Mkuu, hoja zako mara nyingi ni nzuri sana, lakini linapokuja suala la Kyela unageuka kuwa extremely irrational. Kwa sisi tunaofika Kyela mara kwa mara kwa shughuli za kikazi, tunashindwa kuona lengo lako maana, utake usitake, Kyela imebadilika sana chini ya Dk. Mwakyembe. Ndo maana wengine wanakuelewa vingine kuwa lengo lako labda ni kugombea ubunge 2010! Lakini Mkuu, unaweza kuwa na azma hiyo bila kudisdtort ukweli! Muulize mwandishi wa habari yeyote wa Mbeya worth the title, atakueleza kuwa Kyela ina mabadiliko katika shule, miundombinu (barabara, madaraja na umeme) na hata mwamko wa wananchi. Nikisema mengi utaanza kusema nimehongwa! Ndo tulivyo!
Mkuu, hilo la michango ya Dar es Salaam nalijua, kwa vile mimi nilihudhuria vikao vyote! Kwanza, ziara hiyo ya DC, DED na Mwenyekiti wa Halmashauri ilifanyika wakati Mbunge yuko Dodoma, Bungeni! Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni! Juhudi za DC kupata pesa kutoka kwa wana-Kyela zilikwama kwa sababu tatu kuu: 1. Yeye ni mtumishi wa Serikali Kuu, akiishiwa fedha aende Serikalini si kwa wananchi! Sasa akipewa fedha na wananchi, akaila, wananchi watamwajibishaje? 2. Kwa nini alifanya ziara ya kukutana na wananchi wa Kyela bila Mbunge wao ambaye wanaweza kumwajibisha? 3. Kwa nini chombo ambacho wana-Kyela wengi (wanaojua kuchanga fedha na siyo kupiga domo tu), yaani KDF, hakiombwi kufanya kazi hiyo ya harambee?
DC alikosa majibu! Vilevile, ndani ya wana-Kyela, kulikuwepo na "wanusa mambo" ambao walijua kuwa DC huyo kastaafishwa, kilichokuwa kinasubiriwa ni kutangazwa tu! Hivyo, baadhi yetu tukaona zoezi hilo lisiendelee!
Mbunge alipoingia Dar siku mbili baadaye, akaombwa asaidie. Mwakyembe hakusita, akaingia kazini na kesho yake tukapata pledges za sh.20 milion/= kutoka Post Bank, NHC, TBA na NMB kutokana na influence yake. Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake tumpe!
Sasa hayo unayoyasema Mkuu ya "kutoelewana" hadi kumwita DED mwizi, yanatoka wapi? Wana-Kyela wengi walikuwa vilevile wanamwuliza DC, kwa nini mfunge safari ndefu ya wiki moja na kutumia zaidi ya sh. milioni 5 kwa posho na mafuta ya gari, wakati wangeweza kupiga simu tu KDF wachangiwe? Mkuu, tusimwonee Dk. kwa sababu tu hawezi kukujibu! Dk. Mwakyembe atakumbukwa: ameweza kutekeleza yale ambayo kayafanya katika mazingira magumu sana aliyowekewa na watawala kwa kumwacha Mwakipesile Mbeya kama RC! Mwakipesile anayo rekodi ya muda mrefu ya ukorofi na visasi visivyoisha. Akiwa Mbunge wa Kyela, Mwakipesile alikuwa hakai meza moja na DC, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mbunge aliyemtangulia (Kasyupa), na Mhandisi wa Wilaya! Ubabe wake unatokana na kazi yake ya mwanzo kabisa, UPOLISI! Mimi mwenyewe hapa, pamoja na uandishi wangu wa habari, alishanitamkia kunizaba vibao nikiendelea kumdodosa! Hiyo ndo NGUVU MPYA!
Mkuu, nimalizie kwa kusema kuwa yote niliyoyasema hapo juu unaweza kuyahakikisha kwa Mwenyekiti wa Halmashauri (0754 630946); Mkurugenzi wa Kyela (0754738468) na Mbunge wa Kyela (0754284130).