Hebu jikumbushie 'Siku ya Gulio Katerero'

Hebu jikumbushie 'Siku ya Gulio Katerero'

sasa umemaliza kitabu cha kwanza
bibi na babu wanasema kwa herini watoto
baba na mama wanasema kwa herini watoto
juma na roza wanasema kwa herini watoto
lucy na damasi wanasema kwa herini watoto
 
1. Nondo mla watu
2.Jogoo aliyewika
3.manenge na mandawa
4.Heri mimi sijasema
5.
 
nakumbuka darasa la kwanza tukimaliza kipindi tunaimba, saa ya kusoma imekwisha, turudi nyumbani, tuakale ugali wetu ugali wetu mzuri na mboga za majani, hulaaaa, hulaaaa ( hapa mkisema hivi mnasiama na kusogea mlangoni halafu tunaruka juu hulaaaaaa). Nyingine saa ya kusoma imekwisha kwa heri mwl kwaheri, tutaonana keshooooooooooooo (mnaruka na kukimbia nje).

kuna wimbo mwingie ulisema hivi "paka unaumwa, ndio naumwa, ugali utakula, sili naumwa, wali utakula, sili naumwa, nyma utakula, sili naumwa , maziwa utakunywa, loooo! nitakunywa lakini bado naumwa
 
hapo palikuwa na somo linaitwa siasa, hapo ni mambo ya CCM na Historia ya Tanu, Chipukizi na scout vilkuwa ni vitu vya kawaida kabisa

mashairi yaliyokuwa yanatingisha yalikuwa
Azimio la Arusha (darasa la tatu)
Karudi baba mmoja (Darasa la nne)

mnakumbuka Manenge na Mandawa
Hilo somo la siasa nililichukia sana hata walipoliremba kule sekondari wakaliita civics na high school GS....
 
umenikumbusha mbali,enzi zile za elimu ya kujitegemea ilikuwa lazima kwenda na jembe shuleni na wakati mwingine kusomba mawe na matofali kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mwanakijiji.Malipo ilikuwa siri ya mkuu wa shule na kamati yake.
 
Mkuu mnazidi kunikumbusha mbali. habari ya juma na rosa wanasema kwaherini watoto. Pia kulikuwa na maneno kuwa Baba mkubwa kutoka Moshi anasema, kwa herini watoto
 
Sizitaki mbichi hizi
Kambi ya Kaboya
Mpiga filimbi wa Hamelini
Hadithi za Kiingereza: The story of Mkisi; The Scout master's camera;
 
Grandmother and rice, the pumpkin, Mr hyena!, Pazi na jogoo, hawa the bus driver(std6) , mr rabbit.
 
Enzi nzuri sana hizo...halafu kuna kulima shamba la shule na siku ya kuvuna, mnapikiwa mahindi wote kwa madarasa! Old good days
 
Dah! bila kusahau kuweka kioo chini ya miguu ya wasichana ili uchungulie, mchezo wa kifimbo cheza mwanawane muda wote una vijiti kwenye nywele. Wakati wa ukaguzi wa usafi asubuhi ukiwa mstarini unatafuna kucha ili usibambwe. Na pia nilipenda sana kuchungulia wasichana nikikuta binti amesimama hivi namuwekea kioo kwa chini katikati a miguu halafu naona mambo ingawa kuna siku nilimchungulia dada mkuu wa shule nilichopata na mchezo huo ukaishia siku hiyo.....acha kabisa
 
Tulikariri haya darasa la kwanza.....

Juma ana dada,
Dada yake ni Rosa,
Juma ana rafiki,
Rafiki yake ni Damasi
 
Kama sikosei enzi hizo waziri wa elimu alikuwa anaitwa Elinewinga ( not sure of spelling). Kwa kweli shule zilikuwa enjoyable and one couldn't afford to miss. Nakumbuka kulikuwa na michezo mingi baada ya masomo. Hawa kwenye kwaya wakimba kujiandaa na mashindano ya shule mbalimbali , wengine kwenye ngoma za kienyeji. binafsi nilikuwa Mafia nilipenda kucheza Sindimba. aaah we acha tu
 
Mloka achaguliwa kuwa diwani
pioneers meeting in zanzibar
ndoto ya kimweri
siafu wadudu wenye maajabu
musa/maganga mtoto shujaa
mweka nadhiri na shetani
 
Darasa la kwanza..............sasax2, saa ya kwenda kwetux2, kwa herix2 mwalimu..........Tutaonana kesho!

Darasa la 5-7........Hesabu za kichwa..................
 
Shule za Msingi ( UPE )Category:Common Interest - HistoryDescription:
Ushawahi kusoma shule za kukimbia mchakamchaka, kwenda na kidumu cha maji na mfagio mkononi? Kama ndio basi kundi (Group) hili linakufaa.

Hebu jikumbushie haya:

1. Bulicheka na nduguze
2. Mr. & Mrs. Daudi
3. Fikiri na Sadiki
4. Linda amwokoa Kapilima
5. Siku ya gulio katerero
6. Tola anakula gizani
7. Twende tukawinde Ngedere
8. Kibanga ampiga mkoloni
9. Nanzoge anapika.
10. Mafuriko ya mto Rufiji
11. Pazi na jogoo

Waweza ongezea na wewe.

Kama ulisoma academy school, huambulii...
Lazima ujifunze:

1. Sayansi Kimu
2. Uraia
3. Sanaa

Wakati wa mapumziko lazima ucheze,

1. Mpira (Chandimu, one touchi, mputo)
2. Netboli na rede
3. Mdako
4. Bong'oa
5. Kula m'bakishie baba
6. Kubanjua Gololi

Msosi wakati wa mapumziko.

1. Mihogo ya kukaanga na chachandu
2. Aishiklimu
3. Barafu
4. Kashata
5. Bagia (za walimu)

wewe lazima utakuwa umesoma Tanga.. embu tuambiane wapi?
 
Mmesahau na yule aliyekaribisha chui ndani ya nyumba! Hivi ile Mtakuja Primary School iko wapi maana ilifanya shule zetu nyingine zote kuonekana mtoto..
 
Ile kwaya ya Kana Primary School Tanga.....naikumbuka sana..

Mtama wa baba waliwa,
Mtama wa baba waliwa na ndege,
Wakiumaliza tutafanya nini eeh...
Fumbo muhimu sana mwaka 1981 leo tunashuhudia ukweli
 
Back
Top Bottom