kbosho
JF-Expert Member
- Jun 4, 2012
- 13,073
- 6,639
Zitto ni mwanasiasa mzuri lakini pia anahitaji kukomaa. pengine sifa alizozipata akiwa mdogo zinamlewesha na kumzuia kukomaa. Ipo mfano ya matatizo ya watu walioruka rika katika ukuaji wao. Kuna kauli anazitamka zina ukakasi kweli. Amekuwa akikazana kutoa mfano wa Waziri Mkuu wa Malaysia na kujitanabaisha naye akitaka kuaminisha watu kuwa ni yeye tu anayeweza kuleta mabadiliko siyo tu katika chama chake bali hata kwa nchi. Leo nasikia anawaambia watu wake wa Kigoma kuwa iko siku atawaongoza na kuwatumikia watanzania katika nafasi kubwa! Anapaswa kujifunza na kunena kwa kadri. Akumbuke sifa zinapita na zinaweza peperuka kwa upepo.
word...