Halima Mdee: Mimi pamoja na timu yangu (Wabunge 19) tutabaki kuwa WanaCHADEMA kindakindaki. Tutaenda kuyajenga ndani kwetu

Umeitwa hujaenda, unataka chama kichukue uamuzi gani? Chama kimekuvua uanachama, kwa nini uingie bungeni kwa amri ya spika? Kama kweli siyo wachumia tumbo, wamwandikie barua spika kuwa wanalazimika kurudi chamani kukamilisha mchakato wa chama.

Kuendelea kuwa mbunge viti maalumu wa CHADEMA ili hali chama kimewafukuza, ni uchumia tumbo tu huo
 
Natarajia kuwa watakubaliana na uamuzi wa CHADEMA

Kutokutii hayo ni kujiporomosha kisiasa na ni kushindana na taasisi ambayo huto weza kushinda kamwe na ukishinda ni kwa figisu ambazo hazito kusaidia maana una someka sio mwenzao.

Pia nategemea nitasikia wakisema tuna jiuzuru nyazifa za ubunge viti maalum kwa kuwa tulifikiri tofauti na kuzani zina baraka ya chama kumbe hapana.

Mambo rahisi sana nashangaa wana jitutumua pasina msingi wowote.

NB:
Chukueni mfano wa Mh. Mwanadiplomasia nguli B. Membe alishindana na chama lakini hakushinda, aliishia kukubaliana na maanlmuzi ya chama na kukaaa pembeni
Wewe jamaa ni mwana CCM kwenye akili, sio kama Ndugai aka Jingalao.

Sent from my TECNO WX3 using JamiiForums mobile app
 
Wabunge 19 viti maalum kupitia CHADEMA ambao waliapishwa na Spika Ndugai kisha kufutiwa uanachama na chama chao leo wanaongea na waandishi wa habari. Tayari wabunge hao wanawake wamefika ukumbi wa Regency wakiwa wamevalia sare za CHADEMA almaarufu 'Gwanda'. Kuwa nami kukujuza watachokiongea.



=========

9:32 Asubuhi: Halima Mdee na Ester Bulaya kufika baada ya dakika kumi kutokana na kuchelewa

9:45 Asubuhi: Halima Mdee na Ester Bulaya wameingia ukumbini na kinachoendelea ni burudani ya wimbo wa Halima Mdee

9:48 Asubuhi: Ester Lambert anafanya utangulizi na kumkaribisha mzungumzaji, Halima Mdee

Halima Mdee: Niombe radhi kwa kuchelewa dakika 15 kwani ilikuwa tuanze saa tatu na nusu, pili nitambue uwepo wa wazazi wangu wapo na mimi siku zote kwa shida na raha. Tatu nitambue uwepo wa viongozi wenzangu, hawa ni timu ya BAWACHA ambalo tumelizalisha baada ya kazi nzuri sana tuliofanya kujenga baraza nikiwa na timu yangu.

Vile vile tuna viongozi wa chama wanawake na wa kanda pia tuna katibu mkuu wa BAVICHA, Nusrat Hanje mstaafu vilevile tuna wabunge wa Bunge lililopita.

Nimekuja leo kuzungumza na nyie kwa sababu moja kubwa, niliamua kukaa kimya lakini ukikaa kimya vilevile unawapa nafasi wengine wanaongea, wanatengeneza uongo mwingi na uongo ukiwa mwingi unaonekana ni ukweli, imenilazima nije nizungumze kwa nia ya kutuliza haya mambo kwa sababu sio makubwa kama ambavyo yanataka yawe.

Mimi ni mwanachadema na nimekuwa mwanachadema kwa miaka 16 na kwangu mimi ukiacha wazazi wangu, familia yangu ya pili ni CHADEMA na katika muktadha huo maana kuna watu wanasema anakuja kuunga juhudi sijui, pamoja na kwamba mimi na wenzangu tumechukuliwa hatua za kinidhamu na viongozi wetu kwa mantiki ya kamati kuu, niwahakikishie mimi pamoja na timu yangu tutabaki kuwa wanachadema kindakindaki, nataka hilo niliweke wazi.

Mimi sina dhamira ya kuondoka CHADEMA, wenzangu, unaambiwa usiseme nafsi ya mtu lakini kwa historia yao ndani ya chama, hapa sihani kama kuna mtu ana pungufu ya miaka 5 ndani ya chama, kuna miaka 5, wengine wana miaka 10, wengine tuna miaka 16, wengine wana miaka 30 kwahiyo kila mmoja hapa ameijenga CHADEMA, amesaidia kuijenga CHADEMA kwa jasho na damu yake.

Pamoja na changamoto ambayo tunapitia, niwahakikishie wanachadema nchi nzima, Halima mnaemfahamu miaka yote ndio halima yuleyule na uaminifu wake kwa chama utabaki vilevile na ninaamini nikisema Halima maana yake na timu yangu.

Kumekuwa na maneno mengi, kuna watu wanasema Halima amenunuliwa, amepata mpunga mrefu, niseme hivi, mimi Halima Mdee sijawahi kununuliwa, sitanunuliwa, sitarajii kununuliwa.

Watu waliofanya kazi na mimi iwe kwenye chama, bungeni wanajua ukiambiwa taja watu watatu ambao rushwa kwao ni mwiko inawezekana Halima nikawa namba moja. Kwa hiyo mimi sina thamani ya kipande cha fedha, kazi zangu zote nimekuwa nikifanya kwa uaminifu na kwa mapenzi kutoka moyoni, sina maigizo.

Maana sasa hivi wanasema Mdee na wenzake maana mimi ndio napigwa mawe kwelikweli, fedha ukipewa haina siri, yani kama nimepewa bilioni 1, kama milioni 200 haina siri, ama itakuwa kwenye akauti ama itakuwa nyumbani kwenye sandarusi.

Kwakuwa haina siri walionipa watasema kama hapa ninawakana kama hawajanipa, wanasema Halima tulikupa tarehe fulani, hakuna yeyote aliepewa hela na kama kuna mambo yoyote yaliyotokea yalikuwa na dhamira nzuri kabisa ya kujenga taasisi imara, kustreghthen baraza la wanawake.

Hakuna alielipwa, mimi ni muhanga wa siasa za nchi hii, muhanga kwelikweli na tunavyozungumza kuna makesi mengine yaliyobaki. Tunavyozungumza juzi tumetoka kwenye uchaguzi mkuu, mimi kati ya wagombea wengi, ni bahati mbaya mainternet yalizimwa, mimi kati ya wagombea wengi ndiyo nilikuwa wa kwanza kwenda kwenye vituo asubuhi kuonyesha namna uchaguzi umekuwa rigged kwa hiyo nitakuwa mwendawazimu, jana nimeonyesha uchaguzi ulivyoenda halafu leo ninapokea mpunga, so what.

Kila mtu ametoka kwake hapa, hatujawahi kupata ulinzi sio tu wa usalama wa Taifa hata wa mgambo. Hakuna ulinzi wowote, sisi tulindwa na Mungu kwa hiyo ninashauri sana huyo mtu huko ajue kwamba atasubiri sana kama ataweza akanchonganisha na chama changu, atasubiri sana kama anadhani anaweza akanichonganisha na wanachama na Taifa kwa ujumla.

USULI WA MAMBO
Halima Mdee:
Kuhudhuria kamati kuu, tarehe 25 mimi binafsi nilipata barua saa kumi kasorobo jioni, nilipata barua kwa njia ya simu naamini mheshimiwa Matiko naye hakupata lakini wengine kila mtu alipata kwa muda wake yeye lakini wote kwa wote tulipata tarehe 25 tukitakiwa kuhudhuria kikao cha kamati kuu tarehe 27 saa mbili asubuhi.

Kutokana na sintofahamu iliyojitokeza, tarehe 26/11 tulimuandikia barua katibu mkuu tukimuomba asogeze kikao mbele japo kwa wiki moja na tulifanya hivyo, mosi utaratibu wetu wa katiba wa kikawaida, unasema mtu anatakiwa kujulishwa makosa yake kwa maandishi na kutakiwa kutoa majibu katika muda usiopungua wiki mbili apewe nafasi ya kujitetea mbele ya kikao kinachohusika na baada ya kusikilizwa na kujitetea, uamuzi utatoka baada ya wiki mbili lakini katiba yetu vilevile inaruhusu mazingira ya dharura ambayo kama tunadhani kwa maslahi ya chama jambo linahitaji kusikilizwa haraka, linaweza likasikilizwa kwa haraka.

Siko hapa kusema kwamba, tulivyopewa short notice kulikuwa na makosa, hapana. Short notice ilikuwa ni sahihi kwa mtu alieandika barua ya suala la dharura lakini kwa upande wetu tulidhani kutokana na presha kubwa iliyopo na kutokana na press ambayo ilikuwa imeshazungumzwa na katibu mkuu ikaongea mambo mazito sana, tukadhani ni busara labda tuombe extension ili hasira zetu zipungue, kila upande ulikuw na haki ya kuwa na hasira vile ilivyokuwa kwa hiyyo tuliandika barua ya kuomba extension ya wiki moja tukitambua kwamba katiba ina provision inayosema si chini wiki mbili ili ituwezeshe kila mmoja wetu tukiweza kwenda kwenye kikao, twende kwenye kikao hasira zikiwa zimepungua kidogo ili tukifanya maamuzi, tusifanye maamuzi yenye hasira kali.

=>Ijumaa tarehe 27 tulivuliwa uanachama na nyadhifa zote. Hapa tumevaa kombati, sisi tutaendelea kuwa wanachama wa hiyari ndani ya CHADEMA

=> Tutafanya michakato ya kikatiba ndani ya chama, jana jioni Mimi nilipata barua kutoka kwa Katibu Mkuu ya taarifa ya uamuzi

=>Muda ambao tulitakiwa kufike kwenye kikao kulikuwa na uhamasishaji kwenye Mitandao ya Kijamii wa baadhi ya viongozi wakihamasisha watu waje watupige mawe, watupige mayai viza

=> Tulidhani kiusalama haikuwa jambo rahisi kuhudhuria kikao katika mazingira hayo

=>Tutaanza kutafakari pamoja na wanasheria wetu ili kuangalia ni namna gani bora tunaweza kutatua tatizo hili

=> Leo sitaki kuwa na story nyingi, itoshe kusema tunaipenda CHADEMA ana hatutaondoka CHADEMA tutabaki wanachama wa hiari mpaka pale tutakapenda kujadili

=>Mwenyekiti (Freeman Mbowe) alisema hawa wanawake 19 ni majembe kweli kweli. Mimi kupoteza jeshi kama hili ni jambo ambalo sitalipenda

=> Tutaenda kuyajenga ndani kwetu, leo sitaki kuongea mambo mengi kwasababu ninyi wanahabari mnatafuta habari

=>Nataka hili jambo tulimalize, lirudi kwenye channel za chama. Sio sawa chama chetu kuwa kwenye magazeti, huyu anaongea hili na mwingine anaongea lile

=> Mliofuatilia mlishuhudia siku ya kikao kuna watu walijitokeza lakini si kwa kiwango kilichohamasishwa

=>Katika chaguzi zote tangu vyama vingi vimeanza kuanzia 2010, 2015 na 2020 hakuna uchaguzi ambao tuliuukubali

=>Lakini Wabunge si walienda? Kwanini 2020 wasiende mpaka sasa Madiwani wanaapa na Mbunge aliyechaguliwa ameapa
Usishangae sisi au wengine wakienda

=>Kutokubali Uchaguzi haimaanishi hautaingia kwenye vikao vya maamuzi kwa ngazi ya nchi. Mimi sidhani kama ni ujanja kukimbia kwenye vyombo vinavyofanya maamuzi

=>Unasema mapungufu kisha unaenda kwenye vikao hivyo kupambana na changamoto hiyo
inaitwa MBATA ya utosi kwa MATAGA na Ndugu-aai wao, yaani Mdee kawapiga nje Ndani, i mean Mzee Mdee.
 
Halima Mdee kamvua boxer feminist subwoofer. Bado yupo saaana CHADEMA. Wanaenda kuyajenga. Ubunge wa kikongwa kongwa siyo issue. Issue uanachama.
 
Wapo watakaokulaumu kwa vyovyote utakavyofanya bila ya kujali unalolifanya sasa ni jema au baya, kwa vile mwanzoni ulikosea, utaendelea kuwa mbaya tu siku zote.

Lakini wapo binadamu watakaokulaumu kwa kile ulichofanya wakati huo. Ukifanya vyema, bila ya kujali huko nyuma ulikosea, watakupongeza. Mimi nipo kwenye kundi hili.

Sikupongezi kwa sababu ulienda kuapa kinyume na maamuzi ya chama, sikupongezi kwa sababu umekuwa mbunge wala sikupongezi kwa sababu Ndugai amesema atakulinda. Bali nakupongeza kwa namna unavyokabiliana na tatizo lililopo mbele yako.

Wengi leo walitarajia umseme vibaya Mbowe na CHADEMA. Na hao ndio wanaodhani wamekuwa marafiki zako wapya.

Halima Mdee umeteseka sana kwa sababu ya kupigania haki na demokrasia Tanzania. Umeteseka sana kwa sababu tu umekuwa CHADEMA. Waliokuwa wanakusweka ndani, waliokuwa wanakutengenezea kesi, waliokuvunja mkono, waliokuwa wanakukejeli kwa maneno mengi ya dharau, leo wanajifanya ni marafiki zako.

Kumbuka kuwa mzazi wako hata kama anavaa lubega ni dhahiri ana upendo nawe zaidi kuliko jambazi mwenye jumba la ghorofa hata kama atakutoa kwa baba yako mwenye nyumba ya nyasi akawa anakulaza ghorofani kwenye chumba cha kifahari.

Nakupongeza kwa jinsi ulivyojibu hoja mbalimbali na kuonesha unatambua kuwa ni nani wanaokupenda na nani ni maadui lakini wanasema kuwa ndio walinzi wako. Yaani wauaji na watesaji wako leo wanakuwa walinzi na marafiki zako.

Nakupongeza kwa sababu hukuitusi CHADEMA, hukuitusi Kamati Kuu, hukumtusi Mbowe. Na hapa naipongeza Kamati kuu ya CHADEMA na Mh. Mbowe maana nao hata walipokuwa wakisoma maazimio ya Kamati kuu kuhusiana na Halima Mdee na wenzake, hawakuonesha kejeli wala chuki bali upendo wa dhahiri. Ni kama mzazi anayemchapa mwanae lakini anamchapa kwa sababu anataka abadilike na kuwa mtoto mwema na msikivu zaidi.

Mengine yatabakia katika maamizi ya Chama na ninyi wenyewe, lakini mpaka hapa umevuka kiunzi cha kwanza ambacho maadui wa CHADEMA na Mbowe walikuwa wakikisuburia kwa hamu.

Kwa njia uliyopita, kwa nguvu uliyoiweka, na imani uliyoitengeneza ndani ya CHADEMA, kwa Watanzania na Jamii ya kimataifa, usikubali kuipoteza imani hiyo kwa wepesi kiasi hicho.

Tunafahamu chama kitapitia njia ngumu, viongozi wa CHADEMA watapitia njia ya miiba lakini isiwe sababu ya kujijongesha kwa wadhalimu. Tengenezeni utaratibu, watu wenye mapenzi mema tuchangie kila mwezi ili kukitegemeza chama na watendaji wake. Hakika miongoni mwenu hakuna atakayekufa njaa wala kushindwa kutibiwa alimradi kuwepo utaratibu unaoeleweka.
 
CCM very low... mlishadadia Dr. Slaa mkaishia na aibu baada ya kale ka press mlikoa
mwandalia kudharaulika na wanachi.

Msivyo na busara mkahamia kwa Mashinji..mkaishia na aibu.

Mkajitosa kwa wale wabunge Nasari, Lijuabaridi ; Shilinde na wenzao pia mkaishia kupata aibu ya mwaka..mkaangukia pua.

Sasa kwa kuwa hamna mshipa wa aibu safari hii mmehamia kwa hawa wa dada...sasa hii ndiyo itakuwa aibu ya mwaka hadi nje ya nchi...mataifa watawadharau na hizo mnazoziwinda za Mabeberu mtazisikia tu mtapishana nazo!!
 
Umeitwa hujaenda, unataka chama kichukue uamuzi gani? Chama kimekuvua uanachama, kwa nini uingie bungeni kwa amri ya sipika? Kama kweli siyowachumia tumbo, wamwandikie barua spika kuwa wanalazimika kurudi chamani kukamilisha mchakato wa chama.

Kuendelea kuwa mbunge viti maalumu wa chadema ili hali chama kimewafukuza, ni uchumia tumbo tu huo

CHADEMA nzima ni wachumia tumbo tu kuanzia mwenyekiti
 
Wapo watakaokulaumu kwa vyovyote utakavyofanya bila ya kujali unalolifanya sasa ni jema au baya, kwa vile mwanzoni ulikosea, utaendelea kuwa mbaya tu siku zote.

Lakini wapo binadamu watakaokulaumu kwa kile ulichofanya wakati huo. Ukifanya vyema, bila ya kujali huko nyuma ulikosea, watakupongeza. Mimi nipo kwenye kundi hili.

Sikupongezi kwa sababu ulienda kuapa kinyume na maamuzi ya chama, sikupongezi kwa sababu umekuwa mbunge wala sikupongezi kwa sababu Ndugai amesema atakulinda. Bali nakupongeza kwa namna unavyokabiliana na tatizo lililopo mbele yako.

Wengi leo walitarajia umseme vibaya Mbowe na CHADEMA. Na hao ndio wanaodhani wamekuwa marafiki zako wapya.

Halima Mdee umeteseka sana kwa sababu ya kupigania haki na demokrasia Tanzania. Umeteseka sana kwa sababu tu umekuwa CHADEMA. Waliokuwa wanakusweka ndani, waliokuwa wanakutengenezea kesi, waliokuvunja mkono, waliokuwa wanakukejeli kwa maneno mengi ya dharau, leo wanajifanya ni marafiki zako.

Kumbuka kuwa mzazi wako hata kama anavaa lubega ni dhahiri ana upendo nawe zaidi kuliko jambazi mwenye jumba la ghorofa hata kama atakutoa kwa baba yako mwenye nyumba ya nyasi akawa anakulaza ghorofani kwenye chumba cha kifahari.

Nakupongeza kwa jinsi ulivyojibu hoja mbalimbali na kuonesha unatambua kuwa ni nani wanaokupenda na nani ni maadui lakini wanasema kuwa ndio walinzi wako. Yaani wauaji na watesaji wako leo wanakuwa walinzi na marafiki zako.

Nakupongeza kwa sababu hukuitusi CHADEMA, hukuitusi Kamati Kuu, hukumtusi Mbowe. Na hapa naipongeza Kamati kuu ya CHADEMA na Mh. Mbowe maana nao hata walipokuwa wakisoma maazimio ya Kamati kuu kuhusiana na Halima Mdee na wenzake, hawakuonesha kejeli wala chuki bali upendo wa dhahiri. Ni kama mzazi anayemchapa mwanae lakini anamchapa kwa sababu anataka abadilike na kuwa mtoto mwema na msikivu zaidi.

Mengine yatabakia katika maamizi ya Chama na ninyi wenyewe, lakini mpaka hapa umevuka kiunzi cha kwanza ambacho maadui wa CHADEMA na Mbowe walikuwa wakikisuburia kwa hamu.

Kwa njia uliyopita, kwa nguvu uliyoiweka, na imani uliyoitengeneza ndani ya CHADEMA, kwa Watanzania na Jamii ya kimataifa, usikubali kuipoteza imani hiyo kwa wepesi kiasi hicho.

Tunafahamu chama kitapitia njia ngumu, viongozi wa CHADEMA watapitia njia ya miiba lakini isiwe sababu ya kujijongesha kwa wadhalimu. Tengenezeni utaratibu, watu wenye mapenzi mema tuchangie kila mwezi ili kukitegemeza chama na watendaji wake. Hakika miongoni mwenu hakuna atakayekufa njaa wala kushindwa kutibiwa alimradi kuwepo utaratibu unaoeleweka.
Wasiliana na Saccos yako mbona walishazindua kuchangia saccos kupitia digitali mkuu!!?
 
Mdee tokaaaàaaaaaass CHADEMA Yuda mkubwaaaaaaaaa we, saliti lisilo ma aibu, bora askari magereza wangekuvunja mbavu kabisa
 
Mwanzo mzuri waje kwe meza ya maridhiano waombe msahama wajiuzuru ubunge viti maalumu, zipatikane baraka za chama kwenye teuzi zote.
 
Hapa ninachoona ni kwamba, kama wakisema tumekubali maana yake ubunge wameukosa. Mimi mwenyewe lazima niseme ni mwanachama ili niendelee hata kimahakama kuwa mbunge. Kuna maswali mengi kuliko majibu katika hili. Swali kuu, kwanini waliapa na wengine kutolewa magereza.
 
Back
Top Bottom