7. .............
8. ............
9. ............
10. ...........

Jamani anayezikumbuka atuwekeeeeeeeeeeeeee hapa!!!!!!!!
 
Mambo yote ni mchakamchaka!

Jua lile literemke mama!
Kajogoo kanawika, wika eheee
Kipande cha papa ugali kwa muhoga kula!
Rule rule rulenge....
 
hivi kweli hakuna uwezekano wa kuvichapisha hivyo vitaabu hivyo, ? maana nakumbuka sana vitabu hivyo,kwa sisi tuliosoma hapa Dar es salaam, kama hukuweza kukariri maneno aliyoyasema Umslopagasi wakati analinda ngazi kuu , wewe ulikuwa unahesabiwa kama wakuja, maneno yenyewe ni kama yafuatayo naomba mutanisamehe kwani kipindi kirefu kimepita na baadhi yake nimeyasahau, Alisema hivi, ''mimi gota gota,mimi muuaji,mimi mwenya mbio, mimi mwenye damu ya mfalme Chaka,nasikia harufu ya damu, nani anataka kulibusu shoka langu?''' SASA MANENO MENGI NIMEYASAHAU MWENYE KUKUMBUKA TUKUMBUSHANE, pia palikuwa na vitabu vinginevyo kama safari za Gulliver, Elisi katika nchi ya ajabu, Alfu lela u lela, Animal Farm,nk:redfaces::redfaces::redfaces::redfaces::redfaces::redfaces::redfaces:
Hahahaaa! Umenikumbusha Umslopagaazi Mlengaji mkuu wa shabaha; na shoka lake Inkosikazi. Aliwaona wote kulungu tu!
 
Chama Mapinduzi Ungali kijana,
Baba yako na mama yako wameshakufa.
Hapa naahidi....
 
Karudi Baba mmoja toka safari ya mbali,
kavimba yote mapaja
na kutetemeka mwili

Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali
kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili
watoto wake wakaja, ili kumtaka hali
wakataka na kauli, iwafae maishani

Akatamka mgonjwa, ninaumwa kwelikweli
Hata kama nikichanjwa, haitoki homa kali
Roho naona yachinjwa, kifo kinanikabili
Semeni niseme nini, kiwafae maishani.
 
Kufagia ni kwa vikosi mfano: - Kikosi cha Jamhuri, Azimio, Kambarage, Mapinduzi, Chapakazi n.k. Kwa vitabu unasikia majina kama Adili na Nduguze, Tusome kwa Furaha humo utamkuta Mpiga Filimbi wa Hamerini. Vitabu vya darasani - Kiswahili kulikuwa na Karibu mwenge hapa kwetu Mavurunza. English darasa la 6 kulikuwa na hadithi ya Ng'holo Ja Kifuho na nyingine Sizimwa etc. Aaaah Jamani shule wakati huo ilikuwa raha tupu. Sijui kama siku hizi watoto wana vitabu vyenye kuleta msisimko kwenye usomaji!!
 
Back
Top Bottom