Hali ya Usafiri wa Mwendokasi Mbezi Luis asubuhi ya leo ni shida kama zote

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,462
Ndugu zangu wana JF hii video ni ya leo asubuhi katika Kituo cha Mabasi ya Mwendokasi Mbezi Luis, yaani kimekuwa na changamoto ya uhaba wa magari asubuhi ya leo Oktoba 16, 2023.

Foleni imekuwa kubwa ya abiria kusubiri mabasi, wapo ambao wamelazimika kusubiri mabasi hayo kwa saa tatu.

Upande wa Mabasi ya Mwendokasi yanayotokea Kibaha pia kulikuwa na abiria wengi kwenye vituo, mabasi ni machache na hivyo kusababisha msuguano wakati wa kuingia ndani ya usafiri huku baadhi yakipata tabu mlango kufunga kutokana na mbanano hadi kwenye milango.

Nilitamani kupiga picha nyingi ila nikashindwa baada ya kuona sura za watu zikiwa hazina matumaini, nikaona isiwe tabu ngoja nishudie kwa macho zaidi.

Wiki moja iliyopita viongozi wa Mkoa wa Dar na Wakala ya Mabasi Yaendayo Haraka (DART), Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) walinukuliwa wakisema wanashughulikia changamoto hiyo ya uhaba wa magari ili isijirudie.
 
Mafuta yakipanda UDA wanapunguza magari barabarani kupata faida na sio kutoa huduma kifupi huu mradi umeshakufa na aliyeua huu mradi ni King Magufuli kuondoa mfumo wa kadi kwa kuwatoa Maxmalipo. Kuna wizi mkubwa sana kwenye vituo vya kukatia tiketi.
 
Kuna mradi wo wote au taasisi yo yote ambayo inasimamiwa na serikali ambayo imewahi kufanya kazi kwa weledi, ukiachilia mbali, labda vyombo vyetu vya ulinzi na usalama?

Sisi hatuwezi kitu hata kiwe kizuri namna gani tutakiharibu tu na sababu kubwa ni hii rushwa na ufisadi wa kihayawani tulionao.

Mwendokasi ya Mbagala mradi umechelewa lakini tayari kuna tetesi kuwa watu wamepiga hela hatari na mradi umejengwa chini ya kiwango kiasi kwamba una matatizo tayari hata kabla ya kuanza kufanya kazi.

Sisi hatuwezi kitu labda tu uzembe, roho mbaya, ubinafsi, rushwa, kupendeleana na ufisadi! 🚮🚮🚮
 
Kuna mradi wo wote au taasisi yo yote ambayo inasimamiwa na serikali ambayo imewahi kufanya kazi kwa weledi?

Sisi hatuwezi kitu hata kiwe kizuri namna gani tutakiharibu tu na sababu kubwa ni hii rushwa na ufisadi huu wa kihayawani tulionao...
Kwa walivyoudororesha pale kupiga lazima. Haijawahi tokea Yani kituo kimoja kinajrngwa huu mwaka wa pili na hakijaisha
 
Ndugu zangu wana JF hii video ni ya leo asubuhi katika Kituo cha Mabasi ya Mwendokasi Mbezi Luis, yaani kimekuwa na changamoto ya uhaba wa magari asubuhi ya leo Oktoba 16, 2023...
Taarifa kama.hizi kuna majinamizi yamekaa ofisini yanakenua kuwa jambo lao linawiva soon

Utasikia shirika limegenishwa, tutaambiwa zitakuja basi zinazojiendesha zenyewe
 
Na bado kuna barabara mpya kibao za mwendokasi zinajengwa mjini hapo, zitakapoisha hayohayo mabasi yasiyotosha mbezi yatagawanywa na mbagala.
 
Ndugu zangu wana JF hii video ni ya leo asubuhi katika Kituo cha Mabasi ya Mwendokasi Mbezi Luis, yaani kimekuwa na changamoto ya uhaba wa magari asubuhi ya leo Oktoba 16, 2023...
Wakishauriwa kuwa hizo tenda waruhusiwe wengine walete mabasi kwenye hiyo njia hawataki.. dar inakua na inahitaji usafiri wa uhakika kila wakati hususan ahsubuhi na jioni ndio muda watu huenda makazini na kurudi hivyo usafiri changamoto na haitatuliwi kwa usahihi bali ni kwa matamko.

Hawa viongozi waingie ubia na kampuni zingine mabasi yawe mengi kwa faida ya maendeleo yetu na ufanisi mzuri katika kwa wa safiri wanaotumia mwendo kasi. Mabasi yaliyopo hayatoshi.

Ni mara nyjngi watu(abiria) wanasubiria basi zaidi ya nusu saa au lisaa hili ni tatzo katika maswala ya uchumi na utafutaji watu hawafiki kwa wakati. Walala hoi tunategemea saana mwendo kasi kwenda gererzan kununua bidhaa zetu za umachinga nk
 
Ndugu zangu wana JF hii video ni ya leo asubuhi katika Kituo cha Mabasi ya Mwendokasi Mbezi Luis, yaani kimekuwa na changamoto ya uhaba wa magari asubuhi ya leo Oktoba 16, 2023...
Naomba mheshimiwa Rais anipe ukuu wa hili shirika niendeshe,probation miezi 12,akiona sina ufanisi anirudishe ninapofanya kazi na anishushe pia;

Kuna shida nchi hii zinatengenezwa tu na watu wachache!
 
Back
Top Bottom