Hawa ndio wanyama 10 wenye akili duniani

Hawa ndio wanyama 10 wenye akili duniani

Binadamu mtamu zaidi.


Ndio maana ukianza kula nyama ya mtu huachi, alisema Nyerere.
Ngoja nikuibie siri moja ya utamu wa nyama mkuu.

Unajua nyama inakuwa tamu kulingana na kiasi cha glucose (sugar) mwilini mwake na viumbe wengi wanaopaa wanatumia kiasi kikubwa sana cha glucose ili wawe na energy hivyo ni viumbe wengi wenye asili ya ndege warukao wana glucose nyingi sana mwilini na ni watamu sana sababu ya kiasi kikubwa cha sugar content ndani ya miili yao.

Ndio maana njiwa, kunguru, kuku ni wanoni kuliko ng'ombe n.k
 
PANYA mnamchukulia poa? mbona hayupo hapo??

PANYA anategua mabomu.. huyo POMBOO anategua nini?
 
Nikikuwa naangalia NatGeo Wild sasa hvi walikuwa wanaongelea mada hii hii mkuu. Vipi na ww unaangalia nini? Naona kunguru anasifiwa sana
Kunguru alimlisha chakula mtume Philip sijui alikuwa anakitoa wapi
 
Rudia tena kusoma kipengele cha sokwe kwenye hii mada.

Mtoa mada amesema sokwe anao uwezo wa "kujenga makazi" kwa kutumia zana mbalimbali, wewe ukasema sokwe hana uwezo wa kujenga "nyumba ya kujisitiri". Mimi nikasema "nyumba" si mahitaji yake kwa maana ya kwamba hawezi kujenga kitu ambacho hakitumii (bila kujalisha kinaitwa nyumba au makazi kama mlivyoeleza hapo juu wewe na mtoa mada) kwa sababu sokwe anakaa, anaishi na kujisitiri kwenye miti. Kwa maneno mengine ni kwamba nilikua najaribu kuhoji kuwa unaupimaje uwezo wa kiakili wa kiumbe kinachoishi kwenye miti kwa uwezo wake wa kujenga nyumba/makazi ambayo kimsingi ameshajengewa na nature (ile miti) ?
 
Binadamu ni MNYAMA pasipo kuacha shaka ya aina yoyote yenye mashiko. (Beyond any reasonable doubt).
seemz una uelewa na hayo mambo hebu nielekeze Jellyfish anaweza kutokuwa na ubongo akasurvive!?..
Nikimaanisha kujikinga na maadui, kuemploy flight technics kuwakimbia, kujua strategy gan aitumie na kwa wakati gani as naamini hivyo vitu vinachakatwa kwenye ubongo kwanza!.
 
Labda angesema "hawa ni viumbe vyenye akili sana ukiondoa binadamu "
 
seemz una uelewa na hayo mambo hebu nielekeze Jellyfish anaweza kutokuwa na ubongo akasurvive!?..
Nikimaanisha kujikinga na maadui, kuemploy flight technics kuwakimbia, kujua strategy gan aitumie na kwa wakati gani as naamini hivyo vitu vinachakatwa kwenye ubongo kwanza!.

Swali lako lina jibu refu mno ili tuelewane, ila nitajitahidi kufupisha kwa kadri ya nitakavyoweza ili mradi tu uelewe ama upate japo mwanga.

Kibaiolojia viumbe hai tuna kazi au majukumu "matatu tu ya msingi";
1. kula (feeding)
2. Kutokuliwa / kutogeuzwa chakula cha mwingine. (defense)
3. Kuhakikisha kizazi chenu mnazidi kuwepo duniani/kuzaliana (reproducing)

katika kuyatimiza hayo, kazi ya mfumo wa fahamu/neva (nervous system) ni kusaidia mwili wa kiumbe kujitambua wenyewe na kuyatambua mazingira yake, yaani kuhisi adui yako yuko wapi ili umuepuke, kuhisi mwenza wako yuko wapi ili umfikie mzaliane na pia kuhisi chakula chako kiko wapi ili ule.

Mazingira unayoishi ndio yataamua aina ya chakula na aina ya maadui zako na hivyo kuamua utata wa mfumo wako wa fahamu (complexity of your nervous system). Mfumo wa fahamu wa kiumbe unaweza kuwa rahisi ukihusisha neva chache pekee au ukawa tata ukihusisha mamilioni ya neva, "ubongo" na "uti wa mgongo".

Ubongo ni nini ?
Kwa kifupi, ubongo ni mkusanyiko wa neva za fahamu zinazofanya kazi pamoja kama kiungo kinachoratibu mambo yote ya utambuzi na maamuzi katika mwili wa kiumbe. Mkusanyiko huo hufanyika sehemu ya juu au ya mbele ya kiumbe hali ambayo inapelekea sehemu hiyo kuitwa "kichwani". Kitendo cha neva kukusanyika (concentration of nervous ganglia) upande wa mbele/juu wa kiumbe (tunakokuita kichwani) na kutengeneza kitu kinachoitwa "ubongo" kwa lugha ya kiingereza kitendo hicho kinaitwa "Cephalization".

Jellyfishes are not cephalized. Kwahiyo hii ni kusema kwamba hao viumbe wanao mfumo wa fahamu, lakini hawana "ubongo". Mfumo wao wa fahamu una neva zilizo tandaa (kama nyuzi za chandarua vile/net like nerves) na hizo ndizo zinamsaidia katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku.

Sababu za kuwa na mfumo rahisi wa fahamu ni kwamba kwa mujibu wa maisha yake na mazingira yake huo mfumo ndio unaomfaa. Hii ni kwa maana ya kwamba, anaweza kuzaliana kwa njia zote mbili "sexually" na "asexually", anaweza kuishi katika njia mbili za vizazi (two alteration of generations) kati ya "medusa" na "polyp", ana uwezo wa kutoa sumu kwa ajili ya kuwashughulikia maadui zake, namna ya ulaji wake ni kula kwa kufyonza (filter feeder) hakumtaki ahangaike sana kukimbizana na "vitoweo" na mengineyo mengi.

Ninadhani kwa kiwango fulani nimejibu swali lako.
 
Swali lako lina jibu refu mno ili tuelewane, ila nitajitahidi kufupisha kwa kadri ya nitakavyoweza ili mradi tu uelewe ama upate japo mwanga.
Ninadhani kwa kiwango fulani nimejibu swali lako.
Nimekuelewa!.
 
Nahisi kama kuna wanyama wenye akili kuliko hao waliotajwa, mfano
1. Honey burger
2. Tai
3. Chui
Naona wanyama hao pamoja na mfalme wao Simba, hutumia akili sana kuliko hata Tembo na Nguluwe. Wakati Fulani nahisi kama Paka ana akili kuliko mbwa
 
Mkuu, umri wa dunia ni miaka bilioni kadhaa, umri wa "maisha" hapa duniani ni mamilioni mengi sana ya miaka, hivyo, japokuwa sina hakika na idadi ya miaka ya kuishi kwa hao viumbe kama alivyotanabaisha mdau hapo juu, nakuhakikishia uwezekano wa kuishi miaka hiyo upo maana maisha yamekuwapo kwa miaka mingi sana.

Hii unaambiwa huu ni mwaka 2018, ni mfumo tu wa kuhesabu miaka kikalenda lakini ukweli ni kwamba kumekuwapo na maisha kwa miaka mingi sana zaidi ya ''hutu tumiaka buku mbili"
Umenikuna kwa majibu yako murua
 
Back
Top Bottom