Gundu la kinyesi

Gundu la kinyesi

Gundu ni kiambishi cha kuelezea mambo kwenda mrama mambo kuharibika, mambo kutanzika! Hali ya kuchukiwa na hata kutengwa.
Kinyesi pamoja na kwamba ni samadi nzuri kikishaoza na uvundo kwisha lakini. ! ni makapi ya chochote ulichokula, yani mwili umeshachukua vyote vya maana kwahiyo hicho kilichobaki ni uchafu

Kinyesi ni kitu kingine kabisa licha ya uvundo wake lakini ukikikanyaga lazima uchechemee kama mtu aliyechomwa na mwiba..yani unapata hisia fulani mbaya kabisa akilini ukiwa umekikanyaga....na ndio maana hakuna nyumba inayokamilika bila kuwa na choo ya kuhifadhia hiyo kitu
Ukisikia mtu ana kimavi, muonee huruma maana ni mwendo wa mikosi mwanzo mwisho

Sasa hebu pata picha hii
Unaamka asubuhi na kukuta barazani kwako au getini kuna bonge la kimba! Unajiuliza na kutafakari mengi lakini unapuuzia na kufanya maarifa ya kusafirisha

Hii inaweza kutokea hata zaidi ya mara tatu na kudhani ni watu wakorofi au pengine wavuta bhangi....pole sana ni heri wawe ni hao kuliko kama ni mambo ya kishirikina..kwakuwa baada ya hapo kila kitu kitaanza kuyumba, vile watu wanavyokiogopa kinyesi na kujitenga nacho ndio hivyo hivyo nawe utakuwa
Ni mambo mabaya ya kishetani huja na madawa na manuizi ya uharibifu mbaya...na akimaliza huseta ukuta kwa makalio yake

Naamini wengi walishakutana na jambo kama hili kwa namna moja au nyingine na baada ya hapo ukaanza kukutana na milima na mabonde, hutakiwi kutafuta waganga wa kienyeji. ....kwa imani yako fanya utaratibu wa ibada ya kutakasa makazi. ..hiyo ndio dawa pekee ya kuweza kukuokoa na hili janga

NB: ushauri wa bure
Kama wewe si mpenzi wa hizi mada nakushauri upite kimya
ahsante mkuu nime elimika
 
Mungu atusaidie Watanzania kuondokana na imani potofu za kishirikina. Ndio maana nchi inachelewa sana nawasihi tubadilike tuachane na mambo ya kishetani.
Kweli tunafikia hatua kinyesi inakuwa mada leo hii duh hasara kubwa ya kiroho naiona. Hebu tuache ujinga bana hivi kama jumba lako unalijenga miaka nenda rudi unategemea lisigeuzwe choo au genge la wazinzi au wavuta bangi? Hebu acheni upuuzi
 
116-logo%20cerceveli.jpg
Kuna jeans niliiacha kuinunua kwasababu ya hio brand name ingawa ilikuwa kali sana.
 
Wakati mwingine wezi wajapo kuiba asubuhi unakutana na kimba pia. Nia yao ni nini?
 
Naomba nifafanue kidogo hapa kuhusu huo ushirikina
1.kinyesi kinachopakazwa kwenye kuta lengo lake ni kuitia nyumba gundu ujenzi usiendelee
2. Kile cha Kuwekwa getini au mlangoni aidha kinamlenga atakayeanza kutoka au mlengwa aliyetajwa kwa jina kwenye huo ushirikina
Kumbuka mada ya malango na ile ya nafsi katika utambulisho
Mshana jr na kuna ile wezi wanaingia ndani usiku wanaiba,wakishamaliza lazima mmoja ashushe kimba la nguvu ndani,hii ilikuwa maarufu sana zamani,siku hizi haisikiki sana,sijui maana yao hasa huwa ni nini.na wakati mwingine kama kuna chakula wanakula halafu wanaachia kimba ndani ya sufuria.
 
Mshana jr na kuna ile wezi wanaingia ndani usiku wanaiba,wakishamaliza lazima mmoja ashushe kimba la nguvu ndani,hii ilikuwa maarufu sana zamani,siku hizi haisikiki sana,sijui maana yao hasa huwa ni nini.na wakati mwingine kama kuna chakula wanakula halafu wanaachia kimba ndani ya sufuria.
Ni kweli kabisa nakumbuka sana hiyo kitu kama si mibangi basi pengine ni masharti ya mganga
 
Ni kweli kabisa nakumbuka sana hiyo kitu kama si mibangi basi pengine ni masharti ya mganga
Kkuna mama wa kihindi customer wetu kwenye bank,aliomba apelekwe locker room,kuingia kule akaanza kujisaidia chini,hata alipopelekwa chooni alijisaidia chini.uzi wako umenikumbusha kisa hiki.
 
Kkuna mama wa kihindi customer wetu kwenye bank,aliomba apelekwe locker room,kuingia kule akaanza kujisaidia chini,hata alipopelekwa chooni alijisaidia chini.uzi wako umenikumbusha kisa hiki.
Mmh halafu ikawaje?
 
Mmh halafu ikawaje?
Tulipomuuliza kama anaumwa?akasema hapana ni bahati mbaya.ikabidi cleaners wafanye usafi,niliwahurumia sana kwa kweli,tukadhani labda mama yule wa kihindi kwa tendo la aibu alilofanya atachukua muda mrefu kurudi,lakini alikuja baada ya siku 2,yuko kawaida kabisa kama hakuna lililotokea.na hadi leo ana locker lake hapa.
 
Mkuu upo sawa kabisa mimi baada ya kumaliza ujenzi siku ya kuhamia tulikuta kinyesi kibichi sebuleni nailihali milango na madirisha vikiwa vimefungwa wajuzi wa mambo wakaniambia hilo nibalaa tusiingie wala kukitoa mpaka tupate mtaalam wakimaanisha mganga lakini badala yake nilitafuta wachungaji tukafanya maombi mpakaleo nimiaka 7 tunaishi bila wasiwasi
 
Back
Top Bottom