Habari Njema Kutoka Barrick Gold kwa Watanzania, Tunaanza Kufaidi Rasilimali Zetu, Donge Nono la Dola Milioni 100 zalipwa

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,513
113,643
Wanabodi,

Hatimaye Tanzania sasa tunaanza kufaidi rasilimali zetu za madini, ambapo leo, donge nono la dola za Marekani milioni 100, zimelipwa kwenye kile kibubu chetu pale kwenye ule mfuko Mkuu wa hazina ya serikali kama advance payment ya kile kishika Uchumba cha dola milioni 300, ambacho baadae tulikigeuza kuwa ndio mahari kamili ya yule binti yetu makinikia.

Kiasi kilichobaki cha dola milioni 200, kitalipwa kwa mikupuo mitano ya dola milioni 40 kila mkupuo ambacho kitalipwa ndani ya miaka 5, kwa kila mkupuo kulipwa ndani ya mwaka mmoja mmoja.

Habari njema hii ni kwa mujibu wa Barrick,
Karibu ujisomee
Barrick Partnership with Tanzanian Government Delivers First Major Outcomes

Japo deni letu la makinikia ya Barrick lilikuwa Dola bilioni 190 ambazo zingetosha kumnunulia Noah kila Mtanzania, tukaahidiwa kishika Uchumba cha dola milioni 300!, lakini kufuatia majadiliano marefu, tulisamehe deni lote, na kile kishika Uchumba cha dola milioni 300, tulikikubali kuwa sasa ndio mahari kamili, hivyo hili donge nono la dola milioni 100, ndio mwanzo wa utekelezaji wa makubaliano na Barrick.

Donge nono hili la dola milioni 100 ni nje ya gawio la hisa asilimia 16% za bure bure, ambayo Tanzania tumepewa kwenye kampuni mpya ya ubia wa Tanzania na Barrick, kampuni ya Twiga, na manufaa makubwa kabisa, manene na manono kabisa yanayosubiriwa kwa hamu, ni mgawo wa 50/50, yaani pasu kwa pasu ya manufaa ya Kiuchumi ya kila kinachopatikana kwenye madini yetu.

Huu ni ukombozi mkubwa sana kwa taifa letu. Hongera sana JPM.
Mungu Ibariki Tanzania

Paskali
Update.
Bunge letu ndio limetangaziwa rasmi fedha hizi mchana huu, sasa hivi, hivyo wewe as mwana jf, you were the first to know, na kwenye magazeti ni kesho!.
Viva if
Mungu Ibariki JF
Mungu Ibariki Tanzania
P
Update 2
P
 
Ni kweli makinikia yaendelea kusafirishwa nje?

Pascal Mayala nimekuwa nikijua wewe ni msomi kumbe ni wale wale.

Barrick wamelipa $100million kati ya $300m waliohaidi kulipa.

$100million imetokana na mauzo ya kwanza ya container 1600 za makinikia zilizokuwa zimezuiwa na serikali.

$200million zilizobaki wamehsidi kulipa ndani ya miaka 5. Yani kila mwaka ni $40mln.

Kupigwa kupo pale pale.

Kama safari moja ya container 1600 wamefanya mauzo nakupata faida ya zaid ya $100million. Jiulize kwa mwaka wanapeleke contsiner ngapi? Na kila mwaka tunaambulia $40m only!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pascal,

Haya ni mauzo ya makinikia bwana. Hawa jamaa wajanja sana,mie nilijua watatoa mzigo kule walipoiba,kumbe humu humu.

Bora tungeyapiga mnada wenyewe tu yale makontena.

Sent using iphone pro max

Je kabla ya magufuli.. hayo mauzo ya makinikia tulikuwa tunalipwa bei gani?
Magufuli ni jembe.. mbona awamu za 3 na 4 hatukulipwa na makinikia yalikuwa yanasafiri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…