Habari za afya ya Dr. Harrison Mwakyembe

Habari za afya ya Dr. Harrison Mwakyembe

Mtanzania,

Mkuu wangu kulingana na habari hiyo, mwenye Guest na hao waliowaliwiti watoto wa shule ya msingi wote wana makosa!..

Mkandara,

Mwenye guest atakuwa na makosa yapi? Ninaweza kukubali kwamba wafanyakazi walioruhusu hao wanafunzi waingia hapo ndani wana makosa, lakini sio mmiliki. Mimi leo Mtanzania niwe na nyumba yangu ya kulala wageni Kyela, kosa litendeke pale mimi niko mbali, utasema nina makosa? How?

Hizo nyumba zenyewe ni zile sijui hata uziitaje yaani control hakuna. Kama nchi yetu inafuata sheria nyumba kama hizo ni kufunga kabisa. Ziko nyingi kweli Kyela mjini, ni takataka tu. Kwasababu ya biashara ya Malawi basi hata nyumba za hovyo zinapata wateja.

Case yenyewe siijui vizuri kwahiyo siwezi ku comment zaidi lakini nijuavyo hao vijana walikamatwa na kuchukuliwa hatua.
 
Samwel Nijuavyo aliwajengea au ana mpango wa kujenga shule maana kwenye fundraising hata mie niliwachangieni tena si kitoto! Au hiyo shule nayo ni hewa?[/quote said:
Womenofsubstance,

Usiwasikilize sana hawa vijana. Asante kwa kuchangia, naamini pesa zako zilifikishwa na kutumiwa vizuri.

Kuna shule nyingi sana zimejengwa Kyela kuanzia 2006 kuitikia wito wa Lowassa. Pia DC Mashimba kafanya kazi kubwa sana kwenye ujenzi wa hizo shule. Yeye ndiye alikuwa mfuatiliaji kwasababu mbunge muda mwingi hayuko Kyela.

Naamini viongozi wote akiwemo mbunge walishirikiana pamoja na wananchi kutimiza hilo lengo.
 
Mtanzania,
Watoto wa shule ya msingi (under age) hawaruhusiwi kabisa kuingia guest house na mtu mzima.. Ni kutokana na mazingira yetu kuwa guest house ni sehemu ya ufuska..Ni sawa na mtoto mdogo huku Ulaya Strip Club!..kwa hiyo kiraia ni mkosa kwa kuruhusu vitendo hivyo kufanyika ktk guest yake na Kiuongozi vitendo vile kutokea chini ya himaya yake anatakiwa kujiuzuru..
Ni jukumu la mwenye guest kuweka sheria ambazo zinawalinda watoto wadogo tena mtu mwenyewe kama ni Diwani ndio kabisa inazidisha uchafu huo.. Huyu anatakiwa kuwa mfano bora na mwenye kuhimiza matunzo bora kwa watoto.
Mkuu, if he can let that go by unafikiri kweli huyu mtu anaweza kuongoza!..Hivi kweli unataka kunambia mkuu wa mkkoa wa Shinyanga au Mbeya won't be responsible na vifo vya Albino hata kama vimefanyika nyumbani kwake kwa sababu hakufanya yeye!..
 
Yaani mmiliki wa jengo fulani ambapo uhalifu umefanyika dhidi ya watoto awajibishwe!? Kosa ni la waliopanga, polisi, watu wa halmashauri n.k siyo mmiliki...
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu wangu sheria inaifahamu au unazungumza kwa kufikiria..
Kuna tofauti kubwa kati ya nyumba ya kupangisha na Guest house... Hii ni sehemu ya biashara na moja ya masharti yake ni pamoja na kulinda watoto..hawa watoto wameingia ndani ya nyumba unayofamnya biashara..
Huyu Diwani hakupangisha jengo hilo kwa mtu mwingine ambaye ndiye anaendesha biashara hiyo...na katika biashara hiyo ndipo kumefanyika matusi hayo.
Hapa kwetu Club zikilia risasi tu na akafa mtu club hufungiwa.. aliyeua sii mwenye Club, Club ikijulikana kunauzwa Unga hata kama mwenye Club hahusiki itafungwa na wahusika watapelekwa jela acha mbali mtu huyo awe kiongozi wa wananchi hao hao anaotakiwa kuwalinda. Vitendo hivyo vitachunguzwa na ikijulikana kama kuna uhusiano kati ya mwenye mali na mahisuka kesi inazidi kuwa kubwa zaidi..
Mbali na yote haya swala hapa ni waandishi ambao hawakuona kuwa habari kama hii ina uzito mkubwa kwa visingizio kwamba sio wao wahariri wa gazeti isipokuwa ya Mwakyembe ndiyo yanauzika.. Priorities mkuu wangu ndicho kinachogomba siku zote.
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu wangu sheria inaifahamu au unazungumza kwa kufikiria..
Kuna tofauti kubwa kati ya nyumba ya kupangisha na Guest house... Hii ni sehemu ya biashara na moja ya masharti yake ni pamoja na kulinda watoto.. Huyu Diwani hakupangisha jengo hilo kwa mtu yeyote ni biahsra yake na katika biashara hiyo ndipo kumefanyika matusi hayo.
Hapa kwetu Club zikilia risasi tu na akafa mtu club hufungiwa.. aliyeua sii mwenye Club, Club ikijulikana kunauzwa Unga hata kama mwenye Club hahusiki itafungwa na wahusika watapelekwa jela acha mbali mtu huyo awe kiongozi wa wananchi hao hao anaotakiwa kuwalinda.

Unakumbuka yaliyotokea Tabora mkuu wangu? Mmiliki aliwajibishwa kwa kosa gani!? Naelewa unachosema nataka kukumbushia tu kuwa linapokuja suala la watoto, hatuna rekodi nzuri kama Taifa!
 
Mkuu Mkandara,

Madai ni kwamba kuna wanafunzi walifanyiwa hivyo vitendo kwenye guest house ambayo mmiliki wake ndiye diwani wa Kyela mjini.

Sasa hapo mwenye kosa ni mmiliki wa guest au hao waliofanya kosa na kukamatwa?

Huyo jamaa ni Mkinga na pia haelewani na mheshimiwa. Ghafla kuna vita kibao juu yake na madai kama haya ya akina Nsesi. Juzi kwenye kura za Albino, wametuma vijana wao wakaandika jina la huyo diwani kama ni jambazi. Kuna maneno kibao ya kibaguzi yanaendeshwa. Ukienda kuangalia, huyo diwani anajituma kwenye maendeleo kuliko hata madiwani wengine. Lakini kwasababu sio Mnyakyusa tayari maneno, kwani waliomchagua mbona walijua hilo?

Ni siasa za Kyela tu na ujinga wa watu kutumia elimu zao, magazeti yao kuendeleza chuki badala ya umoja.
Tulikuwa na DC wa maana sana pale Kyela kwa ufuatiliaji na kafanya kazi kubwa kweli kwenye ujenzi wa shule. Kawabana watendaji, kafuatilia maendeleo lakini nasikia majungu yamepigwa mpaka jamaa kaondolewa. Nsesi alikuja hapa akaandika kahongwa gari na Kiwira Coal Mine, hivi hata anaijua Kiwira? Wafanyakazi wa Kiwira Coal Mine wako hoi mno, hata hizo pesa za kumnunulia gari mkuu wa wilaya watatoa wapi? Watu wanashindwa hata kutoa 70,000 ya kulipia ada za watoto wao kwa mwaka, kweli watamnunulia gari DC?

Kule kwetu nafikiri ifike mahali tupigane viboko, ujinga umekuwa mwingi sana.

ebanaee

du.

1. hatuhitaji watu watumie elimu zao au media zao kuendeleza chuki. chuki hazipalilii maendeleo

2. alivyoondolewa huyo DC ujenzi wa skuli unasuasua?

3. tukianza kuchapana we utaanza kumchapa nani? unanikumbusha bakora za 'ndengere' sorry ule mti sijui kiswahili chake mpaka leo
 
Mzee Mwanakijiji,
Usisahau tu kuwa hili ni Taifa la Kulindana!..

Ohh by the way, my point bado inasimama kwamba mwenye nyumba ya kupangisha hana makosa isipokuwa mmliki wa biashara yenyewe..Kwa maana hiyo Diwani anaweza tu kutokuwa na makosa kama nyumba ni yake lakini kapangisha mtu anayefanya biashara ya guest house, lakini kama ni nyumba yake na biashara ni yake au yeye kapangisha na kufanya biashara hiyi, bila shaka ana makosa yote!
 
Hizo nyumba zenyewe ni zile sijui hata uziitaje yaani control hakuna. Kama nchi yetu inafuata sheria nyumba kama hizo ni kufunga kabisa. Ziko nyingi kweli Kyela mjini, ni takataka tu. Kwasababu ya biashara ya Malawi basi hata nyumba za hovyo zinapata wateja.

mi naifaham ile guest. niliwah kulala pale. kama hajaweka control ni kosa lake na wala si guest ya uchochoroni. iko mjini kabisa karibu na stend ya mabas

si ghali lakin ni salama kwa kuwa mjini zaid. si unaisema ile guest inayotizamana na iliyokuwa kyela commercial college? half london kitu kama hicho? ndo unasema ya uchochoron? hapa umetia chumvi

kama wateja wapo kwa biashara ya malawi si ndo vizur? cha muhimu wazid kujenga zaid

arusha maeneo ya ngarenaro kupata nyumba ya kupanga shida (nyumba mjengo wa nyumba zilizo nying ilala na magomen). wenye nazo wamezigeuza guest au mabaa. sasa kumbe je! na zinajaa acha mcheso! lakin pia kuna mahoteli makubwa kibao
 
Mkuu, una introduce a very interesting element katika suala zima la uandishi na michango yetu wanaJF. Hivi asiye mteule wa Dr. Mwakyembe anatakiwa aandike vipi, na wewe mwenzetu ni mteule wa nani? Fataki

Pengine aliuliza suala hilo kwa vile ni jambo la kawaida humu kuandika kwa kubase upande mmoja na sia tulishajuulishwa kuwa lawama hizo kazitowa mwenyew Mwakyembe na akachagua waandishi wasiomwandika vibaya ndio wahudhurie mkutano. Duh ushujaa mwengine wa kupose na kupigwa picha!
 
Mi natokea Kyela nafanya kazi Karatu.Mbunge wetu Mwakyembe hajafanya chochote cha maana na baada ya kuona uchaguzi unakaribia unatapa tapa.Ufisadi ni swala la kitaifa zaidi na tulitaka mbunge wetu ashugulikie matatizo yetu kwa muda mwingi na kupambana na ufisadi 'in his spare time'.Mimi sio mpenzi wa chadema lakini namsifu Dr.Slaa ambaye yuko karibu sana na wapiga kura wake na utamuona jimboni hata siku za mwisho wa wiki bunge likiwa kwenye vikao.
 
Hivi Mwakyembe amefanya kitu gani kinachoonekana katika kutoa majibu/ mikakati ya kutatua matatizo ya jimbo lake la uchaguzi? Nakubaliana na Uporoto01 kuwa kusakama mafisadi ni vizuri lakini kwanza yeye ni mbunge wa Kyela ashughulikie jimbo lake la uchaguzi, atafute jinsi ya kukabiliana na mafuriko, na kutatua tatizo la njaa na masuala ya afya.
 
Jamaa ni msanii wa kutupwa. Juzi kaitisha mkutano wa vijana wanaochangishana wanaitwa vijana wa Vikoba. Akaanza kuwaambia atafungua bank, atamwita Mengi na Mengi ana uwezo hata wa kuchangia milioni 100.

Baadaye akawaita wale washirika wake pale mjini na kuwauliza waelezee wanachokijua. Wakaanza kusema mipango ndio iko hatua za mwisho na ujinga mwingine mwingi tu.

Mtu unabaki kujiuliza, hawa ndio wasomi wa nchi hii, kwanini wanakuwa wahaba wa ukweli?

DC aliyeondoka ndiye alikuwa na wazo la kuunda bank ya wilaya lakini hakuungwa mkono. Sasa mheshimiwa anajifanya hilo ndilo lengo lake.

Kama atatekeleza ni vizuri, ingawaje kwa jinsi wanavyoongea, unajua ni usanii tu kwa ajili ya mwaka kesho.
 
Tatizo kwa dk Mwakyembe ni kuwa yy ni right person in the wrong groups, sasa yanayomfika wananchi wake wanalalamika nini, ww utaishije na draculars wakati ww hunywi damu, huna meno marefu,kucha zako fupi. Comeon dk Mwakyembe so long as wananchi wako wanakuunga mkono quit from these "draculars" wanaojiita wanamapinduzi,wanyinyaji wakubwa kabla hawaja kutafuna ukageuka kama wao.Dont say i did not warn you dk.
 
Bahati nzuri nimeishi Kyela muda mrefu na nimeoa huku. Nazijua sana siasa za Kyela na Mkoa wa Mbeya. Mwakyembe kajitahidi kufanya yale aliyoyaweza ila hizi kelele mnazoziskia ni za wale wale walioko katika payroll ya mafisadi. Endapo wataendelea tutawafichua kwa kutoa vielelezo vya vikao vyao na namna wanavyo network ili kumhujumu Mwakyembe.

Mwakyembe ni mtu mzuri ila jambo litakalomharibia ana laana aliyowasaidia wa Moravian waliojitenga kutoka Rungwe. Alifanya kazi kubwa sana ya kisheria na kifedha kufanya jambo hili. Inawezekana alikuwa sahihi ila kwa vile yeye ni mwanasiasa anayehitajika kuungwa mkono na watu wengi, hilo lilikuwa kosa kubwa sana. Yeye angechukua neutral ground au hata angeunga mkono kundi hili kimyakimya lakini sio kwa kwenda front. Ajifunze kwa Mkuu wa Majeshi yeye sio mwanasiasa lakini anakubalika kwenye makanisa yote mawili yaani ya Rungwe na Kyela.

Mwakyembe anaungana na watu wanaotaka kuwa na dhehebu la wanyakyusa wa wilaya ya kyela tu. Je kweli kwa zama hizi hilo linawezekana?. Kanisa la Moravian ndio kanisa kubwa sana mkoa wa mbeya, na hata sasa wa moravian wengi hawajisikii vizuri kwa vile linaonekana kanisa la kimkoa zaidi na jitihada zinafanyika kufungua makanisa kwenye mikoa mingine kama Arusha, Mtwara, zanzibar, Ruvuma etc ili kulipa sura ya kitaifa. Sasa mtu kama Dr anashabikia watu wanaotaka kuuunda kanisa la wanyakyusa wa kyela hapo ndipo namuona ana tatizo. Ushauri wangu ajichanganye asi base sana kwa kanisa moja.

Hata kama Rungwe walifanya makosa yeye anatakiwa kuwa makini, lakini akitubu dhambi hiyo laana hiyo itaondoka na atakuwa mbunge safi na muumini mzuri. Anachotakiwa kufanya ni kwenda kanisa la Moravian ( Rungwe) pale Kyela aseme jamani mimi kuanzia leo naondoa uadui kati yetu na naacha kuunga mkono moravian Kyela watu watampigia makofi na kumshangilia basi amemaliza. Pia afanye hivyo huko Dar basi atakuwa amemaliza.

Ushauri mwingine Mwakyembe ndio ni msomi sana tunamkubali lakini anahitaji mtu mkomavu kumuongoza katika kumshauri nini aongee na nini asiongee. Ukimya wa Mwandosya unamsaidia sana watu kutojua madhaifu yake (kama anayo, offcourse ni mwanadamu) maana kwa kukaa kwake kimya najonekana ni mtu mwenye hekima sana.

Dr mimi nimesema haya kwasababu nakuaminia na ni shabiki wako wa kutupwa ukirekebisha hayo hakuna wa kukuletea vikwazo kwenye kazi yako ya kupambana na mafisadi- Mwakyembe for Presidency.................
 
Bahati nzuri nimeishi Kyela muda mrefu na nimeoa huku. Nazijua sana siasa za Kyela na Mkoa wa Mbeya. Mwakyembe kajitahidi kufanya yale aliyoyaweza ila hizi kelele mnazoziskia ni za wale wale walioko katika payroll ya mafisadi. Endapo wataendelea tutawafichua kwa kutoa vielelezo vya vikao vyao na namna wanavyo network ili kumhujumu Mwakyembe.

Ntambaswala,

Hiyo ndio kazi ya JF, kufumua yale yanayofichwa chini chini. Kama una taarifa kama hiyo kwanini uifiche? Anika tu hivyo vikao vyao na wananchi tutachambua pumba na mchele.
 
Engineer,Mtanzania,ntambaswala,

..majuzi si nilisikia Mwakyembe kawaita wana Kyela kuchangia mfuko wa elimu?

..lakini pia ni vizuri wananchi wa Kyela wakachambua mchango wake ktk kulihudumia jimbo lake.
 
Engineer,Mtanzania,ntambaswala,

..majuzi si nilisikia Mwakyembe kawaita wana Kyela kuchangia mfuko wa elimu?

..lakini pia ni vizuri wananchi wa Kyela wakachambua mchango wake ktk kulihudumia jimbo lake.

JokaKuu,

Nafikiri ni kweli aliwaita wana Kyela kuchangia na kuna watu wengi tu wamechangia.

Ila niliambiwa hata huo mkutano ulivurugika baada ya kushindwa kuelewana juu
ya nani akabidhiwe hizo fedha kati ya kundi la mbunge na lile la DC.

DC akapewa za kwake na mbunge naye akapewa za kwake.

Nafikiri ni muhimu kuhakikisha hayo makundi yanakufa maana yanayumbisha watu bila sababu za msingi. Kwenye masuala ya pesa transparency ndio dawa yake. Hao wanaosema unakula pesa wape wao ndio washike hizo pesa au ndio wawe waangalizi wa hiyo account na maneno yote ya pembeni yataisha hapo hapo.
 
Mi natokea Kyela nafanya kazi Karatu.Mbunge wetu Mwakyembe hajafanya chochote cha maana na baada ya kuona uchaguzi unakaribia unatapa tapa.Ufisadi ni swala la kitaifa zaidi na tulitaka mbunge wetu ashugulikie matatizo yetu kwa muda mwingi na kupambana na ufisadi 'in his spare time'.Mimi sio mpenzi wa chadema lakini namsifu Dr.Slaa ambaye yuko karibu sana na wapiga kura wake na utamuona jimboni hata siku za mwisho wa wiki bunge likiwa kwenye vikao.

Mkuu, JF ni forum ya ku"fertilize" ideas na kubadilishana on the basis of concrete data, reasoned positions. Unachotupa hapa Mkuu Uporoto, with due respect, ni UDAKU!
 
Jamaa ni msanii wa kutupwa. Juzi kaitisha mkutano wa vijana wanaochangishana wanaitwa vijana wa Vikoba. Akaanza kuwaambia atafungua bank, atamwita Mengi na Mengi ana uwezo hata wa kuchangia milioni 100.

Baadaye akawaita wale washirika wake pale mjini na kuwauliza waelezee wanachokijua. Wakaanza kusema mipango ndio iko hatua za mwisho na ujinga mwingine mwingi tu.

Mtu unabaki kujiuliza, hawa ndio wasomi wa nchi hii, kwanini wanakuwa wahaba wa ukweli?

DC aliyeondoka ndiye alikuwa na wazo la kuunda bank ya wilaya lakini hakuungwa mkono. Sasa mheshimiwa anajifanya hilo ndilo lengo lake.

Kama atatekeleza ni vizuri, ingawaje kwa jinsi wanavyoongea, unajua ni usanii tu kwa ajili ya mwaka kesho.


UDAKU MWINGINE! Hivi JF tutafika?
 
Back
Top Bottom