Mwanjelwa,
Mimi natofautiana na wewe kwenye hili japo nakubaliana pia na baadhi ya hoja zako.
Kwenye maendeleo kuna vitu vitatu muhimu ambavyo ni resources, watu na uongozi bora. Nyerere aliweka vitu vinne kwa kuongeza siasa safi. Uongozi bora kwa mawazo yangu unajumlisha siasa safi.
Tatizo la sehemu nyingi Tanzania ni capacity ndogo ya watu. Watu wanaweza kuwa na resources kwa mfano ardhi na wao wenyewe wakawa na nguvu za kuchapa kazi lakini hawana capacity ya kujiletea mabadiliko katika maisha yao.
Ndio maana hapa duniani hata kwenye makampuni makubwa uongozi bora ni nguzo kubwa. Ndio maana hao watu wanalipwa mamilioni ya pesa.
Ndio maana team moja leo inakaribia kushuka daraja, akija kocha mwingine unakuta wanaanza kupanda juu mara moja, watu ni wale wale, resources ni zile zile, kinachobadilika ni uongozi.
Sasa kwa experience yangu ya Tanzania, uongozi bora ni tatizo kuanzia wilayani mpaka kwenye taifa. Mbunge anayejua wajibu wake anaweza kuwa chachu ya maendeleo kwa kuunganisha resources zilizopo na watu waliopo. Anaweza kuona gap iliyopo na kisha kutumia njia mbali kama technology transfer akaiziba hiyo gap na hivyo akawa amewaletea wananchi maendeleo.
Politicians wana role kubwa ya ku play katika jamii, na wamekuwa wakifanya hivyo kwenye nchi mbalimbali. Ndio maana kuanguka kwa Wakomunist ghafla tukaona baadhi ya nchi zinabadilika. Hata kwa Tanzania, mbunge ambaye ni makini anaweza kuleta mabadiliko katika jimbo lake.
Nikupe mifano michache ambayo wengine tumewahi kufanya kule tunakotoka. Katika pita pita tukagundua wananchi wanalanguliwa kweli kwa mikopo ya ajabu ajabu, asilimia 30% kwa miezi sita. Mimi sikupenda hicho kitu, kuuliza wilaya wanafanya nini kutatua tatizo hilo? Hakuna aliyekuwa interested. Kuuliza jamaa mbalimbali nikagundua PRIDE wanatoa mikopo kama hiyo kwa riba nafuu sana, nikawatafuta na kuwaambia, japo mwanzoni walisita, baada ya muda wakaenda kuchunguza na kugundua kumbe soko ni kubwa sana. Leo hii hiyo wilaya iko katika kumi bora za PRIDE na vijana wengi wamefaidika kwenye biashara zao. Kuna mifano mingine mingi ambayo ukitaka niandikie PM nitakuambia.
Kuna viongozi wako pale miaka na hawaoni ni tatizo, wakati mtu mwingine unaenda siku moja na kuona hili ni tatizo inatakiwa litatuliwe kwa faida ya wananchi.
Kwa mawazo yangu viongozi na hata politicians wana role kubwa ya ku play katika kuwaletea maendeleo wananchi. Tukisema kuwaletea maendeleo wananchi haina maana kutumia pesa zao, ina maana wao kuwa catalyst of change. Kuwa troubleshooters wa matatizo yaliyoko wilayani kwao na kuandaa strategies ambazo zitasaidia kutatua hayo matatizo na hivyo kusogeza maendeleo mbele.
I don't understand. How can you be ushered with abundant rosources at the same time you don't have capacity to utulise them! Do you need someone to tell you what to do? Are the politicians meant for this purposes?! Utakuwa ujinga sana kusubiri, ati Mwakyembe akuambie namna ya kutumia raslimali zako mwenyewe! Mwakyembe kama yeye yuko pale ili mjadiliane namna ya kuendeleza kile mlichonacho na si kuanzisha namna ya kutumia kile ulichonacho.