Hebu jikumbushie 'Siku ya Gulio Katerero'

Nondo Mla Watu (Mgoya main chacter)!
Miiko ya Uongozi (Mperembi - main actor)!
 
lugha.JPG
 
aah zamani,wakuu kwa sisi tuliosoma enzi hizo somo la hisabati linaanzia darasa la tatu,ole wako kama hujui kuimba tebo(table) hasa ya 7,8 na 9
 
Hicho sina mkuu, ukikipata nimuvuzishie.
Bila shaka kiongozi.
Kuna kijitabu kingine nakumbuka kilikuwa na shairi moja hivi:
Mgeni siku ya kwanza mpe chele na.....(nimesahau mboga), siku pili...., siku ya tatu mpe jembe akalime
 
Bila shaka kiongozi.
Kuna kijitabu kingine nakumbuka kilikuwa na shairi moja hivi:
Mgeni siku ya kwanza mpe chele na.....(nimesahau mboga), siku pili...., siku ya tatu mpe jembe akalime

Nadhani hicho ni cha kina Bulicheka na Mkewe Lizabeta pamoja na Makari Hodari, ila hilo shairi lipo mtandaoni - ligugo.
 
hapo palikuwa na somo linaitwa siasa, hapo ni mambo ya CCM na Historia ya Tanu, Chipukizi na scout vilkuwa ni vitu vya kawaida kabisa

mashairi yaliyokuwa yanatingisha yalikuwa
Azimio la Arusha (darasa la tatu)
Karudi baba mmoja (Darasa la nne)

mnakumbuka Manenge na Mandawa
 
Wakuu posts zote hapa zimenisisimua sana. Watoto siku hizi hawafaidi. Darasa la sita kama sijasahau kitabu cha Kiswahili kilikuwa na sura "Kutembelea Uwanja wa Ndege." Tulipata nafasi ya kutembelea uwanja wa ndege kutokana na juhudi binafsi za Mwalimu wetu Emmanuel Mbelele. Napenda kuonesha shukrani zangu kwake. Naamini nimekuwa na wakati mzuri sana katika maisha ya utotoni. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa ofa hii.
wewe ni mtoto mtukufuuuuuuu aliposema neno mtukufu akapulizia chai fuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu. wazazi wako wanakusifuuuuuuuuuu waliposema wanakusifu akapulizia chai fuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!
 
huyu ni baba
baba ni mnene
baba ana ngombe
ngombe wake ni mweusi
baba anasema
kimbia ngombe
kimbia upesi
kimbia nyumbani
baba ana njaa
 
unavaa kaptula 3 kukwepa bakora zisikuingie mwilini tena za jeans au unaweka maboksi na makaratasi kwenye makalio duh!zamani bakola zilikuwa zinatembea sana!
ilikuwa inaitwa dabali (kutokana na neno double)
 
huyu ni juma
juma ana dada
dada ya juma ni roza
juma anesema
tia maziwa
tia sukari
juma anauliza
roza una kiu
kunywa chai roza
 
ukiwahi unakimbilia kuchota maji mtoni then kumwagilia mchicha na maua mwalimu anapima kwa kuchomeka fimbo kama kimelowa sasa ole wako aone hakijaloana maji hayajafika chini pia tulikuwa tunaagizwa mbolea ya mavi ya ngombe,kuku na mbuzi pia udongo uliooza na miradi ya shule kuuza mapera ya shule dah!enzi hzo ilikuwa raha sana!
nakumbuka kuna jamaa lipewa adhabu na mwl ya kumwagilia maua hadi palie vyura kwa siku hiyo hiyo
 
Back
Top Bottom