mwengeso
JF-Expert Member
- Nov 27, 2014
- 9,286
- 6,727
Si kweli kama wanajamvi wengi walivyosema ati ni harufu ya nyoka, hasa chatu, akiwa mawindoni. Maeneo mengi, yasiyo msitu, kuna nyoka na hata chatu lakini harufu hiyo haipo.Habari za jumapili wana JF.
Bila kupoteza muda wadau naomba kuuliza,Je ile harufu ya wali (wali nazi) ambayo tunaisikia tukiwa porini au msituni tena sehemu ambayo haina makazi ya watu inatokana na nini?
Cc. mshana jr
Harufu hii na nyinginezo huwapo kwenye misitu mikubwa na maeneo yenye uoto mwingi; viumbe hai wadogo sana (micro-organisms) km minyoo ya ardhini, bakteria; madini km chuma, magnesium; unyevunyevu; maji (ya vijito au mito); uozo km wa magome ya miti na majani; na mizoga ya wanyama.
Aina ya harufu itategemea aina ya udongo, na kilichooza. Mathalani waweza kunusa harufu ya wali kutokana na udongo wenye kiasi kingi cha chuma mara baada ya mvua (hewa ya oxygen iliyomo kwenye maji kuungana na chuma - kutu).
Ikumbukwe kuwa madini (ambayo ni mhimu kwa ustawi wa mimea) hutokana na kuoza kwa vitu (matter) ambapo hubadilika kuwa madini tena.
CHUNGUZA CHAMBUA AMUA CHUKUA HATUA