Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,305
- 9,734
Ndugu zangu Watanzania,
Leo nataka niwapeni uchambuzi wangu na Elimu kidogo juu ya nani angefaa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA baada ya Mbowe kung'atuka uongozini na kuruhusu mawazo mapya na fikra mpya na mikakati mipya ndani ya chama kuchukua nafasi yake. Kwanza ni lazima tukubaliane kwa pamoja kuwa ni ngumu sana kuirejesha CHADEMA ile ya Dkt Slaa ya 2010-2015.pili ni ngumu kwa CHADEMA kuitikisa nchi tena na kuliteka kundi la vijana kama ilivyokuwa miaka hiyo.tatu ni ngumu sana CHADEMA kupata imani kubwa na kuwa na ushawishi mkubwa kama iliyopata kuwa nao kwa watanzania miaka hiyohiyo ya Dkt Slaa.
Miaka ambayo kuvaa tisheti na sare za CCM na ukakatisha nazo mjini kama pale Mbeya mjini au Tunduma ilikuwa ni ngumu sana, miaka ambayo katika uchaguzi wa serikali za wanafunzi vyuo vikuu vilitekwa na vijana wa CHASO, miaka ambayo CCM ilionekana ni chama cha wazee na cha watu wasio na Elimu, miaka ambayo msomi kuwa mwana CCM ilionekana kama wewe ni fisadi, miaka ambayo magwanda na kombati za CHADEMA zilitamba sana mijini,miaka ambayo CHADEMA mikutano yao ilikuwa inafurika watu pale Luandanzovwe pale Mbeya mpaka unahisi watu wameisha majumbani mwao.
Miaka ambayo CHADEMA iliteka na kuwa na ushawishi katika miji na majiji yote makubwa hapa Nchini,miaka ambayo CCM ilipata wakati mgumu sana kufanya mikutano yake mijini na kupata wahudhuriaji kama wale waliohudhuria kwenye mikutano ya CHADEMA. kwa hakika miaka hiyo haitakaa irejee tena kwa kuwa wananchi wameshatambua kuwa CHADEMA ni wababaishaji na wasakatonge tu na ndio maana wamekuwa vigeugeu na wasio na misimamo kwa mambo wanayoyasimamia ,na hapa unaweza rejea kilichotokea 2015.
Sasa turudi kwenye mada.napenda kuwaambia ya kuwa Mheshimiwa Halima James Mdee ndiye mtu pekee ambaye alikuwa anastahili na kuweza kuiongoza CHADEMA baada Ya Mheshimiwa Mbowe. sababu ni kuwa Mdee ni mtu aliyekulia ndani ya CHADEMA,ni mtu ambaye tangia ubinti wake amekuwa CHADEMA,hajawahi kuwa chama chochote nje ya CHADEMA,ni mtu ambaye anaweza endana na vijana ndani ya CHADEMA,ni mtu ambaye anakubalika na vijana wengi.Ni mtulivu na asiye na Papara.ni msiri na msatahimilivu sana.hapa unaweza kurejea namna alivyokuwa mtulivu katika kujibu majibu pale anaposhambuliwa na baadhi ya vijana kuhusiana na uwepo wake Bungeni kwa sasa.
Hana hasira wala jazba ndio maana majibu yake yamekuwa ya staha sana hata ukimfuatilia mitandaoni.ni mtu ambaye anakubalika hata nje ya chama chake,ni mtu ambaye anaweza watuliza na kuonyesha njia anaowaongoza bila kuacha mpasuko ndani ya chama.ni mtu mwenye staha,adabu,hekima, busara na muungwana sana.ndio maana huwezi kukuta akitoa lugha za matusi au kumsikia akiwatukana viongozi wa serikali au CCM Kama wanavyofanya waropokaji na wenye mihemuko kama Lissu au Lema au Heche .Mdee hana mihemuko wala kukurupuka wala kuropoka ropoka hovyoo, ni mtu mwenye nidhamu ya kinywa ,ulimi na mdomo wake.ni mtu mwenye muunganiko mzuri kati ya akili yake na mdomo wake na anajuwa wakati gani aongee na wakati gani akae kimya na wakati gani apuuze tu jambo na maneno yaliyoelekezwa kwake kama mshale..
Ni mtulivu sana tena sana.amejaa hekima,mcheshi, mkarimu wa maneno na mwenye kujuwa hasa namna ya kujenga hoja.ni mtu anayeweza kiungaisha chama vizuri sana kwa sababu anakifahamu vizuri sana na anafahamu wapi kimetoka na njia kilizopita.
Ikumbukwe ya kuwa CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani hapa nchini lazima kipate mtu aina ya Halima Mdee, ambaye anaweza kukaa hata na mtawala mezani kuzungumza kwa maslahi mapana ya pande zote mbili.unajuwa siasa za mabavu, kutunishiana misuli na kukimbizana na mabomu mtaani na hata kupelekea majeraha,vilema na hata vifo havina sababu na wala siyo siasa zinazohitajika kwa wakati huu. Kwa sababu zinajenga chuki, uhasama, uadui, visasi na kutokuaminiana na hatimaye kuligawa Taifa letu. Hivyo anahitajika kiongozi aina ya Mdee ambaye anaweza kuwa na kifua cha kuhakikisha kuwa siasa anazoziongoza ni siasa za maridhiano ,kukubaliana kutokukubaliana na kufikia muafaka katika meza ya mazungumzo.
Watu kama akina Lissu au Lema waropokaji,ikiwa CHADEMA ikarogwa ikawapa uwenyekiti ndio utakuwa mwisho wake kwa sababu watakisambaratisha na kukivuruga sana CHADEMA na kukiacha kikiwa hoi bin taabani juu ya mawe.
Nampenda sana Mheshimiwa Halima Mdee namna anavyofanya siasa zake,anavyojenga hoja kwa utulivu na ninatamani sana angekuwa mwana CCM na kuwa ndani ya CCM.
Lakini mwisho naomba kumkaribisha sana tena sana ndani ya CCM ,Chama ambacho ni mtetezi wa watanzania na kilicho dhamiria kuwainua Watanzania kiuchumi na kubeba matumaini yao. Naomba kama itampendeza ajiunge CCM ili aje aungane na Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania mama Samia Suluhu Hasssan katika kuwapigania watanzania. CCM ni mahali ambapo anaweza kutimiza ndoto zake za kuwasemea wananchi tofauti na huko kwa pinga pinga.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
Leo nataka niwapeni uchambuzi wangu na Elimu kidogo juu ya nani angefaa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA baada ya Mbowe kung'atuka uongozini na kuruhusu mawazo mapya na fikra mpya na mikakati mipya ndani ya chama kuchukua nafasi yake. Kwanza ni lazima tukubaliane kwa pamoja kuwa ni ngumu sana kuirejesha CHADEMA ile ya Dkt Slaa ya 2010-2015.pili ni ngumu kwa CHADEMA kuitikisa nchi tena na kuliteka kundi la vijana kama ilivyokuwa miaka hiyo.tatu ni ngumu sana CHADEMA kupata imani kubwa na kuwa na ushawishi mkubwa kama iliyopata kuwa nao kwa watanzania miaka hiyohiyo ya Dkt Slaa.
Miaka ambayo kuvaa tisheti na sare za CCM na ukakatisha nazo mjini kama pale Mbeya mjini au Tunduma ilikuwa ni ngumu sana, miaka ambayo katika uchaguzi wa serikali za wanafunzi vyuo vikuu vilitekwa na vijana wa CHASO, miaka ambayo CCM ilionekana ni chama cha wazee na cha watu wasio na Elimu, miaka ambayo msomi kuwa mwana CCM ilionekana kama wewe ni fisadi, miaka ambayo magwanda na kombati za CHADEMA zilitamba sana mijini,miaka ambayo CHADEMA mikutano yao ilikuwa inafurika watu pale Luandanzovwe pale Mbeya mpaka unahisi watu wameisha majumbani mwao.
Miaka ambayo CHADEMA iliteka na kuwa na ushawishi katika miji na majiji yote makubwa hapa Nchini,miaka ambayo CCM ilipata wakati mgumu sana kufanya mikutano yake mijini na kupata wahudhuriaji kama wale waliohudhuria kwenye mikutano ya CHADEMA. kwa hakika miaka hiyo haitakaa irejee tena kwa kuwa wananchi wameshatambua kuwa CHADEMA ni wababaishaji na wasakatonge tu na ndio maana wamekuwa vigeugeu na wasio na misimamo kwa mambo wanayoyasimamia ,na hapa unaweza rejea kilichotokea 2015.
Sasa turudi kwenye mada.napenda kuwaambia ya kuwa Mheshimiwa Halima James Mdee ndiye mtu pekee ambaye alikuwa anastahili na kuweza kuiongoza CHADEMA baada Ya Mheshimiwa Mbowe. sababu ni kuwa Mdee ni mtu aliyekulia ndani ya CHADEMA,ni mtu ambaye tangia ubinti wake amekuwa CHADEMA,hajawahi kuwa chama chochote nje ya CHADEMA,ni mtu ambaye anaweza endana na vijana ndani ya CHADEMA,ni mtu ambaye anakubalika na vijana wengi.Ni mtulivu na asiye na Papara.ni msiri na msatahimilivu sana.hapa unaweza kurejea namna alivyokuwa mtulivu katika kujibu majibu pale anaposhambuliwa na baadhi ya vijana kuhusiana na uwepo wake Bungeni kwa sasa.
Hana hasira wala jazba ndio maana majibu yake yamekuwa ya staha sana hata ukimfuatilia mitandaoni.ni mtu ambaye anakubalika hata nje ya chama chake,ni mtu ambaye anaweza watuliza na kuonyesha njia anaowaongoza bila kuacha mpasuko ndani ya chama.ni mtu mwenye staha,adabu,hekima, busara na muungwana sana.ndio maana huwezi kukuta akitoa lugha za matusi au kumsikia akiwatukana viongozi wa serikali au CCM Kama wanavyofanya waropokaji na wenye mihemuko kama Lissu au Lema au Heche .Mdee hana mihemuko wala kukurupuka wala kuropoka ropoka hovyoo, ni mtu mwenye nidhamu ya kinywa ,ulimi na mdomo wake.ni mtu mwenye muunganiko mzuri kati ya akili yake na mdomo wake na anajuwa wakati gani aongee na wakati gani akae kimya na wakati gani apuuze tu jambo na maneno yaliyoelekezwa kwake kama mshale..
Ni mtulivu sana tena sana.amejaa hekima,mcheshi, mkarimu wa maneno na mwenye kujuwa hasa namna ya kujenga hoja.ni mtu anayeweza kiungaisha chama vizuri sana kwa sababu anakifahamu vizuri sana na anafahamu wapi kimetoka na njia kilizopita.
Ikumbukwe ya kuwa CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani hapa nchini lazima kipate mtu aina ya Halima Mdee, ambaye anaweza kukaa hata na mtawala mezani kuzungumza kwa maslahi mapana ya pande zote mbili.unajuwa siasa za mabavu, kutunishiana misuli na kukimbizana na mabomu mtaani na hata kupelekea majeraha,vilema na hata vifo havina sababu na wala siyo siasa zinazohitajika kwa wakati huu. Kwa sababu zinajenga chuki, uhasama, uadui, visasi na kutokuaminiana na hatimaye kuligawa Taifa letu. Hivyo anahitajika kiongozi aina ya Mdee ambaye anaweza kuwa na kifua cha kuhakikisha kuwa siasa anazoziongoza ni siasa za maridhiano ,kukubaliana kutokukubaliana na kufikia muafaka katika meza ya mazungumzo.
Watu kama akina Lissu au Lema waropokaji,ikiwa CHADEMA ikarogwa ikawapa uwenyekiti ndio utakuwa mwisho wake kwa sababu watakisambaratisha na kukivuruga sana CHADEMA na kukiacha kikiwa hoi bin taabani juu ya mawe.
Nampenda sana Mheshimiwa Halima Mdee namna anavyofanya siasa zake,anavyojenga hoja kwa utulivu na ninatamani sana angekuwa mwana CCM na kuwa ndani ya CCM.
Lakini mwisho naomba kumkaribisha sana tena sana ndani ya CCM ,Chama ambacho ni mtetezi wa watanzania na kilicho dhamiria kuwainua Watanzania kiuchumi na kubeba matumaini yao. Naomba kama itampendeza ajiunge CCM ili aje aungane na Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania mama Samia Suluhu Hasssan katika kuwapigania watanzania. CCM ni mahali ambapo anaweza kutimiza ndoto zake za kuwasemea wananchi tofauti na huko kwa pinga pinga.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.