Hali ya mabasi ya Mwendokasi Mbezi Mwisho ni kero tupu kama kawaida leo Novemba 15, 2023

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049

Kituo cha Mabasi ya Mwendokasi Mbezi Mwisho hali ni mbaya, abiria tupo wengi lakini mabasi hakuna, kuna watu wako hapa tangu Saa 12:10 Asubuhi (leo Novemba 15, 2023) lakini hakuna msaada wowote.

Hivi viongozi wetu wanaishi wapi mpaka hawaoni hii kero? Kila siku ni kilio cha Mwendokasi tu.

Hapa watu wameshakata tiketi, wengine wana hela za ngama, basi linakuja moja kisha lingine linakuja baada ya dakika 40 au zaidi.

Hakuna mvua kama ilivyosemwa na watabiri, labda ingetumika kama kisingizio, mamlaka zinatakiwa kuwajibika na ikiwezekana viongozi wanaosimamia usafiri huu wawajibishwe au wawajibike wao wenyewe, hii ni zaidi ya kero na shughuli nyingi za uchumi zimesimama.
 

Kituo cha Mabasi ya Mwendokasi Mbezi Mwisho hali ni mbaya, abiria tupo wengi lakini mabasi hakuna, kuna watu wako hapa tangu Saa 12:10 Asubuhi (leo Novemba 15, 2023) lakini hakuna msaada wowote.

Hivi viongozi wetu wanaishi wapi mpaka hawaoni hii kero? Kila siku ni kilio cha Mwendokasi tu.

Hapa watu wameshakata tiketi, wengine wana hela za ngama, basi linakuja moja kisha lingine linakuja baada ya dakika 40 au zaidi.

Hakuna mvua kama ilivyosemwa na watabiri, labda ingetumika kama kisingizio, mamlaka zinatakiwa kuwajibika na ikiwezekana viongozi wanaosimamia usafiri huu wawajibishwe au wawajibike wao wenyewe, hii ni zaidi ya kero na shughuli nyingi za uchumi zimesimama.
Rudini mkalale
 
Mvua ipo.. Tabata inanyesha sahivi.

Alafu kwani ni lazima mpande mwendokasi? Zamani mlikuwa mnaendaje huko ktk mizunguko yenu?
Mimi sio muhanga lakini nahisi zamani kulikuwa na mabasi ya moja kwa moja hadi mjini ambayo yalikatwa/kupunguzwa baada ya mwendokasi kuanza. Mwendokasi waliwataka abiria hao wote wao peke yao bila ushindani, sasa wanawaelemea.
 
Mimi sio muhanga lakini nahisi zamani kulikuwa na mabasi ya moja kwa moja hadi mjini ambayo yalikatwa/kupunguzwa baada ya mwendokasi kuanza. Mwendokasi waliwataka abiria hao wote wao peke yao bila ushindani, sasa wanawaelemea.
Si kweli, Bus zipo za kutosha.. hiyo njia napitaga mara nyingi tu, na kuna options nyingi za kufata ikiwemo kama usafiri ni wa tabu basi geuza na gari, gari iende mbezi urudi nayo simply. Ila watu watasema nauli hawana. Yaan huo umati wote hakuna mwenye 800 hapo au buku? Kujidekeza.

Pia kuna Bajaji zipo hapo zinaenda mjini kwa buku mbili mbili.
 
Mvua ipo.. Tabata inanyesha sahivi.

Alafu kwani ni lazima mpande mwendokasi? Zamani mlikuwa mnaendaje huko ktk mizunguko yenu?
Wakati bado uko kijijini Tandahimba na mwendokasi haujajengwa kulikuwepo na daladala nyingi za kwenda Mbezi ambazo zimesitishwa na kupunguzwa ili mwendokasi upate wateja wengi.
Kama isingekuwa hivyo mwendokasi ingekuwa na ushindani na mapato yao yangepungua ila akili ingewakaa sawa. Hata Gongolamboto itakuwa hivyo, kero.
 
Wakati bado uko kijijini Tandahimba na mwendokasi haujajengwa kulikuwepo na daladala nyingi za kwenda Mbezi ambazo zimesitishwa na kupunguzwa ili mwendokasi upate wateja wengi.
Kama isingekuwa hivyo mwendokasi ingekuwa na ushindani na mapato yao yangepungua ila akili ingewakaa sawa. Hata Gongolamboto itakuwa hivyo, kero.
Kuna mtu amewazuia kuunganisha gari? Ni lazima upande gari la moja kwa moja? Unashindwa kuunganisha gari?.
 
Kuna mtu amewazuia kuunganisha gari? Ni lazima upande gari la moja kwa moja? Unashindwa kuunganisha gari?.
Mjini sio kila mtu ana hela ya ziada mkuu. Kuna watu wanaishi ukitoa 500 kwenye mzunguko tiyari umeharibu. Na ujue ile imani kwamba gari litakuja, utasubiri utaona uongeze dakika 10, utaongeza 10 nyingine, 10 nyingine na ukitoka na daladala tu gari la mwendokasi ndio linafika. Na hapo utaunganisha kwenye foleni.
 
Back
Top Bottom