ndiyo maana unampinga Dr naona umekaa kimwakipesile mwakipesile hivi!
ILa nakuhusia ndugu yangu Yesu hataniwi, afanyiwi mdhaa wa dhihaka ya aina yoyote. Usije sema sikukuonya ndugu yangu
Huyu Mwakipesile alikuwa kama viongozi wa Tabora. Watu wa Kyela wakaamua kumtosa na baada ya kusikiliza hotuba za Mwakyembe na mambo yake, wote wakaamini huyu atakuwa si tu kiongozi, ila mshikaji. Aliposhinda, watu wakamwambia, nenda kapatane na Mwakipesile. Siku hizo Mwaki alikuwa looser fulani hivi. Jamaa kwa kuwa kashashinda, akaanza kufungua makucha. Akatukana kabisa, kuwa yeye na looser ni mbalimbali. Siku kadhaa zinapita, jamaa kawa mkuu wa mkoa, KIKO WAPI? Angelikuwa kashapatana naye, saa hizi wangelikuwa washikaji.
Bado naamini Mwakyembe ana uwezo MKUBWA SANA. He can do better than that. Mie ni mshabiki sana wa Mwakyembe ila nisikufiche, nilipopewa hizi habari, nilitaka kulia. Sikuamini mtu niliyeanza kujenga imani kwake kubwa namna hiyo, anafanya vitu kama hivi.
Amini usiamini, ningelikuwa simpendi Mwakyembe, wala nisingelikuwa naandika hizi habari. Hawa wote sijawahi kuwaona hata siku moja live. Mie mtu wa Sikonge huku ila nina jamaa/ndugu zangu Kyela. Jamaa wakiwa Sikonge, wakiwa kwangu ni kuwa wako nyumbani. Najiandaa na mie kwenda Kyela maana undugu ni kutembeleana.
Sasa kijana, hujui wimbo wa "Yesu kwetu ni RAFIKI...?" Yesu ni rafiki yetu ila Mungu mhhhh KIGINGI. Hapo ndiyo siwezi hata kuweka utani. Ila Jesus ni wetu sana. Tunaweza hata kumtania. Kwani unafikiri wanafunzi wake walikuwa hawamtaninii? Si ajabu walikuwa wanamsakizia hata totoz. Ehhh Yesu, hebu cheki kitu hicho, kimejaza paja la nguvu kama la Mnyakyusa.
Viongozi gani mliwowachagua Tabora! mzee naona ujumbe wako nimzito au unafukuzia tenda
Mzee, viongozi wa Tabora, kwi kwiii kwiiiiiiii. Duu mzinga wa SOOO!!! Yaani ni Choo kirefu haswa haswa. Ukianzia na Seleli aliyemfunga Rage, ukija na Papa Aziz sijui Nyangumi Aziz? Weka na Saidi Nkumba.
Ngoja nikuambie juu ya Saidi Nkumba, mbunge wa Sikonge. In fact jamaa ni FISI sana. Bungeni siku zote husubiri wengine wauwe mnyama na yeye aje tu kuongeza "....Ni kweli jamani, hii haiwezi kuwa..." Sanasana yeye HUTAKA KUJUA....... Ila kali zaidi ngoja nikuambie. Nilipata habari kuwa hata akija pale Bungeni Dodoma na mchuma wake na kwa sababu ana nidhamu ya WOGA, jamaa huwa wa kwanza. Akifika pale basi parking ya magari huwa nyeupeee, hivyo badala ya kuweka gari lake mbele kabisa, basi FISI yule huenda MBAAALIII kabisa kama siyo mwishoni na kuweka mchuma wake kule. Kisa ni kwamba, HATAKI KUZIBA NAFASI ZA AKINA MWAKYEMBE. Hili jamaa lilikuwa linashinda kwa sababu tu baba yake alikuwa mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Tabora. Ila sasa hivi hayupo tena na nina imani mwakani KWISHIENI.
Duuu, mzee, eti Viongozi wa Tabora, hahaa haaaaaa hahaaa. Yaani umenifanya niwe na furaha badala ya majozi. Sijui nihamie tu Kyela? Ila tu sijui toto za Kyela zikoje. Wanyamwezi unajuwa tena, toto zenye rangi nyeupe nyeupe (kama Warangi vile/Wambulu) twalipa ng'ombe wengi.
Ngoja nicheke zaidi, eti viongozi wa Tabora, Haaa haaa!!!!!!!!