Habari za afya ya Dr. Harrison Mwakyembe

Habari za afya ya Dr. Harrison Mwakyembe

Ogah,
Wengine tumejaribu kushirikiana, lakini ili ushirikiano uwepo si ni lazima pande zote mbili ziwe tayari kushirikiana?

Suala la Kyela mimi sasa nimejiondoa kuongelea watu hivyo sitaingia ndani zaidi.

Mbona hujatupongeza kwa kutokuwa wabaguzi? Hata dadako na wajomba zako wanaruhusiwa kugombea vyeo Kyela.

ooppps i missed this....(unajua tena mabox)........honestly.....Ukarimu wa watu wa Kyela umenifanya kila ninapokuwa Tanzania kupanga safari ya kutembelea mashemeji zangu huko (that is my experience) hata niliposikia kuwa watu wametupiana makonde nilishangaa sana......najua kuwa ni watu wenye misimamo kwa sana tu......

Ndugu yangu Mtanzania......HONGERENI SANA kwa kuonyesha ishara ya kutokuwa wabaguzi (at least kwa vielelezo vilivyotolewa so far).......
 
CCM WAMBANA MWAKYEMBE
Na Israel Mwaisaka,Mbeya

HALMASHAURI kuu ya CCM ya wilaya Kyela imemtuhumu mbunge wao Dkt,Harrison Mwakyembe pamoja na mwenyekiti wa CCM wilaya Bw,Japhet Mwakasumi kuwa ndiyo vinara wa kukigawa chama hicho katika makundi na kusababisha viongozi kushindwa kuelewana miongoni mwao iliyopelekea hivi karibuni makatibu kata kuwapiga viongozi wa wilaya

Tuhuma hizo zilitolewa na wajumbe wa kikao cha halmashauri kuu ya CCM wilaya kilichoketi jana ili kujadili maamuzi ya halmashauri ya mkoa ya chama hicho baada ya kukataa mapendekezo ya kamati ya siasa ya wilaya Kyela ya kuwavua uanachama makatibu kata wanne waliowapiga viongozi wa wilaya na kumsababishia maumivu makali katibu wa wilaya Bi,Maria Mwambanga

Katika kikao hicho wengi ya wajumbe walimshushia makomboraDkt,Mwakyembe kuwa toka yeye awe mbunge wa jimbo hilo ametengeneza makundi ndani ya chama huku akidaiwa kummiliki mwenyekiti wake wa chama wa wilaya ambaye ameonekana kuyumbishwa katika maamuzi yake mbalimbali

Walisema kufuatia hari hiyo ndani ya chama hicho kumekuwaepo na kutoelewana miongoni mwao na uhasama mkubwa kitu ambacho kimepelekea baadhi yao kuonekana wananyanyaswa na hawana haki ndani ya chama hicho na kuamua kuidai haki hiyo kwa kutumia nguvu kama walivyofanya siku hiyo viongozi hao wa kata
 
Tukizungumzia maslahi ya Taifa na sio Binafsi..Mbinu za kumchafua Mwakyembe haziwezi kushinda... inajulikna kwamba kuna kundi linataka kuona Mwakyembe, Mama Kilango, Sitta na baadhi wabunge hawarudi ktk uchaguzi wa mwaka 2010 kwa sababu wabunge hawa wamekuwa chachu ya chama hicho hata kusababisha kundi kubwa la viongozi kuondolewa madarakani..
Kwa hiyo yatasemwa mengi sana, lakini ukweli unabakia kwamba makundi ndani ya chama hayakuanzishwa na Mwakyembe.. tunayaona Busanda na kila kata, wilaya mkoa kwa sababu hakuna kiongozi asiyetaka kukaa meza kubwa ktk kugawana umaskini..
Na Machafuko ndani ya CCM yanaweza kuwa sababu kubwa ya ushindi kwa vyama vya Upinzani hivyo wao waendelee tu kujimaliza na siasa uchwara za kupigana makonde wakati sinia la ubwabwa linaisha.

.......nina interest Kyela kama ifuatavyo:
1.raia wa Tanzania na napenda maendeleo ya kila sehemu Tanzania
2.wajomba zangu i.e. watoto wa dada yangu (Kiafrika watakuwa ni watu wa Kyela)

It is unfortunate kuwa Udhaifu alionao Dr. Mwakyembe "DHARAU" inamletea matatizo......dharau hiyo niliishuhudia pale alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari (...it was something to do with usomi...)

......na unfortunate again Mafisadi wanatumia udhaifu huo kuonyesha madhara yake kwa maendeleo ya wana-Kyela (so it is claimed) kupitia njia mbali mbali..........

Cha msingi ninachomshauri Dr Mwakyembe ni ku-stick kwa yale aliyowaahidi wana-Kyela.....hata kama hujakamilisha lakini efforts zionekane.......ukitumia propaganda na wapinzani wako pia watatumia propaganda......sasa hapo itategemea propaganada za nani zina nguvu.............na ujue wazi kuwa PROPAGANDA NI PESA.......

...hutawatendea haki wananchi wa Kyela kama utatumia propaganda za vita yako ya Ufisadi (of which im giving you an A) kuwagawa wanakyela......kinachohitajika Kyela ni Kazi na maendeleo. You can do it im sure.....na time unayo
UKIINGIA KYELA PIGA MZIGOKWA AJILI YA WANANCHI WAKO.......UKITOKA KYELA PAMBANA NA MAFISADI.......kupokelewa kwa maandamano hakutampatia mwana-Kyela mkate....ni vikao tu vya kutathmini uwajibikaji ndivyo vitaleta maendeleo Kyela......ALL THE BEST Dr. Mwakyembe
 
Ogah,
Mkuu nakubaliana sana na mawazo yako lakini tazama madai wanayomshushia Dr. Mwakyembe. Hivi Kyela lini imefikiriwa ktk maendeleo ya wilaya hiyo!...Sikumbuki. Ni wilaya ambayo kwa miaka kibao imekuwa nyuma sana ukilinganisha na wilaya nyingine kama sikosei hivyo wanachotaka wao ni mwanzo mpya na sii kwamba Dr. Mwakyembe amewarudisha nyuma...

Kitu wanachokosea wengi ni kwamba Mwakyembe kama wabunge wengine anawakilisha Kyela na matatizo yao kisha yafikisha..Utekelezaji wa ahadi alizowapa wananchi zinapitishwa na serikali iliyopo madarakani na mara zote mkuu wa wilaya na halamashauri ya wilaya wanaweza kabisa kumwangusha mbunge hata kama fungu lipo..

Ni matatizo ambayo yanawakuta hata Wabunge wa vyama vya Upinzani.. na kama unakumbuka niliwahi kusema Mbunge anatakiwa kuwa na nguvu za mkuu wa wilaya kisha utekelezaji ubakie na halmashauri lakini kama Mbunge atabakia kuwa mwakilkishi wa wilaya Bungeni bila mamlaka yoyote ya matumizi ya fungu waliopewa itakuwa kazi kubwa ktk nchi hii ambayo Ufisadi umetawala...Mtu kama Mwanakijiji hapa ni mchawi na atatafutiwa fitna hadi akome lakini haiwezi kuondoa nguvu na juhudi zake ktk kuhakikisha haki inapatikana wala sisi kuchukia juhudi hizo.

Pili swala la Mafisadi ni kazi aliyopewa na rais nje ya kazi za Ubunge wake wa Kyela.. alistahili pongezi lakini badala ya kupongezwa imechukuliwa kama kigezo cha Mwanakijiji au FMES hapa JF ktk vita yao against Ufisadi, ati ina wa cost wana Kyela kugawanyika!...Ukweli ni kwamba Mwanakijiji ha cost kitu JF na makundi yanayotokea hapa ni wale wanaopinga juhudi zake,wao ndio wamejikata sii Mwanakijiji kwani lengo la Ukumbi huu ni kuzungumzia kero za wananchi..
Hivyo mnataka kweli watu hawa waachane kabisa na vita hii?.je, FMES anaposema hapa hapendwi mtu ni majigambo?.. au Mwanakijiji anapoidai Hoja kujibiwa kwa hoja ni kujigamba au kujihami! sidhani.. haya Je, Mwakyembe akiacha kupambana na Mafisadi kazi alopewa na kamati maalum ya rais, kamati ya bunge ktk madini..nguvu ya Kyela itatoka wapi!.. somehow hii ndio silaha yake iwe leo au kesho Kyela inajulikana kutokana na uwakilishi wake na nina hakika kuilinda Kyele inahitaji mtu kaa Mwakyembe..Who knows, mwaka 2015 anaweza kuwa Rais!..Mwakyembe ni binadamu mwenye malengo na sidhani kama anatazama nje ya Kyela sasa hivi kama mbunge.

Ebu fikiria Mwakyembe ajiunge na Mafisadi ati kwa sababu upinzani wake una wa cost wana Kyela..unadhani watafanya kipi tofauti zaidi ya kuhakikisha Mwakyembe ana account visiwa vya virgin, still wana Kyela watabakia na matatizo yao..watazame kina Sophia, Malima na wengine wamefanya kipi cha maana wilayani mwao! nothing.. hakuna mbunge hata mmoja aliye pamoja na Mafisadi anafanya makubwa wilayani mwake hakuna.. and that is the fact. Ni muhimu sana kwa wana Kyela kuitazama the all picture badala ya kulaumu mtu ambaye hana nguvu wala ubavu wa kuleta maendeleo...

Mkuu wangu hadi leo hii tunazungumza umeme nchini upo ktk asilimia 15 tu wakati tuna majimbo zaidi ya mia..maji safi pengine chini ya asilimia hiyo, barabara mbovu tanzania nzima labda juhudi ndogo iliyofanywa ni ktk majengo ya shule na zahanati kitu ambacho hata Kyela kinafanyika kama wilaya nyinginezo.

Haya maswala ya kuwagawa watu yametoka wapi na kwa nini wasizungumzie upinzani unatokana na kitu gani!.. Ilani, sera na malengo ya chama ni yale yale... Je, Mwakyembe anakiuka maswala hayo au anawakanya wale walijaribu kupindisha. Watu hamuwezi kugawanyika ikiwa kuna mwongozo na siku zote watu hutokubaliana kwa sababu hakuna mwongozo mmoja unaokubalika. Kama ilivyo ktk dini, madhehebu hutokana na kutokukubaliana na baadhi ya ibara za mwongozo..ndipo unakuta makundi ya watu wakigawanyika lakini kinachotokea Kyela ni makundi ya ushabiki wa Yanga na Simba wakicheza mpira mmoja..

Swala la Mwakyembe kulinga na usomi wake sii jambo la ajabu.. ni hulka ya ndugu zetu wengi sana tena basi mimi nakutana nao sana tu. Unajua tena jamaa zangu wa Ziwa magharibi, wao maneno mawili majigambo lazima yafuate, lakini kama mtu anaweza ku perform, anaweza kuleta mafanikio kwangu basi huyu ndio mtu. Hiyo lugha, majigambo na hata uungwana wa mbunge hayawezi kuniletea wala kuniondelea mkate mezani...
 
Bob,

Tuko ukurasa mmoja kabisa.....na ukikumbuka huko mwanzoni nilionya kuwa watu wanawa-underestimate mafisadi......mtandao wa mafisadi ni mkubwa....kati ya watu wanaompinga Dr. Mwakyembe...I may say only 5% ndio wako genuine..........wengine ni vibaraka wa mafisadi.........kwani jamaa ni tishio kwao kwa saana tu........

Na ndio maana nikasema hapo juu its very unfortunate.........jamaa anapigana na mafisadi ambao wamemuingilia hadi nyumbani kwake........hata sasa anashindwa ni nani wa kumuamini........na ndio maana nikasisitiza......na kushauri kuwa ajitahidi kutimiza waliyomtuma wana Kyela.....kwani hayo ndiyo atakayokuwa accountable for at the end of the day......na sisi wa pembeni tutafurahi kumuona mpiganaji wetu kurudi uwanjani tena hiyo 2010.........
 
Ogah,
Mkuu nakukubali.. ila vita hii sidhani kama anaiweza kwani alobakia nao ni walalahoi kama ya Mtikila. Hawezi kushinda kabisa na pengine kinachomweka hai na kupata usingizi ni JK mwenyewe..
Kitu kimoja ambacho nitarudia kusema, JK pia ana matatizo yake lakini To say the truth, hata kama ningekuwa mimi nisingeweza kuwatema zaidi ya 70% ya viongozi wa chama ambao leo wanajulikana kama Mafisadi, watu ambao wamemweka madarakani.. Hili ni pigo kwa chama na utawala.. utaangamiza kabisa chama na lawama zake hutasameheka kabisa. Kwa ujumla hivyo nachoweza kufanya ni kuwaondoa tu ktk Uongozi wa serikali..

Ebu fikiria Kikwete awasimamishe baraza zima la kwanza la Mawaziri kizimbani ikiwa ni pamoja na kina Mkapa na wengineo (Mafisadi) kweli huyu mtu atapona nchi hii?..Sidhani, sidhani kwa sababu hata yeye mwenyewe alikuwa kundi hilo na kama umeona leo hii Mramba na Yona wamevua mashati na sio kwa sababu hatuna ushahidi isipokuwa kila mashtaka yamemhusisha Mkapa..Na haiwezekani kabisa kumsimamisha bingwa huyo akiwa shahidi wala mshitakiwa kwani wengi watahusika ikiwa ni pamoja na uongozi uliopo..Kilichofuata ni kuondoa mashtaka.. Imetoka hiyo!..

Hivyo nadhani ushauri uliompa Dr. Mwakyembe ndio pekee unaoweza kumweka hai Kyela pamoja na kwamba sii kazi ndogo hata kidogo..Wana Kyela watakuja yaona matunda ya juhudi zake baadaye sii leo wakati nchi inaliwa mbele na nyuma..(samahani)..Wasitegemee mbunge atakuja kubadilisha Kyela ikiwa nchi nzima tunagawana umaskini..
 
Mkandara,
Omba hotuba hata moja ya mbunge wa Kyela wakati anagombea hilo jimbo, utaelewa ukweli mzima.

Pia si ulimwona kwenye ile press conference ya Dar akilaani vyombo vya RA kumchafua? Soma gazeti la majira ya jana utaona anavyomchafua huyo kijana aliyeko UK bila hata tone moja la ukweli?

Ninabaki kujiuliza kweli hizi ndio siasa za Tanzania zitakazotuletea maendeleo? Huwezi kulalamika unachafuliwa huku na wewe unaenda kuchafua watu hivyo hivyo.

Akitaka kufanikiwa asikilize ushauri wa Ogah hapo juu, yeye atimize aliyoahidi na pale anaposhindwa awaambie wananchi ukweli. Ukianza usanii, siku hizi wananchi sio mabwege tena watakugundua tu.

Mwakyembe si ni huyo huyo aliyepokewa kwa mbwembwe zote Kyela baada ya Richmond? Ukiona sasa wananchi wanaanza kuhoji baadhi ya maamuzi yake jua kuna tatizo. Jawabu sio kuwatuhumu watu wengi bali kurekebisha mapungufu yake na kuongeza ufanisi.

Kwa taarifa kama kuna wilaya ambayo ni ngumu sana watu kushawishika kwa pesa basi Kyela ni moja wapo. Ukitaka kujua ni 2005, Mwakipesile alikuwa na fedha hasa na wajumbe wote walikuwa wa kwake. Dr. alikuwa hajulikani kabisa Kyela wala hakuwahi kufanya hata jambo moja la maana kule, lakini wasomi mbalimbali walipoungana kumtangaza, vijana walikaa nje ya ukumbi mpaka na mapanga kwamba wajumbe huko ndani mkipitisha jina lingine lolote zaidi ya Dr hamtatoka humo ndani. Pamoja na manguvu ya polisi, lakini hawakufanikiwa. Kule Kyela wakiamua wako kama Mara tu, Jumbe anajua hilo maana yalishamtokea.

Nina uhakika kama kuna mtu atamwondoa Dr. basi tofauti zao zitakuwa juu ya mtazamo kwenye maendeleo na wala sio nani fisadi au nani kapewa pesa na mafisadi.
 
Mtanzania,

Mkuu nakubali sana maelezo yenu hasa upande wa ushauri lakini Mwakyembe he has to fight ikiwa wamemfuata kwake. What I tell my wife is non of your business hata kama tunakuzungumzia wewe. Wewe ukienda mwambia kitu mke wangu tena nyumbani kwangu, hapo unanitafuta ubaya na pengine kweli sii vizuri kushindana na mtu ambaye mkeo anaanza kumwamini..but still, I have to fight.

Swala la Rostam linajulikana na sii Mwakyembe aliyeanza isipokuwa ni kazi aliyotumwa na serikali kuifanya na akaiwakilisha kinyume cha matakwa ya Rostam na kundi lake... Mwakyembe hakuzuka tu kama mbunge na kuanza kumtafuta Rostam isipokuwa ukweli ndio umemuuma Rostam na akaanza kumtafuta kwa SMS.. Huyo kijana wa UK inasemekana kweli anatafuta kiti na pengine kweli anatumiwa maanake binafsi Mwakyembe has done nothing wrong..huyu kijana anatokea wapi ikiwa yeye anaishi UK maswala ya Kyela na hotuba za Mwakyembe zinamhusu nini?

Sasa unapotafuta Ubunge kwa kutumia mbinu za mafisadi ni lazima hata mimi nikufikirie vinginevyo. It's human nature.. na Kisiasa ndio kabisaaa. Ukiwa upande wa kushoto hata kama unazungumza ukweli nitakupiga vita kwa sababu imani yangu inatoka kulia na kila shambulizi lako nitaliona kama njama ya kutoka kushoto..

Ebu nambie mkuu wangu ni kitu gani ktk Hotuba hiyo kinachokufanya wewe au mtu mwingine amwone Mwakyembe kuwa hafai kuwakilisha wananchi wa Kyela. Maswala ya Rostam na mengineyo yote hayahusiani kabisa na uongozi wake Kyela lakini wamemfuata ktk kazi yake ya Ubunge nje kabisa ya kazi alizopewa katika kamati zote mbili ambazo ndizo chanzo cha kutoelewana..

Nachokiaona hapa ni ile ile tabia ya Kiafrika.. Warioba alipotoa ile report ya Mafisadi alikuja laumiwa yeye kwa kazi alizofanya akiwa Waziri mkuu! wapi na wapi ili mradi waondoe hoja inayohusiana na Ufisadi nchini. Wakamshusha hadi kumweka ktk kundi la Mafisadi ili mradi tu anyamaze lakini wasizungumzie yaliyomo ktk report ile kama ni kweli au laa.

Hii ndio tabia yetu, huwa tunatafuta mapungufu ya mtu kuyaweka kama ni makosa ili kufuta ile dhana ya ukweli uliopo. Hayakuanza jana toka Mtikila, Mrema, Mwakyembe, Mama Kilango, Zitto, Dr. Slaa.. U name it.. wote hawa wamepitia matatizo mengi nje kabisa ya issue iliyopo ubaoni..Kisha basi wale waliokaa kimya ndio wanapeta hivyo tunapoona wabunge wakikaa kimya bungeni na kuuchapa usingizi tunaanza tena kulaumu...Hivi tunataka mtu afanye kipi ili Wadanganyika mridhike kuwa huyu ni mchapa kazi na anajali maslahi ya Taifa!
 
Sikonge,

Mbongo huyo huyo wa UK sasa wanapita makanisani kupandikiza chuki kwamba misaada anayosaidia, kapewa pesa na Lowassa, ndio siasa zetu za Tanzania, ni mufilisi. Jamaa mwenyewe anasaidia kwao kila mwaka kuanzia miaka ya 90, basi huyo Lowassa keshamjaza jamaa mapesa mengi kweli kweli.

Jamaa mwenyewe huko aliko anacheka tu. Boksi linachosha bwana, wacha jamaa akunje pesa za EPA naye atanue kidogo kwi kwi kwi!!!

Vijana mnaotaka kwenda huko mwakani jiandaeni kweli kweli kwa vita.

Ila uzuri wa dunia hii ukipandikiza chuki utavuna chuki, ukipandikiza neema unavuna neema. Watanzania sio mabwege tena!

Bro Mtanzania

Nimefuatilia sana post zako na kwa kweli pamoja na ujuzi wako wa kuandika na kuficha msimamo wako lakini ni dhahiri kabisa unaonekana uko kinyume na Dr na umekuwa ukijitahidi kulionesha hilo. Sasa hakuna binadamu asiye na kasoro ila Dr amejitahidi sana pengine kuliko wabunge engi sana waliopita.

Roho inauma sana pale watu wachache wanapoamua kujitoa mhanga kwa ajiri ya nchi na shukrani yao inakuwa ni kuwatafutia weakness ndogo ndogo kama hizo. Ndiyo maana laana hii inatuandama sana. Binafsi nachukia sana watu wanaotaka kuwa moderate hasa katika khali ya sasa ya nchi ilivyo. kwangu ni muhimu mtu akawa kambi ya mafisadi au wachukia mafisadi. katikati na kusubiri upepo unaenda wapi naona ni hatari sana.
 
Bro Mtanzania

Nimefuatilia sana post zako na kwa kweli pamoja na ujuzi wako wa kuandika na kuficha msimamo wako lakini ni dhahiri kabisa unaonekana uko kinyume na Dr na umekuwa ukijitahidi kulionesha hilo. Sasa hakuna binadamu asiye na kasoro ila Dr amejitahidi sana pengine kuliko wabunge engi sana waliopita.

Roho inauma sana pale watu wachache wanapoamua kujitoa mhanga kwa ajiri ya nchi na shukrani yao inakuwa ni kuwatafutia weakness ndogo ndogo kama hizo. Ndiyo maana laana hii inatuandama sana. Binafsi nachukia sana watu wanaotaka kuwa moderate hasa katika khali ya sasa ya nchi ilivyo. kwangu ni muhimu mtu akawa kambi ya mafisadi au wachukia mafisadi. katikati na kusubiri upepo unaenda wapi naona ni hatari sana.

Mkuu Shalom.
Kajitahidi kafanya nini?.Kawafanyia nini wanachi waliomchagua?
Kuandikwa na magazeti ya mengi ndiyo kujitahidi?.

Ameshindwa kuunganisha nguvu ya wanachi na kufanya kazi nao pamoja.
Ofisi yake muda wote imefungwa na yeye yuko dar kula kuku.
 
Bro Mtanzania

Nimefuatilia sana post zako na kwa kweli pamoja na ujuzi wako wa kuandika na kuficha msimamo wako lakini ni dhahiri kabisa unaonekana uko kinyume na Dr na umekuwa ukijitahidi kulionesha hilo. Sasa hakuna binadamu asiye na kasoro ila Dr amejitahidi sana pengine kuliko wabunge engi sana waliopita.

Roho inauma sana pale watu wachache wanapoamua kujitoa mhanga kwa ajiri ya nchi na shukrani yao inakuwa ni kuwatafutia weakness ndogo ndogo kama hizo. Ndiyo maana laana hii inatuandama sana. Binafsi nachukia sana watu wanaotaka kuwa moderate hasa katika khali ya sasa ya nchi ilivyo. kwangu ni muhimu mtu akawa kambi ya mafisadi au wachukia mafisadi. katikati na kusubiri upepo unaenda wapi naona ni hatari sana.

Shalom,

Mhhh, naona unachanganya Yesu na Wayahudi? Hapo tu ni mwanzo wa mchanyato mzuri sana. Haya, Shaloom!!

Labda niseme kwa ufupi tu kuwa, ndugu yangu, wee ndiyo Mpenzi wa Dr. na roho inakuuma kwa sababu ya mapenzi yako. Ukipenda, chongo utasema Kengeza. Ila hayo ndiyo mapenzi na una haki ya mapenzi hayo.

Mwakyembe hadi leo hii bado anavuna alichokipanda. Huu ugawaji wa watu tulianza kuusema hapa zamani sana. Ukianzia mwanzo wa hii makala hata mie nilikuwa upande wake sana. Nilipokuja kupewa habari za dharau zake na kugawa watu sikuamini. Leo kikao cha CCM kimemsema waziwazi na hata mwenyewe kakubali hilo. Alikuwepo hapa kwa jina la Lazarus Mtindi (soma makala zake huko nyuma), uone alivyokuwa akiandika na hapo ndipo uje tuanze maongezi. Kwa sasa unakuwa kama vile unadandia train la Kifaransa (TGV) kwa mbele.

Labda tu nikukatishe tamaa. Mafiadi wana karata fulani wameshika against Mwakyembe. Mie hadi leo nimeshasikia mbili. Hizi kwa uhakika wanasubiri mwakani ndiyo wazitumie. Karata hizo siyo nzuri kwa Dr. Kwa hiyo kama unafikiri sisi hapa hatumpendi Mwakyembe, basi unakosea sana. Tumejitahidi sana kumpa mawazo ili ajijengee ngome nzito na hapo mwakani hata wakimshambulia, basi wapunguze tu ngome yake ila wasimmalize. Yatakayomuuwa Mwakyembe ni mawili tu na haya ni hata kabla MAFISADI hawajaanza kumshushia kipigo:-

1. Siasa za AU UKO NA MIMI, AU WEWE NI ADUI YANGU.
(Kugawa watu wa Kyela).

2. Dharau kwa watu wa kawaida, kwani yeye ni msomi (dr wa sheria!!).

Kama aliweza kuwakusanya watu kabla ya uchaguzi, kitu gani kimefanya leo hii watu hao waanze kumpinga? Mtu gani anapeleka hadi kuligawa kanisa langu la Moravian? Jamani!!!! Unagawa watu hadi kwa YESU!!
 
Shalom,

Mhhh, naona unachanganya Yesu na Wayahudi? Hapo tu ni mwanzo wa mchanyato mzuri sana. Haya, Shaloom!!

Labda niseme kwa ufupi tu kuwa, ndugu yangu, wee ndiyo Mpenzi wa Dr. na roho inakuuma kwa sababu ya mapenzi yako. Ukipenda, chongo utasema Kengeza. Ila hayo ndiyo mapenzi na una haki ya mapenzi hayo.

Mwakyembe hadi leo hii bado anavuna alichokipanda. Huu ugawaji wa watu tulianza kuusema hapa zamani sana. Ukianzia mwanzo wa hii makala hata mie nilikuwa upande wake sana. Nilipokuja kupewa habari za dharau zake na kugawa watu sikuamini. Leo kikao cha CCM kimemsema waziwazi na hata mwenyewe kakubali hilo. Alikuwepo hapa kwa jina la Lazarus Mtindi (soma makala zake huko nyuma), uone alivyokuwa akiandika na hapo ndipo uje tuanze maongezi. Kwa sasa unakuwa kama vile unadandia train la Kifaransa (TGV) kwa mbele.

Labda tu nikukatishe tamaa. Mafiadi wana karata fulani wameshika against Mwakyembe. Mie hadi leo nimeshasikia mbili. Hizi kwa uhakika wanasubiri mwakani ndiyo wazitumie. Karata hizo siyo nzuri kwa Dr. Kwa hiyo kama unafikiri sisi hapa hatumpendi Mwakyembe, basi unakosea sana. Tumejitahidi sana kumpa mawazo ili ajijengee ngome nzito na hapo mwakani hata wakimshambulia, basi wapunguze tu ngome yake ila wasimmalize. Yatakayomuuwa Mwakyembe ni mawili tu na haya ni hata kabla MAFISADI hawajaanza kumshushia kipigo:-

1. Siasa za AU UKO NA MIMI, AU WEWE NI ADUI YANGU.
(Kugawa watu wa Kyela).

2. Dharau kwa watu wa kawaida, kwani yeye ni msomi (dr wa sheria!!).

Kama aliweza kuwakusanya watu kabla ya uchaguzi, kitu gani kimefanya leo hii watu hao waanze kumpinga? Mtu gani anapeleka hadi kuligawa kanisa langu la Moravian? Jamani!!!! Unagawa watu hadi kwa YESU!!

Sikonge

Karata mbili za mafisadi zitakazo weza kumjeruhi Dr ni

1. Kumtoa roho yake
2. Kuhakikisha wanaipeleka ahera kabisa maana wakiitoa na akaenda peponi itakuwa ni ushindi mkubwa sana kwake.

DR ana fall back position siyo kama wabunge wetu wengi ambao wanahemea hapo. yeye anaweza kupata kazi sehemu yeyote hapa duniani na kuwa na maisha mazuri zaidi ya haya ya kujibishana na wapiga kura wasioelewa kitu. kwa hiyo kutoa ubunge kwa DR sio kumharibia DR bali sisi watu wa kyela. Nomba ufahamu hilo

Yes inawezekana watu mnamwona ana dharau lakini sisi tunataka maendeleo magoti kama yale ya mgombea wa busanda yatatusaidia nini?. au Huyu anaye hudhuria kila misiba na kila shughuli yamelisaidia nini taifa? Kama anadharau watakao ziona ni wale wanaomfuata mfuata.

Siasa za uko na mimi au na adui zangu zina tatizo gani wewe unapenda wanafiki? hata mimi huo ndiyo msimamo wangu sitaki watu walio vuguvugu kwenye issue yoyote na wanyakyusa nadhani wengi ndiyo wako hivyo. Ndiyo maana hata nyerere alikuwa hatupendi kwa msimamo huo.

halafu mimi nikate tamaa mara ngapi sasa, mafisadi kama wana issue wangetumia sasa kwani mwakani ni too late kabisa na skendo zenyewe eti ana kiwanda cha kufua umeme wa upepo au alimtongoza fulani sasa hayo si ndiyo maisha ya watanzania 80% . we endelea kuwaendekeza mafisadi na kuwapa moyo kwamba wana karata mbili. Ungekuwa unampenda kwa sababu umesema unazijua ungezimwaga hapa nasi tutamfikishia lakini hauna mapenzi naye yoyote zaid ya kumchukia si jui kwa lipi eti ana dharau! nikuorodheshee list ya enye dharau hapa na hujawahi kusema hata siku moja ila aliye wataja mafisadi ndiyo anadharau

Mhhh, naona unachanganya Yesu na Wayahudi? Hapo tu ni mwanzo wa mchanyato mzuri sana. Haya, Shaloom- unamaana Dr ni myahudi na yesu ni mwakipesile? kuwa straight ndugu
 
Mkuu Shalom.
Kajitahidi kafanya nini?.Kawafanyia nini wanachi waliomchagua?
Kuandikwa na magazeti ya mengi ndiyo kujitahidi?.

Ameshindwa kuunganisha nguvu ya wanachi na kufanya kazi nao pamoja.
Ofisi yake muda wote imefungwa na yeye yuko dar kula kuku.

Si kweli samweli. Jamaa yuko kyela muda mwingi kuliko Dar naweza kuja na data kwa mwaka jana. Hilo umeshachemsha!

Hebu wakati anachukua jimbo kulikuwa na shule ngapi na sasa kuna shule ngapi!

hebu nitajie mbuge yupi aliyewekewa mkuu wa mkoa kumcheck kuhakikisha kuwa hafanyi jambo lolote la maana ili asije akawa popular nitajie mmoja tu ukiacha magufuri ambaye anahamishwa kila wizara ili kazi yake isipimike

Kuku lazima ale kwa kuwa ni msomi na anafanya kazi vizuri na ajaanza kula kuku sasa ni kabla hajawa mbunge na hata akiacha ubunge anaweza kwenda hapo kenya na kupata kazi ya $10,000 kwa mwezi kilahisi sana. Kwa hiyo juhudi zake ndiyo zinazomfanya ale kuku

Sisi wanyaki tunajulikana sana kwa wivu lakini ni lazima tujue kwamba tunahitaji kuendeleza kale kaeneo kenye mafuriko na mbu kibao ili kawe kanakalika kidogona siyo kutumiwa tu kwa wivu wetu
 
Sikonge

Karata mbili za mafisadi zitakazo weza kumjeruhi Dr ni

1. Kumtoa roho yake
2. Kuhakikisha wanaipeleka ahera kabisa maana wakiitoa na akaenda peponi itakuwa ni ushindi mkubwa sana kwake.

DR ana fall back position siyo kama wabunge wetu wengi ambao wanahemea hapo. yeye anaweza kupata kazi sehemu yeyote hapa duniani na kuwa na maisha mazuri zaidi ya haya ya kujibishana na wapiga kura wasioelewa kitu. kwa hiyo kutoa ubunge kwa DR sio kumharibia DR bali sisi watu wa kyela. Nomba ufahamu hilo

Yes inawezekana watu mnamwona ana dharau lakini sisi tunataka maendeleo magoti kama yale ya mgombea wa busanda yatatusaidia nini?. au Huyu anaye hudhuria kila misiba na kila shughuli yamelisaidia nini taifa? Kama anadharau watakao ziona ni wale wanaomfuata mfuata.

Siasa za uko na mimi au na adui zangu zina tatizo gani wewe unapenda wanafiki? hata mimi huo ndiyo msimamo wangu sitaki watu walio vuguvugu kwenye issue yoyote na wanyakyusa nadhani wengi ndiyo wako hivyo. Ndiyo maana hata nyerere alikuwa hatupendi kwa msimamo huo.

halafu mimi nikate tamaa mara ngapi sasa, mafisadi kama wana issue wangetumia sasa kwani mwakani ni too late kabisa na skendo zenyewe eti ana kiwanda cha kufua umeme wa upepo au alimtongoza fulani sasa hayo si ndiyo maisha ya watanzania 80% . we endelea kuwaendekeza mafisadi na kuwapa moyo kwamba wana karata mbili. Ungekuwa unampenda kwa sababu umesema unazijua ungezimwaga hapa nasi tutamfikishia lakini hauna mapenzi naye yoyote zaid ya kumchukia si jui kwa lipi eti ana dharau! nikuorodheshee list ya enye dharau hapa na hujawahi kusema hata siku moja ila aliye wataja mafisadi ndiyo anadharau

Mhhh, naona unachanganya Yesu na Wayahudi? Hapo tu ni mwanzo wa mchanyato mzuri sana. Haya, Shaloom- unamaana Dr ni myahudi na yesu ni mwakipesile? kuwa straight ndugu

Mkuu Shalom.

Naona sasa unaanza kuishiwa.
Kama ana kazi nyingine ya kufanya,basi mshauri aende huko na sio kuwagawa watu.

Wakati wenzetu wanafikiria kuungana,leo hii wewe unashabikia mtu anayegawa watu.

Walichokosea wana kyela ni kumchagua mtu ambaye walikuwa hawamjui.Sio siri ndugu yangu Shalon, wote tulimpenda sana huyu DK.Lakini upendo wetu kwake kumbe ni kazi bure.

Sisi wana kyela tumeamua kwa nia moja.Kwamba yeyote atayekuja .Swali la kwanza ni kumuuliza.Umetufanyia nini na sio utatufanyia nini.

Hayo ya utatuifanyia nini ndiyo yaliyotufikisha hapa tulipo sana.Kwamba mke na mume hawapatani kutokana na Mwakyembe kukamilisha lengo lake la kutugawa.

Labda hana uchungu na wilaya yetu kutokana na kwamba yeye ni mzaliwa wa Tukuyu.Kule tukuyu wako mbele sana na sasa yeye kazi yake ni kukaa Dar wakati huko kwao Mwandosya na Mwakyusa wakifanya kweli.

Shalom,Mshauri dk akatafute kazi nyingine ,ili aishi maisha bora kuliko huo ubunge wa kugawa watu.

Amen
 
Sikonge

Karata mbili za mafisadi zitakazo weza kumjeruhi Dr ni

1. Kumtoa roho yake
2. Kuhakikisha wanaipeleka ahera kabisa maana wakiitoa na akaenda peponi itakuwa ni ushindi mkubwa sana kwake.

we endelea kuwaendekeza mafisadi na kuwapa moyo kwamba wana karata mbili. Ungekuwa unampenda kwa sababu umesema unazijua ungezimwaga hapa nasi tutamfikishia lakini hauna mapenzi naye yoyote zaid ya kumchukia si jui kwa lipi eti ana dharau! nikuorodheshee list ya enye dharau hapa na hujawahi kusema hata siku moja ila aliye wataja mafisadi ndiyo anadharau

Mhhh, naona unachanganya Yesu na Wayahudi? Hapo tu ni mwanzo wa mchanyato mzuri sana. Haya, Shaloom- unamaana Dr ni myahudi na yesu ni mwakipesile? kuwa straight ndugu

Shalom,
Mbona unakuwa kituko? Nilianza kukupa heshima na kufikiri ni mtu unayetaka hapa tuelimishane, kumbe wee somehow unaboil! Too sad.

Karata mbili ninazozifahamu mie, mbona waziuliza wakati mwenyewe umeziandika hapo juu? Si zi-copy hizo karata mbili na umpelekee Mwakyembe? Atakusifu sana kijana kuwa "wee kijana una akili sana" na milele hata kuja kusahau BUSARA zako na werevu wako ukiachilia mbali ujasiri wa kumpelekea KARATA za maana namna ile.

Mwakyembe huwa anakuja hapa na tulimwambia yeye INDIRECT/DIRECT. Tulijifanya hatujamfahamu ila kumbe tulishamgundua. Hata sasa hivi niko njiani kum-trace na hivi kipunde ntamgundua tena yuko kwa jina gani. Huwa akija anajifanya kukosea kila kitu na akibanwa hukiri tuliyokuwa tunasema. Tatizo yeye anafikiri yeye kwa sababu ni Dr. basi wengine wote ni mabwege. Inawezekana siye si Ma.dr. wa sheria ila kitendo cha yeye kuambiwa na Chriss kuwa "na kuwa mwana sheria unashindwa kuongoza kikao kwa kufuata sheria......" huo ni mzinga wa soo.

Kama tukiacha utani, karata hizo, moja alishaiandika humu ndani Field Marshal ES. Sintataka kukuambia iko wapi na ukitaka waweza kumuuliza. Nyingine ilijianika hata bila ya yeye kujua. Hii ilifumuka wakati wa mazishi ya Marehemu mama yake (RIP). Sasa kama yeye ana akili na ni Dr. wa sheria, mwambie hivyo tu na atajua ni kitu gani hicho alichojianika. Kama waliokuja kwenye Mazishi wakiwa ni ndugu, jamaa na marafiki hadi leo hawajamwambia, basi kweli hana ndugu, jamaa na marafiki wa kweli au ni kuwa dharau zake hata hao watu wake wa karibu wanaamua wamuache azame katika tope hizo chafu.

Muda wa MAFISADI bado sana. Nina imani watamfumua mwezi mmoja kabla ya uchaguzi na hapo hatapata hata muda wa kuamka tena. Kama unalaani sisi hatumuambii moja kwa moja, basi rudi nyuma na usome jumbe zetu. Tulimuonya zamani sana. Huwezi tenga watu hata kama ni Wanafiki. Wee kama Mwanasiasa, lazima ujuwe kuwa KINYONGA. Kama hujui basi utawezaje kuongoza watu wanaokupinga na wasiokupinga? Angelimaliza ugomvi na Mwakipesile (alikuwa na uwezo huo - Mfano wa Obama na Clinton), akawavuta wapinzani wake wote na kuwa nao chini, sasa hivi wala tusingelikuwa tunaongelea hili. Mbona Dr. Slaa kwake kimya?

Shalom, Mwakyembe siyo siri ana uwezo MKUBWA SANA SANA wa kufanya mambo makubwa na hata tuseme MAAJABU. Kinachomuuwa hi hizo sababu mbili nilisema mwanzo za Au uko na mimi au uko against me/Dharau. Angejirekebisha hayo makosa mawili, basi angelibaki na ugomvi na MAFISADI tu na sisi wote humu ndani tungelikuwa upande wake.

Mwisho usitutishe kuwa ANAWEZA KWENDA KUFANYA KAZI NYINGINE. Si aende akafanye hata leo hii, njia NYEUPE. Tuliimba/tuliimbiwa kuwa bila Nyerere, Tanzania ingelikuwaje, mbona ipo? Tanzania itakuwepo/Kyela itakuwepo bila ya kujali Mwakyembe yupo au hayupo. Mchimba shimo, kajiingiza mwenyewe na dharau zake.

Haya chukua ring la baiskeli, endesha mbio kwa Mwakyembe kamwambie yote uliyoyasikia hapa. Na kama wee ndiyo Mwakyembe mwenyewe, basi ujumbe umefika. Kama ni ndugu basi Msimlemaze ndugu yenu, mpeni shure kwani ukweli unauma ila kesho atakuja kusema ASANTE.
 
Mhhh, naona unachanganya Yesu na Wayahudi? Hapo tu ni mwanzo wa mchanyato mzuri sana. Haya, Shaloom- unamaana Dr ni myahudi na yesu ni mwakipesile? kuwa straight ndugu

Wee Mtu vipi? Unachukua neno hata hujui maana yake? Shalom ni Salamu ya WAYAHUDI. Wayahudi ni WAPINZANI wakubwa sana wa Yesu. Sasa unaposema I Love Jesus na pembeni SHALOM, si Mchanyato huo? Hili halikuwa na umuhimu wowote hata hivyo. Lilinifurahisha tu na halina UHUSIANO wowote na hii mada na ningeliweza kuliandika katika jumbe zako zozote zile.

Mwakipesile awe YESU? Mwakyembe awe MYAHUDI? PULIZII!!!!!!
 
Mkuu Shalom.

Naona sasa unaanza kuishiwa.
Kama ana kazi nyingine ya kufanya,basi mshauri aende huko na sio kuwagawa watu.

Wakati wenzetu wanafikiria kuungana,leo hii wewe unashabikia mtu anayegawa watu.

Walichokosea wana kyela ni kumchagua mtu ambaye walikuwa hawamjui.Sio siri ndugu yangu Shalon, wote tulimpenda sana huyu DK.Lakini upendo wetu kwake kumbe ni kazi bure.

Sisi wana kyela tumeamua kwa nia moja.Kwamba yeyote atayekuja .Swali la kwanza ni kumuuliza.Umetufanyia nini na sio utatufanyia nini.

Hayo ya utatuifanyia nini ndiyo yaliyotufikisha hapa tulipo sana.Kwamba mke na mume hawapatani kutokana na Mwakyembe kukamilisha lengo lake la kutugawa.

Labda hana uchungu na wilaya yetu kutokana na kwamba yeye ni mzaliwa wa Tukuyu.Kule tukuyu wako mbele sana na sasa yeye kazi yake ni kukaa Dar wakati huko kwao Mwandosya na Mwakyusa wakifanya kweli.

Shalom,Mshauri dk akatafute kazi nyingine ,ili aishi maisha bora kuliko huo ubunge wa kugawa watu.

Amen

Samweli,

Wasomaji watajua nani ameishiwa hapa mchana kweupe kabisa!

Mwandosya anafanikiwa kule Tukuyu kwa sababu wenzetu wa Tukuyu ni wataarabu na wana msimamo na wanapenda kazi. Sasa kyela kila mtu ni brother men na hawataki kufanya kazi na unakuja kumlaumu Dr Shame on you

Mwandosya ni mbunge wa miaka karibu kumi na tatu sasa. Dr ana miaka mitatu tu ukitaka kumpima na Mwandosya ina bidi uchukue na miaka kumi ya mzembe wetu mwakipesile ambaye amefanya zero kabisa na anaua kabisa mkoa wetu wa mbeya. Nilikuwa na plani ya kurudi mbeya kuinua mkoa wetu sasa siend siwezi kukubali kuona naongozwa na kiongozi wa type ile. Najiendea nje sasa

Ukitaka kumpima Dr inabidi umpine na Mwakipesile hapa ndipo utakapoona amefanya nini. Kama amekugawa wewe na mke wako basi mkeo ujue ana akili sasa ulitaka akufuate wewe na mwakipesile mnaoendekeza mafisadi

Halafu huoni aibu kusema kuwa amezaliwa Tukuyu sasa sisi tuliozliwa Ocean Road ni wazalamu, kuna kosa gani kwa baba zetu kusoma na kufanya kazi na sisi kuzaliwa huko walikokuwa wanafanya kazi kuna kosa gani. kama wewe mwenzetu unaona ni bahati kwa baba yako kutokupata nafasi ya kufanya kazi na ukazaliwa ikolo basi ndiyo mzawa halisi wa kyela -poteza muda jamaa ni damu ya chifu mwakyembe awe amezaliwa ileje au tukuyu au chunya.

Eti ametugawa huoni kuwa hayo ni matusi kwa watu wa kyela wewe unafikiri watu kugawiwa na mtu huwa ni sifa? watu huwa wanajigawa kutokana na interest fulani lakini watu wanaogawiwa ni wajinga yaani wanakubali mtu mmoja awaambie wewe huku na wewe huku.

Kwa taarifa yako ukitoa nguvu za mtandao hao watu wenu ni weupe sana. mtu anayetumia nguvu ya mtu mwingine kuwa na jeuri na asije akasimama mbele za watu kujisifu wala kutoa hoja wala kuchambua mwingine. nyie subirini tu mwakyembe atoke nyie wakina mwakipesile muungie labda safari hii mtakuwa mmejifunza kitu fulani.
 
Wee Mtu vipi? Unachukua neno hata hujui maana yake? Shalom ni Salamu ya WAYAHUDI. Wayahudi ni WAPINZANI wakubwa sana wa Yesu. Sasa unaposema I Love Jesus na pembeni SHALOM, si Mchanyato huo? Hili halikuwa na umuhimu wowote hata hivyo. Lilinifurahisha tu na halina UHUSIANO wowote na hii mada na ningeliweza kuliandika katika jumbe zako zozote zile.

Mwakipesile awe YESU? Mwakyembe awe MYAHUDI? PULIZII!!!!!!

Du wewe ndiyo umechemka kweli shalom maanayake ni hiyo apo chini

The Hebrew word SHALOM is understood around the world to mean peace. But peace is only one small part of the meaning of the word SHALOM. Here in Israel, even though we don't have much in the way of peace, we use the word SHALOM on a daily basis. We use it to greet people with, and we use it to bid farewell to people. However, SHALOM means much more than peace, hello or goodbye.
Strong's Concordance 7965 - Hebrew Shalom..... A word study in the New King James Version for SHALOM says: Completeness, wholeness, health, peace, welfare, safety soundness, tranquillity, prosperity, perfect ness, fullness, rest, harmony, the absence of agitation or discord.
Hata hivyo Yesu nampenda na wayahudi nawapenda kwani ni taifa teule la Mungu sasa hiyo ni weather unataka au unapenda.

Wayahudi walifanya vile kutimiza neno ile mimi na wewe tupate kukombolewa sasa nbaada ya kuwashukuru unaanza kuwawekea hila. Kumbuka nitambariki atakayewabariki na nitamlaani takaye walaani -ogopa sana. Mfano mzuri ni nchi yako TZ baada ya kuwafukuza wwayahudi laana tupu, kenya ufisadi wa kutisha lakini nchi iko juu tanzania hatuwafikii kwa ufisadi ila tuko choka mbaya sana 1978 tulijipeleka kwenye laana wenyewe -IMEANDIKWA
 
Last edited:
Na Israel Mwaisaka,Mbeya

HALMASHAURI kuu ya CCM ya wilaya Kyela imemtuhumu mbunge wao Dkt,Harrison Mwakyembe pamoja na mwenyekiti wa CCM wilaya Bw,Japhet Mwakasumi kuwa ndiyo vinara wa kukigawa chama hicho katika makundi na kusababisha viongozi kushindwa kuelewana miongoni mwao iliyopelekea hivi karibuni makatibu kata kuwapiga viongozi wa wilaya

Katika kikao hicho wengi ya wajumbe walimshushia makomboraDkt,Mwakyembe kuwa toka yeye awe mbunge wa jimbo hilo ametengeneza makundi ndani ya chama huku akidaiwa kummiliki mwenyekiti wake wa chama wa wilaya ambaye ameonekana kuyumbishwa katika maamuzi yake mbalimbali

Shalom,
Hebu acha hizo. Unajifanya hukusoma huu ujumbe ambao umeandikwa kwenye IPPMEDIA? Usiseme ni sisi tumemwambia Mwakyembe kuwa anagawa watu. Soma hapo juu. Na kibaya zaidi ni kuwa yeye ANAMMILIKI MWENYEKITI WAKE. Sijui ina maana gani, ila maana hiyo bila kujali ikoje, itakuwa si NZURI. Wee Mwakyembe UTAMMLIKI VIPI Binadamu mwenzio? Si ndiyo hizi tunasema DHARAU?? Kama huamini, please soma hapo juu.
 
Du wewe ndiyo umechemka kweli shalom maanayake ni hiyo apo chini

The Hebrew word SHALOM is understood around the world to mean peace. But peace is only one small part of the meaning of the word SHALOM. Here in Israel, even though we don't have much in the way of peace, we use the word SHALOM on a daily basis. We use it to greet people with, and we use it to bid farewell to people. However, SHALOM means much more than peace, hello or goodbye.
Strong's Concordance 7965 - Hebrew Shalom..... A word study in the New King James Version for SHALOM says: Completeness, wholeness, health, peace, welfare, safety soundness, tranquillity, prosperity, perfect ness, fullness, rest, harmony, the absence of agitation or discord.
Hata hivyo Yesu nampenda na wayahudi nawapenda kwani ni taifa teule la Mungu sasa hiyo ni weather unataka au unapenda

Yaani wewe mpaka utafute kwenye MTANDAO? Mie nilishawahi kukaa na WAYAHUDI wenyewe na ninafahamu maana yake bila ya kufungua kwenye Internet. Ndiyo maana nikakuambia kuwa Wanatuma Wayahudi. Sasa kwenda kuhangaika na kupoteza muda kote huko kulikuwa kwa nini? Pole sana MJOMBA. Mwisho nilikuambia hili wala si MUHIMU, lilinifurahisha tu kuona WAYAHUDI na YESU wamesimama sehemu moja.

Maadamu Unawapenda wote, si waambie wote WALETE MAHALI KWA MZEE?? Yes, sasa ndiyo nachemsha!!
 
Back
Top Bottom